Profesa BAREGU ndiye kinara wa kupinga dual citizenship

Profesa BAREGU ndiye kinara wa kupinga dual citizenship

kila JK akizungumzia suala hili la dual citizenship anasema kuna profesa yuko UD anaongoza kwa kupinga hili suala

sasa kwa kuwa hapa we dare TALK OPENLY nathubutu kumtaja kuwa ni profesa BAREGU sababu zake hazina msingi. kama kweli tuko serious kwa nini tusifanye kama CHINA au ISRAEL au NIGERIA au KENYA au ETHIOPIA tukawatumia hawa diaspora?


In the end inashangaza sana PROFESA BAREGU kuwa na mawazo mgando kama haya

Mwenye kutaka uraia wa nchi mbili si akane uraia wa tz akachukue wa kenya then wa uk. uraua wa nchi mbili kwa ajili gani. ina maana huna imani na nchi yako au??? mtanzania wa kweli ni yule anaeipenda Tanzania na yuko tayari kufa kwa ajili ya Tanzania
 
kila JK akizungumzia suala hili la dual citizenship anasema kuna profesa yuko UD anaongoza kwa kupinga hili suala

sasa kwa kuwa hapa we dare TALK OPENLY nathubutu kumtaja kuwa ni profesa BAREGU sababu zake hazina msingi. kama kweli tuko serious kwa nini tusifanye kama CHINA au ISRAEL au NIGERIA au KENYA au ETHIOPIA tukawatumia hawa diaspora?


In the end inashangaza sana PROFESA BAREGU kuwa na mawazo mgando kama haya
Mkuu, China itoe kwenye orodha yako.
 
Kuna Madakari wengi wapo nje pamoja na wasomi/na wabeba box wanakosa hizi fursa.
 
Na kumbuka mambo mengi hapa duniani ni kwa faida ya wachache na si wengi kama ufikiliavyo.nipe mfano wa jambo ambalo lipo kwa faida ya wengi.kila jambo hapa duniani huwa ni kwa faida ya vikundi vidogovidogo na hata kwa uraia pacha ipo hivyo na tusiwanyime hiyo faida kwa hao wachache watakaofaidika nayo

Utakuwaje mzalendo kwa nchi mbili?! Chagua moja kusuka au kunyoa mkuu, hakuna kitu kinaweza nibadilisha utaifa wangu Abadan.
 
U dual ni upuuzi sana . Naungana na Prof huyo au yeyote anayepiga kuwa na u DUAL . Hatuhitaji u DUAL diaspora are no issues at all .
 
Tukiwa na vita wanaopigana ni wanajeshi

Kuhusu dual citizenship waliokimbia Rwanda hawakuwa nazo

It is also silly kuongrlea vita kwani havitokei kila siku... I would rather focus on opportunities za investment na kupuza mchoto wa wageni kwa kulink zaidi priviledges za biashara kwa more than one country has a kwenye funding na companies restrictions

Vita watapigana wanajeshi!!!! Ile ya Uganda hivi walipigana wanajeshi pekeyao? Hata kama vita haitokei kila siku lakini yaweza kutokea, ingawa hii scenario yaweza kuwa extreme lakini hizi ni issues zinazotakiwa kuwa addressed na sikupuuzwa. Udhaifu wetu kiutawala tunaufahamu hivyo tusiangalie upande mmoja na kupuuza mwingine. Yote yachukuliwe yafanyiwe analysis na watu waamue. Tukumbuke nia njema pia huzaa majanga.
 
Tanzania tuna msimamo dhaifu sana kuhus hili la uraia wa nchi mbili. Wengine wanachukulia kama ni njia ya kuadhibu wale waliokosa kazi Tanzania wakaamua kuhamia nchi nyingine kufanya kazi huku wakiwa na ndugu zao wote huko Tanzania, na wengine huchukulia kuwa kuchukua uraia wa nchi nyingine ni unakuwa umeasi utanzania. Wanasahau kuwa watanzania ni watu wenye extended familyohood kubwa sana kiasi kuwa mtu akiwa nje huwa nusu ya moyo wake uko kwao Tanzania; home is always best. In the end, msimamo wa Tanzania kwa jumla umekuwa ni wa kuwachukia ndugu zao wanaoishi nje ya nchi.

Hebu fikiria ndugu aliyeondoka Tanzania kwenda kufanya kazi huko ughaibuni, akajibana kuwa anatuma nusu ya mapato yake nyumbani kwenda kuwekeza kwao. Kutokana na yeye kuishi huko ughaibuni muda mrefu, watoto wake wote wamezaliwa huko huko kwa hiyo kwa kuzaliwa na raia wa huko ingawa kwa damu ni raia wa Tanzania. Je ndugu huyu akifariki, hao watoto wake hawatakuwa na haki yoyote Tanzania kutokana na kuwa wao walizaliwa nje na wamshapita miaka 18 wakiwa ni raia wa huko ughaibuni?.

Kuna nchi nyingi sana za kiafrika zinaruhusu uraia wa nchi mbili, na sisi kwa Tanzania tumezungukwa na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Msumbiji ambazo zinaruhusu uraia wa nchi mbili. Je tunawazidi nini kutokana na wao kuwa hivyo? Sana sana wao ndio wanatuzidi kwa kuwa na opportunities nyingi. Kenya hawana raslimali sana lakini wanakuwa na opportunities nyingi sana kwa kuvutia wawekezaji kwa vile raia wa Kenya wanaokuwa pia ni raia wenye madaraka katika nchi nyingine huweza kutumia nafasi zao huko waliko kuvutia wawekezaji waende kwao Kenya: Home is always the best.

Unapochukua uraia wa nchi nyingine inayoruhusu uraia wa nchi mbili unatakiwa kuapa kuwa utakuwa mwaminifu kwa nchi yako mpya, ila kama nchi unayotoka hairuhusu uraia wa nchi mbili basi kiapo chako kiangeza na kuukataa uraia wa nchi hiyo. Kwa hiyo watanzania wakichukua uraia wa nchi nyingine ni lazima waapa kuukataaa uraia wa Tanzania wakati wale wa Kenya wakichukua uraia wa nchi nyingine hawatakaiwi kuukana uraia wa Kenya. Sehemu hiyo ya kiapo kuukana utanzania inatokana na sera za Tanzania sasa, tukibadili basi watanzania hawatatakiwa kuukana utanzania.
 
Vita watapigana wanajeshi!!!! Ile ya Uganda hivi walipigana wanajeshi pekeyao? Hata kama vita haitokei kila siku lakini yaweza kutokea, ingawa hii scenario yaweza kuwa extreme lakini hizi ni issues zinazotakiwa kuwa addressed na sikupuuzwa. Udhaifu wetu kiutawala tunaufahamu hivyo tusiangalie upande mmoja na kupuuza mwingine. Yote yachukuliwe yafanyiwe analysis na watu waamue. Tukumbuke nia njema pia huzaa majanga.
hapo kwenye red umemaliza kila kitu, kwahiyo unaweza kuwanyima dual citizenship kwa nia njema ukapata majanga vilevile

kuhusu jibu la kwanza, si kila mtanzania alipigana vita, kuna criteria za kufanya mtu aende vitani,

i'd rather have a Tanzanian with a dual citizenship than wanasiasa wezi, wanyonyaji na wazandiki kama tulionao sasa...

kumbuka dunia imekua kijiji, na information imeondoa barriers nyingi sana zilizokua sababu ya kuzuia dual citizenship; tuna benk nyumbani ambazo payroll zao zinaandaliwa south africa, tuna kampuni ambazo data banks zake na hata assets zake zinakua managed overseas etc

we need to think beyond era ya zama za mawe... report za remittance za diaspora ni tosha kuonesha opportunities na threats vilevile
 
Hiyo sheria mbovu ndiyo tunayozungumza!
kuna haja ya kuweka elimu ya kutosha tukiangalia mazingira, tehcnology advancement, sheria chovu tunazokomalia, opportunities za kiuchumi na hata ile exposure nk.

kuna watu humu wanabisha kwasbabu mjomba au shangazi alisema something

i wouldnt be a dual citizen ila nadhani dual citizenship ina faida za kutosha... tunapoteza vichwa muhimu sana na kubaki na makapi type ya mwigulu
 
Kwa Mtanzania wa kweli sidhani kama anaweza kushabikia hoja hii. Bila shaka manufaa ni kwa kundi dogo sana la watu ambalo mwisho wa siku watakuja ku-abuse hiyo haki.

WaTanzania wa kweli tuna tabai za kujikinzani. Tuko mstari wa mbele kuimba 'utandawazi', 'utandawazi' lakini tunasahau kuwa dual citizenship ni sehemu ya huo wimbo🙁 tatizo ni elimu ya kukariri - tunakariri sana na kuimbishwa nyimbo ambazo hatujui maana zake🙁
 
kitu cha kwanza cha kufaham ni diaspora na dual citizenship ni vitu viwili tofauti, alafu wakat mwingine tusipende kumfurahisha kila mtu sababu ni kitu kisichowezekana. Dual citizenship is something very risky, let's not be blinded by investment. Hasara zinazoweza sababishwa na dual citizenship kwa nchi masikini na changa km TZ ni nyingi compared to faida. c kila kitu ni cha kuiga jaman kumbukeni hao wanao taka dual citizenship endapo mambo yatakwenda ndivyo sivyo wataikimbia TZ na kurudi kwenye nchi walizochukua uraia kwa maneno marahisi u can't get true patriot citizens through dual citizenship
 
kitu cha kwanza cha kufaham ni diaspora na dual citizenship ni vitu viwili tofauti, alafu wakat mwingine tusipende kumfurahisha kila mtu sababu ni kitu kisichowezekana. Dual citizenship is something very risky, let's not be blinded by investment. Hasara zinazoweza sababishwa na dual citizenship kwa nchi masikini na changa km TZ ni nyingi compared to faida. c kila kitu ni cha kuiga jaman kumbukeni hao wanao taka dual citizenship endapo mambo yatakwenda ndivyo sivyo wataikimbia TZ na kurudi kwenye nchi walizochukua uraia kwa maneno marahisi u can't get true patriot citizens through dual citizenship

Na ndio maana hawatatuhusiwa kugombea ktk baadhi ya nafasi za uongozi.lakini pia asilimia kubwa ya watanzania si wazalendo hilo si kwa sababu ya uraia pacha.umejionea posho inavyowatoa roho watu pale bungeni je hayo yanasababishwa na uraia pacha?
Tuwape nafasi ya watanzania waliopo nje ya Tanzania kuja kulitumikia taifa lao.mbona mnawapa uraia wasomali, waganda, waburundi, wahindi, na wengine wengi tu.tena eti kwasababu wameishi nchini miaka zaidi ya 10, na vita ikitokea bado watarudi makwao tu.iweje mtanzani aliyezaliwa Tanzania. Kasomea Tanzania kaolea Tanzania wazazi wake wote wanaishi Tanzania asipewe uraia wa nchi yake ma kumlazimisha aukane
Yaani mnawaamini wahindi kuwa ni wazalendo kuliko huyu mtanzania mwenye vinasaba vya pale KITETO ama CHILONWA?
 
Utakuwaje mzalendo kwa nchi mbili?! Chagua moja kusuka au kunyoa mkuu, hakuna kitu kinaweza nibadilisha utaifa wangu Abadan.

Utaifa na uraia ni vitu viwili tofauti. Utaifa akweli hauwezi kubadilishwa kama usivyoweza kubadili kabila au ukoo. Kwa upande wa utaifa, ukizaliwa Tanzania madhalani wewe utaifa wako ni wa Tanzania hata kama utabadili na kuwa raia wa nchi nyingine. Ndio maana unakuta ukiwa nchi za wengine (maana uraia hauandikwi kwenye paja la uso, lakini utaifa) wanaweza kukuuliza utarudi lini kwenu hata kama wewe ni raia wa nchi ile. Utaifa unabeba nasaba/asili ya mtu wakati uraia si lazima.

Ubaya wa sheria ya Tanzania ya sasa ni kuwa unapokana uraia wa Tanzania hapohapo unakuwa umeukana utaifa wako. Mkuu utaifa ni kitu rahisi kufahamika. Mtu wa taifa la India, Ujerumani, Uchina, Japan, Thailand, Poland, Misri, n.k. ni rahisi sana kufahamika. Lakini nchi hizo kama zinaruhusu uraia wa kujiandikisha ni vyepesi mno kuwa na raia ambao utaifa wao hauendani na nchi hizo.
Uzalendo nao ni zaidi ya kuwa raia wa nchi fulani. Si raia wote wa Tanzania ni wazalendo. Wako ambao si wazalendo maana hawako tayari hata kidogo kuifia nchi yao. Kama wewe huko tayari kuifia Tanzania wala usijisumbue kujihesabu kuwa ni mzalendo eti tu kwa sababu hujaukana uraia wa Tanzania, maana utakuwa unajidanganya. Na kwa taarifa yako kwa hali ya mambo ilivyo walio wazalendo wa kweli Tanzania ni adimu sana.
 
swala la kumzuia mtanzania asiwe na uraia pacha ni kumdulumu haki yake ya kuwa mtanzania,
nimezaliwa tanzania na ni raia wa tanzania nikienda nje ya Tanzania na nikaona kuna unafuu wa mambo kama vile elimu,afya,mikopo na mengineyo na sharti likawa ni kuwa raia,kwanini nisiombe uraia wa nchi ile,lakini wakati huo huo bado niendelee kuwa raia wa nchi yangu niliko zaliwa?
wanakuja wazungu na wahindi hawa hata kiswahili hawajui na bado wanapewa uraia wa Tanzania,yaani huyo anaaminiwa sana kuliko mie niliyezaliwa mpwapwa,nimekulia mpwapwa,nimesomea mpwapwa,nimeolea mpwapwa na kutafutia maisha nje ya Tanzania?


Ndugu katafiti tena wanaopewaga uraia huwa wanakuwa wameukana uraia wa huko wanakotoka.
 
Utakuwaje mzalendo kwa nchi mbili?! Chagua moja kusuka au kunyoa mkuu, hakuna kitu kinaweza nibadilisha utaifa wangu Abadan.

Utaifa na uraia ni vitu viwili tofauti. Utaifa akweli hauwezi kubadilishwa kama usivyoweza kubadili kabila au ukoo. Kwa upande wa utaifa, ukizaliwa Tanzania madhalani wewe utaifa wako ni wa Tanzania hata kama utabadili na kuwa raia wa nchi nyingine. Ndio maana unakuta ukiwa nchi za wengine (maana uraia hauandikwi kwenye paja la uso, lakini utaifa) wanaweza kukuuliza utarudi lini kwenu hata kama wewe ni raia wa nchi ile. Utaifa unabeba nasaba/asili ya mtu wakati uraia si lazima.

Ubaya wa sheria ya Tanzania ya sasa ni kuwa unapokana uraia wa Tanzania hapohapo unakuwa umeukana utaifa wako. Mkuu utaifa ni kitu rahisi kufahamika. Mtu wa taifa la India, Ujerumani, Uchina, Japan, Thailand, Poland, Misri, n.k. ni rahisi sana kufahamika. Lakini nchi hizo kama zinaruhusu uraia wa kujiandikisha ni vyepesi mno kuwa na raia ambao utaifa wao hauendani na nchi hizo.
Uzalendo nao ni zaidi ya kuwa raia wa nchi fulani. Si raia wote wa Tanzania ni wazalendo. Wako ambao si wazalendo maana hawako tayari hata kidogo kuifia nchi yao. Kama wewe huko tayari kuifia Tanzania wala usijisumbue kujihesabu kuwa ni mzalendo eti tu kwa sababu hujaukana uraia wa Tanzania, maana utakuwa unajidanganya. Na kwa taarifa yako kwa hali ya mambo ilivyo walio wazalendo wa kweli Tanzania ni adimu sana.
 
Siku zilizopita, katika mjadala kama huu niliwahi kutoa maoni yafuatayo. Pengine yanaweza kuwa mchango mzuri katika mjadala huu.

Wenye uraia wa nchi mbili Tanzania inawahitaji zaidi kuliko ambavyo wao wanaihitaji Tanzania. Tusichukulie tu kwamba kila mtu sasa ataruhusiwa kuwa raia wa nchi mbili, la hasha. Kikubwa katika hili ni kulinda utaifa wa Watanzania wenzetu waliochukua uraia wa nchi nyingine. Maana yake ni kuwa kama mtu amezaliwa akiwa Mtanzania basi asipoteze utaifa wake (yeye na uzao wake) hata kama atakuwa raia wa nchi nyingine. Haina maana kuwa raia wa nchi nyingine wanaoomba uraia wa Tanzania basi nao waruhusiwe kubaki na uraia wa nchi wanazotoka, hii si lazima.

Manufaa ya watu kuwa na uraia wa nchi mbili yapo.
Kwanza katika kusafiri nchi za watu ni vyepesi zaidi kwenda kama wewe ni raia wa nchi yao na zipo nchi kadhaa ambazo zinaruhusu uraia wa nchi zaidi ya moja. Raia wa mataifa yenye nguvu huja kwetu wapendavyo lakini sisi kwenda kwao shughuli yake pevu kabisa.

Pili, ni kuonyesha kuwathamini Watanzania popote walipo kwamba watabaki kuwa Watanzania. Jambo hili lina manufaa katika mipango ya watu hawa wanapokuwa na uhakika kuwa bado wanathaminiwa nyumbani pamoja na vizazi vyao. Kuna ambao wanaleta fedha kwa ndugu na jamaa zao na kuwa za manufaa mazuri tu. Lakini hali hiyo itapungua haraka sana kama vizazi vinavyofuata havitakuwa na mashikamano ya karibu na ndugu zao walioko Tanzania. Njia ya kuhakikisha kuwa mashikamano yanaendelea ni kuwaruhusu kuwa raia wa Tanzania.

Tatu, kuna faida nyingine ambayo ni nguvu ya ushawishi katika nchi walipo. Kwa mfano kama Tanzania inahitaji jambo fulani kutoka Kanada na kukiwa na jumuiya ya kutosha, inakuwa vyepesi watu hawa kuishawishi serikali ya Kanada kuwa na mtazamo mzuri kwa Tanzania. Lakini tukiwatupa eti walikwenda wakatukimbia basi hasira zetu hazitusaidii chochote. Sisi bado ni taifa tegemezi na tunahitai kila nguvu ya aliyezaliwa katika nchi hii hasa ikizingatiwa kuwa katika kundi hili wengi wana elimu nzuri (waliyoipata kwa kulipiwa na serikali ya Tanzania) na wengine wana mitaji mikubwa tu vyote ambavyo vinahitajika katika nchi hii. Tusiweke vichwa vyetu mchangani (kama mbuni) kwa kuwa tu eti mtu binafsi hatanufaika kwani kuna mambo mengi yamewekwa ambayo hayanufaishi Watanzania wote moja kwa moja. Kwa mfano si Watanzania wote ambao wanahitajji na kumiliki pasi za kusafiria, lakini zipo na zinawanufaisha wanaozihitaji na kwa namna moja au nyingine na sisi tusiosafiri tunanufaika kwa baadhi ya wenzetu kusafiri nje ya nchi.

Kuna mifano ya nchi zilizonufaika kwa raia wao kuwa nchi za nje na kuwatambua hata kama wamechukua uraia wa nchi nyingine. Kwa mfano, Poland ilinufaika sana na ujio wa raia wake baada ya siasa za Kikomunisti kufikia tamati kwa kuwa waliwatambua kama raia wa nchi yao hata kama walikuwa na uraia wa nchi nyingine. Chunguza manufaa ya nchi kama India na China katika nyanja hizi. Tena zingine wala haziweki kwenye sheria zao lakini wanatekeleza tu mambo yanayofanana na hayo. Sisi kwanini tujipige risasi mguuni? Kisa Chakubanga kapata uraia wa Marekani eti sasa yeye ni muasi au mhujumu. Kwani hata asipopewa uraia wa Tanzania nani atamzuia kuja? Hivi unajua idhini (visa) za kuingia kwa baadhi ya wageni zinatolewa sehemu wanayoingilia? Halafu unadhani kuwanyima uraia wa nchi mbili Watanzania wa kuzaliwa inatusaidia! mwee!

Tukiwakataa Watanzania walio nje (na kuwanyima uraia pacha) kwa vigezo potofu nao kuna siku tutawahitaji watatukataa vilevile. Kwani Waswahili wanasema; "Ukiniona wa nini, wewe wa kazi gani?"
 
Unajua sifa za kuupata uraia wa nchi nyingine kwa mjibu wa sheria ya sasa hapa Tanzania?

kwa nchi ambazo haziruhusu uraia pacha ni lazima ukane uraia wa nchi yako na kwa nchi zinazoruhusu uraia wa nchi pacha huna haja ya kuukana uraia wako,lakini kama nchi unayotoka kama Tanzania hairuhusu uraia pacha hakuna jinsi ni lazima uukane utane utanzania na kwa sasa tunapigania hili la kuukana utanzania lisiwepo.
 
Ndugu yangu kwa kila hali mimi sikubaliani na hiyo dhana ya uraia pacha - haiwezekani mtu mmoja akawa na uzalendo pacha. Loyalty cannot be divided.

hivi hujiulizi hawa wazungu tunaowapa uraia hapa Tanzania wao wanaendelea kutambulika kwao? sasa kama ni hivyo nini unakataa na nini unazuia?
 
Utakuwaje mzalendo kwa nchi mbili?! Chagua moja kusuka au kunyoa mkuu, hakuna kitu kinaweza nibadilisha utaifa wangu Abadan.

sasa kama hakuna kitu kinachoweza kubadilisha utaifa wako kwanini isiwe hivyo kwa watanzania wanaokwenda kutafuta maisha nje ya Tanzania nao wakazaidiwa ili UTAIFA wao ukaendelea kuwa vile vile kama awali?
 
Back
Top Bottom