gambagumu, pole sana kwa msongo wa mawazo. ili nikuelewe uzuri:
1 unasema unafanya kazi 12 hrs, muda na nguvu za kunywa pombe kila siku unaupata wapi?
2 kipato unasema hakitoshi, inakuwaje bajeti ya pombe haikosekani?
ukishajijibu maswali hayo, pitia hapa kwa moskwito
https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/185126-mafanikio-kimaisha-3.html#post2693062
Ushauri wangu sasa ni huu:
1 Badilisha mtazamo wako kuhusu maisha, kuwa positive na mshukuru Mungu kwa yale aliyokujaalia (kuna thread humu watu wana masters na wako jobless kwa miaka, kuna wagonjwa, kuna wenye family crisis)
2 fanya kitu cha kukusaidia kubadili maisha yako ya baadae, mfano badala ya kunywa pombe ungewekeza kwenye masomo ya jioni. hii itakusaidia kubadili nafasi yako kazini kama sio kupata kazi yenye kipato zaidi
3 usijichukulie serious sana. kuna maisha zaidi ya maghorofa na magari (mfano tu). adjust malengo yako kulingana na hali halisi na ufurahie baraka za Mungu kwako
4 Shughulikia mahusiano yako na familia na mwenza wako. Haya mengine yanapita tu, angalia wanacholalamikia na uone kama ni muhimu kwako, na pia kama ni muhimu kuliko uhusiano wako na wao
kila la kheri
Wandugu tafadhalini naombeni ushauri nifanye nini mimi kijana wenu..nilimaliza chuo kikuu mwaka 2008, nikabahatika kuajiriwa baada ya mwaka mmoja.baada ya ajira nlijiwekea malengo kadhaa lakini mpaka sasa sjatimiza hata moja. Mazingira ya kazi ni magumu sana nafanya kazi 12 hours kwa siku sita. Nimepoteza kabisa morale ya kazi na nataka kuacha kazi ila sijui ntaishi vipi ..mahusiano na mpenzi wangu yamevurugika nimekua mbali sana na familia. Nilikua sinywi pombe ila sasa nakunywa tena kila siku..