Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,561
- 19,059
George au "Big" kama tunavomuita kutokana na umbo lake kubwa ni rafiki yangu japo sio tena kama ule urafiki wa miaka kadhaa iliyopita ambapo hata familia zetu kwa maana ya wake zetu walikua karibu na ukaribu wa kutembeleana na hata kufanya mitoko na safari za pamoja za kwenda kula mema ya nchi
Big hakua mtu wa totoz au hakua macho juu kiviile, na pale alipojaribu kuchepuka kwa ku date na dada mmoja mfanyakazi mwenzie akajikuta kabobea na kazama kichwa na miguu! Mkewe(walikua wanaishi pamoja tu walikua hawajaona) akimjua huyo dada kua ni workmate wa mumewe na mwanzoni hakua na wasiwasi nae hata chembe
Mimi alikuja kuniambia wife wangu kua mama P(mke wa Big tulimuita kwa jina la mtoto wa dada yake yeye hakua na mtoto) amegundua kua Big ana cheat na huyo mfanyakazi mwenzie. Ameambiwa na watu (maana alikua na connection na wafanyakazi wengine wa ofisi ya kina George) na kwamba ameshafanya uchunguzi wa kutosha na sasa na yeye ana lipa kisasi kwa kuondoka kabisa hapo kwake na kashafanya maandalizi
Licha ya kuonywa na wife wangu kua nisije nikamwambia rafiki yangu kuhusu habari hiyo mimi nikaona bora nimtonye mwanaume mwenzangu achukue hatua za kujirekebisha fasta ili mambo yasiharibike. Nikamweleza kila kitu, akanishukuru sana na aka ahidi kufanyia kazi kimya kimya na kujirudi
Ilikua siku ya Jumamosi jioni siku kama nne baada ya kumueleza ile issue Big, akanipigia simu kunialika tukapate Ice cream pale Snow Cream na atakua na mama P kama sitojali niende na wife, wazo ambalo tulilikubali maramoja na baada ya kujiandaa kidogo tukaelekea hapo kujiunga na marafiki zetu
Ice cream zilikua tamu sana maana jamaa wa Snow Cream wanajua hasa kuzitengeneza. Katikati ya utamu wa Banana Boat Ice Cream, na mazungumzo na utani wa hapa na pale, Big akanigeukia na kuniambia, "Sesten hebu sema sasa yale maneno uliyoniambia juzi"
Kwanza sikumuelewa ila aliposisitiza na kunikumbusha nikaanza kumsihi kwa kumwambia "George hebu kausha bana. Acha mambo ya kitoto" Lakini jamaa akashikilia niongee na alipoona nimekataa akaimwaga ile stori yoote niliyomwambia ambayo mimi pia niliambiwa na wife kwa sharti la kutomwambia rafiki yangu
Ilikua ni kipindi kigumu sana sana kwangu na nilijisikia vibaya mno. Mke wangu alikua kimya muda wote huku akionekana mwenye kufadhaishwa na hali ile. Mama P alikua kakunja mikono kifuani nae anaangalia tu hali ilivokua
Mwishoe wife wangu akasema anamajukumu mengine anataka kuondoka na mimi nikaunga mkono hoja na licha ya Big kuendelea kusisitiza lazima nielezee yale niliyomwambia tuliondoka eneo lile na njia nzima hatukusemeshana
Usiku ule tayari uliharibiwa na jitihada zangu zoote za kuomba "chakula cha usiku" hazikufanikiwa maana wife alikua anang'ang'ania hajisikii vizuri nimuache. Asubuhi kulipokucha ikabidi nitumie mbinu za hali ya juu kama vile namtongoza upya ndipo nikafanikiwa kupata 'Amka na BBC'
Baada ya pale wife ndio akafunguka kuanza kunisema kwa kitendo changu cha kumweleza rafiki yangu Big mambo tuliyokubaliana tukae kimya. Nilifurahi jambo moja na ndio maana nikataka kwanza nipate haki yangu ya ndoa ili nimlainishe. Wife wangu alikua akikasirika hasemi kitu ananuna tu. Akiaanza kukueleza kosa lako ujue hapo hasira zinapungua, mtafikia muafaka na ndivyo ilivyokua
Baada ya miezi mitano tangia siku nilivyo aibishwa mbele ya wife, mwanamke wa George alikua anavalishwa pete na mwanaume mwingine. Na habari yoote hiyo nilikua naijua hata kabda haijawa critical. Nilikuja kumueleza Big baadae kua nilikua najua kila kitu kupitia wife wangu ila nisengethubutu kufungua mdomo kukwambia, akawa anantumbulia mimacho yake mikubwa tu
Kwa ufupi yule mchepuko wake kumbe ulikua mchumba wa mtu na keshaolewa. Aliyekua wife wake (walikua wanaishi pamoja tu hawakua wamefunga ndoa) keshaolewa na mwanaume mwingine na yeye alikuja kuoa kibinti flani kidogo sana kwake kikawa kinampeleka speed hasa maana kila wakati yupo na company ya vivulana
Big hakua mtu wa totoz au hakua macho juu kiviile, na pale alipojaribu kuchepuka kwa ku date na dada mmoja mfanyakazi mwenzie akajikuta kabobea na kazama kichwa na miguu! Mkewe(walikua wanaishi pamoja tu walikua hawajaona) akimjua huyo dada kua ni workmate wa mumewe na mwanzoni hakua na wasiwasi nae hata chembe
Mimi alikuja kuniambia wife wangu kua mama P(mke wa Big tulimuita kwa jina la mtoto wa dada yake yeye hakua na mtoto) amegundua kua Big ana cheat na huyo mfanyakazi mwenzie. Ameambiwa na watu (maana alikua na connection na wafanyakazi wengine wa ofisi ya kina George) na kwamba ameshafanya uchunguzi wa kutosha na sasa na yeye ana lipa kisasi kwa kuondoka kabisa hapo kwake na kashafanya maandalizi
Licha ya kuonywa na wife wangu kua nisije nikamwambia rafiki yangu kuhusu habari hiyo mimi nikaona bora nimtonye mwanaume mwenzangu achukue hatua za kujirekebisha fasta ili mambo yasiharibike. Nikamweleza kila kitu, akanishukuru sana na aka ahidi kufanyia kazi kimya kimya na kujirudi
Ilikua siku ya Jumamosi jioni siku kama nne baada ya kumueleza ile issue Big, akanipigia simu kunialika tukapate Ice cream pale Snow Cream na atakua na mama P kama sitojali niende na wife, wazo ambalo tulilikubali maramoja na baada ya kujiandaa kidogo tukaelekea hapo kujiunga na marafiki zetu
Ice cream zilikua tamu sana maana jamaa wa Snow Cream wanajua hasa kuzitengeneza. Katikati ya utamu wa Banana Boat Ice Cream, na mazungumzo na utani wa hapa na pale, Big akanigeukia na kuniambia, "Sesten hebu sema sasa yale maneno uliyoniambia juzi"
Kwanza sikumuelewa ila aliposisitiza na kunikumbusha nikaanza kumsihi kwa kumwambia "George hebu kausha bana. Acha mambo ya kitoto" Lakini jamaa akashikilia niongee na alipoona nimekataa akaimwaga ile stori yoote niliyomwambia ambayo mimi pia niliambiwa na wife kwa sharti la kutomwambia rafiki yangu
Ilikua ni kipindi kigumu sana sana kwangu na nilijisikia vibaya mno. Mke wangu alikua kimya muda wote huku akionekana mwenye kufadhaishwa na hali ile. Mama P alikua kakunja mikono kifuani nae anaangalia tu hali ilivokua
Mwishoe wife wangu akasema anamajukumu mengine anataka kuondoka na mimi nikaunga mkono hoja na licha ya Big kuendelea kusisitiza lazima nielezee yale niliyomwambia tuliondoka eneo lile na njia nzima hatukusemeshana
Usiku ule tayari uliharibiwa na jitihada zangu zoote za kuomba "chakula cha usiku" hazikufanikiwa maana wife alikua anang'ang'ania hajisikii vizuri nimuache. Asubuhi kulipokucha ikabidi nitumie mbinu za hali ya juu kama vile namtongoza upya ndipo nikafanikiwa kupata 'Amka na BBC'
Baada ya pale wife ndio akafunguka kuanza kunisema kwa kitendo changu cha kumweleza rafiki yangu Big mambo tuliyokubaliana tukae kimya. Nilifurahi jambo moja na ndio maana nikataka kwanza nipate haki yangu ya ndoa ili nimlainishe. Wife wangu alikua akikasirika hasemi kitu ananuna tu. Akiaanza kukueleza kosa lako ujue hapo hasira zinapungua, mtafikia muafaka na ndivyo ilivyokua
Baada ya miezi mitano tangia siku nilivyo aibishwa mbele ya wife, mwanamke wa George alikua anavalishwa pete na mwanaume mwingine. Na habari yoote hiyo nilikua naijua hata kabda haijawa critical. Nilikuja kumueleza Big baadae kua nilikua najua kila kitu kupitia wife wangu ila nisengethubutu kufungua mdomo kukwambia, akawa anantumbulia mimacho yake mikubwa tu
Kwa ufupi yule mchepuko wake kumbe ulikua mchumba wa mtu na keshaolewa. Aliyekua wife wake (walikua wanaishi pamoja tu hawakua wamefunga ndoa) keshaolewa na mwanaume mwingine na yeye alikuja kuoa kibinti flani kidogo sana kwake kikawa kinampeleka speed hasa maana kila wakati yupo na company ya vivulana