Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 699
Wanasiasa siku zote huwa wanawafanya wananchi kuwa ni wajinga na hawana uwezo wa kufikiri. Haijalishi mwanasiasa anatokea chama gani au jimbo gani wote hutegemea umbumbumbu wetu kuwa ni mtaji wao.Si tumewasikia wakipinga posho za vikao vya bunge?wengine wamefika mbali hata kuandika barua kusema hawataki posho na wameelekeza kuwa posho zisiingie mfuko wa "shati" bali ziingizwe moja kwa moja kwenye mfuko wa "koti" kimantiki wanasema hawataki posho dhumuni likiwa kubana matumizi ya serikali sasa unapoikataa na kuelekeza ile ile posho upewe lakini kwa kutumia utaratibu mwingine ni usanii na kiini macho!
Nashangaa watu wameshindwa kuelewa hili na kulisifia! Sijui ni upovu au ni umbumbumbu wetu ndio unaotufanya tuwe hatuoni! au sijui ni "ukipenda chongo"?Tumeshuhudia posho zao wanazopeana tena huku wakikataa zisikatwe kodi ambayo itasaidia kuongeza makusanyo ya serikali. Kwa akili ya kawaida na mwenye uwezo wa kufikiri hawa wanaopiga kelel kuhusu posho tuwaulize wao wakiwa nje ya makao makuu kwa ajili ya shughuli za chama kama zile zilizozoeleka za "maandamano ya nguvu za umma" wanalipana posho kiasi gani? nusu ya hizo wanazogomea au zimezidi? au hawalipani kitu kwa kukwa wapo kwenye kazi walizopewa na chama? Kama wanalipana basi wanatafuna pia mapato yanayotokana na mlipa kodi kwani wanatumia ruzuku wanayopewa ambayo inatokana na kodi zetu!
My take:Kwa kuonyesha nia njema haitakuwa vibaya vyamka vya siasa vikaomba kupunguziwa ruzuku ili pesa nyingine zitakazobaki zikaelekezwa kwenye kufidia bajeti kuu. Najua hili litakuwa gumu sana lakini madhalan chama kina pokea 100 kikipokea 50 n a hamsini ikaelekezwa kwenye maendeleo si jambo baya na hii iapply kwa vyama vyote pamoja na chama tawala.<br><br><br>Naomba kuwakilisha.
Kwani mwizi akikiri kosa katika famili, anaambiwa ni mnafiki au assibe tena. Watu wangine tumekosa uzalendo kabisa kiasi cha kua vipofu. Walimu watu wanaolipwa 200,000 wanapata teaching allowance kwa kufundisha kwanye mazingira magumu. Zile seat za bunge letu ni too comfotable to get an allowance. Wako wafanyakazi wanaofanya kazi za hatari sana na hawapewi allowance. Trilioni moja, hela ya kujikimu, mshahara millioni 12. yote hayo unamwambia nini mkulima wa Tanzania. Eti unafiki. Rafiki!