Raia 7 wa Kigeni wachomwa moto wakiwa hai katika Jiji la Johannesburg, chini Afrika Kusini

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Hofu ya ghasia na mauaji ya chuki dhidi ya wageni imerejea Johannesburg ambapo Jumamosi iliyoisha nyakati za asubuhi takriban wageni saba walichomwa moto wakiwa hai katika kitongoji cha Diepsloot nje ya mji wa Johannesburg.

Hii ilifuatia msako mkubwa wa wanajamii kutafuta waharifu Ijumaa usiku na Jumamosi asubuhi.

Marehemu, wote wakiwa wanaume, walishukiwa kufanya uhalifu mbalimbali katika mitaa ya extension 12 na 13 katika kitongoji cha Diepsloot.

Wakiwa na silaha kali na mawe mikononi mwao, wanajamii waliwawinda waharifu.

Siku ya Ijumaa usiku, wawili kati ya wanaume hao wanaosadikika kuwa ni waharifu walikamatwa na jamii.

Waliwavamia na silaha kali na kuanza kuwapiga kwa fimbo na hata mawe.

Kisha wakawaweka kwenye mafuta ya petroli kabla ya kuwasha.

Kwa mujibu wa Diwani wa eneo hilo bwana Abraham Mabhuke, watu hao wanashukiwa kufanya uhalifu wa kikatili katika kitongoji hicho.

Diwani Mabhuke alidai wanaume wote ni raia wa Zimbabwe.

Alisema "Wazimbabwe wawili ambao wanadaiwa kuhusika na uhalifu unaofanyika katika Diepsloot Ext 12 & 13 walikamatwa na wanajamii."

Alisema wanajamii wa gatvol walikuwa wamevamia siku ya Jumamosi asubuhi, wakiwasaka wale wanaosadikika kuwa ni wahalifu wengine waliotoroka katika msako wa Ijumaa usiku.

"Katika hali ya kushangaza, watu watano zaidi wanaodaiwa kuwa Wazimbabwe waliuawa kwa kupigwa mawe asubuhi ya leo na wanajamii wenye hasira."

Alisema siku ya Ijumaa, watu wanne ambao ni raia walipigwa risasi na wanaodaiwa kuwa wahalifu. Mmoja alifariki, na wengine watatu walikuwa hospitalini wakitibiwa majeraha ya risasi.

Mauaji ya Jumamosi ya washukiwa hao yamefikisha watu saba, idadi ya watu walioteketezwa kwa moto wakiwa hai.

Wakaazi wanasema kila jioni kunakuwa na milio ya risasi katika mji wa Johannesburg wenye msongamano na idadi kubwa ya watu.

Lizzy Maluleke kutoka mtaa wa ext 12 aliiambia chombo cha Habari cha Scrolla Africa kwamba si salama kukaa katika kitongoji hicho. "Tunajiweka ndani na kufunga milango mapema sana kama mida ya saa 1 usiku, nyakati hizo kila mtu anakuwa ndani ya nyumba. Inasikitisha" alisema.

Tangu mwanzoni mwa mwaka huu, wakazi wa Diepsloot wamekuwa wakiandamana kupinga uhalifu.

Viongozi wake watatu walikamatwa kwa kuchochea ghasia za umma.

Mnamo Juni, walidai kukutana na Rais Ramaphosa. Hata walisafiri hadi kwenye Majengo ya Muungano huko Pretoria kwa nia ya kukutana na rais wa jimbo.

Wakaazi wanasema wataendelea kuwawinda wahalifu wenyewe kwa mikono yao na kuwatokomeza, wakidai kuwa polisi wamewafeli.
 
Hofu ya ghasia na mauaji ya chuki dhidi ya wageni imerejea Johannesburg ambapo Jumamosi iliyoisha nyakati za asubuhi takriban wageni saba walichomwa moto wakiwa hai katika kitongoji cha Diepsloot nje ya mji wa Johannesburg.

Hii ilifuatia msako mkubwa wa wanajamii kutafuta waharifu Ijumaa usiku na Jumamosi asubuhi.

Marehemu, wote wakiwa wanaume, walishukiwa kufanya uhalifu mbalimbali katika mitaa ya extension 12 na 13 katika kitongoji cha Diepsloot.

Wakiwa na silaha kali na mawe mikononi mwao, wanajamii waliwawinda waharifu.

Siku ya Ijumaa usiku, wawili kati ya wanaume hao wanaosadikika kuwa ni waharifu walikamatwa na jamii.

Waliwavamia na silaha kali na kuanza kuwapiga kwa fimbo na hata mawe.

Kisha wakawaweka kwenye mafuta ya petroli kabla ya kuwasha.

Kwa mujibu wa Diwani wa eneo hilo bwana Abraham Mabhuke, watu hao wanashukiwa kufanya uhalifu wa kikatili katika kitongoji hicho.

Diwani Mabhuke alidai wanaume wote ni raia wa Zimbabwe.

Alisema "Wazimbabwe wawili ambao wanadaiwa kuhusika na uhalifu unaofanyika katika Diepsloot Ext 12 & 13 walikamatwa na wanajamii."

Alisema wanajamii wa gatvol walikuwa wamevamia siku ya Jumamosi asubuhi, wakiwasaka wale wanaosadikika kuwa ni wahalifu wengine waliotoroka katika msako wa Ijumaa usiku.

"Katika hali ya kushangaza, watu watano zaidi wanaodaiwa kuwa Wazimbabwe waliuawa kwa kupigwa mawe asubuhi ya leo na wanajamii wenye hasira."

Alisema siku ya Ijumaa, watu wanne ambao ni raia walipigwa risasi na wanaodaiwa kuwa wahalifu. Mmoja alifariki, na wengine watatu walikuwa hospitalini wakitibiwa majeraha ya risasi.

Mauaji ya Jumamosi ya washukiwa hao yamefikisha watu saba, idadi ya watu walioteketezwa kwa moto wakiwa hai.

Wakaazi wanasema kila jioni kunakuwa na milio ya risasi katika mji wa Johannesburg wenye msongamano na idadi kubwa ya watu.

Lizzy Maluleke kutoka mtaa wa ext 12 aliiambia chombo cha Habari cha Scrolla Africa kwamba si salama kukaa katika kitongoji hicho. "Tunajiweka ndani na kufunga milango mapema sana kama mida ya saa 1 usiku, nyakati hizo kila mtu anakuwa ndani ya nyumba. Inasikitisha" alisema.

Tangu mwanzoni mwa mwaka huu, wakazi wa Diepsloot wamekuwa wakiandamana kupinga uhalifu.

Viongozi wake watatu walikamatwa kwa kuchochea ghasia za umma.

Mnamo Juni, walidai kukutana na Rais Ramaphosa. Hata walisafiri hadi kwenye Majengo ya Muungano huko Pretoria kwa nia ya kukutana na rais wa jimbo.

Wakaazi wanasema wataendelea kuwawinda wahalifu wenyewe kwa mikono yao na kuwatokomeza, wakidai kuwa polisi wamewafeli.
Mnaendaga kufanya nini huko?
 
Diepsloot ni kitongoji chenye Uhalifu wa hali ya juu sana kesi za robbery na rape zipo kwa kiwango cha juu sana kwa Johannesburg.
Wananchi huwa wanaandamana ili Polisi waingilie kati na muda mwingine viongozi wao wa vitongoji wanajichukulia sheria mkononi ya kuwasaka waharifu na kuwachoma moto au kuwaua kama sasa hivi waliwakamata vijana wawili usiku wa ijumaa wenye umri unaokadiliwa miaka 20 waliwafunga kamba na kuwaua na wengine watano alfajiri yake sijaona wakizungumza kuwa ni wageni ila ni mob attack..
Viongozi wa eneo hilo waliohusika na hayo mauaji na baadhi ya raia waoishakamatwa na kufunguliwa kesi ya Murder...
 
Hio adhabu wangepewa wabakaji huku bongo ingesaidia sana kuwalinda watoto
 
Wasauzi wana stress sana za maisha, naona sasa ni kama wameamua kumalizia wageni hasira zao, hiyo nchi sio salama kwa mgeni kuishi wakati huu, hao jamaa wenyewe ndio wahalifu namba moja zaidi hata ya hao wageni wanaowawinda.

Wanapata kiburi cha kutenda uhalifu wao kwasababu wako kwao, wanajiona sasa wana hati miliki ya kutoa uhai wa wengine.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Wasauzi wana stress sana za maisha, naona sasa ni kama wameamua kumalizia wageni hasira zao, hiyo nchi sio salama kwa mgeni kuishi wakati huu, hao jamaa wenyewe ndio wahalifu namba moja zaidi hata ya hao wageni wanaowawinda.
Taarifa haijasema walikuwa wanawinda WAGENI, inasema walikuwa wanawinda WAHALIFU
 
Hatari sana, uhalifu unapozidi watu wanachukua sheria mkononi kwa hasira kali kama movie ile ya Hollywood - The Purge 2013 - serikali inawacha watu watoe hukumu kutokana na uhalifu kuvizidi vyombo vya ulinzi na usalama.
 
Back
Top Bottom