Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Nyie watanzania wenzangu ukweli nisawa na jua haufichwi ukafichika. Hoja ya CHADEMA niyamsingi sana kwa maslahi ya taifa letu, najua kunawatanzania wanaweza kulipwa au kuwalipa watu ili kupotosha msingi wa hoja hii ya posho. Mimi nawashauri kabla ya kuifanya kaz hiyo wafirie juu ya hatma ya taifa letu na vizaz vijavyo, kurundika pesa kwa wanasiasa, watawala na kuwanyima civil servant, kutumia vyombo vya dola kuwatishia na kuwajeruhi. JE UMMA UTAVUMILIA MPAKA LINI HALI HII? Tunaumia jamani.
 
kujiuzulu sio suluhisho.suluhisho ni bunge kukaa na kufuta sheria hiyo inayoruhusu kupokea posho.waziri mkuu kazi yake anasimamia sheria zilizopo na zitto ndio kazi yake pia.hivyo wakwanza kujiuzulu inabidi awe ni zitto kwa kutosimamia sheria zilizotungwa na bunge.au auambie umma wa watanzania kuwa alikuwa anatafuta umaarufu wa kijinga.
 
CHADEMA Kama kweli wana dhamira ya kweli wakatae kusaini ili wafukuzwe na Watanzania tutaliona hilo lakini hili la matamko yasiyofuatana na matendo mimi naona ni ulaghai mtupu. !

Exactly...!!

Ni jambo la ajabu sana kuilalamikia posho unayoendelea kuichukua, huu ni unafiki ulioifikisha nchii hii hapa ilipo na ndio maana akina Pinda wanapata mlango wa kulipuuza hili kwa sababu hii move inaonekana kujaa blah blah pasi umoja wenye nia ya dhati ya kubeba gharama zake, ni vyema sasa wanasiasa waanze kuongea yale wanayoweza kuyatenda au la wakae kimya...
 
huyo pinda nae si ndo wale wale si alisema hajui kwa nini watanzania ni maskini kwa kuwa yeye anapokea posho nyingi,akiwa kama waziri mkuu hajui tutegemeee nini?hii nchi inaelekea ukingoni very soon kitanuka
 
kujiuzulu sio suluhisho.suluhisho ni bunge kukaa na kufuta sheria hiyo inayoruhusu kupokea posho.waziri mkuu kazi yake anasimamia sheria zilizopo na zitto ndio kazi yake pia.hivyo wakwanza kujiuzulu inabidi awe ni zitto kwa kutosimamia sheria zilizotungwa na bunge.au auambie umma wa watanzania kuwa alikuwa anatafuta umaarufu wa kijinga.

Nadhani hujaelewa somo! Hoja ni kwamba, kama ulifuatilia vizuri bunge wakati J.makamba anachangia hotuba juu ya mpango wa serikali wa miaka mitano, alisema hivi, hoja ya posho sio hoja ya chadema, ni sera ya serikali, ambayo imo kwenye mpango wa maendeleo wa miaka mitano, ambao umepitishwa na mawaziri na kusainiwa na rais, na mpango huo unaeleza wazi kwamba, posho zitaangaliwa upya ama kuondondolewa kabisa kwa kuwa ni mzigo kwa serikali.
Pinda kama waziri mkuu ndiye msimamizi wa mambo haya, leo anageuka sera za serikali na kusema posho haziwezi ondolewa! Hapa ndipo zitto anahoji, huyu waziri mkuu kama haamini anayosimamia aachie kiti hicho, kwani anapigana na sera anazozisimamia
 
Tatizo viongozi wengi Tanzania wamejilimbikiza mali kiasi kwamba hawatambui kuwa Tzania ni masikini. Kama wanakula Tsh.12m kwa mwezi, watatambua vipi kuwa kuna watu wanaishi kwa Tsh. 50,000 kwa mwezi. Mpaka hapo viongozi wetu watakapo tambua kuwa nchi yetu ni masikini, watu wengi wataumia sana
 
Jambo moja ni kwamba Pinda hajawahi kuwa msafi na hana record ya kutenda . Kama kuna ubuishi niwekeni sawa hapa . Ndiyo maana sishangai matamshi yake na kejeli kwamba hizo ni pesa ndogo . Huyu ni mtoto wa Mkulima . Ni aibu kwamba ni mkatoliki mwenzangu na mseminary mwenzangu pia .Aibu mno .
 
Gezeti la Daily News linatumika kueneza cheap propaganda! Point si wabunge walipokea na walitumia kukopa benki, point ni je wapo taayari kuachana na hii dhuluma na kujilimbikia maslahi huku walimu hawana hata kipato kinachowahakikishia mlo waa siku? Nimeisoma habari hii daily news nimeona inalengo la kutaka kuwaaminisha CCM sio wao pekee ambao ni mafisadi? Mhariri anatoa hoja zisizo na msaada wowote kuhusu suala zima la posho!
 
Wako wapi wale Pro-Chadema walikuwa wanapinga eti hakuna benki inayoweza kutoa mikopo kupitia posho, LAT na wenzako mpooo???
 
Nyie Pro-Chadema msiwe kama makinda ya bata yanamfata mama yao ata popote anapokwenda kama anavuka barabara. Hawo viongozi wenu wameishachukuwa mikopo benki kupitia hizo posho wanazozisema tena wa kwanza kuchukuwa ni Mbowe 200 milioni Zitto 150 milioni, mdhamini wao ni ofisi ya katibu wa bunge
 
Ayaah..!!sasa huo mkopo wanaulipaje hawa jamaa..jesus christ on a bicycle..!!hii mijianasiasa ni mijizi yote .
 
Kwa taarifa yako hakuna mbunge yeyote wa cdm aliyechukua posho tangu bunge hili linza wiki jana!!
Mwongo mkubwa.

Yeye mwenyewe Mnyika kasema "...Posho ya Kikao (Sitting Allowance) ambayo inalipwa hivi sasa kwa kuwekwa kwenye akaunti za wabunge moja kwa moja... " Hela wanaingiziwa moja kwa moja kwenye akaunti, hakuna aliyeirudisha!

You see, uzuri wa John Mnyika hasemi semi uongo most of the time. Mnyika kafananisha posho na nyama tamu, na kuacha posho kasema ni kama kumsusia fisi bucha yako ya nyama.

"Kabla ya kubadilishwa kwa mfumo mzima wa posho si jambo lenye maslahi ya umma kuziachia posho hizo zikatumiwa kiubadhirifu na serikali inayoongozwa na CCM badala yake ni lazima kuweka mazingira ya kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwenye masuala ya kimaendeleo kinyume na hapo itakuwa ni sawa sawa na ‘kumsusia fisi bucha.'' Chanzo

Kwa hiyo Mnyika hakatai kwamba huwa anakula posho, mikopo, mishahara, hela za mashangingi, wewe taja. Simtengenezi haya mambo, namnukuu:

"Nilichukua pia msimamo kama huo kwenye suala la mikopo ya magari ya wabunge, wakati wa kampeni nilipinga kiwango cha mikopo kinachotolewa cha milioni 90 kwa ajili ya gari kuwa ni kikubwa; na baada ya kuchaguliwa nilipewa mkopo huo na kuupokea." Chanzo

Hahahahahahaha....... Siasa za Tanzania na viongozi wetu zinatia udhia na machungu kupindukia lakini kwa sababu watu wazima haturuhusiwi kulia unaishia kucheka. John Mnyika, among the best and the brightest in the annals of our political leadership anakwambia ana msimamo mkali wa kupinga mikopo ya mashangingi lakini ukimpa atakula!
 
Mimi nashangazwa na matamko ya CHADEMA. Kila mtu anatoa tamko. Nimesoma la Mnyika linaanza na kauli ambao inaonyesha kuwa anaandika kama yeye akiwa Katibu wa Bunge wa CHADEMA na wala si Wabunge wote wa CHADEMA. Anasema ameshangazwa na siyo kwamba wameshangazwa! CHADEMA si watoe msimamo wa jumla na kama ni kukataa kusaini basi wote wasisaini ili wafukuzwe wote. Kama kweli wana dhamira ya kweli wakatae kusaini ili wafukuzwe na Watanzania tutaliona hilo lakini hili la matamko yasiyofuatana na matendo mimi naona ni ulaghai mtupu.

Angalieni CHADEMA baada ya maandamano mnageukia matamko sasa na matamko yenyewe kila mtu ana lake. Afadhali tamko la Zitto naona linafuatana na vitendo ila haya ya wengine mmhhhh!

Sioni sababu ya kuwashinikiza wabunge wa Chadema wasichukue posho hiyo kabla haijaondolewa, kinachopiganiwa posho hiyo iondolewe si kwa wabunge tu ila watumishi wote wa umma, kwa nini mnakomalia tu wabunge wa chadema wasichukue? Hamna uchungu na nji hii, duh!
 
WHILE some Members of Parliament from the opposition camp have asked for a review of their allowances, which they claim are colossal, it has been reliably established that the payments are actually the collateral that enabled them to secure bank loans.

‘Daily News’ investigations have found that the majority of MPs, from both CCM and the Opposition, took loans ranging from 60m/- to 200m/- from CRDB and NMB banks whose final deductions would be due in 2015 when their tenure expires.

Ironically, two top CHADEMA leaders, who have been vocal and championed the debate to have MPs sitting allowances slashed, are among the biggest creditors. One has taken a 196m/- loan and another 100m/- both from CRDB Bank.

Records show that each MP (Daily News is in possession of the long list of the creditors) gets a 2,305,000/- monthly salary plus 5,115,000/- as constituency allowance, making the total deductible pay to 7,420,000,000/-.

The documents indicate that 883,000/- is deducted every month for five years to cover the 45m/- personal car loan each MP was advanced and a further 588,000/- paid as government taxes. However, the package does not cover per diem and sitting allowances which are only paid if an MP has attended Bunge sessions.


“So, the claim by the opposition MPs that they want the sitting allowances slashed is purely a publicity stunt,” said an impeccable source. The source, who preferred anonymity, said that the legislators, who are beneficiaries of the bank loans whose guarantors are the office of the National Assembly, are not allowed to divert them to another account without a written consent by the three parties.

For example, a document from NMB shows that a 200m/- loan attracts a monthly deduction of 19,815,340/- if it is to be paid within one year, 10,183,540/- ( for 24 months), 7,177,760/- (36 months), 5,722,600/- (48 months) while the same package is charged 4,871,740,000/- per month in a five-year period.

When contacted for comment on Sunday, the Acting Clerk, Mr John Joel, said that bank guarantees are only given to loans whose source of income must come from payments made by the National Assembly.

“The National Assembly does not guarantee personal loans by MPs who use other collaterals apart from salaries and some other allowances,” he said. On June 7, this year, Mr Zitto Kabwe Kigoma North – Chadema) wrote to the Parliament Clerk asking for a total ban on the sitting allowance, which he said was a misuse of public funds. He claimed that such allowance was uncalled for, adding that attending sessions was part of his official duties, thus not deserving to be paid.

However, he instructed the House Clerk to channel his sitting allowance through Kigoma Development Initiative (KDI) of which he is the Chairman of the Board of Trustees until a new system to permanently slash the payment has been put in place.

A number of Chadema MPs told this paper here on Friday last week that they disagreed with their fellow MP on slashing the allowances.

They said that Mr Kabwe was advancing his personal views to gain political gains while the party is heading towards picking a presidential candidate for the 2015 general elections. Last week, the Prime Minister, Mr Mizengo Pinda, defended the allowances paid to MPs, saying much as they were seen to be mouth-watering on paper they in actual fact only cover a small fraction of expenses the legislators are incurring to make them discharge their duties smoothly.

Meanwhile, the National Assembly session resumes here on Monday morning with a debate on the 2011/12 budget estimates.
Source; Daily News
My take:
Pamoja na hayo ni makosa makubwa benki kutoa siri za wateja kirahisi rahisi hivi. Kwa wenzetu Uswiss, si tu ni kosa kutoa taarifa bali hata kuomba taarifa you risk to be jailed!

Mkuu naomba nikurekebishe kidogo,

Sheria ya benki ya mwaka 1961, 1991, na duniani kote duty of confidentiality ends if the information inquiry is of the matter of national interest, judicial inquiry or tax purposes (with authorisation from the commissioner). Hivyo basi Daily News hawajafanya kosa lolote. Ila mie najiuliza kama mshahara wako ni kidogo kwanini ukope hela nyingi hivyo milioni 200 kwa mshahara wa 2.5 na posho ya milioni 5???? Kweli Tanzania hakuna mkombozi wala mzalendo wamejaa walafi na watu wenye njaa tu.
 
<“So, the claim by the opposition MPs that they want the sitting allowances slashed is purely a publicity stunt,” said an impeccable source. >
1. Kama ni 'publicity stunt' inayoweza kuokoa mabilioni na yakawanunulia watoto wetu madawati ya kusomea, basi ni bora hiyo 'publicity stunt' mara kumi kuliko 'ndiyo mzee' inayoangamiza kizazi kizima.

2. Tumwamini yupi: mhariri wa Daily News au Mtoto wa Mkulima? Mtoto wa Mkulima amesema hizi posho ndio zinawawezesha Wahishiwa kuwamegea wapiga kura wao ndogo ndogo pindi wanapokumbana nao katika geti la Jengo la Bunge wakiomba nauli, karo za watoto, nk. Wakati huo huo Mhariri wa DN anatamka bila kutafuna maneno kuwa hizo posho ndio nguzo ya Wahishiwa kukopesheka!!

3. Ukishangaa ya Musa, basi subiri uyaone ya Bongo!!!!!
 
Nilishapata taarifa hapa hapa JF kuwa kulikuwa na habari iliyosambazwa kwa vyombo vya habari kutokea Ikulu kuhusu hili sakata la posho. Nadhani hii ni fotokopi ya habari hizo zilizotayarishwa na ikulu (ya walaji)
 
Sioni tatizo, sasa wafanye nini? Wakae nazo tu hizo hela huku zina depreciate? Huo utakuwa uzembe wa hali ya juu, you have to make your money work for you.
Pia Benki imevunja sheria kutoa data za watu kiholela, liangaliwe hili.
 
Nyie Pro-Chadema msiwe kama makinda ya bata yanamfata mama yao ata popote anapokwenda kama anavuka barabara. Hawo viongozi wenu wameishachukuwa mikopo benki kupitia hizo posho wanazozisema tena wa kwanza kuchukuwa ni Mbowe 200 milioni Zitto 150 milioni, mdhamini wao ni ofisi ya katibu wa bunge

Kama habari ndio hiyo nani wa kumfunga paka kengele?
 
Nyie Pro-Chadema msiwe kama makinda ya bata yanamfata mama yao ata popote anapokwenda kama anavuka barabara. Hawo viongozi wenu wameishachukuwa mikopo benki kupitia hizo posho wanazozisema tena wa kwanza kuchukuwa ni Mbowe 200 milioni Zitto 150 milioni, mdhamini wao ni ofisi ya katibu wa bunge
Kwa hiyo??? Unatetea posho za wabunge kwakuwa Mbowe na Zitto wamekopa?? Kweli wewe akili zako kama za Kiwete Mkwer.e
 
Back
Top Bottom