Rais Kikwete azuiliwa kuingia Denmark

Rais Kikwete azuiliwa kuingia Denmark

Mheshimiwa Raisi unaanza kuwaaga Wazungu badala ya kuanza na sisi tuliokuchagua?
 
Sijui ziara za kuzungukia mikoa kwaajili ya kuaga ataanza lini....

Ataanza baada ya kutoka ziara za kujiaibisha kwa Wazungu. Eti anaaga!!! Wazungu wanamwona hamnazo kwani nchi yake iko katika harakati za mchakato wa uchaguzi yeye anaenda kuzubaazubaa kwao. Mswahili huyu.
 
Hapa kwetu mbona TeamLowassa ndio wanapewa coverage na vyombo vyote tena kwa heading za kutisha !?.
Magazeti 'pendwa' pekee ya Shigongo ndio nayaona yanatembeza 'vijembe' kwa Team hiyo !


Sasa unaniuliza Mimi ili iwdje? mi nimetoa ushauri kwa vyote visitoe coverage kwa upendeleo!!!
 
Last edited by a moderator:
Sasa unaniuliza Mimi ili iwdje? mi nimetoa ushauri kwa vyote visitoe coverage kwa upendeleo!!!

Mie nimeuliza hadhira ya JF na TeamLowassa, tena kwa mshangao. Labda kuna mtu anajua kilicho nyuma ya hilo.
 
Last edited by a moderator:
Hii mbona ni kawaida hata Ommy Diampoz alizuiliwa kuingia USA
 
KENGE kweli wewe wivu wanini sasa? unauliza then Una conclude mwenyewe kabla ya jibu Una shida ktk ubongo wako.

Mbona una hasira hivyo ! ni majeruhi wa huo mtoko nini ? maana per diem kwa US dolar lusungo
 
Last edited by a moderator:
Kwani yeye JK hakujua kuwa hao wazungu wanafanya uchaguzi week ijayo? na washauri wake wanafanya kazi gani na intelijensia yao ikoje?

Hawa viongozi na watu wa CCM vipi? wanadhani kila kitu hapa duniani ni kufanya kienyeji tu hadi nchi za wenye akili kama wanavyovuruga hapa Tanzania na wanaachiwa tuu! Ni ishara nyingine ya 'poor coordination' ktk protocal za utawala wa CCM.

Siku zinakuja...Oktoba CCM mkeshang'olewa itakuwa fundisho na taifa hili litarudi ktk mstari wake! No more of this careless mess!!
 
Kwani yeye JK hakujua kuwa hao wazungu wanafanya uchaguzi week ijayo? na washauri wake wanafanya kazi gani na intelijensia yao ikoje?

Hawa viongozi na watu wa CCM vipi? wanadhani kila kitu hapa duniani ni kufanya kienyeji tu hadi nchi za wenye akili kama wanavyovuruga hapa Tanzania na wanaachiwa tuu! Ni ishara nyingine ya 'poor coordination' ktk protocal za utawala wa CCM.

Siku zinakuja...Oktoba CCM mkeshang'olewa itakuwa fundisho na taifa hili litarudi ktk mstari wake! No more of this careless mess!!


Hata Mimi nashangaa Sana!!!

Aina ya watu aliochagua wamzunguke wanamwaibisha Sana!!

Pale ikulu ndo balaa ukiona wanaoingia pale utaduwaa!!!
 
Amealikwa au kajiaLika? Kwani alipigiwa kura na wa denmark mpaka awaage?
 
Sidhani kama kuna rais aliyepiga per diem za kutosha kuliko huyu! Yaani hawa wadau wa maendeleo waliokwamisha kutekelezwa kwa bajeti juzi, leo anazunguka kuwaaga wakati juzijuzi kasema nchi ina heshima yake na haiwezi kubabaishwa na wafadhili!?

Huku ni kutalii tu na kufuja pesa za umma. Hawa wafadhili kwasasa hawana interest na JK. Macho yao yote yapo kwa rais ajaye. Kwanini anapoteza pesa bure kwa ziara zisizo na sababu wala maslahi kwa taifa? Kwani hawezi kuaga kupitia mabalozi au njia zingine za mawasiliano? Aibu yetu hii sisi ngozi nyeusi.
Alipoingia madarakani alianza ziara za kujitambulisha. Sasa ana ziara za kuaga

Utamaduni huu haukuwepo kwa marais waliotangulia, na wala marais wa nchi jirani na kwingineko hawana muda wa kupoteza namna hii

Kesho tunalalamika Kenyatta anafanya mambo! Yes, katulia na anafikiri namna ya kutumia resource za nchi yake. Hivi unakwendaje kushukuru kwa kupitisha bakuli!

Inasikitisha sana!
 
Alipoingia madarakani alianza ziara za kujitambulisha. Sasa ana ziara za kuaga

Utamaduni huu haukuwepo kwa marais waliotangulia, na wala marais wa nchi jirani na kwingineko hawana muda wa kupoteza namna hii

Kesho tunalalamika Kenyatta anafanya mambo! Yes, katulia na anafikiri namna ya kutumia resource za nchi yake. Hivi unakwendaje kushukuru kwa kupitisha bakuli!

Inasikitisha sana!

Anatia aibu sana huyu jamaa serikali yake imetia fora kwa ufisadi mpaka tumenyimwa misaada lakini jamaa halioni hilo bado anazurura kuomba omba tu, wanamshangaa sana kutwa yuko angani utafikiri anaruka kwa mbawa zake na si mafuta ambayo tuna nunua kwa fedha za kigeni, halafu eti anasikitika kutuacha maskini jamaa ni zaidi ya msanii.
 
Back
Top Bottom