Rafiki yangu kampenda dada mwenye Sickle Cell

Rafiki yangu kampenda dada mwenye Sickle Cell

Nilisikia mtu mwenye sickle cell anaemia akishavuka miaka 22 hatari inapungua! Awe nae tu, ikiwezekana aambatane nae kwa daktari ili afahamu jinsi ya kuishi nae vizuri.
 
Dah!! umenikumbusha mkuu kuna mdada nilitokea kumpenda mwaka 2013 nikiwa bariadi na alikuwa na huo ugonjwa wa sell mundu jamani mapenzi upofu niliambiwa kila kitu kuhusu huo ugonjwa kuhusu huyo mdada lakini sikusikia hata kidogo.

Ila baadaye nilihamia mkoa mwingine kutokana na umbali wa mkoa niliokuwa na yeye alikuwa shule sijawahi kupata mawasiliano.
Jamani wewe acha tuuhh! Ndugu yangu kachanganyikiwa.
 
Hatumkatishi tamaa lakini anything can happen any time. Pia kuna uwezekano mkubwa wa kuzaa watoto wenye hilo tatizo kwa sababu huo ni ugonjwa wa kurithi.

Umenikumbusha msiba wa rafiki yangu kipenzi aliyekuwa na hilo tatizo.
Mpka wote muwe carrier otherwize mtazaa mtoto asiye na huo ugonjwa but atakuwa carrier.
 
MwanaFA nasikia pia ana sickle cell
Sidhani kama ni ugonjwa wa kuuogopa sana

Ila tatizo linakuja kuwa nasikia unaweza kurithishwa kwa mtoto
Hiyo ni ishu ya genes!!!

Kama mwanaume sio carrier wa sickle cell, hawawezi pata mtoto mwenye sickle cell, bali watazaa watoto waliobeba hizo cells!!
Inakua hatari kama mwanaume atakua AS na mwanamke ni SS.
 
Circle cell ni ugonjwa usioambukiza Bali hurithishwa na si lazima warithi wanao yaweza kua wajukuu wakaja rithi, Nina ndugu yangu anahudhuria tiba pale muhimbili na masharti yake kama chakula ni sawa tu tunavyotakiwa kula yeyote asiye ugua wao wanasisitiziwa zaidi vitamins protein na fat kwa ajili ya kuimarisha miili yao maana ni wadhoofu kidogo (japo kwa mtu mpenda mazoezi huwezi mjua)
Kikubwa kama huyo rafiki yako ni mkorofi mkorofi ni bora akamuacha binti wa tu maana wale hawatakiwi kupigwa (atapata kesi) lakini pia wanashauriwa wasichukie (wasikasirike) hovyo, hivyo rafiki yako anatakiwa awe mfariji wa huyo binti badala ya kua sehemu ya tatizo lake, kuzaa wanazaa japo wengi uzazi wao huwa wa shida hii huambatana pia na kuchelewa kuvunja ungo (kubalehe)
 
Hatumkatishi tamaa lakini anything can happen any time. Pia kuna uwezekano mkubwa wa kuzaa watoto wenye hilo tatizo kwa sababu huo ni ugonjwa wa kurithi.

Umenikumbusha msiba wa rafiki yangu kipenzi aliyekuwa na hilo tatizo.
Sio lazima ugonjwa huu utokee kwa watoto wake ila unaweza kutokea hata kwa vitukuu na watoto wakawa wazima kabisa
 
Seli mundu au sickle sell kama mnavyoita wenye wazungu ni ugonjwa usio na shida hasa kwa wale ambo wamevuka 18 yrs.

Naomba umwambie rafiki yako ajitahidi sana kama moyo haupo tayari kumuoa kwa sababu ya hiyo seli mundu amuache bila kumsababishia jeraha.

Mwaka huu kuna binti tumezika huko kasulu kisa jamaa alimuacha kwa sababu ya huo ugonjwa mbaya zaidi walikuwa wameshatambulishana na shughuli za ndoa zilikuwa moto moto. Binti alikuwa anajiandaa kwa ajili ya send off ndio mashilawadu wakamwambia mwanaume kuwa binti ana ugonjwa wa seli mundu na tayari binti alikuwa na mimba ya watoto mapacha tumboni.

Jamaa alipopewa zile taarifa alienda kuomba ushauri kwa wazazi wake ambao waliona ule ugonjwa ni kama nuksi vile ikabidi wamzuie kijana wao kumuoa yule binti. Binti alikuwa mwalimu wa sekondari huko Mwanza kwa msongo wa mawazo alioupata ukizingatia alishachangisha watu michanganyo ya send off na harusi leo hii aje kuwaambia ndio imeota mbawa kama ya Vicky Kamata. Binti akaiaga dunia akiwa mapacha wake tumboni.

Chonde chonde kijana naomba umuombe rafiki yako amuache kwa tahadhari kubwa sana huyo binti ili asije akafariki kwa upweke na mawazo.

Ila sickle sell sio ugonjwa wa kumuogopa mtu ispokuwa watoto au wajukuu wa huyo mama au mwenye hayo maradhi lazima wataurithi tu.
 
MwanaFA nasikia pia ana sickle cell
Sidhani kama ni ugonjwa wa kuuogopa sana

Ila tatizo linakuja kuwa nasikia unaweza kurithishwa kwa mtoto
Mtoto atakuwa na sickle cell trait kama mzazi mmoja atakuwa na ugonjwa huo, ila kama wazazi wote watakuwa wakumbwa na ugonjwa huo bsi mtoto atarith Hbss
 
MwanaFA nasikia pia ana sickle cell
Sidhani kama ni ugonjwa wa kuuogopa sana

Ila tatizo linakuja kuwa nasikia unaweza kurithishwa kwa mtoto
Mtoto anaweza kurithi kama huyo mzazi mwingine ni carrier ila kama mmoja ni normal mwingine ana sickle cell nadhani hakuna shida.
 
Mimi binafsi Nina sickle cell, Ila naishi maisha ya kawaida kama waishivyo wengine. Tena najiona Nina bahati ya kuwa ugonjwa mzuri sana ksb ni ugonjwa unaonitaka Nile balance diet muda wote, ninywe Maji ya kutosha, niyale na kuyathamini sana matunda. Kiufupi Nina afya bora. Sickle cell imenifanya nithamini sana kuwa na afya bora kuliko kitu chochote kile.
Ni MTU mzima mwenye watoto wawili, mtoto mmoja karithi anao kama Mimi, Ila mwingine hana. Kupitia ugonjwa huu tumejikuta family nzima tunathamini na ukizingatia sana mlo kamili, mazoezi,Maji, kwa ufupi afya bora. Tunaishi kwa furaha kabisa, changamoto nilizonazo ni za kawaida tu ,ukizingatia kuwa maisha hayakosi changamoto.
Angalia tabia za MTU, Ila kuhusu magonjwa ya kurithi mengine yana changamoto kubwa kikubwa ni kuzingatia masharti ya wataalam na kumwomba Mungu zaidi. Zaidi sana Jikubali ,jipende, jithamini, jilinde, jiombee ili uyafurahie maisha.
 
Ajilinde kila awezavyo asiwe anaugua malaria Mara kwa Mara, ale balanced diet, anywe Maji ya kutosha kila siku, afanye mazoezi , akienda hospital aonane na Dr wa huu ugongwa anaweza kushauriwa kunywa folic acid, ale vyakula vingi /matunda yanayoongeza damu. Apate muda Wa kupumzika. Asifanye kazi ngumu sana, mfano za kuchimba barabara kwa sululu.
Kuna kipindi namtania mwanangu, namwambia kuwa huu ugonjwa tulionao tunatakiwa tuishi maisha mazuri hivyo azingatie sana elimu ksb kazi ngumu sana Mungu kampa upendeleo Wa kutokufanya.
Ukimpenda mtu mwenye sickle cell wala usimwache eti ksb ana ugonjwa au ana vimelea vya ugonjwa huo, labda umwache ksb zingine. Kikubwa muonane na wataalam ili awape ushauri Wa kitaalam ili muishi kwa furaha ,amani na upendo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom