Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

kuna watu hapa nchini wanatumia miguu kufikiria.
slaa alikataa mshahara wa m7 kwa mbunge (anawakilisha jimbo moja)
anachukua m7 kama katibu mkuu(anawakilisha tanzania nzima)

hapo watu hawaoni tofauti ya halima mdee na slaa.au kigwangwala na mukama?
tanzania kweli ccm imetufikisha pabaya wa2 badala ya kutizama kwa macho wanatazama kwa masikio.
 
Wabunge wa CHADEMA sio kuwa wao hawazitaki hizo posho, hapo ndio watu mnaposhindwa kuwaelewa. Hakuna asiye taka pesa. Ila wao wanapigania mfumo mpya utakao ondoa hizo sitting allowance ili fedha hizo ziweze kufanya majukumu mengine ya manufaa.
Ukiliangalia hili kwa pupa utaona ni jambo la mzaha,ila kama Bunge litajiondolea posho za aina hiyo ina maana hakuna idara au wizara ambayo fedha za aina hiyo zitapitishwa na Bunge tena. Tutaokoa ngapi kama taifa? NYINGI. Kususia sio ufumbuzi wa tatizo

Posho tu kwa Bajeti 2011/2013 inachukua 13% ya Bajeti yote. Fikiria hizi pesa zingepelekwa kwenye miradi ya maendeleo.
 
Posho tu kwa Bajeti 2011/2013 inachukua 13% ya Bajeti yote. Fikiria hizi pesa zingepelekwa kwenye miradi ya maendeleo.

Ni kweli gambatoto, na ni wakati sasa kwa MPs wetu wa CDM kulikataa hili kwa vitendo.... Zitto ameonesha njia... Mh. Mnyika, Nyerere kule musoma, Godbless na wengine. Tafadhalini angalieni kwa umakini hoja na pendekezo hili... Naamini ni kwa manufaa si ya wananchi wale watakaofikiwa na pesa hii tuu, bali ni kwa manufaa ya chama pia.
 
Kuziacha hizo posho si kitu rahisi, kila mtu anapenda pesa. Lakini kwa mtu anayekerwa ki-ukweli na umasikni wa mtanzania, si rahisi akakubali kupokea hii mega potion wkt kinamama wakipewa bajaj kijiji kizima kama ambulence!

Cha muhimu hapo ni kuwa na mipango itakayohakikisha kuwa pesa hizo zinatumika kuondoa kero kwa mtanzania aliyekata tamaa. HONGERA ZITTO! Wewe ni kiongozi kaka!
 
hili swala ambalo ameliibua mbunge wa chadema mh.zitto kabwe kuhusu matumizi ya posho serikalini nakubaliana naye 100% kabsa haiwezakani mwalimu mwenye mshahara laki na nusu atoe fedha ake katka mshahara wake anunue chai na chakula akiwa shuleni anafundisha wakati wabunge na wengine maofisini wasio kuwa na majukumu mazito wanapewa posho za chakula hadi za kusinzia kazini na mishahara yao ni mamilioni uwoni tunategeneza gap la alienacho aendelee kuongezewa wakati asionacho anyanganywe ckubaliani nalo psodho futilia mbali nipeni mawazo yenu mwanaharakati mwenye kusubiri kufa
 
ni sera ya ccm, chadema ni kubadilisha mfumo huo. Nafikiri watafanikiwa chadema wanakubalika na ccm watafyata mkia maana wakigoma baada ya bunge tutaanza maandamano kupinga hata kabla ya bunge kuisha
 
wabunge ccm hawataki posho izungumziwe, wanaungwa mkono na spika mama yetu aliyetuzibia njia hapa kwetu sinza, pia wanaungwa mkono na ccm yaani pitia tamko la chiligati. Sasa wanalalamika chadema wametumwa kutupunguzia ulaji uliotuleta bungeni na ubunge tulinunua kwa gharama kubwa. Chadema hapa mmeshinda maana umma hautakubali na umewaelewa kaeni kimkakati zaidi hoja ipenye zaidi na hili ni goli safi sana la kisigino na mkakati utawaondoa ktk ulafi wa kupenda kushinda kwa wizi wa kununua safi sana. Keep it up tuko nyuma yenu ila mjiandae kwa makubwa
 
  • Thanks
Reactions: oba
itakuwa mgoli kuanzaa kuandamana kupinga bajeti ambayo kilichoandikwa na kinachozungumzwa na kilichotolewa haviendani ata kidogo uo c ni uwizi wa kimachomacho jamani mkulo kasema hiv kule kimeandikwa vile naibu anasematutafuata ilioko sa uo c ni bora liende tu au
 
pengine ccmagamba walinunua ubunge?penye nia pana njema laja cdm pambana na hao watalaam wa kupora jasho la wanyonge,ipo siku ya ushindi yaja.
 
Kama angekuwa panya tungesema kabanwa kwenye kona. Ni aibu kumsikia mtanzania anadai eti 150,000 per day, anaitetea then anasema haitoshi!! Sasa wanafunzi wanaopewa 5000 kwa siku waseme nini?
 
Ni ktk bajeti hii wabunge wa chadema wakiongozwa na waziri kivuli wa wizara ya fedha, ZITTO ZUBER KABWE(ZZK), kwa mara nyingine wanajaribu kuwashawishi wabunge wa ccm na vyama vingine, wajiondolee posho za vikao mbalimbali, na badala yake fedha hizo zikatumike kwa manufaa ya umma. Ni jambo la kupongeza na zuri, na mimi natamani lingetendeka jana badala ya leo. ZZK amekwenda mbali kidogo hadi kufikia hatua ya kumwandikia barua katibu wa bunge akimtaka asimamishe malipo ya posho kwake na badala yake fedha hiyo iende kwenye akaunti ya ngo ya KDI. Safi sana.
Kwa muelekeo, hadi hivi sasa hoja hii nzuri inaelekea kushindwa kwani inapambana na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wa ccm. Nina uhakika mwisho wa siku hoja hiyo iliyo kwa ajili ya manufaa ya umma na taifa itashindwa na haitatekelezwa.
Baada ya kushindwa hoja hiyo, nini kifanyike?
(i)Wabunge wa chadema waendelee na msimamo huo. Na kwa pamoja wahakikishe wanakubaliana kwa dhati.
(ii) Wafungue akaunti benki, ambayo itazikusanya fedha zao zote wanazolipwa kama posho.
Baada ya kukusanywa fedha hizo zifanye kazi gani?
(i) Zitumike ktk kuimarisha miundo mbinu ya chama, hii ni pamoja kujenga au kununua majengo ya ofisi za mikoa yote ya tz.
(ii)kununua vifaa vya uenezi kama maspika na amplifier ktk kila wilaya.
(iii)kugharamia shughuli zote zinazohusiana na chama chetu chadema.
Ndugu wana chadema wenzangu, kama tupo sirias, na hoja yetu ikakataliwa bungeni. Basi tuzigeuze pesa hizo kuwa mwiba kwa ccm kwa kuimarisha chama chetu. Endapo tutaweka mikakati mizuri na tangible juu ya pesa hizo, wao wenyewe ccm watapeleka hoja kuziondosha posho hizo kwani tumezigeuza kuwa miiba ktk miili yao. Wakikataa kuziondosha, tusizikatae, tuzichukue tuimarishe chama chetu kama nilivyoshauri.
Naomba kuwasilisha.
 
Leo mtakuwa wapi na Nape?...huu ni msimu wa viwavi mashambani,jamani wakulima tujiadhari!
 
wanafunzi kwa siku 5000 wabunge wanaona inatosha; ila wabunge posho ya kujikimu 80,000 kwa siku haitoshi-wanahitaji na sitting allowances 70,000 zaidi. Mmmmmmmmmh!!!!!!!!!!!! Kazi ipo, CDM onesheni njia tafadhali.
 
Kweli wabunge wa CCM ni wachovu wa kufikiri, kwa jinsi wanavyotoa majibu ya kifisadi ni sawa na kujifunga goli wenyewe kwani watanzania hawa wanoishi kwa mlo mmoja kwa siku hawatakaa wawasikilize tena na upuuzi wao huu. Asante sana CDM kazeni uzi hawa magamba kwishney kabisa.
 
Binafsi nilivutiwa sana na wazo la Zito Kabwe Lakini nahisi alilifanya haraka sana bila kushauriana na wenzake vizuri ingawa najua kuwa suala la posho ni lamtu binafsi lakini kama alivoeleza kwenye Barua yake kuwa CHADEMA wemetoa pendekezo hilo kwenye Bajet mbadala ya kambi ya upinzani ilikupunguza matumizi ya serikali yasiyo ya lazima lakini lakini nahisi amelifanya kibinafsi sana natumaini kama angewashirikisha wenzake wangekuja na CONSTRUCTIVE IDEA ya pamoja ambayo ingekuwa na impact ya kichama zaidi kuliko ya kuonekana ni ya mtu binafsi, Kwa mtazamo wangu alichokifanya Zitto kinaweza kikawaweka wenzake kwenye mtego hasa ukizingatia pendekezoalilolitoa Zitto la Kupeleka posho yake kwenye NGO (KDI) haitakubaliwa na vipi kama kulikuwa na wabunge wa CDM ambao hawakuunga mkono hoja hiyo? nafikiri CDMA walipaswa kujipanga Kwanza na kuja na Mkakati wa KICHAMA Z zaidi.

Thanks Nawakilisha
 
Wanasiasa siku zote huwa wanawafanya wananchi kuwa ni wajinga na hawana uwezo wa kufikiri. Haijalishi mwanasiasa anatokea chama gani au jimbo gani wote hutegemea umbumbumbu wetu kuwa ni mtaji wao.Si tumewasikia wakipinga posho za vikao vya bunge?wengine wamefika mbali hata kuandika barua kusema hawataki posho na wameelekeza kuwa posho zisiingie mfuko wa "shati" bali ziingizwe moja kwa moja kwenye mfuko wa "koti" kimantiki wanasema hawataki posho dhumuni likiwa kubana matumizi ya serikali sasa unapoikataa na kuelekeza ile ile posho upewe lakini kwa kutumia utaratibu mwingine ni usanii na kiini macho!

Nashangaa watu wameshindwa kuelewa hili na kulisifia! Sijui ni upovu au ni umbumbumbu wetu ndio unaotufanya tuwe hatuoni! au sijui ni "ukipenda chongo"?Tumeshuhudia posho zao wanazopeana tena huku wakikataa zisikatwe kodi ambayo itasaidia kuongeza makusanyo ya serikali. Kwa akili ya kawaida na mwenye uwezo wa kufikiri hawa wanaopiga kelel kuhusu posho tuwaulize wao wakiwa nje ya makao makuu kwa ajili ya shughuli za chama kama zile zilizozoeleka za "maandamano ya nguvu za umma" wanalipana posho kiasi gani? nusu ya hizo wanazogomea au zimezidi? au hawalipani kitu kwa kukwa wapo kwenye kazi walizopewa na chama? Kama wanalipana basi wanatafuna pia mapato yanayotokana na mlipa kodi kwani wanatumia ruzuku wanayopewa ambayo inatokana na kodi zetu!

My take:Kwa kuonyesha nia njema haitakuwa vibaya vyamka vya siasa vikaomba kupunguziwa ruzuku ili pesa nyingine zitakazobaki zikaelekezwa kwenye kufidia bajeti kuu. Najua hili litakuwa gumu sana lakini madhalan chama kina pokea 100 kikipokea 50 n a hamsini ikaelekezwa kwenye maendeleo si jambo baya na hii iapply kwa vyama vyote pamoja na chama tawala.<br><br><br>Naomba kuwakilisha.
 
Ni ktk bajeti hii wabunge wa chadema wakiongozwa na waziri kivuli wa wizara ya fedha, ZITTO ZUBER KABWE(ZZK), kwa mara nyingine wanajaribu kuwashawishi wabunge wa ccm na vyama vingine, wajiondolee posho za vikao mbalimbali, na badala yake fedha hizo zikatumike kwa manufaa ya umma. Ni jambo la kupongeza na zuri, na mimi natamani lingetendeka jana badala ya leo. ZZK amekwenda mbali kidogo hadi kufikia hatua ya kumwandikia barua katibu wa bunge akimtaka asimamishe malipo ya posho kwake na badala yake fedha hiyo iende kwenye akaunti ya ngo ya KDI. Safi sana.
Kwa muelekeo, hadi hivi sasa hoja hii nzuri inaelekea kushindwa kwani inapambana na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wa ccm. Nina uhakika mwisho wa siku hoja hiyo iliyo kwa ajili ya manufaa ya umma na taifa itashindwa na haitatekelezwa.
Baada ya kushindwa hoja hiyo, nini kifanyike?
(i)Wabunge wa chadema waendelee na msimamo huo. Na kwa pamoja wahakikishe wanakubaliana kwa dhati.
(ii) Wafungue akaunti benki, ambayo itazikusanya fedha zao zote wanazolipwa kama posho.
Baada ya kukusanywa fedha hizo zifanye kazi gani?
(i) Zitumike ktk kuimarisha miundo mbinu ya chama, hii ni pamoja kujenga au kununua majengo ya ofisi za mikoa yote ya tz.
(ii)kununua vifaa vya uenezi kama maspika na amplifier ktk kila wilaya.
(iii)kugharamia shughuli zote zinazohusiana na chama chetu chadema.
Ndugu wana chadema wenzangu, kama tupo sirias, na hoja yetu ikakataliwa bungeni. Basi tuzigeuze pesa hizo kuwa mwiba kwa ccm kwa kuimarisha chama chetu. Endapo tutaweka mikakati mizuri na tangible juu ya pesa hizo, wao wenyewe ccm watapeleka hoja kuziondosha posho hizo kwani tumezigeuza kuwa miiba ktk miili yao. Wakikataa kuziondosha, tusizikatae, tuzichukue tuimarishe chama chetu kama nilivyoshauri.
Naomba kuwasilisha.

Hii posho ni haramu, office za CDM na mahitaji mengine yatachangiwa na wana CDM. wazikatae tu na kushitaki kwa umma.
 
nani kasema MALARIA SUGU HANA POINT.......?
BIG UP MS.......KWA KUWAZA UTAIFA.....BIG UP MEEEEN
 
Back
Top Bottom