Rafiki yangu kampenda dada mwenye Sickle Cell

Oook!
Ukipima genotype kuna za aina tatu.
AA, AS au SS
AA- huyu hana kabisa ata chembechembe za sickle cell
AS - huyu haugui sickle cell anaemia ila amebeba chembechembe za sickle cell
SS - huyu ndo anaumwa sickle cell Anaemia.

Sasa
1. AA + AA = AA (watapata watoto wazima wote)
2. AA + AS = AA, AS (Wana chance ya kupata watoto wazima na waliobeba chembechembe za huo ugonjwa)
3. AA+ SS = AS ( Watapata watoto wote waliobeba chembechembe za huo ugonjwa)
4. AS + AS = AA, AS, SS (watapata watoto wazima, waliobeba chembechembe za huo ugonjwa na mgonjwa)
5. AS + SS = AS, SS (Watapata mtoto aliebeba chembechembe za ugonjwa na mtoto mwenye huo ugonjwa)
6. SS + SS = SS (Yaani hawa kila mtoto watakaepata atakua na huu ugonjwa)

(Nimeelezea kwa nilivyofundishwa, sina background ya udaktari... Madaktari wataweza elezea vizuri zaidi)
Sikujua ilo Dada imekaa pouw
 
Ni probability wanaweza kuza watoto wasio na huo ugonjwa ila lazima kizazi cha hao watoto wao wanaweza pata,ila kuna mtu yuko ivyo na watoto wake hawana ila wajukuu zake ndio wanao
Watoto wake waliubeba ugonjwa... Sasa inaelekea wakazaa na wengine walioubeba ugonjwa ndo maana wajukuu kuna ambao wana huo ugonjwa
 
Napenda wataalamu na watu wenye uzoefu mniambie ni vipi mtu anaweza kumhandle mtu mwenye sickle cell. Huyu rafiki yangu ameambiwa baada ya kuwa tayari kazama kwenye bwawa la mahaba anampenda sana msichana, isitoshe ni kitu matata kichwani, umbo, upole kiufupi wife materials shida hiyo sasa sicklecell, nasikia kuishi kwao siyo garantee jamaa anamwogopa tangu aambiwe hilo tatizo, mtujuze life span yao pia.

Nitanguliza shukrani.
Mwambie rafiki yako mimi nina uwezo wa kutibu hayo Maradhi ya Sicklecell anitafute kwa wakati wake nipate kumtibia mchumba wake rafiki yako.
Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu.
 
huu ugonjwa huwa siuelewi, kuna mdada aliambiwa asibebe mimba wala kuzaa chini ya 20yrs akakaidi

alijifungua salama,ila mpaka sasa ni mlemavu (miguu haina nguvu)
 
Oook!
Ukipima genotype kuna za aina tatu.
AA, AS au SS
AA- huyu hana kabisa ata chembechembe za sickle cell
AS - huyu haugui sickle cell anaemia ila amebeba chembechembe za sickle cell
SS - huyu ndo anaumwa sickle cell Anaemia.

Sasa
1. AA + AA = AA (watapata watoto wazima wote)
2. AA + AS = AA, AS (Wana chance ya kupata watoto wazima na waliobeba chembechembe za huo ugonjwa)
3. AA+ SS = AS ( Watapata watoto wote waliobeba chembechembe za huo ugonjwa)
4. AS + AS = AA, AS, SS (watapata watoto wazima, waliobeba chembechembe za huo ugonjwa na mgonjwa)
5. AS + SS = AS, SS (Watapata mtoto aliebeba chembechembe za ugonjwa na mtoto mwenye huo ugonjwa)
6. SS + SS = SS (Yaani hawa kila mtoto watakaepata atakua na huu ugonjwa)

(Nimeelezea kwa nilivyofundishwa, sina background ya udaktari... Madaktari wataweza elezea vizuri zaidi)

Umeeleza vizuri sana, na hayo ndiyo Dr atakueleza pindi ukitaka kupata elimu juu ya huu ugonjwa.
Jamii bado inahitaji sana kuelemishwa kuhusu huu ugonjwa.
 
Mm ningempenda sana. Nilikua kuwa na mahusiano na binti mwenye hiv. Alininyima penz mpaka nikajilaumu, akaja kuniambia ukwel, nilimpenda sana mpka mwenyewe akaniacha.
 
Kwa wale ambao bado hamzaa Ila mna mahusiano yoyote Yale iwe uchumba au ndoa, nendeni hospital mkapime mapema ili kama mna vimelea vya huo ugonjwa mjue namna ya kuishi pindi mtapoanza familia.
Na isiwe kwa ugonjwa huu Bali ikiwezekana mpime mapema magonjwa yoyote Yale ya kurithi ama kuambukiza.
Kuogopa tu bila kupima haisaidii, chukua hatua nenda hospital.
Halafu jamani, Wagonjwa Wa sickle cell msitutenge ksb ya ugonjwa wetu, sisi ni binadamu kama nyie tunahitaji kupendwa kama wewe upendavyo kupendwa......
 
Tu
Uzuri wake hawaugui Malaria

Tunaugua malaria, tena sisi tukiugua tunaumwa kweli kweli na kibaya zaidi hata damu inapungua.
Tunashauriwa sana tujilinde kila tuwezavyo tusiumwe malaria.
Sickle cell ukifuata masharti yake wala haisumbui sana, utajikuta unaishi kama waishivyo wengine.

Hivyo ukiniona Mimi naangalia TV, au najisomea nikiwa ndani ya neti usinishangae...natania tu ha ha ha ha
 
Hili jambo ni zito sana mkuu ni afadhali uwe H.i.v + kuliko kuishi kwa kufahamu kuwa hautafikisha miaka kadhaa.
VERY SAD !

Ukumbuke ugonjwa huu mtu anazaliwa nao ila HIV mtu anaupata duniani...
Unaweza kufuru ukamkwepa mtu huyu ila wewe ukaja ukazaa mtoto mwenye nao...

UGONJWA WA SELI MUNDU
(SICKLE CELL)


Wapendwa wasomaji katika mada ya leo na kwa faida ya wasomaji wengine nitapenda kujibu baadhi ya maswali mbalimbali kutoka kwa wasomaji wa makala hii ya Daktari kwa kuuelezea ugonjwa wa Seli Mundu ambao ni ugonjwa wa kawaida katika jamii yetu ambayo imekuwa na dhana tofauti kuhusu ugonjwa huu.

Kabla ya kuanza kuuelezea ugonjwa wenyewe ni vyema basi mpendwa msomaji ukafahamu jinsi gani damu husafirishwa katika mwili wa damu.

Himoglobini (haemoglobin) ni molekyuli ambayo ni sehemu ya chembe hai nyekundu zilizoko mwilini.Himoglobini hufanya kazi ya kuzisaidia chembe hai nyekundu kubeba hewa ya oksijenu kutoka kwenye mapafu kwenda sehemu nyingine za mwili.

Kwa kawaida binadamu anapozaliwa huwa na himoglobini ya kawaida ambayo huitwa himoglobini A (Haemoglobin A) au kwa kifupi HbA na Himoglobini ya kichanga ambayo huitwa Himoglobini F (HbF).Himoglobini A ambayo hutengeneza takriban asilimia tisini na saba ya Himoglobini za mtu mzima imeundwa na jozi mbili za minyororo (chains) za alfa (alpha) na beta (beta).

Chembe hai nyekundu za damu za kawaida huwa laini,za duara na huweza kujipenyeza katika mishipa ya damu kirahisi.Pia huweza kuishi kwa takriban siku mia moja na ishirini (120) kabla chembe hai nyekendu za damu mpya hazijatengenezwa.

Watu wenye ugonjwa wa sickle cell wao huwa na chembe hai nyekundu ngumu, zenye umbo la mundu au mwezi mchanga ambazo hupita kwa shida kwenye mishipa ya damu haswa ile midogo.Aina hii ya himoglobini huitwa Himoglobini S (HbS).Tofauti na chembe hai nyekundu za damu za kawaida,zenyewe huishi kwa siku chache zaidi, kwa kawaida takribani siku kumi na sita (16) tu.

Kwa hiyo ugonjwa wa sickle cell ni ugonjwa wa kurithi ambapo mwathirika huwa na himoglobini S ambayo hupelekea chembe hai nyekundu za damu zisizo za kawaida kushindwa kupita kwenye mishipa ya damu kirahisi.Hali hii hupelekea kuwa na upungufu wa damu kwenye baadhi ya sehemu mwilini.

Hata hivyo iwapo chembe hai nyekundu za damu HbA ni zaidi ya HbS huweza kutengeneza HbAS.Hali hii hujulikana kitaalamu kama Sickle cell isiyo na dalili (Sickle Cell Trait).Watu wenye aina hii ya sickle cell huwa na afya nzuri ya kawaida.

Ugonjwa wa sickle cell ni ugonjwa sugu na wa kudumu.Waathirika waweza kuwa wenye afya njema lakini maisha yao huandamwa na vipindi vya mashambulizi ya maumivu.Umri wa kuishi hupungua na baadhi ya tafiti za nyuma zinaonyesha kwamba waweza kuishi kwa wastani wa miaka arobaini (40) mpaka hamsini (50).Ugonjwa huu ni wa kawaida kwa watu wenye asili ya kiafrika haswa walioko chini ya Jangwa la Sahara lakini waweza athiri watu wa mataifa mengine pia.

Jinsi ugonjwa unavyorithiwa

Ugonjwa wa sickle cell waweza kurithiwa kama ilivyo kwa makundi ya damu, rangi ya ngozi, rangi ya macho na tabia ua vitu vingione vinavyoweza kurithiwa.

Kwa mfano kama mzazi mmoja ana himoglobini AS,amabyo huashiria kuwepo kwa sickle cell bila kuonyesha dalili na mzazi akiwa mzima, basi wana uwezekano wa kupata watoto wenye sickle cell ambao hawataonyesha dalili.

Pia kama mzazi mmoja ana sickle cell na mwingine ana sickle cell bila dalili, kuna uwezekano wa asilimia hamsini ya kupata mtoto mwenye sickle cell au sickle cell bila dalili katika kila mimba itakayotungwa.

Na kuna takriban asilimia ishirini na tano ya kupata sickle cell yenye dalili katika kila mimba.

Jinsi Sickle Cell inavyotokea
Ugonjwa wa sickle cell hutokea kutokana na mabadiliko (mutations) katika mnyororo wa beta (beta chain) ambapo amaino asidi (amino acid) aina ya glutameti (glutamate) huitoa amaino asidi ya Valini (Valine) kutoka kwenye nafasi ya sita ya mnyororo wa beta.

Katika mazingira yenye kiwango kidogo cha oksijeni, chembe hai nyekundu za damu zenye umbo la kawaida (mviringo) huharibiwa na kupoteza uwezo wa kutanuka na kusinyaa (elasticity) zipitapo kwenye mishipa ya damu.Hali hii hupelekea chembe hai hizo nyekundu za damu kuharibiwa na mfumo wa damu kwenye bandama (spleen) uitwao kwa kitaalamu reticuloendothelial system.

Pia hupelekea kuziba kwa mishipa midogo ya damu (infarction) kutokana na chembe hai nyekundu za damu zenye umbo la mundu.Hali hii yaweza kupelekea kukosekana kwa damu na oksijeni ya kutosha katika baadhi ya viungo.

Dalili za sickle cell

Ni mara chache kwa dallili za sickle cell kuonekana katika miezi sita ya mwanzo baada ya kuzaliwa.Hii inatokana na kuwepo kwa wingi kwa himoglobini ya kichanga, himoglobini F, ambayo huzilinda chembe hai nyekundu za damu zisibadilike umbo.
Ikumbukwe kwambamabadiliko ya kiumbo ya chembe hai nyekundu za damu ndiyo chanzo cha dalili tutakazoziona hivi punde.

Dalili utotoni
-Maumivu ya pingili (dactylitis) za mikono na miguu
-Kushambuliwa na maradhi kama uti wa mgongo,
nimonia,mafua,kikohozi n.k
-Kuvimba kwa bandam (splenomegally) kutokana na kujaa ghafla
kwa damukwenye bandama
-Kusinyaa kwa bandama(autosplenectomy)

Dalili ukubwani

-Upungufu wa damu
-Maumivu ya tumbo
-Maumivu ya mifupa (viungo)
-Kupooza
-Maumivu ya kifua yafananayo na nimonia (acute chest syndrome)
-Kubana kwa kifua
-Kukojoa damu
-Vidonda sugu miguuni
-Kusimaama kwa uume kuambatanako na maumivu makali (priapism)
-Kuvimba kwa paji la uso au fuvu

Vipimo na Uchunguzi

Vipimo vifuatavyo ni muhimu katika kugundua sickle cell na magonjwa yaambatanayo na sickle cell
-Kipimo cha Sickling (Sickling Test)
-Kipimo cha damu kama kuna Malaria
-Kipimo cha mkojo kuchunguza uwepo wa chembe hai nyekendu za damu katika mkojo
-Picha ya kifua (x-ray) kuangalia iwapo kuna athari katika kifua
-Kipimo cha wingi wa damu (Hb level)
-Kipimo cha kundi la damu (Blood grouping and cross matching)

Matibabu

Aina ya matibabu anayohitaji mgonjwa hutegemeana na aina ya mgonjwa na tatizo linalomsumbua kwa wakati huo. Ni vyema kuchukua hatua mapema iwapo una mtoto mwenye dalili zilizotajwa hapo juu.

Ushauri

Ugonjwa wa Sickle cell ni ugonjwa sugu na wa kudumu.Watu wenye ugonjwa huu huambukizwa kirahisi magonjwa mengine kama vile nimonia, malaria n.k

Wagonjwa wenyewe wanatakiwa kujilinda dhidi ya baridi, magonjwa ya kuambukiza kama nimonia, malaria, magonjwa ya mifupa n.k

Pia ni vizuri kwa mgonjwa wa nimonia kuoa au kuolewa na mwenza ambaye hana sickle cell ili kupunguza uwezekano wa kupata mtoto mwenye sickle cell.

Kwa wakina mama wenye sickle cell na wenye mpango wa kubeba ujauzito ni vema wakafahamu kwamba upo uwezekano wa mtoto kudumaa kiakili akiwa tumboni, kutoka ghafla kwa mimba na kupata kifafa cha mimba. Pia ni vizuri kwa wagonjwa wa aina hii kutiwa moyo.
 
Atapata watoto carrier...ni mhm sana kupanga hilo vinginevyo mtaleta kiumbe duniani ambcho kitapata mateso ambyo si haki ya tena makusudically kuhusu mapenzi...its oky as long as ni mwanamke anayejielewa mpende tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom