Profesa BAREGU ndiye kinara wa kupinga dual citizenship

Profesa BAREGU ndiye kinara wa kupinga dual citizenship

Utakuwaje mzalendo kwa nchi mbili?! Chagua moja kusuka au kunyoa mkuu, hakuna kitu kinaweza nibadilisha utaifa wangu Abadan.

Mkuu nikuulize labda, uzalendo unapimwaje?Ninavyojua mimi uzalendo uko kwenye moyo wa mtu,uzalendo hauwezi kuathiriwa na paperwork au hadhi tu ya kuwa na uraia wa nchi nyingine.So far tuna uraia mmoja mbona kila siku tunaona matendo yasiyoyakizalendo sana yakitendwa tena na hao waliojinadi mbele yenu kuwa ni wazalendo na wengine wakala kiapo kabisa kuzilinda na kuziheshimu sheria za nchi yetu na kututumikia kwa kutanguliza uzalendo,lakini umeona matendo wanayofanya yanafanana na maneno yao?

Ninavyojua mimi mtanzania popote pale alipo, tena hao walioko nje wana uchungu na nchi yao hata kuliko hao waliobaki nchini, fursa yoyote wanayopata kule wanajiskia fahari sana kushare na watu wa nyumbani kwa very obvious reasons kwamba familia yake na jamii yake iko tanzania, pia bila kusahau kuwa kilichompeleka nje sio kwa sababu haipendi Tanzania ila tu kwa sababu ya kutafuta fursa huko nje na kuiendeleza familia yake na jamii yake.Jamii yake hiyo hiyo aliyoaicha Tanzania ambayo ndiyo fahari yake.Ukimnyima hiyo fahari hapo ndo huo uzalendo unaouzungumzia unatoweka completely kwa sababu umeoung'oa Utanzania wake kwa ujumla wake
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nitaanisha sababu za nchi tajwa kushabikia dual citizenship:

  • Kenya hawana ardhi, maana ardhi inahodhiwa wachache, sera ya kupeleka wa-Kenya nje kuwa diaspora ilianzishwa na ma-settler Kenya baada ya kutwaa ardhi kubwa na kuona Tanganyika ni sehemu ya kuwapeleka waKenya. Mzee Kenyatta pia alipenda kuona waKenya wahamie Tanzania kutokana na sera tata za Mkoloni mweusi wa Kenya na mpaka leo inakuja kwa kubebwa na East African Community Revival. Marehemu Tom Mboya miaka ya 1960 walianzisha Air-lift kubwa kuwapeleka vjjana vyuoni Marekani na Obama ni mtoto wa operesheni hiyo inayosababisha diaspora kubwa ya waKenya USA kuanzia miakaya 1950 mwishoni.

    M
  • Israel wao wana wafanya biashara wakubwa nje kama Mark Rich, Wa-Israeli wamehodhi biashara ya Almasi huko Belgium, Mabenki France, UK , USA n.k kuneemesha uchumi wao. Ku-lobby ndo wenyewe mitaa maarufu jijini Paris, France ina majina kama Ben Gurion mwasisi wa Taifa la Israel Mashariki ya Kati.
  • Ethiopia wana maelfu ya wakimbizi kutokana na Mapinduzi yaliyogoa Mfalme Haile Sellasie mwaka 1974 na hivyo baada ya miaka 40 ughaibuni wamekuwa na uwezo kibiashara, kielimu n.k kusaidia nyumbani.
  • Nigeria, mlolongo wa mapinduzi ya kijeshi miaka ya 1960, 1970 na vita ya Biafra imesababisha kuwa na diaspora kuwa Ulaya na Marekani ifikiayo mamilioni kwa zaidi ya miaka 50 kama Ethiopia.
  • China, raia zake wamehodhi uchumi wa nchi nyingi kama ukienda The Philipines, Malaysia, Singapore n.k hivyo watasadi uchumi wa nyumbani.
Swali Kuu, Je , kuna maelfu ya wa-Tanzania wangapi walioishi ughabuni miaka zaidi ya 30 ambao wameweza kuhodhi ughaibuni biashara kubwa, wameajiriwa ktk taasisi nyeti kuweza ku-lobby (kuiunganishia ulaji) Tanzania, ni wabunge ughaibuni, madaktari, wanasheria mahiri ughaibuni?

Jibu ni kuwa Watazania wengi ni watu wa kawaida hata nyumbani Tanzania hawatambuliki kuwa wanaweza kuleta Mabadiliko Makubwa kwa Haraka hivyo basi muda wa Dual citizenship kuifaidisha Tanzania bado haujafika na suala hili litiwe kapuni labda lirejeshwe kujadiliwa baada ya miaka 50 kupita kuanzia sasa.

Mkuu hoja yako ni nzuri ila imejengwa kwenye majority rights bila ku-consider kuwa hata monorities deserves equal rights and justice.Sidhani kuwa ni sahihi kusema kuwa watanzania wanaotambulika ndio wanahaki ya ku-retain uraia wa Tanzania pale wakipata fursa nje ya nchi na kuamua kuchukua uraia wa huko.Ukweli ni kuwa wenye shida sana sana na watakaofaidika na hii dual-citizenship ni watanzania wanaotoka kwenye familia maskini sana ambao wamepata fursa nje ya nchi lakini maisha yakuwa maghumu zaidi kwa kukosa social privileges kama vile, ajira nzuri, unafuu wa healthcare, mikopo,nafuu ya elimu nk wasipokuwa na uraia wa hizo nchi. Hizo gharama watoto wa mafisadi, wafanya biashara wakubwa, matajiri, na watoto wa wanasiasa matajiri hawazishindwi badala yake wanaoathirika ni watoto wa walala hoi ambao wanaishia kwenye ajira zisizo rasmi au hata kufiwa na wapendwa wao kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu to meantion a few.Wanapopata hizi fursa wanaona fahari sana kuinua jamii yao huku nyumbani kwa vile wanafahamu walikotoka na sababu ya msingi iliyowapeleka kutafuta hizo fursa huko nje ambayo ni hali duni ya maisha na fursa chache.
Hoja ya kwamba wanaweza kuleta mabadilko makubwa au la, nadhani anayeweza kupima ukubwa au udogo wa mabadiliko ni yule ambae msaada umemfikia, unaweza ukawa ni msaada usiokuwa na faida inayoonekana katika community level lakini ikawa na faida kubwa sana katika family level. Bado itakuwa imeleta mabadiliko because it's touching people's lives directly.
Hivyo basi mimi naunga hoja ya dual-citizenship, nakubaliana na wengine kwamba ni mabadiliko hayo yanakuja na challenges, we should focus on discussing how those challenges can be met, but not on the right or wrongs Dual Citizenship!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nitaanisha sababu za nchi tajwa kushabikia dual citizenship:

  • Kenya hawana ardhi, maana ardhi inahodhiwa wachache, sera ya kupeleka wa-Kenya nje kuwa diaspora ilianzishwa na ma-settler Kenya baada ya kutwaa ardhi kubwa na kuona Tanganyika ni sehemu ya kuwapeleka waKenya. Mzee Kenyatta pia alipenda kuona waKenya wahamie Tanzania kutokana na sera tata za Mkoloni mweusi wa Kenya na mpaka leo inakuja kwa kubebwa na East African Community Revival. Marehemu Tom Mboya miaka ya 1960 walianzisha Air-lift kubwa kuwapeleka vjjana vyuoni Marekani na Obama ni mtoto wa operesheni hiyo inayosababisha diaspora kubwa ya waKenya USA kuanzia miakaya 1950 mwishoni.

    M
  • Israel wao wana wafanya biashara wakubwa nje kama Mark Rich, Wa-Israeli wamehodhi biashara ya Almasi huko Belgium, Mabenki France, UK , USA n.k kuneemesha uchumi wao. Ku-lobby ndo wenyewe mitaa maarufu jijini Paris, France ina majina kama Ben Gurion mwasisi wa Taifa la Israel Mashariki ya Kati.
  • Ethiopia wana maelfu ya wakimbizi kutokana na Mapinduzi yaliyogoa Mfalme Haile Sellasie mwaka 1974 na hivyo baada ya miaka 40 ughaibuni wamekuwa na uwezo kibiashara, kielimu n.k kusaidia nyumbani.
  • Nigeria, mlolongo wa mapinduzi ya kijeshi miaka ya 1960, 1970 na vita ya Biafra imesababisha kuwa na diaspora kuwa Ulaya na Marekani ifikiayo mamilioni kwa zaidi ya miaka 50 kama Ethiopia.
  • China, raia zake wamehodhi uchumi wa nchi nyingi kama ukienda The Philipines, Malaysia, Singapore n.k hivyo watasadi uchumi wa nyumbani.
Swali Kuu, Je , kuna maelfu ya wa-Tanzania wangapi walioishi ughabuni miaka zaidi ya 30 ambao wameweza kuhodhi ughaibuni biashara kubwa, wameajiriwa ktk taasisi nyeti kuweza ku-lobby (kuiunganishia ulaji) Tanzania, ni wabunge ughaibuni, madaktari, wanasheria mahiri ughaibuni?

Jibu ni kuwa Watazania wengi ni watu wa kawaida hata nyumbani Tanzania hawatambuliki kuwa wanaweza kuleta Mabadiliko Makubwa kwa Haraka hivyo basi muda wa Dual citizenship kuifaidisha Tanzania bado haujafika na suala hili litiwe kapuni labda lirejeshwe kujadiliwa baada ya miaka 50 kupita kuanzia sasa.

Nimekuelewa Mkuu.
 
Mkuu hoja yako ni nzuri ila imejengwa kwenye majority rights bila ku-consider kuwa hata monorities deserves equal rights and justice.Sidhani kuwa ni sahihi kusema kuwa watanzania wanaotambulika ndio wanahaki ya ku-retain uraia wa Tanzania pale wakipata fursa nje ya nchi na kuamua kuchukua uraia wa huko.Ukweli ni kuwa wenye shida sana sana na watakaofaidika na hii dual-citizenship ni watanzania wanaotoka kwenye familia maskini sana ambao wamepata fursa nje ya nchi lakini maisha yakuwa maghumu zaidi kwa kukosa social privileges kama vile, ajira nzuri, unafuu wa healthcare, mikopo,nafuu ya elimu nk wasipokuwa na uraia wa hizo nchi. Hizo gharama watoto wa mafisadi, wafanya biashara wakubwa, matajiri, na watoto wa wanasiasa matajiri hawazishindwi badala yake wanaoathirika ni watoto wa walala hoi ambao wanaishia kwenye ajira zisizo rasmi au hata kufiwa na wapendwa wao kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu to meantion a few.Wanapopata hizi fursa wanaona fahari sana kuinua jamii yao huku nyumbani kwa vile wanafahamu walikotoka na sababu ya msingi iliyowapeleka kutafuta hizo fursa huko nje ambayo ni hali duni ya maisha na fursa chache.
Hoja ya kwamba wanaweza kuleta mabadilko makubwa au la, nadhani anayeweza kupima ukubwa au udogo wa mabadiliko ni yule ambae msaada umemfikia, unaweza ukawa ni msaada usiokuwa na faida inayoonekana katika community level lakini ikawa na faida kubwa sana katika family level. Bado itakuwa imeleta mabadiliko because it's touching people's lives directly.
Hivyo basi mimi naunga hoja ya dual-citizenship, nakubaliana na wengine kwamba ni mabadiliko hayo yanakuja na challenges, we should focus on discussing how those challenges can be met, but not on the right or wrongs Dual Citizenship!!

.....umeandika kwa mchanganuo mzuri sana nami kwa kuongezea nitaandika mifano michache;

Vijana wengi waliokwenda nje kutafuta #Fursa , wamefanikiwa kujenga nyumbani Tanzania bara na Zanzibar ambalo kwa Tanzania bila ajira rasmi hata mkopo wa ujenzi ungekuwa ndoto

Watanzania wengi walokwenda nchi za kusini ya Africa, ulaya na nchi za ghuba ya uajemi kutafuta #Fursa , wamefanikiwa kuanzisha mabiashara ya maduka, mashamba, vyombo vya usafiri hivyo kuongeza #SokoLaAjira nchini na hata kuwaendeleza kielimu ndugu na jamaa zao walobaki Tanzania.

Kwanini twayafumbia macho haya badala yake twang'ang'ania #kuukana utanzania japo pesharudiwa sana maelezo kwamba ili kurahisisha haki za maisha huko ugenini yabidi #KUJILIPUA ?


#MosKwito !
 
Kwa Mtanzania wa kweli sidhani kama anaweza kushabikia hoja hii. Bila shaka manufaa ni kwa kundi dogo sana la watu ambalo mwisho wa siku watakuja ku-abuse hiyo haki.

Kama Tanzania imekubali kuwa inchi ya kidemokrasia , basi hiyo dual citizenship ni moja ya haki ya kiraia vile vile. Karibuni nchi zote zilizoendelea zimewapa raia wake haki hiyo. Dunia ya leo ni ushindani wa kila kitu . Kumnyima mtanzania haki ya kuwa na dual citizenship ni kumnyima nyenzo muhimu katika maisha ya wale wanopenda kusafiri na kuishi shehemu nyengine za dunia.

Tatizo letu kubwa hapa TZ , ni kwamba tumeathiriwa vibaya na siasa zile za ujamaa na kujitegemea. Kikubwa tulichokipata ni umasikini usio na mwisho. Niliwahi kukutana na mzungu mmoja Zanzibar mwaka 1988 , akanimabia kama yeye ni mmarekani lakini ana uraia wa Sweden , USA na Israel . Anazunguka dunia nzima bila ya kipingamizi chechote...

Leo hii nenda ubalozi wa Marekani na Passport yako ya Tz kuomba visa uone usumbufu utakao pewa.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Siyo lazima wawe maarufu ndiyo walete mabadiliko. Kama wakifanya kazi na kutuma hela nyumbani (remittances) watasaidia uchumi. Kama mbeba boski anatuma mfano euro 500 (euro 6000 per annum) kila mwezi kwa familia yake kule kijijini, hi si ni hata zaidi ya yule mtalii mzungu anayekuja mara moja kwa mwaka na kulipa airport taxes, na kiingilio cha mbugani? Huyu mbeba boksi si atasomesha mdogo wake shule? Mdogo wake akimaliza shule si atachangia kwenye uchumi akianza kazi?
hapo ndo napata shida kuelewa,kwani huyo mbeba mabox hawezi kufanya haya kwa sasa?mbona kuna watz wengi wanawatumia ndugu zao hela na wanasomesha ndugu zao bila wao kuwa tz physically?
 
hapo ndo napata shida kuelewa,kwani huyo mbeba mabox hawezi kufanya haya kwa sasa?mbona kuna watz wengi wanawatumia ndugu zao hela na wanasomesha ndugu zao bila wao kuwa tz physically?

.....ndugu, wajipa shida bure ya kuifahamu hoja hii.

Dhumuni la mdahalo huu ni kuwasaidia waTanzania hao wanaoishi nje haki ya uraia wao, sababu sheria ya sasa hairuhusu #DualCitizenship .


#MosKwito !
 
Tutajirudisha nyuma sana kama tutakataa uraia double ambayo ingewezesha Watanzania wanaishi nje kupata haki huko kama Raia na kwao bila kunyang'anywa passport kama ilivyo sasa
 
Back
Top Bottom