CAG: Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inazidai Taasisi za Serikali trilioni 1.73

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,818
4,569
1713179458689.png

Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imeonyesha taasisi za Serikali zinadaiwa mikopo ya muda mrefu yenye thamani ya Sh1.73 trilioni ambazo hazijalipwa kuanzia mwaka mmoja hadi 16.

Kwa mujibu wa kitabu cha Ripoti ya CAG ya Mashirika ya Umma, ambacho ni miongoni mwa ripoti 21 zilizowasilishwa leo Jumatatu, Aprili 15, 2024 bungeni jijini Dodoma, fedha hizo zilichukuliwa kwa nyakati tofauti kwenye Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii kwa sekta binafsi, na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa umma.

CAG amesema hali hiyo imesababisha kupunguza uwezo wa mifuko ya jamii kufanya uwekezaji zaidi.

“Pia, Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii kwa sekta binafsi (NSSF), Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa umma (PSSSF) na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) haikukusanya michango ipatayo Sh856.78 bilioni kutoka kwa wanachama, hivyo kudhoofisha uwezo wa mifuko kuhudumia wanufaika.”

“Vilevile, nilibaini Shirika la Bima la Taifa, NSSF na PSSSF hawakukusanya kodi ya Sh47.20 bilioni kutoka kwa wapangaji katika vitega uchumi vyao,” amesema Kichere.

PIA SOMA:
- Ripoti 21 za CAG zatua Bungeni kwaajili ya kuanza kujadiliwa
 
Serikali irudishe hizo pesa na kikotoo cha zamani kirejeshwe.
 
Hilo deni la billion 856 ni top ya pension za watumishi kutoka serikalini; halafu hao watumishi wenyewe sasa kwenye vichwa vyao serikali ina unlimited resources.

Hawajui ugumu wanaopitia kulipa hizo nyongeza ili wapate pension zao uzeeni; wakitoka hapo utasikia hela yangu wakati umechangia 5% ya mshahara wako.

Sio rahisi hivyo kwa nchi maskini haya mambo serikali inajitahidi sana kuwafikiria wafanyakazi wake ukifika muda wa kustaafu kwa gharama za uwekezaji mwingine wa jamii. Very ungrateful people.
 
Hilo deni la billion 856 ni top ya pension za watumishi kutoka serikalini; halafu hao watumishi wenyewe sasa kwenye vichwa vyao serikali ina unlimited resources.

Hawajui ugumu wanaopitia kulipa hizo nyongeza ili wapate pension zao uzeeni; wakitoka hapo utasikia hela yangu wakati umechangia 5% ya mshahara wako.

Sio rahisi hivyo kwa nchi maskini haya mambo serikali inajitahidi sana kuwafikiria wafanyakazi wake ukifika muda wa kustaafu kwa gharama za uwekezaji mwingine wa jamii. Very ungrateful people.
Kwahiyo wewe unataka tuchangie kiasi gani?? Leo nachangia asilimia 5 ya mshahara ghafi, na nitafanya hivyo kwa miaka zaidi ya 25. Hiyo fedha ningewekeza mwenyewe unadhani thamani yake ingekuwa kiasi gani? Punguzo ganja dogo
 
Kwahiyo wewe unataka tuchangie kiasi gani?? Leo nachangia asilimia 5 ya mshahara ghafi, na nitafanya hivyo kwa miaka zaidi ya 25. Hiyo fedha ningewekeza mwenyewe unadhani thamani yake ingekuwa kiasi gani? Punguzo ganja dogo
Jaribu kupeleka bank hiyo hela hata kwa compound interest uone kama itafika robo ya pension fund wanayokupa.

Usisahau wewe unatoa 5% serikali inakuchangia 15% ili upate hiyo pension na bado inakupa guarantee ya kulipwa.
 
Jaribu kupeleka bank hiyo hela hata kwa compound interest uone kama itafika robo ya pension fund wanayokupa.

Usisahau wewe unatoa 5% serikali inakuchangia 15% ili upate hiyo pension na bado inakupa guarantee ya kulipwa.
Sahihi mtu anaongea utasikia serekali haijali wafanyakazi wakati inachangia mfanyakazi asilimia 15 ya mshahara wake kila mwezi ili akifika kustaafu atoke vizuri.Watu hawana shukrani
 
Jaribu kupeleka bank hiyo hela hata kwa compound interest uone kama itafika robo ya pension fund wanayokupa.

Usisahau wewe unatoa 5% serikali inakuchangia 15% ili upate hiyo pension na bado inakupa guarantee ya kulipwa.
Sio lazima tupeleke benki. Benki wanafanya biashara. Tuchukulie mfano kila mwaka unachukua hiyo asilimia 5 kwa kila mwaka unanunua shamba unapanda miti ya mbao. Baada ya miaka 15 utakua na shamba kubwa tu. Tatizo la serikali yetu ni kuingilia mifuko hiyo lakn kama ingeachwa ikiendeshwa kibiashara haya matatizo yasingetokea
 
Back
Top Bottom