Saturday, 26 March 2011 09:56
Exuper Kachenje
KATIKA kinachoonekana serikali inachangia kuzorota kwa mifuko ya hifadhi ya jamii, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imelezwa kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Mashirika ya Umma (PSPF), unaidai serikali Sh3.1 trilioni.
Maofisa wa PSPF walifika mbele ya kamati hiyo jana, walieleza kuwa taarifa zake za ukaguzi wa hesabu zinaonyesha mfuko huo upo hatarini kufa.Habari kutoka ndani ya mkutano huo, zinadai PSPF ililalamika kuwa deni hilo limechukua muda mrefu na kwamba, Serikali haikuwa imeonyesha juhudi zozote za kulipa.
Hata hivyo, akitoa muhtasari wa kikao kati yake na PSPF, Mwenyekiti wa Kamati ya POAC, Zitto Kabwe, alisema uwapo wa mfuko huo unahatarishwa na deni lake kwa serikali.
"Asubuhi tulikuwa na mkutano na PSPF na tulimwita pia Katibu Mkuu Wizara ya Fedha. Niseme, PSPF uwapo wake unahatarishwa na deni lake kwa Serikali," alisema Zitto na kuongeza:
"Auditor (Mkaguzi wa hesabu) aliyekagua hesabu za PSPF anasema mfuo huo utakufa."
Alithibitisha kuwa serikali inadaiwa fedha hizo na PSPF, lakini akasema kwamba kamati yake imechukua hatua kadhaa kurekebisha hali hiyo ili kuuokoa.
"Serikali inadaiwa Sh3.1 trilioni, lakini Kaimu Katibu Mkuu Hazina alikuwapo naye akaeleza yake, sisi tukatoa maagizo yetu kama kamati," alisema Zitto.
Alisema baada ya taarifa ya mfuko huo kwa kamati yake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dk Servacius Likwelike, aliyekuwapo katika mkutano huo alieleza kuwa, jana serikali imeanza kulipa deni hilo.
Kwa mujibu wa Zitto, Dk Likwelile aliiambia kamati yake kuwa, serikali imeandika hundi ya Sh5.9 bilioni kwa mfuko huo kama malipo ya awali.
Kutokana na hali hiyo, Zitto alisema kamati yake imewaagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kuchunguza ili kujua kama kweli fedha inayodaiwa serikali hiyo au zaidi.
Katika hatua nyingine, kamati hiyo imetoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia Wizara ya Fedha, kufanya tathmini ya mchakato wa uuzaji Kampuni ya Zain kwa wamiliki wake wa sasa Airtel ya India ili kufahamu upungufu wa kisheria uliokosesha serikali fedha.
Pia, kamati hiyo imetaka TRA kutuma timu ya wataalam nchini Nigeria, kujifunza ilivyofaidika na uuzaji wa Kampuni ya Zain wakati Tanzania ingeweza kunufaika na zaidi ya Sh308
SOURCE MWANANCHI
Exuper Kachenje
KATIKA kinachoonekana serikali inachangia kuzorota kwa mifuko ya hifadhi ya jamii, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imelezwa kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Mashirika ya Umma (PSPF), unaidai serikali Sh3.1 trilioni.
Maofisa wa PSPF walifika mbele ya kamati hiyo jana, walieleza kuwa taarifa zake za ukaguzi wa hesabu zinaonyesha mfuko huo upo hatarini kufa.Habari kutoka ndani ya mkutano huo, zinadai PSPF ililalamika kuwa deni hilo limechukua muda mrefu na kwamba, Serikali haikuwa imeonyesha juhudi zozote za kulipa.
Hata hivyo, akitoa muhtasari wa kikao kati yake na PSPF, Mwenyekiti wa Kamati ya POAC, Zitto Kabwe, alisema uwapo wa mfuko huo unahatarishwa na deni lake kwa serikali.
"Asubuhi tulikuwa na mkutano na PSPF na tulimwita pia Katibu Mkuu Wizara ya Fedha. Niseme, PSPF uwapo wake unahatarishwa na deni lake kwa Serikali," alisema Zitto na kuongeza:
"Auditor (Mkaguzi wa hesabu) aliyekagua hesabu za PSPF anasema mfuo huo utakufa."
Alithibitisha kuwa serikali inadaiwa fedha hizo na PSPF, lakini akasema kwamba kamati yake imechukua hatua kadhaa kurekebisha hali hiyo ili kuuokoa.
"Serikali inadaiwa Sh3.1 trilioni, lakini Kaimu Katibu Mkuu Hazina alikuwapo naye akaeleza yake, sisi tukatoa maagizo yetu kama kamati," alisema Zitto.
Alisema baada ya taarifa ya mfuko huo kwa kamati yake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dk Servacius Likwelike, aliyekuwapo katika mkutano huo alieleza kuwa, jana serikali imeanza kulipa deni hilo.
Kwa mujibu wa Zitto, Dk Likwelile aliiambia kamati yake kuwa, serikali imeandika hundi ya Sh5.9 bilioni kwa mfuko huo kama malipo ya awali.
Kutokana na hali hiyo, Zitto alisema kamati yake imewaagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kuchunguza ili kujua kama kweli fedha inayodaiwa serikali hiyo au zaidi.
Katika hatua nyingine, kamati hiyo imetoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia Wizara ya Fedha, kufanya tathmini ya mchakato wa uuzaji Kampuni ya Zain kwa wamiliki wake wa sasa Airtel ya India ili kufahamu upungufu wa kisheria uliokosesha serikali fedha.
Pia, kamati hiyo imetaka TRA kutuma timu ya wataalam nchini Nigeria, kujifunza ilivyofaidika na uuzaji wa Kampuni ya Zain wakati Tanzania ingeweza kunufaika na zaidi ya Sh308
SOURCE MWANANCHI