Je, ni kweli Nabii hakubaliki kwao? Raia wa Afrika Kusini wataka Jeshi la Polisi Tanzania kwenda kuzuia uhalifu nchini kwao

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Moja ya changamoto kubwa sana tuliyokuwa nayo Tanzania, ni kuona kila kitu tulichokuwa nacho hakifai.

Wakati nchini Tanzania hadi tume ya kupitia mfumo wa Haki Jinai ikiwa imeundwa na tayari ipo kazini, raia wa Afrika Kusini wameonyeshwa kuvutiwa sana na utendaji kazi wa Jeshi la Polisi la Tanzania katika kupambana na uhalifu hadi kufanikisha kukamatwa kwa wahalifu waliotikisi taifa lao siku za hivi karibuni.

Katika tweets zao, raia hawa wa Afrika Kusini wamefikia hatua ya kuomba Jeshi letu la Polisi kwenda kufanya kazi ya kuzuia uhalifu nchini mwao!

Sasa nimeamini nabii hatambuliki kwao. Heko kwa Jeshi letu la Polisi, pamoja na changamoto kweli mmetuheshimisha.

Screenshot_20230413_112533_Twitter.jpg
Screenshot_20230413_112500_Twitter.jpg
 
Ukiachia viongozi wachache wa ccm wanaowaamrisha polisi kufunya vitu vya ajabu kwa sababu za kisiasa na polisi wachache wasiojielewa.

Bado jeshi letu ni nzuri tu na wanajitahidi sana.
Moboresho
*kuwe na sera mpya ya jeshi la pilisi itayoendana na mazingira ya sasa tuachane na sera za toka ukoloni na uhuru.

*serikali iongeze askari na budget kwenye jeshi kuwe na vifaa vya kutosha na magari ya patrol kila kata au mtaa 24 hrs.
Maslah ya polisi pia yazingatiwe angalau yawe km ya jeshi la wananchi.

*waajiriwa wapya wa jeshi elimu ya chini iwe certificates angalau professional km (laws, ict na community dev na the like zipewe kipao mbele kwenye jeshi hilo.

Tukiamua tunaweza kuanza na hii hata dar es salaam kwanza ..au km wilaya moja kwanza then tukasambaza service bora taratibu sehemu nyingine.
 
Katika kudhibiti uhalifu. Jeshi la Polisi Tanzania limeithibitishia dunia kuwa moja ya Jeshi bora kabisa hadi sasa

Afrika kusini kuna watu sio makondoo kama hapa kwetu. Hawa polisi wa Tanzania wanaona sifa kupiga raia wasio na silaha, wakienda south wote watarudi wakiwa kwenye majeneza. Huko Afrika kusini hawakimbizi mwenge wa uhuru boss, hivyo raia wake sio waoga kihivyo.
 
Afrika kusini kuna watu sio makondoo kama hapa kwetu. Hawa polisi wa Tanzania wanaona sifa kupiga raia wasio na silaha, wakienda south wote watarudi wakiwa kwenye majeneza. Huko Afrika kusini hawakimbizi mwenge wa uhuru boss, hivyo raia wake sio waoga kihivyo.
Unajua kiwango cha uhalifu South Afrika?
 
Moja ya changamoto kubwa sana tuliyokuwa nayo Tanzania, ni kuona kila kitu tulichokuwa nacho hakifai.

Wakati nchini Tanzania hadi tume ya kupitia mfumo wa Haki Jinai ikiwa imeundwa na tayari ipo kazini, raia wa Afrika Kusini wameonyeshwa kuvutiwa sana na utendaji kazi wa Jeshi la Polisi la Tanzania katika kupambana na uhalifu hadi kufanikisha kukamatwa kwa wahalifu waliotikisi taifa lao siku za hivi karibuni.

Katika tweets zao, raia hawa wa Afrika Kusini wamefikia hatua ya kuomba Jeshi letu la Polisi kwenda kufanya kazi ya kuzuia uhalifu nchini mwao!

Sasa nimeamini nabii hatambuliki kwao. Heko kwa Jeshi letu la Polisi, pamoja na changamoto kweli mmetuheshimisha.

View attachment 2586250View attachment 2586251
Wanakurupuka, ukisoma kisa mpaka kukamatwa kwa huyo bester, ni hao hao S.A walipenyeza ripoti kuwa yuko TZ wala si jeshi letu lililokuwa na taarifa.
 
Back
Top Bottom