Rais ajaye akerwe na udini kwa vitendo

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,304
12,600
Kanuni za uteuzi na ajira lazima zipitiwe upya ili ziruhusu watu wa dini zote wateuliwe na kuajiriwa kwa uwiano, hasa baada ya vigezo muhimu vya elimu na uzoefu wa kazi husika kuzingatiwa.

Inahuzunisha sana kukuta wafanyakazi wote wa ofisi ya umma au taasisi ya umma Ni wa dini fulani tu. Inasikitisha unakwenda kwenye semina au workshop au mkutano na kukuta washiriki wengi Kama sio wote ni wa dini fulani tu. Hivyo kusababisha vikao kufunguliwa na kufungwa kwa maombi ya dini fulani tu.

Ukifika kwenye ofisi za umma utakuta Mtumishi kaweka kwa sauti music wa dini fulani na watu hawahoji kwakuwa ni wa upande huo.

Hii sio bahati mbaya Wala coincidence. Ikumbukwe kuwa mishahara ya ajira na posho za vikao na mikutano ndizo zinazokwenda kuwekezwa kwenye elimu za watoto na maendeleo ya familia za watu waliopewa fursa ya ajira na kuhudhuria mikutano na kupata hela. Hivyo, wale wanaoikosa fursa hata familia na maendeleo yao yatakuwa duni.

Hii inasababisha maisha na familia za jamii inayopatiwa fursa hizi kuwa mbele kimaisha na kielimu. Hivyo familia za wanufaika kuendelea kutoa watumishi bora na wenye elimu shindani na wale wanaonyimwa fursa kuendelea kutoa watu wasiokuwa bora na elimu shindani kwenye ajira, "vicious cycle"

Rais anayekuja lazima azimulike ofisi zote za umma na taasisi, washa, mikutano, workshops na teuzi zote ili kujiridhisha na uwiano wa kidini pia baada ya vigezo vingine kukamilika.

Taasisi zetu za dini hazijui kazi zao au zinaogopa kutimiza kazi zao? Au ni hayo hayo matokeo ya kukosa fursa za elimu kwa njia hii?

Rais ajae pamoja na Mambo mengine ya jumla lakini autazame pia huu ufa kwenye taifa.
 
Isiishie huko tu hadi kwenye shughuli binafsi unakuta ni wadini fulani tu ndio wameajiriwa, hili lipo sana. Hapa mamlaka za ajira na mifuko ya Jamii ziliangalie hili maana hata wao wanawajua kupitia list za majina wanayokata michango ya wafanyakazi hii itasaidia kuleta balance.
 
Ndugu zetu hawawezi kuwa sawa na sisi. Tatizo lao kubwa, wanawafundisha zaidi vijana wao Elimu Ahera zaidi ya Elimu Dunia. Si Jambo baya, lakin wanakosa ujuzi kutokana na kuwa na Elimu ndogo. Nakubali kuwa, wengi wao waliobahatika kutoboa, wako vizuri kichwani and their good leaders japo itikadi huwa zinawazidi.

Chukulia mfano, Kati ya wanafunzi mia mbili wa Udaktari wanaodahiliwa kila Mwaka na Chuo Kama Muhimbili, Hawa ndugu zetu huwa hawazidi ishirini.

Na si kwamba wanabaniwa, Ila ufaulu wao mdogo unawanyima fursa sawa ya kudahiliwa. Nawashauri, wajifunze kwetu, nguvu wanayotumia kujenga nyumba nzuri za ibada hapa mjini, wazitumie pia kujenga shule Bora Kama za kwetu. Kwa elimu za Ubungo Seminary hawawezo kushindana na Msolwa.

Asante.
 
Ndugu zetu hawawezi kuwa sawa na sisi. Tatizo lao kubwa, wanawafundisha zaidi vijana wao Elimu Ahera zaidi ya Elimu Dunia. Si Jambo baya, lakin wanakosa ujuzi kutokana na kuwa na Elimu ndogo. Nakubali kuwa, wengi wao waliobahatika kutoboa, wako vizuri kichwani and their good leaders japo itikadi huwa zinawazidi...
Wakijenga shule nzuri watasoma watoto wale wa kule pia kwani wazazi wao ndio wenye ajira, wenye teuzi na wanaohudhuria semina na workshops kila Mara hivyo wanaweza kulipa ada kwenye shule bora zisizoweza kushindana na zike za kata.

Hivyo hutashangaa kuona wanaokwenda vyuo vikuu wengi wao Ni wale wanaotokakwenye zile shule bora na ghari. Hawa ndio watakaovijaza vyuo vikuu huko muhimbili unakosema. Tatizo sio watoto Bali wazazi wao na wazazi wao sio tatizo Bali waliotoa fursa bila kuzingatia
 
Naunga mkono hoja, Jiwe ni mdini mpaka anatia aibu.

Kawanyina nafasi za utumishi serikali mpaka inashangaza sana.

Tunataka serikali adilifu kwa raia wake wote.

Kiukweli kuna ubaguzi wa kimfumo dhifi ya waislamu katika nyanja za utumishi wa umma na serikalini.

Hili ni bomu linalosubiri kupasuka!
 
Hebu kila waziri aagize orodha za watu waliohudhuria kwenye semina, workshops nk zote zilizofanyika mwaka huu tu aone Ni akina Nani wamealikwa, kuhudhuria na kulipwa posho. Baada ya kulipwa posho si wanaenda kulipia ada za watoto wao? Kununua kiwanja? Kufuga kuku? Kupiga rangi nyumba zao?
 
Ushauri kwenu nyie wa hiyo dini
1) kuwekeza kwenye elimu ya mtoto wako sio lazima uwe umeajiriwa na kulipwa posho za semina kama ulivyosema hapo juu. Sasa ivi watu wengi wanajishughulisha na biashara pamoja na kilimo ambazo zinawaingizia pesa nyingi tu. So kuwekeza kwenye elimu ni wewe mwenyewe tu

2) Zanzibar mpo karibu 99% ya watu wote wanaoishi huko na hivyo dini hiyo ndio waliojaa kwenye hizo ofisi huko zanzbar, sasa kwa nn msiwe mfano huko zenj kwa kuwekeza kwenye elimu ikiwa nyie mpo wengi sana kwenye ajira huko?? Hebu tueleze hadi sasa mna vyuo vikuu vingapi na bora?

3) Top 10 ya matajiri waliopo Tanzania mpo nyie wote wa hiyo dini, kwa nn msikae nao chini hawa matajiri mkawaomba wawekeze pia kwenye kujenga shule za kisasa pamoja na vyuo vya kisasa ili waweze kusaidia watu maskini wa dini hiyo na wasio na uwezo wa kulipa ada?

4) Wenzenu kwenye ibada wanachangishana hadi leo kwa ajili ya ujenzi wa kujenga shule za awali na za sekondari, na sadaka huwa hadi mara mbili na baada ya hapo wanatafuta pori huko wananunua wanajenga. Na nyie kwenye ibada mchangishane michango kwa ajiki ya ujenzi wa shule za awali na sekondari

5) Hayo juu yanawezekana ikiwa tu mtabadilisha uongozi kwenye nyumba zenu za ibada, kiongozi wenu wa dini asipimwe tu kwa kuijua dini vizuri bali pia awe ana elimu dunia ya kutosha ili kuweza kuwaweka sawa katika kufikia hayo hapo juu.
Kwenye dini fulani hivi dhehebu fulani hivi huwezi kuwa kiongozi wao kama huna elimu( degree ndio minimum)

6) Ukiwa huna uwezo kifedha lakini una akili kichwani basi utatoboa tu.
- mtihani wa darasa la 7 umefaulu vizuri utangiwa sekondari ya serikali kwenye ada ndogo kabisa
- sekondari ukifaulu vizuri pia utapangiwa high school nzuri tu ya serikali kwemye ada ndogo
- high school ukifaulu vizuri tu, utapangiwa chuo cha serikali kizuri tu na mkopo utapewa

7) Point namba 6: kama kwenye dini yenu hakuna watu wengi wanaoweza kufaulu sana basi hili tatizo sio la sirikali bali ni.....
Na kama wanafaulu sana basi inawezekana mpo wachache sana kwenye nchi kwa maana let say mpo jumla ya wanafunzi mil 2 nchini, wenye uwezo wa kufaulu sana moja kwa moja mpo mil 1 na wenzenu let say wapo wanafunzi mil 10 na wanaoweza kufaulu moja kwa moja wapo mil 4, jua tu mtamezwa

8)Dhana ya dini flani wamejaa sana maofisini inaweza kuwa kweli lakini pengine si sababu ya dini yao, kwa sababu mm na jamaa zangu ni wa hiyo dini na tumefaulu vizuri tu na tuna elimu nzuri ila hadi leo tume-suffer sana kupata hizo nafasi lakini hamna kitu. Hakuna atayekusaidia au kukupigia pande kisa wewe ni dini yake
Bali
Anaweza kukusaidia, kukupigia pande, kukupa connection kama wewe ni kabila lake na tu ni ndugu wa karibu ( mtoto wa mjomba, shangazi, mama mkubwa, baba mdogo n.k).
 
Ndugu zetu hawawezi kuwa sawa na sisi. Tatizo lao kubwa, wanawafundisha zaidi vijana wao Elimu Ahera zaidi ya Elimu Dunia. Si Jambo baya, lakin wanakosa ujuzi kutokana na kuwa na Elimu ndogo. Nakubali kuwa, wengi wao waliobahatika kutoboa, wako vizuri kichwani and their good leaders japo itikadi huwa zinawazidi.

Chukulia mfano, Kati ya wanafunzi mia mbili wa Udaktari wanaodahiliwa kila Mwaka na Chuo Kama Muhimbili, Hawa ndugu zetu huwa hawazidi ishirini...
 
Raisi ajaye lini mkuu?,Oct 2020 au,kama una maana hiyo useme jiwe akerwe na udini kwa vitendo.Najua majizi ya kura yanauzoefu wa kutosha kumfanya jiwe arudi oct
 
Ushauri kwenu nyie wa hiyo dini
1) kuwekeza kwenye elimu ya mtoto wako sio lazima uwe umeajiriwa na kulipwa posho za semina kama ulivyosema hapo juu. Sasa ivi watu wengi wanajishughulisha na biashara pamoja na kilimo ambazo zinawaingizia pesa nyingi tu. So kuwekeza kwenye elimu ni wewe mwenyewe tu

2) Zanzibar mpo karibu 99% ya watu wote wanaoishi huko na hivyo dini hiyo ndio waliojaa kwenye hizo ofisi huko zanzbar, sasa kwa nn msiwe mfano huko zenj kwa kuwekeza kwenye elimu ikiwa nyie mpo wengi sana kwenye ajira huko?? Hebu tueleze hadi sasa mna vyuo vikuu vingapi na bora?...
Umesema vema, lakini kumbuka kuwa huwezi kumkamua mbuzi ambae hajazaa, watu wenye kipato/ajira wanakopesheka kwenye vyombo vya fedha, hivyo kumudu kuwekeza kwenye biashara na kilimo Kama unavyosema. Mtu ambae hana ajira/posho atapata wapi mtaji, ada na sadaka ya kutosha?

Kumbuka kwenye makanisa hata wakoloni walikuwa wanasali humo, mawaziri, wakurugenzi, maofisa na watu wengine wenye mishahara na posho za vikao na semina wengi hivyo kutoa hela nyingi ya kujenga nyumba ya ibada au shule Ni Jambo dogo. Siku ya Ijumaa ukitembelea misikiti ya Ijumaa angalia viatu vya waumini walivyoviacha nje wakati wanaingia misikitini, utangundua kuwa Hali sio nzuri kwa waliomo humo ndani
 
Back
Top Bottom