Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Lengo la Mh Zitto kupendekeza kuwa sitting allowances za vikao vya bunge na mikutano mingine ya watumishi wa serikali zifutwe ni kutaka fedha hizo zikafidie katika kodi ya mafuta, ili yapungue bei.

Wamejitokeza wanafiki fulani wa CCM wanasema wanaunga mkono hoja hiyo lakini ianze na wabunge wa CDM!

Mi nasema ok, wabunge wa CDM wakubali, but kabla ya kufanya hivyo, wakae na Nkullo, wakubaliane kuwa endapo wakiziacha posho hizo, kodi ya mafuta itaondolewa, na mafuta kushuka? Lau kama hakutakuwa na badiliko significant kwa kutumia posho za CDM peke yake kufidia kushuka kwa bei ya mafuta, then nawashauri na kuwaunga mkono kuwa waendelee kuzilamba posho zao, wazilete tuandalie maandamano...
 
We must walk the talk. I have written to the Clerk of Bunge that all sitting allowances I am entittled to should be directed to a charity in my constituency up to when the law is changed and sitting allowances scrapped.
I will advise my fellow CHADEMA MPs to take similar measure.

Mheshimiwa Zitto, NINAKUKUBALI na ninaiheshimu dhamira yako ya DHATI ya kutaka kuleta mabadiliko ya kweli kwa mtanzania!! Nashauri hata wabunge wengine wafanye hivyo, na kama ikiwezekana hiyo pesa kwa pamoja (za wabunge wote wa CHADEMA) ziunganishwe na kufanya kitu kitakachokuwa ushahidi kuwa kubadilisha maisha ya mtanzania ni kitu kinawezakana hasa pakiwa na utashi na dhamira ya kufanya hivyo! Namshukuru Mungu kuwa CDM ina watu kama wewe!!!
 
Vincent,

Mabadiliko haya kimsingi yanalenga kuhalalisha kile ambacho kinaendelea. Kama utakumbuka tuliwahi kukijadili katika mada iliyokuwa inahusiana na Mh mbowe kusema kuwa Dr Slaa analipwa posho na sio mshahara na hivyo hakuna kodi. Kama tulivyosema kwenye mjadala ule, in practice vyama vya siasa, taasisi za serikali na naamini pengine hata bunge lenyewe kwa muda mrefu zimekuwa hazilipi kodi kwenye posho mbalimbali zinazowapa watumishi wake (pamoja na kwamba ilikuwa ni kinyume cha sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004).

Inatia mashaka sana kuanza kubaguana katika namna hii na kimsingi inafanya sheria hiyo kuwa kinyume na katiba. kila mtanzania anapaswa kulipa kodi ya mapato kutokana na kipato chake, iwe ni biashara, ajira au uwekezaji bila kujali source ya kipato hicho. Na kama ulivyosema hatua hii inatoa ishara mbaya juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

Ni bahati mbaya sana kwangu moja ya majukumu ya kazi zangu ni kuangalia kama wateja wangu wanafuata sheria za nchi zikiwemo hizo za kodi. Huwa napata shida sana kwani wafanyakazi wengi wana "Perfect information" jinsi wafanyakazi wengine wa kada zao wanavyolipwa serikalini bila kukatwa kodi kwenye posho zao hasa ukizingatia mishahara hutengenezewa hazina (payroll) wakati posho hukokotolewa kwenye vituo vya kazi na kulipwa huko huko
 
nashindwa hata hii mibunge ya CCM niilinganishe na nini, japo naamini wapo wabunge wa CCM wanatamani kuunga hoja ya chadema lakini wanakwamishwa na kina januari makamba.
 
Haya tutaona bwana kama uongozi ni kuua raia watu huko shinyanga wanalia na njaa then wao hata hawashtuki!
 
Kwani bajeti hujaisoma? Hoja yako haijakaa sawasawa.
 
Jamani kuna siku Chiligati alikuwa anahohijiwa Clouds FM nafikiri ilikuwa J3 jioni alisema kama CDM hawataki kupokea posho waache lakini wao hizo posho ndio huwa zinatumika katika majimbo yao kutatua matatizo ya wananchi, kwiki kwikiwww zee fix lile.
 
Butola ndugu yangu, kinachopiganiwa sio posho ya wabunge pekee,hapo ni pakuanzia tuu. Posho za vikao zitolewazo kwa watumishi wa serikali na mashirika ya umma kwa mwaka ukipata idadi yake utashtuka. Huijui CCM na watu wake wasivyo na haya? Wabunge wa CHADEMA wakisusa wao bila aibu watakuambia ok na mfumo utabaki hivyohivyo. Hauta gusa sekta nyingine na hizo fedha za posho ya Wachadema haziwezi kuleta mabadiliko yeyote.
Nadhani tuunge mkono hoja hii maana ni ya Chama sio ya Zitto au Slaa au mbunge yeyote wa CDM. Wao kama Binadamu binafsi wanaweza kuzipenda hizo pesa lakini wanaheshimu msimamo wa chama kutaka kubadili mfumo huo ili kumsaidia mwananchi wa kawaida katika huduma za jamii anazozikosa kwa ukosefu wa fedha serikalini. Tusichanganye msimamo wa Chama na wa mbunge. Hawa wakina Chiligati wao wanatoa misimamo yao binafsi, tunataka kusikia msimamo wa chama chao. Ingawa CCM ni ngumu sana kujua chama kinasemaje na kauli ya mtu,kwani unaweza pata kauli mia tofauti toka kwa viongozi wake na hawajali/hawaelewi tofauti

Akhsante ndugu, Watu huwa wanashindwa kuelewa mada, na kushindwa kufanya uchambuzi kwa umakini, msimamo wa chama ndio tunaouangalia na sio msimamo wa mbunge mmoja mmoja, wabunge kususia wala haitakaa isaidie nchi hii, wao wanaweza wakachukua pesa hizo na kuzifanyia mambo ya maendelea majimboni kwao, na wamefanya mengi wabunge wa chadema kwa tunaowaona, hapa ni kuwaunga mkono ili hoja yao ifikiriwe na waliopo katika mamlaka, who knows inaweza ikawa ni sera mbaya kwa wabunge wa ccm lakini ikamkuna jk ingawa sizani. na jk akamua kulazimisha hicho kitu kikubalike miongoni mwa wanamagamba wenzie, then kuanzia hapo ndipo tutaona fedha zinapopotelea.

Na kitu kimgine kinachotakiwa kwenda sambamba na hicho ni usimamizi mzuri wa pesa katika halmashauri zetu, pesa zinapelekwa je zinafanyakazi kama ilivyokusudiwa au mchwa wanazitafuna?, maana unaweza badili mfumo ukaongeza kipato lakini kumbe ukapelekea watu wengine wakazifuja.

TUNAHITAJI KUBADILI MFUMO WA UTAWALA.
 
Vincent,

Mabadiliko haya kimsingi yanalenga kuhalalisha kile ambacho kinaendelea. Kama utakumbuka tuliwahi kukijadili katika mada iliyokuwa inahusiana na Mh mbowe kusema kuwa Dr Slaa analipwa posho na sio mshahara na hivyo hakuna kodi. Kama tulivyosema kwenye mjadala ule, in practice vyama vya siasa, taasisi za serikali na naamini pengine hata bunge lenyewe kwa muda mrefu zimekuwa hazilipi kodi kwenye posho mbalimbali zinazowapa watumishi wake (pamoja na kwamba ilikuwa ni kinyume cha sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004).

Inatia mashaka sana kuanza kubaguana katika namna hii na kimsingi inafanya sheria hiyo kuwa kinyume na katiba. kila mtanzania anapaswa kulipa kodi ya mapato kutokana na kipato chake, iwe ni biashara, ajira au uwekezaji bila kujali source ya kipato hicho. Na kama ulivyosema hatua hii inatoa ishara mbaya juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

Ingependeza sana kama ingekuwa kweli in practice kama ilivyo kweli on paper. Kuna wakati fulani, utakuta TRA wanakomalia posho za wafanyakazi fulani, kwamba zikatwe kodi wakati wao wenyewe TRA ambao walitakiwa wawe mfano, utakuta posho zao hazikatwi kodi.

Kuna swala pia la ajira zisizo rasmi, kwa mfano wenye nyumba za kupangisha (wanaopata income kutoka kwa wapangaji wao- achana na wale wenye leseni za hotel na g/house), madalali, madereva na makondakta wa taxi, daladala, malori ya usafirishaji, na wengineo. Hawa utakuta pato lao kwa mwezi ni kubwa kuliko mshahara wa kawaida wa mfanyakazi, lakini utakuta hawalipi income tax, japo barabara, hosptali na huduma zingine wanatumia.

Kwa mtazamo wangu, watu kama hawa pamoja na wafanya biashara ndio ingekuwa source nzuri ya pato la serikali. Serikali kutumia kodi za wafanyakazi (wanaolipwa na serikali) kama chanzo cha mapato ni kama kujidanganya maana ni sawa sawa na Baba awe anapata income kwa kupunguza pocket money anayompa mtoto wake.

Anyway, kwa ujumla, sipingi posho kukatwa kodi, lakini kama zinakatwa, zikatwe kwa wote bila kujali ni mbunge, mfanyakazi wa TRA au wa manispaa Ilala. Na serikali ipanue wigo wa kodi, kuhakikisha kuwa watu wote wenye kipato, rasmi au sio rasmi, walipe kodi. Haiwezekani, dereva wa taxi, au dalali wa nyumba za kupanga, awe anasomesha mtoto Loyola, halafu halipi kodi, wakati miye na mshahara wangu wa laki nne tu, ninalipa.
 
labda wazipokee alafu ndani ya chama wazikusanya na ku-facillitate maendeleo katika eneo fulani kwa kadri watakavyoona kuliko waziacha kwa mkullo atazitumia kwa safari za kikwete
 
Kwani bajeti hujaisoma? Hoja yako haijakaa sawasawa.
Hoja iko sawa. Ni kweli bajeti kibuli ya Zitto haijazomwa. Itakuwa tarehe 16/6. pale ndipo atakapowasilisha bajeti mbadala, yaani bajeti ambayo ingetumika endapo Chadema ingekuwa madarakani, ikiwa na mapendekezo ambayo Kambi ya Rasmi ya Upinzani ingependa yazingatiwe kwenye Bajeti ya Mkulo ambayo tayari imesomwa jana.
 
labda wazipokee alafu ndani ya chama wazikusanya na ku-facillitate maendeleo katika eneo fulani kwa kadri watakavyoona kuliko waziacha kwa mkullo atazitumia kwa safari za kikwete

Good sugestion, iwe isiwe ubinafsi mwingo unaondoa sifa ya kuwa kiongozi.:confused2:
 
Hoja iko sawa. Ni kweli bajeti kibuli ya Zitto haijazomwa. Itakuwa tarehe 16/6. pale ndipo atakapowasilisha bajeti mbadala, yaani bajeti ambayo ingetumika endapo Chadema ingekuwa madarakani, ikiwa na mapendekezo ambayo Kambi ya Rasmi ya Upinzani ingependa yazingatiwe kwenye Bajeti ya Mkulo ambayo tayari imesomwa jana.
Saluti sana mkuu,mpaka zitto kutoa kaili hiyo ni kuwa CDM wako tayari kutumia posho zao kunufaisha WATZ wanaoumizwa na live,sio hao washiba matumbo wao na familia zao tu,CDM wakisoma bajet yao wenyewe wataikubali japo kinafiki.
TEACH OTHERS THE RIGTH THING AT THE RIGHT TIME.
 
Hawa wabunge wengi wa CCM ni vilaza sana hawana uchungu na watanzania,chadema ni dira kwa maisha ya watanzania.VIVA CHADEMA
 
labda wazipokee alafu ndani ya chama wazikusanya na ku-facillitate maendeleo katika eneo fulani kwa kadri watakavyoona kuliko waziacha kwa mkullo atazitumia kwa safari za kikwete
Nakuunga mkono Kichwa Ngumu. Na hizo shughuli za kimaendeleo ziwekwe wazi kwa Wananchi.
 
Dunia hii ina watu wa ajabu sana. Chadema wamependekeza kuondoa sitting allowance kwa wabunge ili kubana matumizi yasiyo na tija. Fedha zitakazookolewa kutokana na uamuzi huo zitumike kwa maendeleo ya wananchi walio wengi. Badala ya kujadili umuhimu wa mpango huo watu wanaanza kuhoji mbona wao wanachukua posho hizo?

Kwa kusema hivyo tu, wanaonyesha kuwa wako tayari na wao kukosa posho hizo kwa maendeleo ya nchi. Katika hilo sioni mantiki ya kuanza kuhoji kwanini wao wanachukua posho. Kiongozi ambaye yuko tayari kupunguza maslahi yake kwa maendeleo ya nchi ndio anatakiwa katika zama hizi. Hata hivyo, cha msingi sio uwingi wa posho. Tunaangalia kiasi cha posho hizo na hali za watanzania. Nani anayesema kuwa Chadema hawataki posho hizo. Kama watanzania wangekua na maisha bora kama tuliyoahidiwa unadhani posho za wabunge ingekuwa hoja?

Tusiwe wapumbavu na washenzi, tuangalie hali ya wafanyakazi wa kima cha chini, wamachinga wanaozunguka kila kukicha, wanafunzi wanaofanya mitihani wakiwa chini, wakina mama wanaojifungua sakafuni na makundi mengine yaliyo katika shida kubwa. Baada ya hayo jaribu kulinganisha na posho za hao wateule. Tuache ushabiki usiokuwa na maana, tuangalie hoja iliyo mbele yetu na wala sio chanzo cha hoja hiyo. Kama umejiunga na JF kwa ajili ya kupinga tu hoja za upande fulani jaribu kuangalia siku zijazo kwako wewe na vizazi vyako vijavyo hali itakuaje.

Ahsante Haki kwa ufafanuzi,

Watu wengine wana umasikini wa fikra, ambao ni mbaya kuliko wa kiuchumi.
 
Ingependeza sana kama ingekuwa kweli in practice kama ilivyo kweli on paper. Kuna wakati fulani, utakuta TRA wanakomalia posho za wafanyakazi fulani, kwamba zikatwe kodi wakati wao wenyewe TRA ambao walitakiwa wawe mfano, utakuta posho zao hazikatwi kodi.

Kuna swala pia la ajira zisizo rasmi, kwa mfano wenye nyumba za kupangisha (wanaopata income kutoka kwa wapangaji wao- achana na wale wenye leseni za hotel na g/house), madalali, madereva na makondakta wa taxi, daladala, malori ya usafirishaji, na wengineo. Hawa utakuta pato lao kwa mwezi ni kubwa kuliko mshahara wa kawaida wa mfanyakazi, lakini utakuta hawalipi income tax, japo barabara, hosptali na huduma zingine wanatumia.

Kwa mtazamo wangu, watu kama hawa pamoja na wafanya biashara ndio ingekuwa source nzuri ya pato la serikali. Serikali kutumia kodi za wafanyakazi (wanaolipwa na serikali) kama chanzo cha mapato ni kama kujidanganya maana ni sawa sawa na Baba awe anapata income kwa kupunguza pocket money anayompa mtoto wake.

Anyway, kwa ujumla, sipingi posho kukatwa kodi, lakini kama zinakatwa, zikatwe kwa wote bila kujali ni mbunge, mfanyakazi wa TRA au wa manispaa Ilala. Na serikali ipanue wigo wa kodi, kuhakikisha kuwa watu wote wenye kipato, rasmi au sio rasmi, walipe kodi. Haiwezekani, dereva wa taxi, au dalali wa nyumba za kupanga, awe anasomesha mtoto Loyola, halafu halipi kodi, wakati miye na mshahara wangu wa laki nne tu, ninalipa.

Mheshimiwa kinachoongelewa hapa ni kwamba kama posho italipwa toka mapato ya Serikali hayatakatwa kodi
 
Back
Top Bottom