Profile la Mwanamke anayehangaikia Ndoa

Profile la Mwanamke anayehangaikia Ndoa

Hatimae umegusa eneo muhimu sana katika funzo la maisha ya kisasa na hata ndoa...

Upendo ndio key, ndio ndoa yenyewe mengine yote yatafata nyuma ila ubaya ni kwamba ndoa nyingi sikuhizi zinafungwa kimasilahi. Upendo umekuwa na conditions, kukiwa na maslahi unapendwa yakiisha au kukata unatupwa kama toilet paper. On to the next one.

Na huo ndio Utapeli wenyewe.

Diamond juzijuzi alikuwa anazungumzia Jambo hilohilo.
Kama uliona Ile Clip, alisema kuwa wanaume watafute Pesa kwani hata yeye anajua anapendwa Baada ya Kupata hizo Pesa. Ndio maana diamond na watu mfano wake hawaizingatii ndoa Kwa sababu wanajua Utapeli wake.
 
changamoto = Ubinafsi/umimi / usiri/ umbea / usafi (mwili / roho) / wenza kutopenda maisha ya sala/ibada ........etc

Alafu utake kuolewa au kuoa.
Yaani unaolewa alafu muda huohuo unasema au unamtazamo hakuna mwanaume WA pekeako. Hiyo ni Ndoa au UHUNI.

Yaani umiliki nyumba alafu muda huohuo unaambiwa hiyo nyumba haina wenyewe.
 
Hii bato kali sana....ngoja watazamaji tuendelee kuangalia....labda serikali nayo itabadilisha sheria ya ndoa,
kipengele cha kugawana mali kifutwe

Na Kwa nini mgawane ilhali mnapendana?
Unajua hicho kipengele kimewakwa Kwa matapeli Kwa sababu wanajua Ipo siku mtamwagana tuu.

Kwenye upendo wa kweli hakuna kuachana, zaidi ya kifo kuwatenganisha,
 
Alafu utake kuolewa au kuoa.
Yaani unaolewa alafu muda huohuo unasema au unamtazamo hakuna mwanaume WA pekeako. Hiyo ni Ndoa au UHUNI.

Yaani umiliki nyumba alafu muda huohuo unaambiwa hiyo nyumba haina wenyewe.
Jamii imetokea kuamini kuwa hakuna mwanaume wa peke yakoo na wengi wameenda mbali wanasema bora wawe na mahusiano na waume/wake za watuu kwa sababu zao binafsii ...... utakumbuka ila kauli na kibonzo "mwamba anaishi kwenye ndoa ya watu kwa miaka inayozidi ndoa yenyewe"
 
Kikawaida Mwili haujidhuru, Kwa sababu unafanya kazi Kwa kushirikiana na kutegemeana.
Hongera mkuu kwa andiko zuri nakupongeza sana,

Ila hapa mkuu nikurekebishe kidogo kuna wakati mwili hua unajidhuru wenyewe pale inapotekea ukafanya kazi yake kinyume mfano mdogo ni magonjwa yasiyoambukiza km Pressure BP, Kisukari, Saratani, nk hayo ni baadhi ya yale ambayo mwili hufanya kujidhuru wenyewe

Pia kuna ugonjwa wa kucha kupasuka pasuka au kucha kuota nje ya njia yake, hapo pia mwili hujidhuru wenyewe
 
Jamii imetokea kuamini kuwa hakuna mwanaume wa peke yakoo na wengi wameenda mbali wanasema bora wawe na mahusiano na waume/wake za watuu kwa sababu zao binafsii ...... utakumbuka ila kauli na kibonzo "mwamba anaishi kwenye ndoa ya watu kwa miaka inayozidi ndoa yenyewe"

Hayo ndio yanafanya Vijana waone ndoa ni ushenzi, uhuni na Utapeli.
Hawa Vijana wanataka na wake za Watu na wengine mabinti wanatoka na waume za Watu, tayari wameshaona kama nao wataoa au kuolewa kama mambo yenyewe ndio hayo basi hakuna umuhimu wa Ndoa.

Yaani kijana awe anatoka na wake za Watu alafu umwambie aoe, hvi hata ingekuwa wewe ungekubali?
Maana huo NI Utapeli, naona kabisa ndani ya Ndoa hakuna uaminifu, upendo, Haki, Ukweli. Yaani kila kitu ni negative.
Huo uzuri WA ndoa atauona wapi?

Ili ndoa iwe ya maana lazima waume za Watu waache kutongoza Wanawake wasiowake zao,
Na Wake za Watu wakitongozwa wakatae.
Ili Vijana waone kuwa kweli ndoa ni sehemu salama
 
PROFILE LA MWANAMKE ANAYEHANGAIKIA NDOA!

Anaandika, Robert Heriel

Ndoa ni Taasisi inayowaunganisha Mwanaume na Mwanamke kuunda Familia moja(serikali moja), kuwa mwili mmoja.
Kisayansi Mwili wa binadamu umejengwa na Cells, Tissue, Organs, Organ system, na mwishowe tunapata Organism yaani kiumbe.
Hivyo mwanaume na Mwanamke wanapoungana Kwa Njia ya Ndoa huunda mwili mmoja.

Kikawaida Mwili haujidhuru, Kwa sababu unafanya kazi Kwa kushirikiana na kutegemeana.
Kwenye mwili wa binadamu kila kiungo kinakazi yake katika kuhakikisha Mwili unafikia na Kupata mahitaji yake ya msingi.
Sikio sio Bora kuliko jicho, pua sio Bora kuliko Ulimi n.k
Halikadhalika kwenye Ndoa, mume sio Bora kuliko MKE na wala MKE sio Bora kuliko Mume.
Wote ni mwili mmoja. Ni kitu kimoja.
Ingawaje Mwanaume ni kichwa lakini haimaanishi yeye ndiye anahudumiwa au kuhudumia Mwili. Hakuna kiungo katika mwili kinachohudumia kiungo kingine. Viungo vyote vina-play majukumu yake kuujenga Mwili.

Mutualism ndio lengo na kusudi la Ndoa. Yaani wote ninyi ni wamoja, mkipatacho ni chenu wote. Wote mnafaidika. Na sio mmoja anafaidika zaidi ya mwingine au anatafuta upendeleo. Huo unaitwa ubinafsi.
Kwenye relationship kuna commensalism ambao wao hutaka kufaidika tuu huku wakiwa Hawana mchango wowote. Ni kama Ile ya Parasites kama Chawa, au Kupe, au wadudu wanyonyaji. Yaani mwenza mmoja anaumia huku mwingine anagain. Hiyo sio Ndoa. Huo ni Utapeli.
Jamii yetu lazima ipate waalimu watakaoweza kubadilisha mitazamao ya Vijana na mabinti wadogo waondokane na mitazamo ya ki- parasites au commensalism.

Ukishaingia kwenye Ndoa wewe ni sehemu ya utawala, Mume ni Kichwa, kiongozi anayeongoza, MKE ni Msaidizi, anayeratibu mambo kumsaidia Mumewe kujenga Familia, Mwili mmoja.
Kama ni sheria mnatengeneza wote, kama ilivyoserikali.
Kama ni mipango mnapanga wote,
Kama ni utekelezaji mnatekeleza wote.
Kama ni Bajeti mnapanga wote.
Kama ni kazi za uzalishaji Mali mnazalisha wote.
Iweje mmoja aseme anataka ahudumiwe, yaani huo mtazamo unatoka wapi?

Wanaohudumiwa ni Watoto ambao hawapo sehemu ya uongozi, utawala.
Ndio maana mnapokuwa kwenye familia epukeni kauli za umimi, Ubinafsi.
Kichwa hakiwezi kuliambia Sikio huu NI mwili wangu, miguu haiwezi kuiambia mikono huu NI mwili wangu au Mimi ni Bora kuliko wewe. Uliona wapi mambo ya hivyo?

Kwa waamini, Biblia inasema Mungu alivyomuumba Mwanamke alimtoa katika mwili wa mwanaume. Kumaanisha wao ni mwili mmoja. Hivyo ndoa ndio mchakato pekee utakaowaunganisha Kwa kile kiitwacho upendo.
Mume ni kiongozi, kichwa, lakini haimaanishi yeye ni Mungu yaani mungu mtu. Kuoneana, kunyanyasana, kutapeliana, kukatiliana huja pale ambapo hakuna Mutual relationship.
Mke hataki kuwa msaidizi, hajishughulishi anaule mtazamo wa kunyonya, yaani ni Parasite nyonyaji.

Ni lazima tuwajenge Binti na Vijana wetu wawe na tabia chanya, Upendo, HAKI na Ukweli ndio vitaunda familia na taifa Huru, lenye furaha na Amani.

Elimu itolewe, matamasha yafanyike kuhakikisha uelewa kuhusu ndoa na familia vinakuwa juu Kwa Vijana na mabinti zetu.
Unyonyaji usiwe sehemu ya Haki Kwa Watu.
Ukandamizaji na unyanyasaji Isiwe Haki ya baadhi ya Watu katika familia zao.

Vijana na mabinti, usikubali kuolewa au kuoa MTU ambaye ni Parasite, Oa au olewa na MTU anayejua maana ya Ndoa na Familia.
Familia Ipo Kwa maslahi ya wote Wawili, mume na MKE. Kisha kuzalisha kizazi Makini na Bora.

Kwenye ndoa sio sehemu ya kuonyeshana upendo, Bali ni sehemu ya kuishi Kwa Upendo. Ndoa sio maonyesho. Ndoa ni Maisha Halisi.
Maisha ya maonyesho ndio yanafanya wengi kuwa watumwa, ili aonekane anaupendo. Upendo ni kama uhai tuu, hauhitaji jitihada kuuonyesha.
Mwenye upendo lazima aone Upendo, huna haja ya kumuonyeshea,
Ikiwa ninyi ni mwili mmoja basi hakuna ubinafsi na Uchoyo. Vyote mlivyonavyo ni vyenu.
Sasa Parasite wao Tabia zao ni zile za Chakwao ni Chao, chakwako ni chawote. Hapo hakuna Ndoa. Huo ni Unyonyaji! Utapeli, uhuni na ushenzi.
Kusudi la Ndoa halipo hivyo. Labda ndoa za mashetani za kutoana kafara.

Upendo hauna kitu kinaitwa Talaka. Ndio maana siku hizi Watu hawapendani yaani hakuna Ndoa Kwa sababu kwenye Ndoa yaani upendo hakuna kuachana. Kifo ndio kinawatengenisha.
Sasa Watu wakiambiwa hivi wanaona wamesemwa vibaya Wakati ndio Ukweli.


Baada ya kusema hayo machache; nitoe Profile la Mwanamke anayepigania Ndoa;

1. Wavivu na ndoa kwao ni Ajira.
Mke Mwema na Bora hawezi kuipigania Ndoa, anajua yeye ni mwanamke mwenye sifa na vigezo vyote vya kuwa MKE, anajua wanaume Bora wanamtafuta Kwa udi na uvumba kumpata Mwanamke kama yeye.
Lakini Wanawake wavivu kwao hupigana vikumbo kusaka ndoa Kwa sababu ndoa kwao ni Ajira.
Binti Hana kazi, Hana anachojishughulisha, anatafuta Ng'ombe wa kumnyonya.

Akipata Ndoa, ni wale wanakula vyakula vya uvivu, hazalishi chochote lakini linataka Kula.
Mwanamke Bora lazima ajishughulishe iwe Mvua liwe jua. Hata kama mumewe atamuambia akae nyumbani lakini hapo nyumbani lazima aanzishe biashara ndogondogo. Au amuambie mumewe anahitaji kununua Hisa kwaajili ya uzalishaji.
Au atafuga Kuku au bata au kulima Bustani ili kuzalisha kipato.

2. Hana VIGEZO vya kitabia na kimaumbile.
Mwanamke ambaye anapigania ndoa kikawaida hajiamini, Hana Tabia nzuri, ingawaje Kwa nje atajionyesha ni Mwanamke Mwema lakini kinachomtia hofu ni tabia zake zilizojificha. Tabia Mbaya.
Kimaumbile keshajiharibu iwe Kwa uchafu wa kutembea tembea hovyo na wanaume au kujikoboa na kuharibu maumbile yake Kwa urembo uliopitiliza.

Mwanamke mwenye Tabia njema, na aliyetunza maumbile yake hawezi kuipigania Ndoa ilhali anauhakika kuwa ataolewa tuu. Tena ataolewa na Mwanaume mwenye upendo na Akili ya nini maana ya Upendo.

3. Ubinafsi na Unyonyaji.
Wanaopigania ndoa wengi wao hutanguliza ubinafsi wao mbele, huwa- judge wanaume wanaokuja kuwachumbia Kwa kigezo cha Uchumi na hadhi zao badala ya kuangalia upendo wa wanaume wanaokuja kuwachumbia.
Hii huwafanya watumie muda mrefu na Wakati mwingine hufikia kuchanganyikiwa.
Kinachounda ndoa NI Upendo sio uchumi wa mwenza iwe Mwanamke au Mwanaume.
Upendo ndio huleta yote ndani ya Ndoa,
Lakini wanyonyaji kwao upendo sio lolote, wanaamini uchumi ndio upendo. Mwishowe wakiingia ndoani huona mambo yakiwa tofauti.

Wito, Ni muhimu Kabla ya Ndoa Watu kujijenga zaidi kiupendo, kiimani kisha kimtazamo/kifikra ili kuzifanya familia ziwe na furaha. Ni kweli wengi tumetoka kwenye Familia zenye dhana nyingi potofu kuhusu Ndoa. Ambazo nyingi zimejengwa katika misingi ya Ubinafsi na wala sio umoja na ushirikiano Jambo ambalo limekuwa likiumiza moja ya wanandoa au wanandoa wote Wawili.

Nitaendelea kusisitiza, ndoa ni muhimu Kwa sababu ndio itakayojenga familia Bora na taifa Bora.
Lakini sio hizi ndoa za kihuni na kitapeli ambazo msingi wake Mkuu umejengwa kinyonyaji, kiukandamizaji, na kiudumavu. Ndoa hizi za kitapeli ndio zinazalisha kizazi hiki kinachoendelea,

Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Taikoni kama Taikoni
Umemaliza
 
Hongera mkuu kwa andiko zuri nakupongeza sana,

Ila hapa mkuu nikurekebishe kidogo kuna wakati mwili hua unajidhuru wenyewe pale inapotekea ukafanya kazi yake kinyume mfano mdogo ni magonjwa yasiyoambukiza km Pressure BP, Kisukari, Saratani, nk hayo ni baadhi ya yale ambayo mwili hufanya kujidhuru wenyewe

Pia kuna ugonjwa wa kucha kupasuka pasuka au kucha kuota nje ya njia yake, hapo pia mwili hujidhuru wenyewe

🙏🏾🙏🏾🙏🏾
Wataalamu wa afya watakuja kulijadili hili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom