Mh Prof Janabi, hongera kwa kazi nzuri kwa Taifa lako Teule na nina kushukuru sana kwakuwa msomi unaye itumia elimu yako vyema kwa jamii yako.
Prof Janabi nilifurahi sikia uteuzi wako ila roho ikaniambia nisifurahi sana ila nikukumbushe kufungua macho nakutafakuri juu ya safari yako.
Tafadhali rejelea zile sifa na huu uzi
Jamani kama kuna wazee hili Taifa wenye kutia neno Mimi naomba mnisikilize na mtakuja sema Taifa lina manabii. Prof Janabi ni kiongozi hanijuwi simjuwi ila kwa kazi anazifanya na uzalendo wake kwa watanzania Mimi nawaomba huyu jamaa apewe form atatupeleka kuwa nchi ya maziwa na asali. Kule...
www.jamiiforums.com
Prof Janabi wewe ni muislam na ktk dini yetu ya kiislam kuna mafundisho ya elimu ahera na elimu dunia.
Sina uhakika kama umewahi soma juu ya elimu ya viumbe kama majini na viumbe vingine.
Leo nataka kidogo nikugusie.
Prof Janabi sio kila kinacho meremeta basi kinaweza kuwa kweli vipo viumbe ukiviona kwa mbali waweza tamani kuvigusa ila ukaribiapo ndipo ukutanapo na dhoruba.
Prof Janabi mimi ni mmoja wa wanafunzi wako wa youtube ila pia nimtu nimetokea kukubali sana hasa akili na uwezo mwenyezi Mungu amekupa.
Natamani Mungu wa Mbinguni akufunulie kesho yako na akuonyeshe mitego ya wanadam inayo fanana na maua mazuri.
Prof Janabi utakubaliana na mimi moyo wako umebeba mambo mazito yakitaifa na kidunia tena mambo yasiri jambo linakutenga na wanadam. Mola akupe subira. Mola akupe imani kama imani Ya mh Jaji Mkuu wetu.
Prof Janabi sijuwi kabila lenu ila nenda kwa wazee wanyumbani kwenu na kwenye makaburi ya wazee wa nyumbani kwenu maana wana neno juu yako.
Toa sadaka kwa wazee wanyumbani kwenu na sadaka nyingine kwa maana wana neno zito juu yako. Utakapo toka huko utakuja ukiyaona ambayo hukuwa unayaona na kuyasikia ambayo hukuwa una yasikia.
Mkwere kwenye hotuba yake hadimu aliwahi sema "ukipenda pigiwa makofi basi usiogope kuzomewa"
Prof Janabi kuna jambo zito mbele yako na nilazima ulishinde Inshallah mimi nakutakia heri. Amina☆☆☆