Ushauri kwenu nyie wa hiyo dini
1) kuwekeza kwenye elimu ya mtoto wako sio lazima uwe umeajiriwa na kulipwa posho za semina kama ulivyosema hapo juu. Sasa ivi watu wengi wanajishughulisha na biashara pamoja na kilimo ambazo zinawaingizia pesa nyingi tu. So kuwekeza kwenye elimu ni wewe mwenyewe tu
2) Zanzibar mpo karibu 99% ya watu wote wanaoishi huko na hivyo dini hiyo ndio waliojaa kwenye hizo ofisi huko zanzbar, sasa kwa nn msiwe mfano huko zenj kwa kuwekeza kwenye elimu ikiwa nyie mpo wengi sana kwenye ajira huko?? Hebu tueleze hadi sasa mna vyuo vikuu vingapi na bora?
3) Top 10 ya matajiri waliopo Tanzania mpo nyie wote wa hiyo dini, kwa nn msikae nao chini hawa matajiri mkawaomba wawekeze pia kwenye kujenga shule za kisasa pamoja na vyuo vya kisasa ili waweze kusaidia watu maskini wa dini hiyo na wasio na uwezo wa kulipa ada?
4) Wenzenu kwenye ibada wanachangishana hadi leo kwa ajili ya ujenzi wa kujenga shule za awali na za sekondari, na sadaka huwa hadi mara mbili na baada ya hapo wanatafuta pori huko wananunua wanajenga. Na nyie kwenye ibada mchangishane michango kwa ajiki ya ujenzi wa shule za awali na sekondari
5) Hayo juu yanawezekana ikiwa tu mtabadilisha uongozi kwenye nyumba zenu za ibada, kiongozi wenu wa dini asipimwe tu kwa kuijua dini vizuri bali pia awe ana elimu dunia ya kutosha ili kuweza kuwaweka sawa katika kufikia hayo hapo juu.
Kwenye dini fulani hivi dhehebu fulani hivi huwezi kuwa kiongozi wao kama huna elimu( degree ndio minimum)
6) Ukiwa huna uwezo kifedha lakini una akili kichwani basi utatoboa tu.
- mtihani wa darasa la 7 umefaulu vizuri utangiwa sekondari ya serikali kwenye ada ndogo kabisa
- sekondari ukifaulu vizuri pia utapangiwa high school nzuri tu ya serikali kwemye ada ndogo
- high school ukifaulu vizuri tu, utapangiwa chuo cha serikali kizuri tu na mkopo utapewa
7) Point namba 6: kama kwenye dini yenu hakuna watu wengi wanaoweza kufaulu sana basi hili tatizo sio la sirikali bali ni.....
Na kama wanafaulu sana basi inawezekana mpo wachache sana kwenye nchi kwa maana let say mpo jumla ya wanafunzi mil 2 nchini, wenye uwezo wa kufaulu sana moja kwa moja mpo mil 1 na wenzenu let say wapo wanafunzi mil 10 na wanaoweza kufaulu moja kwa moja wapo mil 4, jua tu mtamezwa
8)Dhana ya dini flani wamejaa sana maofisini inaweza kuwa kweli lakini pengine si sababu ya dini yao, kwa sababu mm na jamaa zangu ni wa hiyo dini na tumefaulu vizuri tu na tuna elimu nzuri ila hadi leo tume-suffer sana kupata hizo nafasi lakini hamna kitu. Hakuna atayekusaidia au kukupigia pande kisa wewe ni dini yake
Bali
Anaweza kukusaidia, kukupigia pande, kukupa connection kama wewe ni kabila lake na tu ni ndugu wa karibu ( mtoto wa mjomba, shangazi, mama mkubwa, baba mdogo n.k).