Rafiki yangu kampenda dada mwenye Sickle Cell

Rafiki yangu kampenda dada mwenye Sickle Cell

Mimi binafsi Nina sickle cell, Ila naishi maisha ya kawaida kama waishivyo wengine. Tena najiona Nina bahati ya kuwa ugonjwa mzuri sana ksb ni ugonjwa unaonitaka Nile balance diet muda wote, ninywe Maji ya kutosha, niyale na kuyathamini sana matunda. Kiufupi Nina afya bora. Sickle cell imenifanya nithamini sana kuwa na afya bora kuliko kitu chochote kile.
Ni MTU mzima mwenye watoto wawili, mtoto mmoja karithi anao kama Mimi, Ila mwingine hana. Kupitia ugonjwa huu tumejikuta family nzima tunathamini na ukizingatia sana mlo kamili, mazoezi,Maji, kwa ufupi afya bora. Tunaishi kwa furaha kabisa, changamoto nilizonazo ni za kawaida tu ,ukizingatia kuwa maisha hayakosi changamoto.
Angalia tabia za MTU, Ila kuhusu magonjwa ya kurithi mengine yana changamoto kubwa kikubwa ni kuzingatia masharti ya wataalam na kumwomba Mungu zaidi. Zaidi sana Jikubali ,jipende, jithamini, jilinde, jiombee ili uyafurahie maisha.
Duuh, jamani asante kwa ushauri pia pole sana, mkuu Mungu huyu katuficha mengi aisei.
 
Nilisikia mtu mwenye sickle cell anaemia akishavuka miaka 22 hatari inapungua! Awe nae tu, ikiwezekana aambatane nae kwa daktari ili afahamu jinsi ya kuishi nae vizuri.
Tatizo jamaa kapanic pindi hicho mdada wa watu ndiyo kabisa kajihakikishia kwa jamaa.
 
Hiyo ni ishu ya genes!!!

Kama mwanaume sio carrier wa sickle cell, hawawezi pata mtoto mwenye sickle cell, bali watazaa watoto waliobeba hizo cells!!
Inakua hatari kama mwanaume atakua AS na mwanamke ni SS.
Duuh! Kwahiyo madogo watakuwa carier!
 
Circle cell ni ugonjwa usioambukiza Bali hurithishwa na si lazima warithi wanao yaweza kua wajukuu wakaja rithi, Nina ndugu yangu anahudhuria tiba pale muhimbili na masharti yake kama chakula ni sawa tu tunavyotakiwa kula yeyote asiye ugua wao wanasisitiziwa zaidi vitamins protein na fat kwa ajili ya kuimarisha miili yao maana ni wadhoofu kidogo (japo kwa mtu mpenda mazoezi huwezi mjua)
Kikubwa kama huyo rafiki yako ni mkorofi mkorofi ni bora akamuacha binti wa tu maana wale hawatakiwi kupigwa (atapata kesi) lakini pia wanashauriwa wasichukie (wasikasirike) hovyo, hivyo rafiki yako anatakiwa awe mfariji wa huyo binti badala ya kua sehemu ya tatizo lake, kuzaa wanazaa japo wengi uzazi wao huwa wa shida hii huambatana pia na kuchelewa kuvunja ungo (kubalehe)
Aisei, hii ni hatari sana! Ngoja nitajaribu kumwelimisha jamaa tuone ila tayari kapanic sana..!
Nitamwambia ata akitaka kumwacha achukue tahadhari na atafute sababu nje ya hii..! Inauma sana maana yule mdada ataumia mno.
 
Duuuh! Jamani mbona jamaa nikimwambia haya atamwacha ni mkubwa yuko 22 sasa hivi.

Siku zote kuufahamu ukweli ni sawa na kutua mzigo mkubwa sana moyoni, unakuwa huru na unafahamu namna ya kukabiliana na ukweli huo. Upendo una nguvu kubwa sana katika maisha ya mwanadamu. Na tatizo la shemeji yako ni jambo ambalo tumeona watu ambao wameishi miaka mingi na kuwa na mafanikio wakiwa na sickle cell.

Mfahamishe rafiki yako kuhusu sickle cell lakini mwambie kwamba maisha yetu ni Mungu anapanga, sisi kama wanadamu kwa akili zetu hatuwezi kujiongezea hata saa moja ya muda wa kuishi. Akumbuke kwamba siku zote kiapo cha ndoa ni kupendana katika shida na raha mpaka kifo kitutenganishe.

Kila jambo tunalokutana nalo linatokea kwa sababu maalumu. Asimwache kwa kigezo cha sickle cell, maana hakuna hata mmoja wetu ajuaye kesho yake, na hujafa hujaumbika.
 
Hapa ndo unagundua kuna michango ya baadhi ya member ni muhimu zaidi ktk kumpa moyo mtu aliyekata tamaa
.@deception
 
Seli mundu au sickle sell kama mnavyoita wenye wazungu ni ugonjwa usio na shida hasa kwa wale ambo wamevuka 18 yrs.

Naomba umwambie rafiki yako ajitahidi sana kama moyo haupo tayari kumuoa kwa sababu ya hiyo seli mundu amuache bila kumsababishia jeraha.

Mwaka huu kuna binti tumezika huko kasulu kisa jamaa alimuacha kwa sababu ya huo ugonjwa mbaya zaidi walikuwa wameshatambulishana na shughuli za ndoa zilikuwa moto moto. Binti alikuwa anajiandaa kwa ajili ya send off ndio mashilawadu wakamwambia mwanaume kuwa binti ana ugonjwa wa seli mundu na tayari binti alikuwa na mimba ya watoto mapacha tumboni.

Jamaa alipopewa zile taarifa alienda kuomba ushauri kwa wazazi wake ambao waliona ule ugonjwa ni kama nuksi vile ikabidi wamzuie kijana wao kumuoa yule binti. Binti alikuwa mwalimu wa sekondari huko Mwanza kwa msongo wa mawazo alioupata ukizingatia alishachangisha watu michanganyo ya send off na harusi leo hii aje kuwaambia ndio imeota mbawa kama ya Vicky Kamata. Binti akaiaga dunia akiwa mapacha wake tumboni.

Chonde chonde kijana naomba umuombe rafiki yako amuache kwa tahadhari kubwa sana huyo binti ili asije akafariki kwa upweke na mawazo.

Ila sickle sell sio ugonjwa wa kumuogopa mtu ispokuwa watoto au wajukuu wa huyo mama au mwenye hayo maradhi lazima wataurithi tu.
Jamani mbona ni hatari sana..! Mungu amsamehe huyo jamaa aliyesababisha kifo cha binti wa watu..! Inauma sana, shida jamaa yangu tayari kapanic vibata mno, mdada alimwambia baada ya jamaa kumwambia hatokuja kumwacha sasa mshikaji kapanic vibaya mno.
 
Mkuu, kama na huyo jamaa yako anakaasili ka sickle cell(mpaka apimwe) ,basi ajiandae kuzika watoto kila wakizaliwa
Yeye hana hilo tatizo, ila huyo mdada mwenyewe ndiyo mgonjwa ingawa haumwi kivile sana.
 
Ajilinde kila awezavyo asiwe anaugua malaria Mara kwa Mara, ale balanced diet, anywe Maji ya kutosha kila siku, afanye mazoezi , akienda hospital aonane na Dr wa huu ugongwa anaweza kushauriwa kunywa folic acid, ale vyakula vingi /matunda yanayoongeza damu. Apate muda Wa kupumzika. Asifanye kazi ngumu sana, mfano za kuchimba barabara kwa sululu.
Kuna kipindi namtania mwanangu, namwambia kuwa huu ugonjwa tulionao tunatakiwa tuishi maisha mazuri hivyo azingatie sana elimu ksb kazi ngumu sana Mungu kampa upendeleo Wa kutokufanya.
Ukimpenda mtu mwenye sickle cell wala usimwache eti ksb ana ugonjwa au ana vimelea vya ugonjwa huo, labda umwache ksb zingine. Kikubwa muonane na wataalam ili awape ushauri Wa kitaalam ili muishi kwa furaha ,amani na upendo.
Daah! Hapa nafikiria jinsi ya kumwambia mshikaji huu ushauri afu nimezoeana na huyo mdada sijui itakuwaje.
 
Siku zote kuufahamu ukweli ni sawa na kutua mzigo mkubwa sana moyoni, unakuwa huru na unafahamu namna ya kukabiliana na ukweli huo. Upendo una nguvu kubwa sana katika maisha ya mwanadamu. Na tatizo la shemeji yako ni jambo ambalo tumeona watu ambao wameishi miaka mingi na kuwa na mafanikio wakiwa na sickle cell.

Mfahamishe rafiki yako kuhusu sickle cell lakini mwambie kwamba maisha yetu ni Mungu anapanga, sisi kama wanadamu kwa akili zetu hatuwezi kujiongezea hata saa moja ya muda wa kuishi. Akumbuke kwamba siku zote kiapo cha ndoa ni kupendana katika shida na raha mpaka kifo kitutenganishe.

Kila jambo tunalokutana nalo linatokea kwa sababu maalumu. Asimwache kwa kigezo cha sickle cell, maana hakuna hata mmoja wetu ajuaye kesho yake, na hujafa hujaumbika.
Maneno mazito haya, jamani[emoji22][emoji22][emoji22][emoji22]
 
Mkuu hapo kwenye rangi umepotosha. Kama mzazi mmoja hana huo ugonjwa wala si carrier na mwingine SS basi watoto watakuwa ni carrier tu na huo ugonjwa hautawasumbua kabisa bali na wao wakitaka kuoa/kuolewa inabidi wahakikishe mke/mume mtarajiwa hana huo ugonjwa pia si carrier wa hizo cells zenye matatizo.

Kinachotakiwa kufanyika hapa ni kwenda kupima damu wote wawili na kuongea na wataalamu wa ugonjwa huu pale Muhimbili kama wako Dar au kwenye hospitali ya rufaa jirani na mkoa wanapoishi.

Seli mundu au sickle sell kama mnavyoita wenye wazungu ni ugonjwa usio na shida hasa kwa wale ambo wamevuka 18 yrs.

Naomba umwambie rafiki yako ajitahidi sana kama moyo haupo tayari kumuoa kwa sababu ya hiyo seli mundu amuache bila kumsababishia jeraha.

Mwaka huu kuna binti tumezika huko kasulu kisa jamaa alimuacha kwa sababu ya huo ugonjwa mbaya zaidi walikuwa wameshatambulishana na shughuli za ndoa zilikuwa moto moto. Binti alikuwa anajiandaa kwa ajili ya send off ndio mashilawadu wakamwambia mwanaume kuwa binti ana ugonjwa wa seli mundu na tayari binti alikuwa na mimba ya watoto mapacha tumboni.

Jamaa alipopewa zile taarifa alienda kuomba ushauri kwa wazazi wake ambao waliona ule ugonjwa ni kama nuksi vile ikabidi wamzuie kijana wao kumuoa yule binti. Binti alikuwa mwalimu wa sekondari huko Mwanza kwa msongo wa mawazo alioupata ukizingatia alishachangisha watu michanganyo ya send off na harusi leo hii aje kuwaambia ndio imeota mbawa kama ya Vicky Kamata. Binti akaiaga dunia akiwa mapacha wake tumboni.

Chonde chonde kijana naomba umuombe rafiki yako amuache kwa tahadhari kubwa sana huyo binti ili asije akafariki kwa upweke na mawazo.

Ila sickle sell sio ugonjwa wa kumuogopa mtu ispokuwa watoto au wajukuu wa huyo mama au mwenye hayo maradhi lazima wataurithi tu.
 
kwa msichana haina shida as long amevuka 22 yrs,
maana huu ugonjwa una htr mtu akiwa below hio age so akivuka maisha yana kua ya kawaida kama wengne kufa inakua ni mipango ya mungu

tatzo linakuja kwa watoto maana ugonjwa ni wa kurithi ni rahisi nao kurithi hvo nao wanaingia kwenye miaka 22 ya hofu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom