Nitaanisha sababu za nchi tajwa kushabikia dual citizenship:
- Kenya hawana ardhi, maana ardhi inahodhiwa wachache, sera ya kupeleka wa-Kenya nje kuwa diaspora ilianzishwa na ma-settler Kenya baada ya kutwaa ardhi kubwa na kuona Tanganyika ni sehemu ya kuwapeleka waKenya. Mzee Kenyatta pia alipenda kuona waKenya wahamie Tanzania kutokana na sera tata za Mkoloni mweusi wa Kenya na mpaka leo inakuja kwa kubebwa na East African Community Revival. Marehemu Tom Mboya miaka ya 1960 walianzisha Air-lift kubwa kuwapeleka vjjana vyuoni Marekani na Obama ni mtoto wa operesheni hiyo inayosababisha diaspora kubwa ya waKenya USA kuanzia miakaya 1950 mwishoni.
M
- Israel wao wana wafanya biashara wakubwa nje kama Mark Rich, Wa-Israeli wamehodhi biashara ya Almasi huko Belgium, Mabenki France, UK , USA n.k kuneemesha uchumi wao. Ku-lobby ndo wenyewe mitaa maarufu jijini Paris, France ina majina kama Ben Gurion mwasisi wa Taifa la Israel Mashariki ya Kati.
- Ethiopia wana maelfu ya wakimbizi kutokana na Mapinduzi yaliyogoa Mfalme Haile Sellasie mwaka 1974 na hivyo baada ya miaka 40 ughaibuni wamekuwa na uwezo kibiashara, kielimu n.k kusaidia nyumbani.
- Nigeria, mlolongo wa mapinduzi ya kijeshi miaka ya 1960, 1970 na vita ya Biafra imesababisha kuwa na diaspora kuwa Ulaya na Marekani ifikiayo mamilioni kwa zaidi ya miaka 50 kama Ethiopia.
- China, raia zake wamehodhi uchumi wa nchi nyingi kama ukienda The Philipines, Malaysia, Singapore n.k hivyo watasadi uchumi wa nyumbani.
Swali Kuu, Je , kuna maelfu ya wa-Tanzania wangapi walioishi ughabuni miaka zaidi ya 30 ambao wameweza kuhodhi ughaibuni biashara kubwa, wameajiriwa ktk taasisi nyeti kuweza ku-lobby (kuiunganishia ulaji) Tanzania, ni wabunge ughaibuni, madaktari, wanasheria mahiri ughaibuni?
Jibu ni kuwa Watazania wengi ni watu wa kawaida hata nyumbani Tanzania hawatambuliki kuwa wanaweza kuleta Mabadiliko Makubwa kwa Haraka hivyo basi muda wa Dual citizenship kuifaidisha Tanzania bado haujafika na suala hili litiwe kapuni labda lirejeshwe kujadiliwa baada ya miaka 50 kupita kuanzia sasa.