Strong ladg
JF-Expert Member
- Jul 15, 2021
- 691
- 1,673
Niende moja kwa moja kwenye mada leo asubuhi na mapema.
Katika jamii yetu kwa sasa kumekuwa na mijadala mingi kuhusu ndoa hasa kutokana na idadi ya migogoro na talaka kuongezeka kila mwaka. Wakati wa mijadala hii , vijana wa leo wamekuwa wakitupiwa lawama kwa kutozingatia ndoa zao na kuwa wepesi kuachana huku kukiwa na kauli za " mbona mabibi/ mababu zetu walidumu kwenye ndoa hadi uzeeni?"
Sikatai hiyo mfano maana inabidi tujifunze kwa wazee wetu,lakini je tunaposema walidumu tunamaanisha nini? Walidumu kwa sababu hawakuwa na sababu ya kuachana? Walidumu kwa sababu waliishi kwa amani na upendo? Au walidumu kwa sababu hawakuwa na chaguo lingine?
Tunapozungumzia ndoa imara ambazo huzalisha familia bora,je tunaangalia vigezo gani? Je ni cha muhimu wanandoa wako pamoja au wanandoa wanaishi kwa furaha ,upendo na uaminifu?
Sio kwamba changamoto hazitakuwepo kwenye ndoa, changamoto zipo,lakini watu waliojitoa kwa dhati kwenye ndoa,changamoto zitafunikwa na upendo uliopo baina yao na sio changamoto kukausha ule upendo unaowaunganisha pamoja.
Je jamii yetu inahamasisha nini? Inahamasisha ndoa ambazo ziko imara kwa sababu wanandoa wanakuwa waaminifu kwa viapo vyao vya ndoa au ndo zile za "msiachane kwa sababu mna watoto"?.
Katika jamii yetu kwa sasa kumekuwa na mijadala mingi kuhusu ndoa hasa kutokana na idadi ya migogoro na talaka kuongezeka kila mwaka. Wakati wa mijadala hii , vijana wa leo wamekuwa wakitupiwa lawama kwa kutozingatia ndoa zao na kuwa wepesi kuachana huku kukiwa na kauli za " mbona mabibi/ mababu zetu walidumu kwenye ndoa hadi uzeeni?"
Sikatai hiyo mfano maana inabidi tujifunze kwa wazee wetu,lakini je tunaposema walidumu tunamaanisha nini? Walidumu kwa sababu hawakuwa na sababu ya kuachana? Walidumu kwa sababu waliishi kwa amani na upendo? Au walidumu kwa sababu hawakuwa na chaguo lingine?
Tunapozungumzia ndoa imara ambazo huzalisha familia bora,je tunaangalia vigezo gani? Je ni cha muhimu wanandoa wako pamoja au wanandoa wanaishi kwa furaha ,upendo na uaminifu?
Sio kwamba changamoto hazitakuwepo kwenye ndoa, changamoto zipo,lakini watu waliojitoa kwa dhati kwenye ndoa,changamoto zitafunikwa na upendo uliopo baina yao na sio changamoto kukausha ule upendo unaowaunganisha pamoja.
Je jamii yetu inahamasisha nini? Inahamasisha ndoa ambazo ziko imara kwa sababu wanandoa wanakuwa waaminifu kwa viapo vyao vya ndoa au ndo zile za "msiachane kwa sababu mna watoto"?.