Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Siasa za kipuuzi kabisa. Hakuna mikopo kwa kutegemea posho za vikao maana mbunge hulipwa posho baada ya kuhudhuria kikao. Mkopo unatokana na mshahara na posho ya Ubunge ambayo inafikia tshs 5m kwa ajili ya mafuta 2m, kuendesha ofisi nk. Pia mshahara 2.3m! Hakuna mbunge anayeruhusiwa kukopa kwa kutumia posho za kujikimu au za vikao. Hizi ni propaganda za kitoto na zisizo na maana yeyote ambazo wala haziwezi kuzuia uzito wa hoja ya kufuta allowances za vikao.
CRDB nao ni wajinga tu kutoa taarifa kwa serikali au dailynews. Hata hivyo sishangai hata kidogo kwani crdb ndio benki iliyotumika kupitisha fedha za epa zaidi ya benki yeyote. Pia ndio benki inayoongoza kwenye wizi wa fedha za stimulus package.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Wako wapi wale Pro-Chadema walikuwa wanapinga eti hakuna benki inayoweza kutoa mikopo kupitia posho, LAT na wenzako mpooo???

Mkuu hii si mambo ya pro-chadema, logically huwezi kukopa kupitia posho ambayo kupoata kwake ni mpaka uhudhurie hivyo vikao ina maana ukiumwa hupati hiyo posho. Na posho anayoizunguimzia Zitto hutolewa tu pale kunapokuwa na hivyo vikao vya bunge. Je bunge linakaa kila siku au kila mwezi?
 
[ mbunge Mama Madabida, aliwashutumu wabunge wa upinzani kwa kuuiba hoja ya posho baada ya kuikuta kwenye kamati, hivyo kuiteka hoja.]
.

Kama kweli CDM wameiba hii hoja toka ccm basi nawapongeza sana, tena sana na ningeshauri wapitie kwa umakini viji-kabrasha vya ccm na watakapobaini hoja nzuri zenye maslahi mazito kwa taifa basi wazibe - zoooote kabisa. Siku zote ccm wamekuwa wanatundanganya kwa speeches zenye maneno kama 'serikali ina mpango kabambe' mara serikali imedhamiria kuondoa kero' n.k baada ya speech hakuna chochote, makaratasi yanaishia kabatini. Only now, for the first time in the history of this country tunapata wanasiasa wanaosimamia kile wanachosema. Kwa nini basi tusiwaunge mkono wanachama wa aina hiyo? ccm your time is up- mmefilisi hili taifa kwa nidhamu ya woga na mufilisi wa maadili.
 
Sioni sababu ya kuwashinikiza wabunge wa Chadema wasichukue posho hiyo kabla haijaondolewa, kinachopiganiwa posho hiyo iondolewe si kwa wabunge tu ila watumishi wote wa umma, kwa nini mnakomalia tu wabunge wa chadema wasichukue? Hamna uchungu na nji hii, duh!

Mkuu nakuunga mkono kwamba posho ziondolewe kwa watumishi wote wa umma. Lakini sasa CHADEMA wameanzisha hili kwa nia njema kabisa basi waonyeshe kwa vitendo kwamba hawazitaki kama alivyofanya Zitto. Kama wote watazikataa Waziri Mkuu atatoa wapi ujasiri wa kusema wabunge wa CHADEMA wanazimezea mate? Kwa kuwa CHADEMA wana ushawishi mkubwa hapa nchini basi wabunge wao wote kwa umoja wao wajitokeze hadharani na kupinga posho hizo na si kuachia mbunge mmoja mmoja. Au kwa hili la posho CHADEMA hawapo pamoja? Tuambiane ukweli tusipakane mafuta kwa mgongo wa chupa.
 
Siasa za kipuuzi kabisa. Hakuna mikopo kwa kutegemea posho za vikao maana mbunge hulipwa posho baada ya kuhudhuria kikao. Mkopo unatokana na mshahara na posho ya Ubunge ambayo inafikia tshs 5m kwa ajili ya mafuta 2m, kuendesha ofisi nk. Pia mshahara 2.3m! Hakuna mbunge anayeruhusiwa kukopa kwa kutumia posho za kujikimu au za vikao. Hizi ni propaganda za kitoto na zisizo na maana yeyote ambazo wala haziwezi kuzuia uzito wa hoja ya kufuta allowances za vikao.
CRDB nao ni wajinga tu kutoa taarifa kwa serikali au dailynews. Hata hivyo sishangai hata kidogo kwani crdb ndio benki iliyotumika kupitisha fedha za epa zaidi ya benki yeyote. Pia ndio benki inayoongoza kwenye wizi wa fedha za stimulus package.

Mkuu nadhani uandike press release kutoa ufafanuzi kabla huu upuuzi haujasambazwa, na kwa nnavyozijua siasa za bongo issue hapo si kukopa bali nikukopa hizo milioni 150 au 200, this is the centre of the story. They know how poor people are (Ila hawataki kujihangaisha kujua nini sababu ya umasikini huo na namna gani ya kuepukana nao) kwa hiyo wakitaja hayo mamilioni ni katika kuwafanya wananchi wawe na doubt na kazi mnayoifanya. Otherwise Big up na keep it up bro!
 
Mwongo mkubwa.

Yeye mwenyewe Mnyika kasema "...Posho ya Kikao (Sitting Allowance) ambayo inalipwa hivi sasa kwa kuwekwa kwenye akaunti za wabunge moja kwa moja... " Hela wanaingiziwa moja kwa moja kwenye akaunti, hakuna aliyeirudisha!

You see, uzuri wa John Mnyika hasemi semi uongo most of the time. Mnyika kafananisha posho na nyama tamu, na kuacha posho kasema ni kama kumsusia fisi bucha yako ya nyama.

"Kabla ya kubadilishwa kwa mfumo mzima wa posho si jambo lenye maslahi ya umma kuziachia posho hizo zikatumiwa kiubadhirifu na serikali inayoongozwa na CCM badala yake ni lazima kuweka mazingira ya kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwenye masuala ya kimaendeleo kinyume na hapo itakuwa ni sawa sawa na ‘kumsusia fisi bucha.'' Chanzo

Kwa hiyo Mnyika hakatai kwamba huwa anakula posho, mikopo, mishahara, hela za mashangingi, wewe taja. Simtengenezi haya mambo, namnukuu:

"Nilichukua pia msimamo kama huo kwenye suala la mikopo ya magari ya wabunge, wakati wa kampeni nilipinga kiwango cha mikopo kinachotolewa cha milioni 90 kwa ajili ya gari kuwa ni kikubwa; na baada ya kuchaguliwa nilipewa mkopo huo na kuupokea." Chanzo

Hahahahahahaha....... Siasa za Tanzania na viongozi wetu zinatia udhia na machungu kupindukia lakini kwa sababu watu wazima haturuhusiwi kulia unaishia kucheka. John Mnyika, among the best and the brightest in the annals of our political leadership anakwambia ana msimamo mkali wa kupinga mikopo ya mashangingi lakini ukimpa atakula!

Hii nini sasa? Kumbe Mbunge wangu Mnyika alituongopea kwenye kampeni? Anatenda asiyoyaamini? Jamani fedha fedheha hawakukosea wahenga!
 
Siasa za kipuuzi kabisa. Hakuna mikopo kwa kutegemea posho za vikao maana mbunge hulipwa posho baada ya kuhudhuria kikao. Mkopo unatokana na mshahara na posho ya Ubunge ambayo inafikia tshs 5m kwa ajili ya mafuta 2m, kuendesha ofisi nk. Pia mshahara 2.3m! Hakuna mbunge anayeruhusiwa kukopa kwa kutumia posho za kujikimu au za vikao. Hizi ni propaganda za kitoto na zisizo na maana yeyote ambazo wala haziwezi kuzuia uzito wa hoja ya kufuta allowances za vikao.
CRDB nao ni wajinga tu kutoa taarifa kwa serikali au dailynews. Hata hivyo sishangai hata kidogo kwani crdb ndio benki iliyotumika kupitisha fedha za epa zaidi ya benki yeyote. Pia ndio benki inayoongoza kwenye wizi wa fedha za stimulus package.

Simamieni kilicho sahihi,mnaungwa mkono na wananchi na wanaharakati. Hakuna mapambano rahisi kama haya yanayohusisha mfumo wa ubabishaji na propaganda. Hivi ndivyo vimetufikisha hapa miaka 50 hatuwezi ku balance bajeti yetu.

Mh, hivi CRDB waliwasiliana na wateja (wabunge) kwanza kabla ya kutoa taarifa!
 
Muda si mrefu watakubaliana na hiki kinachopigiwa kelele kuhusiana na posho.
 
Nyie Pro-Chadema msiwe kama makinda ya bata yanamfata mama yao ata popote anapokwenda kama anavuka barabara. Hawo viongozi wenu wameishachukuwa mikopo benki kupitia hizo posho wanazozisema tena wa kwanza kuchukuwa ni Mbowe 200 milioni Zitto 150 milioni, mdhamini wao ni ofisi ya katibu wa bunge
Hatupingi posho kwa sbbu cdm wanapinga na hatutaunga mkono posho kwa sbbu cdm wanaziunga, POSHO ZIONDOLEWEEEEEE! Hata ccm wakiamua kusimamia hilo tutawaunga mkono.
 
Magamba wameona wameshikwa pabaya ndo maana wanaweweseka. Mangapi yemewekwa kwenye mipango ya serikali na yakishia kimya kimya? Nilipomsikia huyo mbunge Madabila nilipatwa na kichefuchefu watu wanazungumzia sitting allowance ye analeta hoja ya mdkatari sijui walimu kujikimu.
Mi nawaambia bila kulipigia kelele hili lingisha kimya kimya tu.
 
Wanabodi,

Miongoni mwa wachangiaji kwa simu ni Mhe. Zarina Madabida, aliiweka wazi kuwa suala la posho liko kwenye hotuba ya bajeti. Naye alitetea msimamo wa kuwepo kwa posho muhimu na kutolea mfano posho za madakitari na uwepo wa per diem. Huyu mbunge Mama Madabida, aliwashutumu wabunge wa upinzani kwa kuuiba hoja ya posho baada ya kuikuta kwenye kamati, hivyo kuiteka hoja.
Suala si kuteka hoja bali ni uhalali wa hizo posho. posho za vikao (sitting allowance) ni wizi, narudia tena ni wizi. hata kama zimeainishwa kwenye sheria... aidha naomba niambiwe ni sheria gani imehalalisha sitting allowance. narudia tena, tunaomba tufahamishwe sheria gani inahalalisha sitting allowance. kipengele cha katiba (No. 73) alichotumia Pinda kujibu hoja kipo general kinataja posho, hakitaji sitting allowance. kwa hiyo wahusika waepuke majibu rahisi, watuambie WAPI WAMEANDIKA SITTING ALLOWANCE KWENYE SHERIA. hata kama ipo ni wizi kwa sababu wahusika wanalipwa mshahara kwa ajili ya kazi hiyo.
Na kama sheria ipo mbona fedha za wafadhili wanazotoa hawazitumii kulipa sitting allowance; ukilipa sitting allowance kwa kutumia fedha za DANIDA au USAID lazima utaambiwa uzirudishe!!
Viongozi wa serikali muache kutudanganya; wabunge wa CCM muache kutudanganya na pia muache unafiki!! acheni acheni acheni. na acheni kutumia wananchi kama mtaji wenu.. eti kuna wananchi wapo mlangoni mwa bunge wanasubiri hizo posho zenu,. kumbuka msemo huu - usitoe samaki, bali mfundishe jinsi ya kuvua samaki.
 
Siasa za kipuuzi kabisa. Hakuna mikopo kwa kutegemea posho za vikao maana mbunge hulipwa posho baada ya kuhudhuria kikao. Mkopo unatokana na mshahara na posho ya Ubunge ambayo inafikia tshs 5m kwa ajili ya mafuta 2m, kuendesha ofisi nk. Pia mshahara 2.3m! Hakuna mbunge anayeruhusiwa kukopa kwa kutumia posho za kujikimu au za vikao. Hizi ni propaganda za kitoto na zisizo na maana yeyote ambazo wala haziwezi kuzuia uzito wa hoja ya kufuta allowances za vikao.CRDB nao ni wajinga tu kutoa taarifa kwa serikali au dailynews. Hata hivyo sishangai hata kidogo kwani crdb ndio benki iliyotumika kupitisha fedha za epa zaidi ya benki yeyote. Pia ndio benki inayoongoza kwenye wizi wa fedha za stimulus package.
Zitto, Wewe kweli umechukuwa mkopo benki na ofisi ya katibu wa bunge ndio mdhamini wako? Tunaomba utuweke sawa kwenye hili swala
 
Kama kweli CDM wameiba hii hoja toka ccm basi nawapongeza sana, tena sana na ningeshauri wapitie kwa umakini viji-kabrasha vya ccm na watakapobaini hoja nzuri zenye maslahi mazito kwa taifa basi wazibe - zoooote kabisa. Siku zote ccm wamekuwa wanatundanganya kwa speeches zenye maneno kama 'serikali ina mpango kabambe' mara serikali imedhamiria kuondoa kero' n.k baada ya speech hakuna chochote, makaratasi yanaishia kabatini. Only now, for the first time in the history of this country tunapata wanasiasa wanaosimamia kile wanachosema. Kwa nini basi tusiwaunge mkono wanachama wa aina hiyo? ccm your time is up- mmefilisi hili taifa kwa nidhamu ya woga na mufilisi wa maadili.

Ni hawa hawa juzi tu walituambia wanawapa Magamba siku 60 Wajiondoe, mara wakabadilisha wakasema siku 90, leo KIMYA hatusikii kama kuna gamba wala nini! WAMEJIGUNDUA KWAMBA WOOOTE NI MAGAMBA TUU NA HAKUNA WA KUMVUA MWENZIE.
 
elimu yangu ya mikopo ni ndogo saaaaana ila ninachojua ni kwamba collateral ya mkopo bank kama si mali isiyohamishika basi ni prove ya mshahara (sio posho) wako ambao wao wana-centre kwenye Pension yako ndio maana hata ukiwa mfanyakazi unapata mshahara wa 100Million/month kama hukatwi pension hukopeshwi (NMB na CRDB) so nakataa kwamba posho inayozungumziwa na wapinzani (sio CDM pekee) eti ndio collateral ya mikopo yao benki.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Katika nchi hii, mipango imekuwepo wakati wote lakini hakuna chochote kinachotekelezwa. Kwangu mimi mipango haina maana, na yeyeote anayeelezea mipango tu bila kutekeleza ni sawa na asiyefanya chochote. TUANGALIE ANAYETENDA. CCM na serikali waliliweka suala hilo kwenye mpango wa miaka mitano ambao nao ni mpango hewa, baada ya Mh. Dr Slaa kulizungumzia sana katika bunge lililopita. Waliichukua hoja lakini hawakuwa na dhamira yoyote ya kuitekeleza, waliliweka kwenye maandishi kama kiini macho tu ili kila wakati hoja hiyo ikiletwa waweze kutamka kuwa hilo suala tumeliweka katika mipango yetu.Kama kweli serikali ilikuwa na dhamira, ilitakiwa wafurahie sana baada ya kuona CHADEMA wanataka uamuzi wa kufuta sitting allowance uanze kutekelezwa mara moja. Kama walikuwa na dhamira, basi tunawaambia waanze kutekeleza sasa. Kama waliweza kubadilisha kanuni za bunge kuhusiana na upinzani rasmi bungeni ndani ya siku tatu, wanashindwa nini kuondoa na kufuta kanuni na sheria zinazoruhusu wizi wa fedha za umma ndani ya masaa 24. Hata bila ya kufuta kanuni zilizokuwepo, inaweza kuundwa kanuni na sheria itakayotamka kuwa malipo yeyote kwa mfanyakazi yeyote wa umma zaidi ya mshahara wake, posho ya kujikimu, posho ya nyumba, usafiri, matibabu, --------- (na kuacha kuitamka sitting allowance), ni wizi. Basi kuanzia hapo atakayepokea posho au kutoa posho zaidi ya zile zilizoanishwa akamatwe na kushtakiwa kwa wizi.
 
Hata kama lilizungumziwa kwenye kamati, inaonesha wazihawakulikubalia. Kwani Waziri Mkulo na wengine wanaoshughulika na wizara ya fedha si wajumbe huko? Mbona haijareflect bajeti, pamoja na kueleza katika bajeti kuwa watapunguza posho mbalimbali zisizo na msingi, figures ndiyo kwanza imeongezeka (toka bilioni 500plus mpaka bilioni 900 plus) na bila kueleza posho zipi zitapunguzwa. Kama kweli ingekuwa ni agenda yao, basi tungeona imefanyiwa kazi na kubainisha ni posho zipi zimedhamiriwa kutolewa. Ni aibu kubwa kujilipa posho kwa pesa yetu yote ya makusanyo ya ndani, huku miradi muhimu ya maendeleo tukitegemea kutoka kwa wafadhili kwa masharti lukuki ya kutufunga.
 
  • Huyu mbunge anayesema CDM wameiba wazo la CCM anamaanisha nini?
  • Kwani huu mpango wa miaka mitano unaanza lini mbona mi mnanichanganya! Kama unaanza hii 2011 na swala la kuondoa posho imekubaliwa lianze lini? Kama linatakiwa kuanza kwa pamoja ningetegemea kuona reflection yake kwenye bajeti ya 2011/12 ambayo kila Mwana-CCM anaiunga mkono 100%.
  • Mpango huu wa miaka 5 una bajeti yake au ni hii hii?
 
Mngeungana wabunge wote wa upinzani ingekuwa na nguvu zaidi kuliko ilivyo sasa kwa Chadema only
 
Wanabodi,
Mjadala wa Posho za Wabunge, umerindima kwenye kipindi cha Baragumu ambacho kiko live Channel Ten wakati huu ninapoandika post hii. Mgeni mwalika ni Katibu Uenezi wa CCM, Nape Mnauye na mchokoza mada ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyechokoza mada kwa njia ya simu.

Mtoa hoja ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amefafanua vizuri sana msimamo wa Chadema na kujielekeza suala la posho za Wabunge, ni suala mtambuka zaidi ya posho za wabunge pekee bali ni posho za watumishi wote wa umma kwa ujumla wao, zikikatwa zitaokoa zaidi ya Shilingi Bilioni 900. Mhe. Mbowe, amekwenda mbali zaidi na kufafanua kwa nini Chadema inapigania kufutwa kwa posho hizo na sio kila posho lazima ifutwe, posho kama za kujikimu ni posho muhimu hivyo Mbowe amesema hana tatizo nazo.

Pia Mheshimiwa Mbowe ameweka bayana suala la posho lisionekana ni la Wabunge wa Chadema tuu, linapaswa kuwa ni suala la bunge lote kwa sababu linahusu maslahi ya taifa. Mbowe akasisitiza ukiweka maslahi ya taifa mbele badala ya maslahi binafsi.

Ilipofika zamu ya Nape, aliunga mkono hoja ya Mbowe kuwa kuna posho za lazima na zile ambazo sio za lazima. Amekubaliana na Mbowe kuwa posho ya kujikimu ni posho ya lazima, hivyo iendelee kuwepo. Mhe. Nape, amekwenda mbali zaidi kwa kueleza dhamira yake ya dhati kupunguza gap kati ya wenye nacho na wasio nacho. Amekiri wafaidika wa posho ndio wale wale wenye mishahara minono na marupurupu kibao. Amesisitiza hoja siyo ya Chadema, hoja iko kwenye ule mpango wa miaka 5. Amesema unaungana na hoja za kufutwa kwa posho ambazo sio za lazima, ila kwa vile posho hizo zipo kisheria, basi kuondolewa kwa posho hizo kufuate utaratibu.

Miongoni mwa wachangiaji kwa simu ni Mhe. Zarina Madabida, aliiweka wazi kuwa suala la posho liko kwenye hotuba ya bajeti. Naye alitetea msimamo wa kuwepo kwa posho muhimu na kutolea mfano posho za madakitari na uwepo wa per diem. Huyu mbunge Mama Madabida, aliwashutumu wabunge wa upinzani kwa kuuiba hoja ya posho baada ya kuikuta kwenye kamati, hivyo kuiteka hoja.

MY TAKE.
Mbowe amejieleza vizuri sana kwenye hili suala la posho. Nape pia is good, anasimamia maslahi ya taifa.

Mama Madabida ni Kihiyo. Hajui ni Lini ILANI ya CHADEMA iliandikwa na ni lini MPANGO wa MAENDELEO UMEANDIKWA ndio maana siwapendi Wabunge wa CCM kwa sababu hawapendi kujisomea
 
Back
Top Bottom