Sex addict
JF-Expert Member
- Feb 21, 2023
- 902
- 1,816
Hiii thread imekuwa uselesss daaah 🤢🤢🤢🤢🤢🤢🤢🤮.
mimi ni mzuri fact,mkeo ni mbaya fact
Yaan wewe unamtoa knockout mwanamke kwa Uzuri[emoji15][emoji848] yaani wewe wajisifu umzuri kuliko huyo mwanamke je kwa uzuri wako huo boyfriend wa huyo dada aje kukuchumbia???
Jamani nacheka kama mazuri walai [emoji1]
Nimesema mwili hua unajidhuru wenyewe wewe unachokiongea ni kingine kabisa, Ila ni jambo jema maana hizo ni precautions nzuri mtu kuzizingatia mkuu upo sahihi piaLabda kama haujui matokeo ya hizo changamoto ni ulaji mbovu, diet mbovu, lishe isiyozingatia virutubisho.
Ukiwa unakula kwa kuzingatia lishe bora, unafanya mazoezi, unapumzika vizuri, unakuwa makini na afya yako hayo magonjwa kuupata mwili labda urogwe.
Naomba urejee utaratibu wa lishe bora.
Mwanaume kujiita Mzuri sio ndio dalili za Upinde wa Mvua hizo [emoji848] sijawahi kuona rijali akasema yeye ni Mzuri.Tangu lini uzuri ulikuwa Mali ya Mwanamke pekee?
Embu tupe Rejea hata moja, iwe ya shule, au kidini au hata kimila, tunaomba Rejea..ili tujadili kisomi hapa.
Au hata kisheria.
Tuanzie hapo.
Mwanaume kujiita Mzuri sio ndio dalili za Upinde wa Mvua hizo [emoji848] sijawahi kuona rijali akasema yeye ni Mzuri.
bora hata angejilinganisha na wanaume, anashindana uzuri na mwanamke........mara nyingi wanaokataa ndoa wanasemwa humu ni mashoga,na ame prove hiloMwanaume kujiita Mzuri sio ndio dalili za Upinde wa Mvua hizo [emoji848] sijawahi kuona rijali akasema yeye ni Mzuri.
tena kama ndio wewe umejiweka kwenye profile,KOMA KUNIFUATA FUATA....sura kama kipaka!🤣🤣🤣
Ndio maana nikasema huna kigezo cha Akili.
Tofautisha urembo na Usafi 😀😀
Tofautisha uzuri na urembo.
Wewe sio mzuri ndio maana unalazimisha uhudumiwe ili urembwe walau uonekane onekane.
Wazuri hawahitaji urembo. Uliza popote.
Mimi pia ni rijali na ni mzuri!Mwanaume kujiita Mzuri sio ndio dalili za Upinde wa Mvua hizo [emoji848] sijawahi kuona rijali akasema yeye ni Mzuri.
Sawa Robert wewe ni Mzuri na Mrembo pia,Hiyo ndio Reference?
Suleiman kwenye Biblia kajiita mara kibao Mzuri. Yeye sio mwanaume Rijali?
Kauli ya mwanaume kujiita ni Mzuri, wanaume hawaitumii Kwa sababu haiwaongezei Jambo lolote, lakini sio kosa wala haijakatazwa kisheria iwe sheria za dini, sheria za nchi, sheria za Asili, wala sheria za kiutamaduni.
Ndio maana nikakuambia Nipe Reference.
Kuhusu Mambo ya Ushoga Hilo ni kosa, kidini na kiasili na Baadhi ya sheria za nchi Fulani Fulani.
Labda useme ni dhana na Maoni yako binafsi na ya jamii uliyokuzwa nayo. Lakini hakuna kosa lolote mwanaume kujiita hivyo.
Uzuri hauna mmiliki, MTU yeyote anaweza kujiita. Ikiwa hajadhamiria Jambo Baya au kuvunja sheria
Sawa Robert wewe ni Mzuri na Mrembo pia,
Hongera sana cha uzuri [emoji1787]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787].Mimi pia ni mzuri na handsome na kataa Ndoa njoo uniue sasa
bwabwa lingine hili...Mimi pia ni mzuri na handsome na kataa Ndoa njoo uniue sasa
bwabwa.Mimi pia ni rijali na ni mzuri!
In any difficulty you are going through, make sure you put God first because he has known you since you were in your mother's wombbwabwa lingine hili...
Najikutaga sisomi tunzi za huyu bwana Kwa sababu anachozingumzia uhalisia Upo tatizo anazunguuukaPROFILE LA MWANAMKE ANAYEHANGAIKIA NDOA!
Anaandika, Robert Heriel
Ndoa ni Taasisi inayowaunganisha Mwanaume na Mwanamke kuunda Familia moja(serikali moja), kuwa mwili mmoja.
Kisayansi Mwili wa binadamu umejengwa na Cells, Tissue, Organs, Organ system, na mwishowe tunapata Organism yaani kiumbe.
Hivyo mwanaume na Mwanamke wanapoungana Kwa Njia ya Ndoa huunda mwili mmoja.
Kikawaida Mwili haujidhuru, Kwa sababu unafanya kazi Kwa kushirikiana na kutegemeana.
Kwenye mwili wa binadamu kila kiungo kinakazi yake katika kuhakikisha Mwili unafikia na Kupata mahitaji yake ya msingi.
Sikio sio Bora kuliko jicho, pua sio Bora kuliko Ulimi n.k
Halikadhalika kwenye Ndoa, mume sio Bora kuliko MKE na wala MKE sio Bora kuliko Mume.
Wote ni mwili mmoja. Ni kitu kimoja.
Ingawaje Mwanaume ni kichwa lakini haimaanishi yeye ndiye anahudumiwa au kuhudumia Mwili. Hakuna kiungo katika mwili kinachohudumia kiungo kingine. Viungo vyote vina-play majukumu yake kuujenga Mwili.
Mutualism ndio lengo na kusudi la Ndoa. Yaani wote ninyi ni wamoja, mkipatacho ni chenu wote. Wote mnafaidika. Na sio mmoja anafaidika zaidi ya mwingine au anatafuta upendeleo. Huo unaitwa ubinafsi.
Kwenye relationship kuna commensalism ambao wao hutaka kufaidika tuu huku wakiwa Hawana mchango wowote. Ni kama Ile ya Parasites kama Chawa, au Kupe, au wadudu wanyonyaji. Yaani mwenza mmoja anaumia huku mwingine anagain. Hiyo sio Ndoa. Huo ni Utapeli.
Jamii yetu lazima ipate waalimu watakaoweza kubadilisha mitazamao ya Vijana na mabinti wadogo waondokane na mitazamo ya ki- parasites au commensalism.
Ukishaingia kwenye Ndoa wewe ni sehemu ya utawala, Mume ni Kichwa, kiongozi anayeongoza, MKE ni Msaidizi, anayeratibu mambo kumsaidia Mumewe kujenga Familia, Mwili mmoja.
Kama ni sheria mnatengeneza wote, kama ilivyoserikali.
Kama ni mipango mnapanga wote,
Kama ni utekelezaji mnatekeleza wote.
Kama ni Bajeti mnapanga wote.
Kama ni kazi za uzalishaji Mali mnazalisha wote.
Iweje mmoja aseme anataka ahudumiwe, yaani huo mtazamo unatoka wapi?
Wanaohudumiwa ni Watoto ambao hawapo sehemu ya uongozi, utawala.
Ndio maana mnapokuwa kwenye familia epukeni kauli za umimi, Ubinafsi.
Kichwa hakiwezi kuliambia Sikio huu NI mwili wangu, miguu haiwezi kuiambia mikono huu NI mwili wangu au Mimi ni Bora kuliko wewe. Uliona wapi mambo ya hivyo? Ndio maana mwili una-coordination. Viungo vyote vipo kwaajili ya mwili, kuutunza mwili, kuhakikisha Mwili upo salama.
Mfano, mdudu atakapoung'ata mguu, Kwa upesi Mkono utampiga na kumuondoa mdudu huyo mguuni Kwa kupewa taarifa na ubongo. Licha ya kuwa sio mkono uliong'atwa lakini umewajibika kuondoa hatari hiyo.
Hivyo ndivyo MKE na Mume wanavyotakiwa kuishi, Kwa sababu wao ni mwili mmoja. Ushirikiano, umoja usio na maswali yoyote katika kutekeleza majukumu ni lazima kwani tayari mmekodinatiwa na upendo. Yeyote ayakayeumia wote mmeumia yaani mwili wenu umeumia. Sasa ubinafsi unatoka wapi? Ubinafsi lazima utokee Kwa Watu wasio na upendo ( Coordination)
Kwa waamini, Biblia inasema Mungu alivyomuumba Mwanamke alimtoa katika mwili wa mwanaume. Kumaanisha wao ni mwili mmoja. Hivyo ndoa ndio mchakato pekee utakaowaunganisha Kwa kile kiitwacho upendo.
Mume ni kiongozi, kichwa, lakini haimaanishi yeye ni Mungu yaani mungu mtu. Kuoneana, kunyanyasana, kutapeliana, kukatiliana huja pale ambapo hakuna Mutual relationship.
Mke hataki kuwa msaidizi, hajishughulishi anaule mtazamo wa kunyonya, yaani ni Parasite nyonyaji.
Ni lazima tuwajenge Binti na Vijana wetu wawe na tabia chanya, Upendo, HAKI na Ukweli ndio vitaunda familia na taifa Huru, lenye furaha na Amani.
Elimu itolewe, matamasha yafanyike kuhakikisha uelewa kuhusu ndoa na familia vinakuwa juu Kwa Vijana na mabinti zetu.
Unyonyaji usiwe sehemu ya Haki Kwa Watu.
Ukandamizaji na unyanyasaji Isiwe Haki ya baadhi ya Watu katika familia zao.
Vijana na mabinti, usikubali kuolewa au kuoa MTU ambaye ni Parasite, Oa au olewa na MTU anayejua maana ya Ndoa na Familia.
Familia Ipo Kwa maslahi ya wote Wawili, mume na MKE. Kisha kuzalisha kizazi Makini na Bora.
Kwenye ndoa sio sehemu ya kuonyeshana upendo, Bali ni sehemu ya kuishi Kwa Upendo. Ndoa sio maonyesho. Ndoa ni Maisha Halisi.
Maisha ya maonyesho ndio yanafanya wengi kuwa watumwa, ili aonekane anaupendo. Upendo ni kama uhai tuu, hauhitaji jitihada kuuonyesha.
Mwenye upendo lazima aone Upendo, huna haja ya kumuonyeshea,
Ikiwa ninyi ni mwili mmoja basi hakuna ubinafsi na Uchoyo. Vyote mlivyonavyo ni vyenu.
Sasa Parasite wao Tabia zao ni zile za Chakwao ni Chao, chakwako ni chawote. Hapo hakuna Ndoa. Huo ni Unyonyaji! Utapeli, uhuni na ushenzi.
Kusudi la Ndoa halipo hivyo. Labda ndoa za mashetani za kutoana kafara.
Upendo hauna kitu kinaitwa Talaka. Ndio maana siku hizi Watu hawapendani yaani hakuna Ndoa Kwa sababu kwenye Ndoa yaani upendo hakuna kuachana. Kifo ndio kinawatengenisha.
Sasa Watu wakiambiwa hivi wanaona wamesemwa vibaya Wakati ndio Ukweli.
Baada ya kusema hayo machache; nitoe Profile la Mwanamke anayepigania Ndoa;
1. Wavivu na ndoa kwao ni Ajira.
Mke Mwema na Bora hawezi kuipigania Ndoa, anajua yeye ni mwanamke mwenye sifa na vigezo vyote vya kuwa MKE, anajua wanaume Bora wanamtafuta Kwa udi na uvumba kumpata Mwanamke kama yeye.
Lakini Wanawake wavivu kwao hupigana vikumbo kusaka ndoa Kwa sababu ndoa kwao ni Ajira.
Binti Hana kazi, Hana anachojishughulisha, anatafuta Ng'ombe wa kumnyonya.
Akipata Ndoa, ni wale wanakula vyakula vya uvivu, hazalishi chochote lakini linataka Kula.
Mwanamke Bora lazima ajishughulishe iwe Mvua liwe jua. Hata kama mumewe atamuambia akae nyumbani lakini hapo nyumbani lazima aanzishe biashara ndogondogo. Au amuambie mumewe anahitaji kununua Hisa kwaajili ya uzalishaji.
Au atafuga Kuku au bata au kulima Bustani ili kuzalisha kipato.
2. Hana VIGEZO vya kitabia na kimaumbile.
Mwanamke ambaye anapigania ndoa kikawaida hajiamini, Hana Tabia nzuri, ingawaje Kwa nje atajionyesha ni Mwanamke Mwema lakini kinachomtia hofu ni tabia zake zilizojificha. Tabia Mbaya.
Kimaumbile keshajiharibu iwe Kwa uchafu wa kutembea tembea hovyo na wanaume au kujikoboa na kuharibu maumbile yake Kwa urembo uliopitiliza.
Mwanamke mwenye Tabia njema, na aliyetunza maumbile yake hawezi kuipigania Ndoa ilhali anauhakika kuwa ataolewa tuu. Tena ataolewa na Mwanaume mwenye upendo na Akili ya nini maana ya Upendo.
3. Ubinafsi na Unyonyaji.
Wanaopigania ndoa wengi wao hutanguliza ubinafsi wao mbele, huwa- judge wanaume wanaokuja kuwachumbia Kwa kigezo cha Uchumi na hadhi zao badala ya kuangalia upendo wa wanaume wanaokuja kuwachumbia.
Hii huwafanya watumie muda mrefu na Wakati mwingine hufikia kuchanganyikiwa.
Kinachounda ndoa NI Upendo sio uchumi wa mwenza iwe Mwanamke au Mwanaume.
Upendo ndio huleta yote ndani ya Ndoa,
Lakini wanyonyaji kwao upendo sio lolote, wanaamini uchumi ndio upendo. Mwishowe wakiingia ndoani huona mambo yakiwa tofauti.
Wito, Ni muhimu Kabla ya Ndoa Watu kujijenga zaidi kiupendo, kiimani kisha kimtazamo/kifikra ili kuzifanya familia ziwe na furaha. Ni kweli wengi tumetoka kwenye Familia zenye dhana nyingi potofu kuhusu Ndoa. Ambazo nyingi zimejengwa katika misingi ya Ubinafsi na wala sio umoja na ushirikiano Jambo ambalo limekuwa likiumiza moja ya wanandoa au wanandoa wote Wawili.
Nitaendelea kusisitiza, ndoa ni muhimu Kwa sababu ndio itakayojenga familia Bora na taifa Bora.
Lakini sio hizi ndoa za kihuni na kitapeli ambazo msingi wake Mkuu umejengwa kinyonyaji, kiukandamizaji, na kiudumavu. Ndoa hizi za kitapeli ndio zinazalisha kizazi hiki kinachoendelea,
Nipumzike sasa.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mkuu aina hii ya nyuzi unazipenda sana [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Hatimae umegusa eneo muhimu sana katika funzo la maisha ya kisasa na hata ndoa...
Upendo ndio key, ndio ndoa yenyewe mengine yote yatafata nyuma ila ubaya ni kwamba ndoa nyingi sikuhizi zinafungwa kimasilahi. Upendo umekuwa na conditions, kukiwa na maslahi unapendwa yakiisha au kukata unatupwa kama toilet paper. On to the next one.
Ile clip nliiona jamaa inaonekana anajitambua sanaNa huo ndio Utapeli wenyewe.
Diamond juzijuzi alikuwa anazungumzia Jambo hilohilo.
Kama uliona Ile Clip, alisema kuwa wanaume watafute Pesa kwani hata yeye anajua anapendwa Baada ya Kupata hizo Pesa. Ndio maana diamond na watu mfano wake hawaizingatii ndoa Kwa sababu wanajua Utapeli wake.
We huzipendi mkuu 😀Mkuu aina hii ya nyuzi unazipenda sana [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]