John Gregory
JF-Expert Member
- Jul 14, 2019
- 1,060
- 1,957
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani ametoa waraka unaoelezea kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo suala la mahusiano baina ya waumini. Katika waraka huo Kiongozi huyo ameruhusu makasisi wa kanisa hilo kuwapokea na ikibidi kuwabariki wale wanaojihusisha na mahusiano ya jinsia moja.
Akisisitiza kwamba daima kanisa halipaswi kuwasukuma waumini mbali na kanisa bali linapaswa kuwaleta karibu bila kujali hali zao za kiroho na kusema kama jinsi mvua iwanyesheavyo wema na waovu ndivyo kanisa linapaswa kuwapokea na kuwapa mafundisho wale wote wanaoenda kinyume na miongozo ya kanisa.
Pia kiongozi huyo amesisitiza kwamba kamwe hii haihalalishi mahusiano hayo na daima haiwezi kuwa mbadala wa Sakramenti ya Ndoa Takatifu.
Akisisitiza kwamba daima kanisa halipaswi kuwasukuma waumini mbali na kanisa bali linapaswa kuwaleta karibu bila kujali hali zao za kiroho na kusema kama jinsi mvua iwanyesheavyo wema na waovu ndivyo kanisa linapaswa kuwapokea na kuwapa mafundisho wale wote wanaoenda kinyume na miongozo ya kanisa.
Pia kiongozi huyo amesisitiza kwamba kamwe hii haihalalishi mahusiano hayo na daima haiwezi kuwa mbadala wa Sakramenti ya Ndoa Takatifu.