Profesa BAREGU ndiye kinara wa kupinga dual citizenship

Profesa BAREGU ndiye kinara wa kupinga dual citizenship

Hayo ndio matatizo ya kwenda bar ukiwa na buku mbili,ili uendelee kupata kilaji inabidi uteme pumba kama hivi,asalamaleko wallah!
 
Kwa Mtanzania wa kweli sidhani kama anaweza kushabikia hoja hii. Bila shaka manufaa ni kwa kundi dogo sana la watu ambalo mwisho wa siku watakuja ku-abuse hiyo haki.

Naona unatoa hisia zako. Baati mbaya hii ni sehemu ya kutoa hoja zinazombatana na vielelezo na mifano
 
Wote mnaopinga uraia wa nchi mbili ni WIVU tu na hakuna lingine. Wengi sababu zenu ni mbovu kabisa, mnamitandao someni faida zake. Mnataka muambiwe humu ili iweje?

Acheni wivu na uoga wa wao walivyo kimaishakili zaidi yenu.
 
kumbuka kuwa wakati huo BABA,MAMA,WAJOMBA,SHANGAZI NDUNGU,JAMAA NA MARAFIKI WAPO TANZANIA,sasa kuninyima uraia ambao ndio uhalisia wa vinasaba vyangu ni kuninyima haki ya kuishi,na ndio maana hata wanya pia huwa wanahama,leo SERENGETI,Kesho Kenya,hawapendi,lakini ndio utafutaji wa maisha ulivyo.
Naunga mkono uraia wa nchi 2 kuliko hata hizo posho wanazozitaka ziongezeke.

Hamna jipya zaid ya kujiandaa luiba kama mwenzenu balali. kama unawapenda nduzo kwa nn uwaache na uutake umarekani? Ulitaman uzaliwe ulaya ama marekan. Sasa u've got the opportunity! Hamia sisi hatukuhitaji
 
Wazungu na wahindi wanaoukuja na kupewa uraia huwa wana ukana uraia wa nchi zao ndio wanapewa uraia wa tanzania...kama unaitamani tanzania kana uraia wa ughaibu upata wa tanzania sidhani kama utanyimwa
unafuu wa elimu, afya, mikopo n.k. Yanakufanya uchukue uraia wa kigeni, lakini unataka ubaki na uraia wako wa kuzaliwa! Ninashangaa kwa sababu kule unakochukua uraia wanakutegemea uwe mzalendo na uishi uraia huo. Wakati huo wewe unataka kuishi 'huku wataka kule wataka'...
 
kitu cha kwanza cha kufaham ni diaspora na dual citizenship ni vitu viwili tofauti, alafu wakat mwingine tusipende kumfurahisha kila mtu sababu ni kitu kisichowezekana. Dual citizenship is something very risky, let's not be blinded by investment. Hasara zinazoweza sababishwa na dual citizenship kwa nchi masikini na changa km TZ ni nyingi compared to faida. c kila kitu ni cha kuiga jaman kumbukeni hao wanao taka dual citizenship endapo mambo yatakwenda ndivyo sivyo wataikimbia TZ na kurudi kwenye nchi walizochukua uraia kwa maneno marahisi u can't get true patriot citizens through dual citizenship
Mkuu kula tano..madhara ya dual citizenship ni makubwa kuliko faida ..mie nafikiri hio kitu isikubaliwe kabisaa ni majanga, kwanza tujiulize hivyo sie tulioko ughaibuni ni asilimia ngapi ya population ya Tz..maana wabongo walioko nje ni wachache sana huwezi kucompare eti Kenya au Uganda...pili hivi kuna mbongo haswa anaweza shindwa kuinvest TZ eti kwa vile tu ana uraia wa nchi zingine???mie nimefika bongo mwaka juzi pamoja na uraia wangu wa ughaibuni lakini nimefanya mambo mengi kama raia bila mgogoro wowote na nikitaka hiko kitambulisho cha uraia naweza kupata pia...tuache longo longo uraia wa nchi mbili kwa TZ kwa sasa ni majanga na haswa kipindi hiki muhimu cha uvumbuzi wa mafuta na gesi...tuangalie mambo muhimu kwa faida ya wananchi wengi wa Tanzania na sio hilo la watu wachache sana wanaoishi huku ughaibuni.
Big up Prof. Baregu wewe ni mzalendo wa kweli!!!
 
Wote mnaopinga uraia wa nchi mbili ni WIVU tu na hakuna lingine. Wengi sababu zenu ni mbovu kabisa, mnamitandao someni faida zake. Mnataka muambiwe humu ili iweje?

Acheni wivu na uoga wa wao walivyo kimaishakili zaidi yenu.

Ha ha ha ha!!!!! Nashindwa kuamini macho yangu. Wewe umeganda wakati wa Chama kimoja ambapo watu walikuwa wanatamani kwenda nje angalau kwa kuzamia meli. Siku hizo zimepita. Tanzania ya leo una ruhusa ya kwenda popote na kurudi. Kuna wafanyabiashara wengi sana wa kawaida tu (tena wameishia darasa la saba) ambao Malaysia, Singapore, Dubai, China, etc ni kama nyumbani kwao. Wanaruka kila siku na kurudi. Hawa hawadai uraia wa nchi mbili.

Wengi wenu mnaodai hii kitu ni wabeba mabox huko UK, waliobahatisha green card US ambao nawaita "Cowards" walioshindwa ushindani hapa nyumbani wakakimbilia nje. Maisha yanawagonga huko mnatafuta formula ya kula kote kote. Hatuna sababu ya kuona huo unaouita WIVU, wa nini hasa? Hata kibanda huna hapa nyumbani, ukirudi hata kununua round ya soda (sio bia) unachungulia pochi mara tatu tatu (vitu ambavyo hapa TZ ni kawaida kabisa).

Ukweli ni kuwa, tunawaonea huruma ila tunataka mtambue kuwa kila mtu "anavuna alichopanda". face the consequences of your choices to move abroad illegally. Msitegemee huruma toka kwetu. Tulio nyumbani tunakula raha ya kutosha mkuu.

On the other hand, Wa-TZ ni watu wazuri sana. Kama maisha yamekushinda huko ughaibuni, rudi nyumbani tutakusaidia ku-settle ili uanze upya. Msione aibu ya kurudi mikono mitupu kwani hiyo ni kawaida ya kutafuta, utapata au utakosa. Msitake kuitumbukiza nchi kwenye lindi la matatizo kwa visingizio vya uwekezaji.

Haki ya kuwa Mtanzania ina wajibu wa kutokuwa raia wa nchi nyingine yoyote. Na hilo tutalishinikiza kwenye Katiba mpya ili kukata mzizi wa fitina once and for all.

Ciao....
 
Huwa tunaheshimu maoni ya wenzetu! nao pia ni ustaarabu especially kwenye issues ambazo ni mtambuka kama hii
 
Hivi Baregu gani yuko UD Fanya utafiti kabla ya kuleta mada hapa JF na mijitu mingine inakurupuka kusaport mada bila kujiuliza.

Itakuwa vizuri sana kama discussion hii haitajikita kumjadili Pof. Baregu na anuani yake badala yakulitazama pia swala Zima la dual citizenship
 
Kwa Mtanzania wa kweli sidhani kama anaweza kushabikia hoja hii. Bila shaka manufaa ni kwa kundi dogo sana la watu ambalo mwisho wa siku watakuja ku-abuse hiyo haki.

Wameshapora kwenye shamba la bibi wanatafuta pa kutorokea; kama utajiri lukuki tulio nao bado nchi ni masikini hao diaspora wana nini kipya cha kutuletea zaidi ya kutumika kuwekeza mitaji ya waporaji huko nje? kwa sasa waporaji wanajua mabenki ya nje yanasituka hayataki mapesa yao machafu sasa wanataka kuwatumia hao wafagia vyoo waliolowea nje.
 
Mkuu kula tano..madhara ya dual citizenship ni makubwa kuliko faida ..mie nafikiri hio kitu isikubaliwe kabisaa ni majanga, kwanza tujiulize hivyo sie tulioko ughaibuni ni asilimia ngapi ya population ya Tz..maana wabongo walioko nje ni wachache sana huwezi kucompare eti Kenya au Uganda...pili hivi kuna mbongo haswa anaweza shindwa kuinvest TZ eti kwa vile tu ana uraia wa nchi zingine???mie nimefika bongo mwaka juzi pamoja na uraia wangu wa ughaibuni lakini nimefanya mambo mengi kama raia bila mgogoro wowote na nikitaka hiko kitambulisho cha uraia naweza kupata pia...tuache longo longo uraia wa nchi mbili kwa TZ kwa sasa ni majanga na haswa kipindi hiki muhimu cha uvumbuzi wa mafuta na gesi...tuangalie mambo muhimu kwa faida ya wananchi wengi wa Tanzania na sio hilo la watu wachache sana wanaoishi huku ughaibuni.
Big up Prof. Baregu wewe ni mzalendo wa kweli!!!

..........mkuu,
Kwa mtaji huu nasi tusiwape u Tanzania raia wa kigeni, kwani wao hatuwanyang'anyi uraia wa nchi zao.


#MosKwito !
 
Hivi sababu zilizotufanya tukatae "dual citizenship' hapo awali zime'expire' (zimeisha muda wake) ama bado?

Hivi kama unaipenda nchi yako....kwa nini unaahaa kutafuta nchi uraia wa nchi nyingine...hivi mnajua kwa nini nchi zilizoendelea zinapenda dual citizenship...? Raia wake karibu wote wanaouwezo wakukabliana na yeyote kiuchumi nakadhalika,Tanzania tuna rasilimali nyingi watanzania wengi hawawezi kukabiliana kiuchumi na yeyote...kitendo cha kuruhusu dual citizenship..maana yake sasa hata Mmarekani , mchina ana haki ya kuomba uraia hapa na kupewa huku akiendela kuwa mchina....mmarekani ki-uraia. Naye atataka fursa sawa na mtanzania hoehae (ambao tuko wengi) katika nyanja za kiuchumi...hivyo yeye kwakuwa anao uwezo wakiuchumi atafaidika zaidi na rasilima zetu kuliko wenyeji wa nchi hii. Ili litatudidimiza kabisa...tukubali kuwa na Dual citizenship tukishajiridhisha kuwa Watanzania karibu wote sasa wanao uwezo wakukabiliana na raia yeyote yule hapa Ulimwenguni katika ushindani wa kiuchumi...

Kwa ufupi, Tanzania, hatujawa tayari kuwa na Dual Citizenship...kwa sababu nilizozitoa hapo juu.
 
Mkuu kula tano..madhara ya dual citizenship ni makubwa kuliko faida ..mie nafikiri hio kitu isikubaliwe kabisaa ni majanga, kwanza tujiulize hivyo sie tulioko ughaibuni ni asilimia ngapi ya population ya Tz..maana wabongo walioko nje ni wachache sana huwezi kucompare eti Kenya au Uganda...pili hivi kuna mbongo haswa anaweza shindwa kuinvest TZ eti kwa vile tu ana uraia wa nchi zingine???mie nimefika bongo mwaka juzi pamoja na uraia wangu wa ughaibuni lakini nimefanya mambo mengi kama raia bila mgogoro wowote na nikitaka hiko kitambulisho cha uraia naweza kupata pia...tuache longo longo uraia wa nchi mbili kwa TZ kwa sasa ni majanga na haswa kipindi hiki muhimu cha uvumbuzi wa mafuta na gesi...tuangalie mambo muhimu kwa faida ya wananchi wengi wa Tanzania na sio hilo la watu wachache sana wanaoishi huku ughaibuni.
Big up Prof. Baregu wewe ni mzalendo wa kweli!!!

Ndugu yangu nakupa kumi wala sio tano; wawekezaje wa nje si ndio wanaabudiwa na hata kodi hawalipi? sasa kipi ni kipi kuja kama mtanznia ulipe kodi au kuja kama mtasha usilipe kodi na uabudiwe? ukweli uko wazi hii ni hoja ya mijizi inahofia ikitoka madarakani itafungwa inataka kukimbilia nje. Hivi kule Rwanda na Burundi walikufa wahindi wangapi? au kule Uganda wakati wa vita ya Nduli? au leo hii kule Congo na CAR wanakufa wageni wangapi? si wote wanapanda ndege na kuacha kisanga nyuma? kwa hiyo tunakuwa na rais raia wa nchi mbili Kagame akichachamaa anapanda ndege anamwachia mkuu wa mkoa kisanga manake si ajabu hata mkuu wa majeshi na mawaziri watatimka; sasa nani atasimama wakati wa majanga? yanini mtu aunguze ngozi yake wakati anaweza kukimbia zake? tafakari
 
Pamoja na kuishi nje ya tz sikubaliani na dual citizenship uraia ni wa nchi mmoja ndio mpango mzima, ukitaka wa huko ulipo ni hiyari yako, hakuna faida za uraia wa zaidi ya nchi mmoja,ni kwa faida ya watu wachache sana.

Wewe kweli akili yako inaendana na jina unalolitumia. Kama ungeelimika na kukaa nje ya nchi ungetambua umuimu wa uraia nchi zaidi ya moja. Nchi kama za kenya, nigeria na ethiopia zinapata foreign currency nyigi kutoka watu wanaofanya kazi nje ya nchi. Tatizo la bongo ni wivu wakitoto. Watu wanaouujumu uchumi tanzania uraia wanaupata kama karanga. Watu wanao teseka ni watanzania wakipato cha chini wanao ishi nje ya nchi. Hata somalia wanatambua umuimu wa mchango wa wasomali wanao ishi nje
 
Wakuu,

Sasa hivi tu huo uraia wa nchi mbili haujaruhusiwa mmeua faru wote na tembo wote nchini, ukiruhusiwa je?si ndo mtauza kabisa mbuga na mlima Kilimanjaro na kukimbilia ughaibuni?

Mfumo wetu wa ulinzi bado upo ki-analogia,inabidi tusubiri mpaka pale mfumo wetu utakapokuwa upo-digital kama wenzetu ili kuweza ku-monitor watu wema na wabaya wanaoingia na kutoka na wale wenye uraia wa nchi mbili kwa manufaa Yao binafsi!

Mungu ibariki nchi yetu!
 
Natatizika na baadhi ya hoja,
Kwamba, uraia wa nchi mbili utafanya wageni wadai na kupata fursa ambazo anastahiki mwananchi hohe hahe?

Je, hebu nitajie baadhi ya "fursa" hizo.

Pili, kuna mchangiaji ameandika yatapotokea majanga, viongozi watakimbilia nje kukimbia uwajibikaji.

Je, unataka kunambia ukiwanyima dual citizenship ndio hawawezi kukimbilia nje?


#MosKwito !
 
Wakuu,

Sasa hivi tu huo uraia wa nchi mbili haujaruhusiwa mmeua faru wote na tembo wote nchini, ukiruhusiwa je?si ndo mtauza kabisa mbuga na mlima Kilimanjaro na kukimbilia ughaibuni?

Mfumo wetu wa ulinzi bado upo ki-analogia,inabidi tusubiri mpaka pale mfumo wetu utakapokuwa upo-digital kama wenzetu ili kuweza ku-monitor watu wema na wabaya wanaoingia na kutoka na wale wenye uraia wa nchi mbili kwa manufaa Yao binafsi!

Mungu ibariki nchi yetu!

Ati?
Mfumo wa ki Digital utahusisha nini katika ku "monitor" raia hawa
Toa mifano please.


#MosKwito !
 
Back
Top Bottom