Prof. Kabudi afunika bungeni

Prof. Kabudi afunika bungeni

Ameongea vizuri ila bahati Mbaya sijui kama ataweza kudumu kwenye utawala wa JPM,inaonyesha ni mtu mwenye msimamo wake na mawazo yake.Sijui kama atasurvive
...Hili angalizo lako pia amepewa na mbunge Mwita Waitara kwamba prof umeanza vizuri sana lakini tatizo huko mbele ya safari watakuvuruga
 
Mwenyezi Mungu amwepushe mbali na vile virusi angamizi vya akili vya haya Ma CCM..
Prof Paramagamba John Aidani Mwaluko Kabudi
 
Kuna yule mpindisha sheria za Serikali aliyepindisha sheria za nchi ili kumtesa Lema kwa kumnyima dhamana pia yeye huyo anayepigia kelele vyeti fake ameamua kuangalia pembeni kuhusu vyeti fake vya Bashite wa Kolomije, uvamizi wa Bashite pale Clouds lakini wakati huo huo kumfuta kazi Nape ambaye hakuwa na kosa lolote lile.

Huyu ni lazima afuate mistari ya asiyejaribiwa na pia awe muongo ili kuweza kudumu kwenye nafasi hiyo vinginevyo hana muda mrefu kwenye nafasi hiyo.

..mlinganishe Prof.Kabudi na Mzee wa "catalyst".

..uongozi, haswa wa kisiasa, hauhitaji mtu anayewaza kudhalilisha wenzake wakati wote.

..natumaini ustaarabu na utu uzima wa Prof.Kabudi utalisaidia bunge na serikali.

NB.

..pamoja na ustaarabu wa Prof sijapenda alivyofanyia mzaha suala la wanawake kupigwa. Prof akumbuke matamshi yake bungeni yanarekodiwa kwenye hansard.
 
Yes soma na utanue wigo sio lazima uwe professor pata tu knowledge ya kuweza ku -reason mbivu na mbichi.

Mtu anauliza watu wanalipwa loyalty hila awajui shughuli za mgodi anataka sheria itungwe. Hiyo sheria iruhusu kuwe na wafanyakazi wa halmashauri ndani ya migodi ama anatakaje?

Halafu huyo mtaalamu tunaemsifia anashindwa ata kuelezea ya kwamba hizo kampuni zinakuwa audited kisheria na external accounting firms pamoja na government auditors. Kama wanadhani wanadhulimiwa kwenye mirahaba wanaweza omba income statement za shirika na kuangalia wenyewe.

Mtaalamu wa sheria awezi kutoa jibu kama hilo; sasa ndio mtaalamu gani na utaratibu wa ukaguzi wa mapato upo.

Hayo mengine ya umri, sijui kupigana khaa ivyo vitu vina vyanzo vya asili kwanini watu waendelee amini kama jamii inaona vitu vingine ni abuse bado tu utete asili zilizopitwa na wakati na illogical.

Tupende kusoma jamani ndio maana hawa jamaa wakishakuwa na Phd wanajiona miungu watu wakati mwingine tunasifia vitu ambavyo too basic wanafunzi wanafundishwa at introduction levels.
 
Je, ni sahihi kwa nchi kuwa na sheria ambazo zina favour baadhi ya makabila? Iweje kuwe na sheria zenye vifungu vinavyo-favour ukabila halafu Tanzania kusiwe na ukabila?

Kulikuwa na haja gani ya kujipambanua kuwa yeye ni Prof. wa sheria?

'kwa bahati mbaya' ila kwenye Kiswahili hakuna bahati mbaya. Sasa alitamkaje hilo neno kama hakuna kwenye Kiswahili?

Katoa factors za kubadilisha au kutunga sheria na kuziacha nyingine halafu alikuwa amesahau hiyo ya wa Maasai na Mabohola as if wao muda umesimama.

Je, hiyo sheria ya ndoa bado serikali ina negotiate na Wamaasai na Mabohola?


Ndio hapo sasa. Anatuambia Kiswahili hakina "bahati mbaya" wakati yeye ndio kasema "bahati mbaya"!

Eti sheria ya kuruhusu watoto kuolewa iliwekwa kuwa accomodate Wamasai na Mabohora kwa sababu na wao pia ni Watanzania wenzetu. Kwa hiyo culture yeyote ya "Watanzania wenzetu" tunaikubali? Mbona kukeketa wanawake imepigwa marufuku?

Thinking capacity ya Waziri Kabudi ni very suspect, na si mkweli, eti nchi hii wanaooza watoto wadogo ni Wamasai na Mabohara peke yao! In most of all the peasant communities in the rural countryside mtoto akifeli darasa la saba na umri wa miaka 13 anakaa hapo nyumbani anafanya nini, next ni KUOLEWA! Kabila gani hawafanyi hivyo?

Family Law professor hujui hilo au umeamua kujisemea tu kwa vile umewa underestimate sana wabunge ukaona unaweza kusema lolote likapita?
 
Magufuli anatisha sana. Maana ma prof ma dokta aliowateua ndio wanaonyesha huu uwezo
Hatutaki majibu mazuri bungeni blah blah nyingi tunataka action watu wanatekwa kuna ukatili wa haki za binadamu wanaohusika wachukuliwe hatua
Waziri anabaki kujibu katiba inapinga vikali kwani sheria ikiwepo hakuna wataokaoivunja???

Hii miandiko kutoka Lumumba ina tabu sana hiyo pesa unayolipwa kwa kueneza propaganda kula ila ujue kuwa Nchi haiendeshwi kwa siasa (Majibu marahisi kwenye maswali magumu majukwaani) Nchi inapelekwa mbele kwa vitendo, nia na dhamira ya kweli isiyokuwa na chembe za ushabiki hata kidogo
Naionea huruma TANZANIA nawaonea huruma wakina mama wanaoongwa doti ya kitenge kwa lengo la kupata ridhaa ya wananchi
Kwa viongozi tulio nao pande zote kila mtu ni msakatonge hakuna mwenye dhamira ya kweli na kuumia rohoni kuhusu hali ya mtanzania mmoja mmoja hali ni mbaya sana watanzania wanateseka na kufa kwa matumaini ya kuletewa ahueni na kiongozi fulani

Mzee Mengi Mungu akubariki kila siku naiosoma hii tweet napata sononeko la moyo najua na wewe pia unaumia
Najua literally ulikuwa unamaanisha nini
027c21e1edfa7e9a781a14f9f23d49c9.jpg
 
mlugo bado anaendelea kuonyesha ukilaza wake... eti elimu ya lazima ni chekechea mpaka kidato cha nne!!!
Ndivyo sera mpya ya elimu inavyosema. Au wewe Ni mgeni nchi hii? Mmesema kuanzia chekechea hadi kidato cha nne inaitwa ELIMU MSINGI na Ni ya lazima. Japo sijajua utekelezaji wake utakuwaje lakini ndivyo ilivyo.
 
Mzee...baadhi ya wabongo huwa wanakuwa impressed na vitu vidogo vidogo na vya kawaida mno.

Hapo hujamwona Pasco....si ajabu akakwambia jamaa ni bonge la 'kichwa'...whatever the hell that is...

Ndivyo tulivyo
Kweli kabisa. Nimesikiliza kwa bidii nipate hicho kitu cha ziada kilichosifiwa.
 
Ukweli ni kwamba mawaziri wanapaswa wasiwe wabunge,hizi teuzi za Jpm zimeonesha umuhimu wa kuwa na waziri mbobezi wa sector husika,na kwa Tz wasomi wengi wazuri hawajihusishi na siasa,hivyo kuna umuhimu wa kuwaingiza katika hizi nafasi ili watoe mchango wao ktk maendeleo ya taifa
 
Kajifundishe bunge linavyofanya kazi
Swali la msingi hutolewa mapema na waziri hupewa muda wa kuandaa majibu ila maswali ya nyongeza ni ya hapo kwa hapo hivyo mtu majibu huwa hajaandaa majibu
 
Njaa kitu kibaya, hatari mno.

Ameongea utani na mipasho ya kutetea serikali.

Kifupi kaulizwa kwa nini sheria zilizopendekezwa zibadilishwe na Tume ya 1980 zipo mpaka leo?

Jibu lake, kasema, kwa anavyojua yeye kama profesa wa sheria, na muelewa wa mambo ya legal anthlopology, ni kwamba sheria zinazohusu mambo ya kimila, kiitikadi, kidini, kijima, hazibadilishwi kwa kukurupuka.

Akaendelea kusema, ndio maana mpaka leo kwao yeye Waziri wanakeketa vitoto vya kike, na pia kwao mbunge muuliza swali, ambae ni Mkurya, wanawake zao hawapendeki bila kupigwa. Kwa hiyo sheria hizi inshallah zitakuja kubadilishwa. Ndio maneno ya waziri hayo.

Hapo kwenye jibu hilo kuna weledi gani wa kusifiwa?
Huna akili ndugu....ungepita udsm faculty of law ungemfahamu...kwa kuwa nyinyi mmesoma maporini bakini kama mlivyo nyambaf
 
Mtoa post haukumuona mligi na lucy mayenga wametoa macho hapo hawaelewi kitu......wanasubiri segiment ya matusi tu
 
Unasifia kuwa hana lugha ya kuudhi kisha wewe unatumia lugha ya kuudhi " Sugu .." We wa ajabu kweli.
 
Dr. Mwakyembe nae si aliteuliwa na Joseph photunatus Mohammed au? Kuna dokta uchwara balaaa
 
Ndoa bila cheti cha kuzaliwa hakuna. Walai makanizani na misikitini wangesahau kama kuna kufungisha harusi
 
Tatizo lenu hamna original thinking; you can't make it with reactionary strategy of doing politics. You need to be original. Hivi kuna Mtanzania mwenye akili timamu anaweza kubeza uamuzi wa Serikali kuhakikisha nchi inakuwa na shirika imara ndege (national flag bearer). Nyie sijui mmelogwa na nani. Ndege zimenunuliwa kiwandani kwa mtengenezaji ili kuepuka madalali vishoka wapigaji kama ilivyokuwa wakati wa ununuzi wa radar na ndege ya Rais (2003). Kuweni original thinkers ili watu wenye intellect waweze kuwaunga mkono vinginevyo mtaishia kunawa tu, basi.
Kwa hiyo wewe na iq yako kwa sasa bombadia ndio kipaumbele cha watanzania walio wengi!! Kama ni hivyo basi sawa tuwasubiri kipindi cha kampeni. Hivi USA ina shirika la ndege la kibiashara la serikali? Naomba kujuzwa tu
 
Back
Top Bottom