Thesis
JF-Expert Member
- Aug 30, 2017
- 1,805
- 3,119
Suala la dini ni gumu sana,sijui ni bahati mbaya au ni mpango, dini fulani kubwa watumishi katika ofisi za umma ni wa kutafuta na tochi.Ushauri kwenu nyie wa hiyo dini
1) kuwekeza kwenye elimu ya mtoto wako sio lazima uwe umeajiriwa na kulipwa posho za semina kama ulivyosema hapo juu. Sasa ivi watu wengi wanajishughulisha na biashara pamoja na kilimo ambazo zinawaingizia pesa nyingi tu. So kuwekeza kwenye elimu ni wewe mwenyewe tu
2) Zanzibar mpo karibu 99% ya watu wote wanaoishi huko na hivyo dini hiyo ndio waliojaa kwenye hizo ofisi huko zanzbar, sasa kwa nn msiwe mfano huko zenj kwa kuwekeza kwenye elimu ikiwa nyie mpo wengi sana kwenye ajira huko?? Hebu tueleze hadi sasa mna vyuo vikuu vingapi na bora?..
Nipo kwenye idara yenye watumishi 27 lakini afisa muislam nipo peke yangu! Kusema ukweli kwa kadri ninavofahamu sijawahi kuona kubaguliwa kwasababu ya dini yangu.
Suala la semina na vikao (baadhi) kufunguliwa kwa sala na kufungwa kwa sala tena ya dini fulani nimekutana nalo mara kadhaa, nadhani suala hili lipigwe marufuku, Semina na warsha zifunguliwe kwa wimbo wa taifa ambao pia ni dua ndani yake, yaani MUNGU ibariki Afrika....