ELNIN0
JF-Expert Member
- Nov 26, 2009
- 4,161
- 1,460
Mzee John Malecela - pole sana kwa ajali ya kisiasa iliyokukuta, in fact hii ni ya pili. Ya kwanza kali zaidi ni ile ambayo ukaenguliwa jina lako na maswahiba wako wa karibu chamani - sababu kuu wakikutaka wewe ubakie kuwa mshauri wa chama hiki tawala na si kungombea urais, wakapuuzia justification yako kwamba bado una nguvu na kazi ya urais si kubeba zege bali ni ni kutumia ubongo na ubongo wako bado upo fiti. ukajitosa mikoa yote kuomba wadhamini ulipomaliza kurudisha form maswahiba wako hawa hawa wakakukata jina.
Baada ya kukatwa jina hukuongea chochote na sisi wenye uelewa tukajua kabisa kuwa mzee wetu sasa umekubaliana nao uwe mshauri na mlezi ndani ya chama. Tukashuhudia tena ukionyesha uvumilivu wako kwenda front line kupigana kwenye chaguzi ndogo bila kinyongo, nakumbuka kule buzwagi na kwingineko kazi yako kweli ilionekana wazi wazi mpaka ukapewa jina la TINGATINGA.
Sasa cha ajabu ni hii issue ya juzi juzi, Mzee si uliambiwa upumzike lakini tunashangaa unakurupuka tena kwenda jimboni kwako mtera, sisi tukajua unaenda kuaga alaa kumbe unachukua form tena za uongozi - Tukasema mzee umekuwa kiongozi toka ukiwa na miaka 25 (takribani miaka 50 na zaidi ukiwa kiongozi) hutaki kupumzika tu? Upumzike uangalie vijana wako wakiongoza uwakosoe wakati bado upo arround.
Sasa mzee wangu yamekukuta, rufani yako imetupwa na hii ni doa sababu inakuondolea wewe qualification ya kuitwa mlezi ndani ya chama, kuna kitu gani ulitaka kukitekeleza huko mtera ambacho hujakifanya kwa miaka yote hiyo ya ubunge wako? au uongozi wa nchi?
Mzee John - na wazee wengine igeni mfano wa baba wa taifa, hakuna mtu kwenye haki miliki ya kuongoza hadi kifo.
Hapo sasa Mzee John, aibu yako au aibu yetu? Uliambiwa pumzika ukagoma sasa naona unapumzishwa kwa LAZIMA.
Baada ya kukatwa jina hukuongea chochote na sisi wenye uelewa tukajua kabisa kuwa mzee wetu sasa umekubaliana nao uwe mshauri na mlezi ndani ya chama. Tukashuhudia tena ukionyesha uvumilivu wako kwenda front line kupigana kwenye chaguzi ndogo bila kinyongo, nakumbuka kule buzwagi na kwingineko kazi yako kweli ilionekana wazi wazi mpaka ukapewa jina la TINGATINGA.
Sasa cha ajabu ni hii issue ya juzi juzi, Mzee si uliambiwa upumzike lakini tunashangaa unakurupuka tena kwenda jimboni kwako mtera, sisi tukajua unaenda kuaga alaa kumbe unachukua form tena za uongozi - Tukasema mzee umekuwa kiongozi toka ukiwa na miaka 25 (takribani miaka 50 na zaidi ukiwa kiongozi) hutaki kupumzika tu? Upumzike uangalie vijana wako wakiongoza uwakosoe wakati bado upo arround.
Sasa mzee wangu yamekukuta, rufani yako imetupwa na hii ni doa sababu inakuondolea wewe qualification ya kuitwa mlezi ndani ya chama, kuna kitu gani ulitaka kukitekeleza huko mtera ambacho hujakifanya kwa miaka yote hiyo ya ubunge wako? au uongozi wa nchi?
Mzee John - na wazee wengine igeni mfano wa baba wa taifa, hakuna mtu kwenye haki miliki ya kuongoza hadi kifo.
Hapo sasa Mzee John, aibu yako au aibu yetu? Uliambiwa pumzika ukagoma sasa naona unapumzishwa kwa LAZIMA.