Prof. Kabudi afunika bungeni

Prof. Kabudi afunika bungeni

Mwalimu wa Family Law wa muda mrefu chuo kikuu cha DSM
 
Profesa Kabudi ni namba ingine kwenye kitivo cha ufaulu wake WA digrii ya sheria chuo kikuu cha dar es salaam rekodi yake ya ufaulu haijawahi vunjwa na yeyote toka Tanzania ipate uhuru hadi leo kwa yeyote anayesoma digrii ya sheria. Mwanae pia aliweka rekodi ya ufaulu chuo kikuu cha ardhi ambayo haijawahi vunjwa tokea Tanzania ipate uhuru na haijavunjwa hadi Leo. Huyo huwezi mshindanisha na wapiga yowe na makelele Kama akina Lisu, mbowe, akina lema na Sugu the music rapper.Mwingine mwenye akili kupindukia ni profesa Lipumba alivunja rekodi ya ufaulu kwenye digrii ya uchumi chuo kikuu cha dar es salaam ambayo toka uhuru hadi sasa Hakuna mtanzania aliyevunja rekodi ya Lipumba
Profesa yupi huyu huyu anayelala ofisini?
 
and why mention Sugu... kwa nini usimtaje naibu spika kwamba ndiye anatoa macho

Naibu spika anayajuwa hayo Kwa Kuwa ni daktari wa sheria,sugu yeye hutoa macho na kusubiria kuonesha kidole cha kati.
 
huyu hana maisha marefu ktk hiyo nafasi maana ccm haitaki watu wa aina kama ya kabudi waingie ktk vyombo vya maamuzi.mda utaongea
 
Umemsifia sana lakini naomba nikuulize kwa nini maswali ya nyongeza ya Mh Mulugo amejibu kwa kusoma majibu? Ina maana hata hayo maswali ya nyongeza alishapewa hivyo ni kiini macho
Kwa mfano hayo maswali hata ungepewa na majibu yake ungekuwa mahiri kama Professor kwa mfano!
 
Profesa hatumpimi kwa kuongea au kukariri historia, profesa anapimwa kwa kazi zake zilizoleta msaada kwa jamii na kutatua matatizo hususani kwa taifa kama hili ambalo watu wake bado wanaishi stone age...
 
Mwalimu wa Family Law wa muda mrefu chuo kikuu cha DSM

Kama ni mwalimu wa Family law basi anapaswa kujua kwamba ndoa za utotoni ni mbaya hata kama hazibagui wavulana na wasichana.

Huwezi kutetea ndoa za watoto eti kwa vile sheria inaruhusu hata vivulana vya miaka 14 kuoa. Kwa hiyo ni sawa kwa vile inaumiza hata vivulana?

Hauko tena darasani mbele ya watoto wa chuo , tunategemea Waziri ujenge hoja makini mbele ya Bunge na wananchi.
 
Hakika taifa na bunge la JMT linahitaji watu aina ya huyu profesa!

Mosi, ana uwezo wa hali ya juu wa kujibu hoja bila kuudhi.

Pili, ni ubobezi katika eneo husika la sheria anateleza tu na vifungu mpaka raha.

Tatu, matumizi ya lugha ya kiswahili mwanana anapiga misamiati mpaka baadhi ya wabunge kama sugu wanatoa macho.

Mwisho kabisa, anaonekana ni msikivu na mnyenyekevu kwa wabunge wote hata upinzani. Watanzania tunahitaji wabunge na mawaziri wa namna hii kwa kweli.

Mungu amsimamie afike mbali.

Tazama video ya majibu aliyoyatoa leo bungeni,lazima umkubali.

Pole kwa kutumika vibaya,ila ujue ni dhambi kutumika vibaya hasa kwa upotoshaji.
 
Kujibu maswali uliyoyaandaa kujibu si kazi ngumu kama maswali ya papo kwa papo anayoulizwa waziri mkuu majaliwa
 
Back
Top Bottom