Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Hivi nyie hamna kazi?

Kazi tunayo ya kuandamana na kuchochea vurugu kwa wanavyuo. Leta swali jingine, jitahidi ulete maswali magumu na siyo ya paper ambayo tumesha isovu.
 
Great thinker msijibizane na wapinga mageuzi kama Omr,ritz,Tumain,Ms na wengine! Kufanya hivyo kunaondoa umakini ktk kujadili mstakabali wa taifa letu wa kupinga ufisadi wa ccm!!
hivi hawa uliowataja ni jinsia gani? kwa maana unaweza ukakuta ni chakla badala ya kuvitafuna tunazubaa kupigizana nao kelele kumbe wenzio wako kwenye hit.
tujuzeni vidume.
 
Wewe acha porojo mnataka tu kugawana pesa zetu (Ruzuku) maandamano sababu ya posho tu mbona wabunge wenu wamechukuwa milioni 90 juzi mbona mlikuwa kimya
sisi wananchi tunawashangaa sana

Milioni 90 ni posho, Nape unafanya nini sasa.
 
Hivi nyie hamna kazi?

Kwani we kazi uliyonayo waweza kutimiza majukumu yako, kama kila kukicha thamani ya pesa yetu inaanguka? kutokana na serikali kukopa kwa ajili ya posho ya semina elekezi, na posho za kuhonga wabunge ili walale usingizi, mikataba ya kilaghai isiulizwe wala kuhojiwa?
Nyie ndo wale wale waliouangusha uchumi wetu. But days are numbered
 
Ukuti ukuti wa mtende wa mtene tumpeleke ...mn................
Jamani kwenye saga inayoendelea huko bungen kuondolewa
kwa posho nimeona kimya jamaa zangu hapo juu wamekuwa kimya kweli
kama awako ofisini hivi wanatufundisha nini ..bungen ni sehemu ya kuchimba
madini ya fedha??pengine tunalamikia migodi ya mwanza kumbe kuna mgodi auitaji kuhangaika
zaidi ya piganio lako kuchaguliwa

eembu mh mrema na cheyo tusaidien kwa hili
 
Naona msimamamo wa Zito(yeye binafsi) unaripotiwa sana ila si msimamo wa kambi ya upinzani.nataka kujua ukweli kuhusu hili.
 
Ndugu wana JF,
Nianze kwa kumpongeza Mh. Zitto kwa hatua alizochukua za kukataa wabunge wasilipwe posho ya Tshs 70,000/=. Niwapongeze pia CHADEMA na NCCR-Mageuzi kwa kupigia kelele jambo hili.

Hebu tujiulize, Kuna wabunge 357 kwa siku wanalipwa jumla ya Tshs
24,990,000/=. Ukijaribu kukokotoa zaidi unapata hesabu hizi:

Kwa wiki (5 days) = 24,990,000 x 5 =
124,950,000/=
Kwa Mwezi (4 weeks)= 124,950,000 X 4 = 499,800,000/=
Kwa miezi 2 (Budget session)= 499,800,000 X 2 = 999,600,000 Almost One Billion

Hesabu hii ni makadirio ya chini ya Bunge la Budget ambalo linachukua takribani miezi 2. Hapo zijakokotoa posho za vikao vya kamati za Bunge na posho za watumishi wa Bunge.

Hebu fikirieni, vikao vya kawaida vya Bunge ambavyo huketi takribani wiki 2 (10 days) na kama sikosei ni kama vikao vitatu hivi ambapo jumla ya siku wanazokaa ni kama siku 30 (30 days) kwa vikao vitatu.

Hesabu za posho zao kwa vikao hivyo vitatu ni kama ifuatavyo;
30 days X 24,990,000 = 749,700,000/=

Hivyo basi, wastani wa posho za wabunge kwa mwaka ni;
Budget session (999,600,000) + Other Three sessions (749,700,000) = 1,749,300,000 (~ 1.75 Billion).

Kwa Miaka mitano: 1.75 Bil X 5 = 8.75 Billion

Kama nilivyosema hizi ni posho ambazo hazihusishi posho za vikao vya kamati za Bunge wakati wa Bunge session na baada ya Bunge sesssion (Kuzungukia miradi au kukagua n.k) na hazihusishi watumishi wengine wa Bunge.

Swali:
1. Watu wanaodai hoja ya Zitto na CHADEMA/NCCR-Mageuzi haina mashiko ni kweli , kwa takwimu hizi????
2. Pesa hizi zinaweza kujenga madarasa managapi ya shule za msingi?
2. Zinaweza kutengeneza madawati mangapi ya watoto wetu wa shule ya msingi?
3. Inaweza kulipa walimu wangapi wa shule za kata? n.k

Naomba kutoa hoja.




Tujiulize, Vikao vyote ambavyo wabunge wanakaa kwa Mwaka na kulipwa posho hiyo ni
 
Sikio la kufa halina dawa, unafikiri hawajui au hawaelewi ila fahamu ni hela tu zinawachanganya. Watu wameuza nyumba na Magari wawe wabunge sasa wanataka warudishe hela zao. Hawajali kuna maskini wangapi, mna njaa , au sasa hivi ni hali ngumu ya uchumi!!! Kuna msemo unasema ukitaka kujua tabia ya mtu subiri akiwa na hela au madaraka !!! 2015 sio mbali mkuu tumewaajiri na tuna haki ya kuwafukuza
 
Mbowe anasema ni msimamo wa chama, sasa ngoja tusubiri kesho itakaposomwa bajeti ya upinzani labda litagusiwa.
 
Mbio za sakafuni . . . . . . . Nyakati ndio hizo hazisomeki . . . . . . . Raisi hajui nini anafanya hadi sasa. . . . . . . Inawezekana uchaguzi kabla 2015!
 
Mkuu hizo hesabu zako ni za wabunge tu hujaweka posho za vikao za watumishi wengine serikalini. Ukiziweka hizo nadhani utapata mamia ya mabillioni. Mkuu suala hili ni mtambuka halihusu wabunge peke yao. Ni vema kama wabunge watakataa posho za vikao na kuzifuta na pia zifutwe serikalini. Haiingii akilini kwamba hata vikao vya management watu wanalipana posho, vikao vya kamati mabalimbali wanalipana posho. Posho poosho posho kila mahala.
 
Hebu piga mahesabu ya wabunge wa kuteuliwa na wa viti maalum,hawa pia ni wa kuondolewa,sio mnashabikia sitting allowances pekee,kuna vitu vingi bungeni havimake sense.
 
Mbowe anasema ni msimamo wa chama, sasa ngoja tusubiri kesho itakaposomwa bajeti ya upinzani labda litagusiwa.

Mkuu nadhani budget itagusia hilo. Ila nionavyo mimi hili suala la posho za vikao litaiumiza kambi ya upinzani kwa kuwa inaonekana wengi wanazitaka hizo posho. Kama hawzitaki inakuwaje ni Zito tu na wengine wachache wa NCCR wanaoonekana kupinga. Kama ni msimamo wa Kambi Rasmi ya upinzani bungeni mbona hatuwasikii Wabunge wengine wa CHADEMA wakisimama kidete kumuunga mkono Zito? Nimesikia BBC wakisema kuwa January Makamba naye amepinga posho za vikao. Kasinema haka ngoja tuone.
 
Back
Top Bottom