PSPF hatarini kufa

shadhuly

Senior Member
Jan 8, 2011
145
35
Saturday, 26 March 2011 09:56

Exuper Kachenje

KATIKA kinachoonekana serikali inachangia kuzorota kwa mifuko ya hifadhi ya jamii, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imelezwa kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Mashirika ya Umma (PSPF), unaidai serikali Sh3.1 trilioni.

Maofisa wa PSPF walifika mbele ya kamati hiyo jana, walieleza kuwa taarifa zake za ukaguzi wa hesabu zinaonyesha mfuko huo upo hatarini kufa.Habari kutoka ndani ya mkutano huo, zinadai PSPF ililalamika kuwa deni hilo limechukua muda mrefu na kwamba, Serikali haikuwa imeonyesha juhudi zozote za kulipa.

Hata hivyo, akitoa muhtasari wa kikao kati yake na PSPF, Mwenyekiti wa Kamati ya POAC, Zitto Kabwe, alisema uwapo wa mfuko huo unahatarishwa na deni lake kwa serikali.

"Asubuhi tulikuwa na mkutano na PSPF na tulimwita pia Katibu Mkuu Wizara ya Fedha. Niseme, PSPF uwapo wake unahatarishwa na deni lake kwa Serikali," alisema Zitto na kuongeza:
"Auditor (Mkaguzi wa hesabu) aliyekagua hesabu za PSPF anasema mfuo huo utakufa."
Alithibitisha kuwa serikali inadaiwa fedha hizo na PSPF, lakini akasema kwamba kamati yake imechukua hatua kadhaa kurekebisha hali hiyo ili kuuokoa.

"Serikali inadaiwa Sh3.1 trilioni, lakini Kaimu Katibu Mkuu Hazina alikuwapo naye akaeleza yake, sisi tukatoa maagizo yetu kama kamati," alisema Zitto.

Alisema baada ya taarifa ya mfuko huo kwa kamati yake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dk Servacius Likwelike, aliyekuwapo katika mkutano huo alieleza kuwa, jana serikali imeanza kulipa deni hilo.
Kwa mujibu wa Zitto, Dk Likwelile aliiambia kamati yake kuwa, serikali imeandika hundi ya Sh5.9 bilioni kwa mfuko huo kama malipo ya awali.

Kutokana na hali hiyo, Zitto alisema kamati yake imewaagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kuchunguza ili kujua kama kweli fedha inayodaiwa serikali hiyo au zaidi.

Katika hatua nyingine, kamati hiyo imetoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia Wizara ya Fedha, kufanya tathmini ya mchakato wa uuzaji Kampuni ya Zain kwa wamiliki wake wa sasa Airtel ya India ili kufahamu upungufu wa kisheria uliokosesha serikali fedha.

Pia, kamati hiyo imetaka TRA kutuma timu ya wataalam nchini Nigeria, kujifunza ilivyofaidika na uuzaji wa Kampuni ya Zain wakati Tanzania ingeweza kunufaika na zaidi ya Sh308

SOURCE MWANANCHI
 
Sasa naanza kupata mwanga kwa nini nasumbuliwa na mafao yangu. Tangu mwezi june 2010 nimekuwa nikifuatilia mafao yangu mpaka niandikapo ni njoo kesho jaribu baada ya week 2 na hivi navile. Mara faili lako limekwama mahali fulani na huyo mhusika yuko safari mpaka arudi. Kumbe serikali imejichotea jasho letu na kutumia kwa manufaa yao.
Serikali itaendelea kutesa wananchi wake hadi lini?
 
Hii mifuko ya hifadhi ya jamii ilishashauriwa kufanya kitu inaitwa acturial ili kujua uhai wake ukoje na wengi walipuuzia na matokeo yake ndio haya. wakati mwingine waendeshaji wa mifuko hii nao wanaingiza sana siasa. sasa inakuwa mpaka deni linafikia trilioni zote hizo na wao wapo tu wanaangalia? Kulalamika kwenye kamati ya bunge haliwezi kuwa suluhisho la mattaizo yao na hili wanalo. sasa wajiandae kukabiliana na hasira za wanachama wao
 
Kwanza hii mifuko imekuwa mingi sana,sioni mantiki yakuwa na mifuko mingi hivyo,kwa mfano kwasasa hakuna tofauti kati ya PPF na NSSF wote wanagombea wateja hao hao........mimi nafikiri lingebaki fuko moja tu tena NSSF,ambayo linaonekana liko strong.
 
Asante sana Shadhuly This is my point mifuko yetu ya pension iko katika hali mbaya sana. Wanasiasa wanaiendesha, wakurugenzi wengine wanaifisadi, na kuwekeza kwa ajili ya serikali kutaua mifuko ya pension ya Tanzania. Ikifa mifuko hii uchumi wa Tanzania uko mbioni kuanguka kama sio kuteketea kabisa kwa kukosa pesa ya kujiendesha.
 
Inasikitisha sana.
Nimechangia toka mwaka 2003, na hadi wa leo sijapewa namba yangu ya uanachama, na kwa masikitiko makubwa juzi nimeletewa fomu nyingine nijaze details zangu upya, wakati nilishajaza nikianza kazi mwaka 2003!...sijui ndo nitaanza kuwekewa akiba mwaka huu!??
Kwa kweli, kama serikali imeamua hadi kuchukua hela za raia, yaani za mtu mmojammoja na kuzitumia kwa mambo ya chama hii inatisha!
 
Inasikitisha sana.
Nimechangia toka mwaka 2003, na hadi wa leo sijapewa namba yangu ya uanachama, na kwa masikitiko makubwa juzi nimeletewa fomu nyingine nijaze details zangu upya, wakati nilishajaza nikianza kazi mwaka 2003!...sijui ndo nitaanza kuwekewa akiba mwaka huu!??
Kwa kweli, kama serikali imeamua hadi kuchukua hela za raia, yaani za mtu mmojammoja na kuzitumia kwa mambo ya chama hii inatisha!
Pole mkuu,

Ndio Tanzania yetu hiyo ukija kuidai hela yako usisashangae sintofahamu nyingi!!!!
 
Serikali inadai 3.1trillion. Je ni deni la pesa ambazo serikali imechukua au ni michango ya civil servants ambazo serikali haikupeleka. Ufafanuzi tafadhali
 
Serikali inadai 3.1trillion. Je ni deni la pesa ambazo serikali imechukua au ni michango ya civil servants ambazo serikali haikupeleka. Ufafanuzi tafadhali
Michango mkuu ya watumishi wa serikali ndiyo hiyo inatumika kifisadi namna hiyo. Wawabane basi wawekezaji hawataki kazi kucheka na kima tu matokeo yake ndiyo hayo.
 
Serikali inadai 3.1trillion. Je ni deni la pesa ambazo serikali imechukua au ni michango ya civil servants ambazo serikali haikupeleka. Ufafanuzi tafadhali


Duhhhhhhh!!!!!
sasa deni jumla la serekali ni shilingi ngapi?
maana hiyo peke yake ni zaidi ya ROBO ya bajeti ya nchi hii!
 
Mashirika mengine ya hifadhi ya jamii yanaidai serikali kiasi chochote? Na ni kiasi gani kwa kila shirika?
 
Kwanza hii mifuko imekuwa mingi sana,sioni mantiki yakuwa na mifuko mingi hivyo,kwa mfano kwasasa hakuna tofauti kati ya PPF na NSSF wote wanagombea wateja hao hao........mimi nafikiri lingebaki fuko moja tu tena NSSF,ambayo linaonekana liko strong.

mafuko kweli yamezidi.
Lingebaki moja hata gharama za uendeshaji zingepungua kiasi.
 
Inasikitisha sana.
Nimechangia toka mwaka 2003, na hadi wa leo sijapewa namba yangu ya uanachama, na kwa masikitiko makubwa juzi nimeletewa fomu nyingine nijaze details zangu upya, wakati nilishajaza nikianza kazi mwaka 2003!...sijui ndo nitaanza kuwekewa akiba mwaka huu!??
Kwa kweli, kama serikali imeamua hadi kuchukua hela za raia, yaani za mtu mmojammoja na kuzitumia kwa mambo ya chama hii inatisha!

khaaaa! Pole sana ila inawezekana wamemisplace details zako kwahiyo wanazihitaji tena.
Anza mchakato wa kufatilia mapema.
 
It is very sad news ...... if political interferences continues as it is now the financial sustainability of public pension funds will be questionable with no future.

Director Generals of these funds do not observe single borrower limits and risk concentration principles. Public pension funds' portfolios are not well diversified with too much government involvements. Of course, they always argue that doing business with government is safer because it is the guarantor but too much dependence on one customer does raise a question on their ability to survive shall this customer starts to dishonor s/he obligations timely. The obvious risk is the liquidity risk which may in further trigger other financial problems.

It is time to play safe as any collapse of the fund in this sector has enormous impact in the financial system of the country.

A caution:

Government and political interferences will worsen financial sustainability of the PPFs which will, in turn, create necessary conditions for private pensions to come as an exit door and government's excuse.

SSRA should take a bitter pills asap to arrest poor governance practices in this sector. Measures may include

  • harmonization of the pension formulas,
  • clear definition of what is a government to assist single borrower limit is observed once introduced
  • advise government to reduce unnecessary competition from public pension funds and allow private pension funds to come while these public pension funds are in sound financial situations.
  • etc as they see fit.....
 
PPF ndiyo Parastatal Pension Fund na PSPF Public Servants Pension Fund naomba ufafanuzi kuwa hizo trilion ni za PPF au PSPF? Lakini pia kamati ya zitto inashughulikia mashirika ya umma, tafadhali fafanua.
 
Saturday, 26 March 2011 09:56

Exuper Kachenje

KATIKA kinachoonekana serikali inachangia kuzorota kwa mifuko ya hifadhi ya jamii, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imelezwa kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Mashirika ya Umma (PSPF), unaidai serikali Sh3.1 trilioni.

Maofisa wa PSPF walifika mbele ya kamati hiyo jana, walieleza kuwa taarifa zake za ukaguzi wa hesabu zinaonyesha mfuko huo upo hatarini kufa.Habari kutoka ndani ya mkutano huo, zinadai PSPF ililalamika kuwa deni hilo limechukua muda mrefu na kwamba, Serikali haikuwa imeonyesha juhudi zozote za kulipa.

Hata hivyo, akitoa muhtasari wa kikao kati yake na PSPF, Mwenyekiti wa Kamati ya POAC, Zitto Kabwe, alisema uwapo wa mfuko huo unahatarishwa na deni lake kwa serikali.

"Asubuhi tulikuwa na mkutano na PSPF na tulimwita pia Katibu Mkuu Wizara ya Fedha. Niseme, PSPF uwapo wake unahatarishwa na deni lake kwa Serikali," alisema Zitto na kuongeza:
"Auditor (Mkaguzi wa hesabu) aliyekagua hesabu za PSPF anasema mfuo huo utakufa."
Alithibitisha kuwa serikali inadaiwa fedha hizo na PSPF, lakini akasema kwamba kamati yake imechukua hatua kadhaa kurekebisha hali hiyo ili kuuokoa.

"Serikali inadaiwa Sh3.1 trilioni, lakini Kaimu Katibu Mkuu Hazina alikuwapo naye akaeleza yake, sisi tukatoa maagizo yetu kama kamati," alisema Zitto.

Alisema baada ya taarifa ya mfuko huo kwa kamati yake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dk Servacius Likwelike, aliyekuwapo katika mkutano huo alieleza kuwa, jana serikali imeanza kulipa deni hilo.
Kwa mujibu wa Zitto, Dk Likwelile aliiambia kamati yake kuwa, serikali imeandika hundi ya Sh5.9 bilioni kwa mfuko huo kama malipo ya awali.

Kutokana na hali hiyo, Zitto alisema kamati yake imewaagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kuchunguza ili kujua kama kweli fedha inayodaiwa serikali hiyo au zaidi.

Katika hatua nyingine, kamati hiyo imetoa mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia Wizara ya Fedha, kufanya tathmini ya mchakato wa uuzaji Kampuni ya Zain kwa wamiliki wake wa sasa Airtel ya India ili kufahamu upungufu wa kisheria uliokosesha serikali fedha.

Pia, kamati hiyo imetaka TRA kutuma timu ya wataalam nchini Nigeria, kujifunza ilivyofaidika na uuzaji wa Kampuni ya Zain wakati Tanzania ingeweza kunufaika na zaidi ya Sh308

SOURCE MWANANCHI

PSPF siyo mfuko wa pensheni kwa mashirika ya umma labda kama ulimaanisha PPF
 
Inasikitisha sana.
Nimechangia toka mwaka 2003, na hadi wa leo sijapewa namba yangu ya uanachama, na kwa masikitiko makubwa juzi nimeletewa fomu nyingine nijaze details zangu upya, wakati nilishajaza nikianza kazi mwaka 2003!...sijui ndo nitaanza kuwekewa akiba mwaka huu!??
Kwa kweli, kama serikali imeamua hadi kuchukua hela za raia, yaani za mtu mmojammoja na kuzitumia kwa mambo ya chama hii inatisha!

pole sana,ukweli ni kwamba kuhusu namba inawezekana hiyo fomu uliojaza wameimisplace.lakini nakupa matumaini kwamba pesa huwa hazipotei.michango yote ambayo inalipiwa bila namba huwa inawekwa katika acount maaum inayoitwa SUSPENSE ACCOUNT.then namba ikipatikana michango inakuwa posted ktk account/number ya mwanachama.nakushauri ujaze hiyo fomu ili upate namba ya uanachama.sababu itakuja kusumbua baadae.then washauri muwe mnateembelea ktk hizo ofisi ili mpate kujua balance ya michango yako mfano nssf wanatoa hiyo huduma bure pia itakusaidia kujua kama muajiri wako ana peleka hiyo michango sababu kuna problem baadhi ya waajiri wanawakata wafanyakazi wao lakini hawasubmit hiyo michango.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom