Picha:Umbumbumbu wa magazeti yetu

Nawashauri hao wanaojuwa kulaan waanze kulaani upumbavu huu kwanza halafu ndio nitaelewa kweli wanasimama kwenye misingi ya haki.

[h=3]Yaliyojiri Zanzibar[/h]



Kiongozi wa Jumuiya ya kikundi cha uamsho, Sheikh Farid Hadi Ahmed
Baada ya jeshi la polisi kulazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya baadhi ya wafuasi wa kikundi cha uamsho kufuatia kukamatwa kwa mmoja wa kiongozi wao, hali inaendelea kuwa tete na hivi sasa baadhi ya wafuasi hao wameingia mtaani wakishinikiza kuachiwa kwa kiongozi huyo huku jeshi la polisi likilazimika kutumia mabomu kuwatawanya wafuasi hao …..


1.jpg

Maelfu wa wazanzibari wakiongozwa na Taasisi za Kiislamu na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) wakifanya matembezi ya amani katika barabara za Zanzibar na kupeleka ujumbe wao kwa viongozi wa serikali za Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Umoja wa Mataifa wakitaka Zanzibar huru ambapo baadhi ya watembeaji hao wakiongoza na Kiongozi wa Jumuiya hizo, Sheikh Farid Hadi Ahmed na viongozi wengine
6263284_orig.jpg
4502132_orig.jpg

Maelfu ya wazanzibari leo wamefanya maandamano amani kuishindikiza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuitisha kura ya maoni juu ya Muungano na kupeleka ujumbe kwa Umoja wa Mataifa wa kutaka Zanzibar kujitenga kama ilivyofanya Sudan ya Kusini.
5923108_orig.jpg

Waanamanaji hao wakiongozwa na Sheikh Farid Hadi Ahmed walitembea kutoka viwanja vya Lumumba na kupitia barabara ya Kinazini, Mpigaduri, Michenzani Maskani ya CCM Kisonge, kwa Biziredi na kurudi tena viwanja vya Lumumba.
Maandamano hayo walioyaita matembezi ya amani yalifanyika na kuhudhuriwa na maelfu ya wazanzibari ambapo awali kuliandaliwa kongamano kubwa lililoandaliwa na Taasisi za Kiislamu kwa kushirikiana na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) kwa lengo la kuzungumzia mfumo wa elimu Zanzibar.

Akizungumza na maelfu ya wazanzibari kabla ya kuanza maandamano hayo yaliitwa ni matembezi ya amani, Sheikh Farid alisema wazanzibari wana haki kama walivyokuwa na haki wananchi wengine ulimwenguni kote kudai haki yao ndani ya nchi yao....................
901221_orig.jpg
 
Mbona hizi tarehe 26/27 zina jinamizi huko zenji! Nakumbuka January 27 mwaka fulani kulikuwa na vifo vya risasi huko zenji.

Hawa wahariri kama wanatumia picha ambazo sizo na wala hawajasema ni za maktaba ni hatari kubwa. Watanzania tuna waandishi wa habari wachache sana; tuna wachumia tumbo sawa tu na wanasiasa. Si ajabu ndio maana miaka ya nyuma kabla ya uchaguzi vyombo vya habari vilikuwa vinatuonyesha picha za mauaji ya kimbari huko Rwanda ili kuwatisha watu.

Hivi hata Tanzania Daima nalo limefikia kuonyesha picha za uongo?
 
tatizo la waandashi kupewa memo za maaskofu, wahariri kuommba ruhusa ya madri hii ndio hatari yake
 
Hapa unasemaje Mkuu?


Mjumbe Kutoka Unguja:" Mwenyekiti, Hali Si Shwari"




Hiyo Unguja,eti hali imetulia,jana usiku wamevamia moja ya makanisa yetu Katoliki na kupiga moto ambao haukuleta madhara sana,pia mchana walichoma nyumba yetu moja na kuvunja uzio huko Welezo,juzi walichoma kanisa katoliki kigango cha Mtoni-Manfred
Reactions::

hii nimeipenda ile ya damu ni ya Kubuni. hii ya kanisa nzuri sana. nakumbuka mto wa mbu waislam walipopigwa na wakiristo
 
ARIFU huelewi kwanini? picha iliowekwa sio ya tukio husika.....ni ya tukio lingine kabisa.......
Kimsingi tuko pamoja, kwamba isingekuwa rahisi jamaa ana hasira za kukamatwa kiongozi wake halafu ukamchukua picha tena usoni, so picha za juzi kama zipo, basi ni zile zilizopigwa huku cameraman akiwa kwa mbali kuepuka shari ya MUAMSHO mwenye hasira za kiitikadi kali
 
Last edited by a moderator:
Huyu kiziwi ana kampeni flani,,alianza kwa kuponda gazeti tanzania daima sasa kaja na thread tofauti,,utasumbuka sana kila kitu zanzibar kipo wazi huwezi watetea
 
sasa mkuu wangu umejuwaje kama maandamano yatakuwa makubwa wakati hata kabla waandamanaji wenyewe hawajaandamana?
 
Sema ni gazeti lipi, na ikiwezekana weka hiyo picha hapa. Hebu uwe wazi, sio na wewe unakuja na mambo yako ambayo hayajakamilika. Unakuwa bado unafanana na hao unaowashutumu.


Magazeti hayo hapo mkuu na link hii hapa kaka JUMA MTANDA: MUUMINI WA DINI YA KIISLAM AKIONYESHA KITAMBAA KILICHOTAPAKAA DAMU

Sikutaka kutia neno lakini kama ndio hivi basi hii habari imekuzwa (staged) haiwezekani vyombo vyote vya habari wakatumia picha ya morogoro kwa tukio la zanzibar. Nashindwa kujua wamefanya hivi kwa manufaa ya nani hasa? nia yao ni nini? Hawajivunzi kwa wakenya? tumesahau ya Rwanda?

Nadhani tumechoka kuishi kwa amani kuna watu wanataka kunufaika kupitia machafuko! Alaaniwe liepanga mpango huu!
 

Attachments

  • SAM_2045.JPG
    SAM_2045.JPG
    56 KB · Views: 25
  • SAM_2046.JPG
    SAM_2046.JPG
    54.2 KB · Views: 29
  • SAM_2047.JPG
    SAM_2047.JPG
    57.1 KB · Views: 28
  • SAM_2048.JPG
    SAM_2048.JPG
    53.2 KB · Views: 27
Hizi ni faida na hasara za kutegemea mitandao badala ya kuwa au kutafuta watu waliopo katika tukio, ni rahisi sana na wanaokoa gharama kubwa wanapochukua picha toka mtandaoni kuliko kutuma mtu ama kutafuta mtu aliye eneo la tukio, hii ni download and paste on paper itajatugharimu sana siku moja.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Hakuna Shaka kuwa magazeti haya yana agenda ya siri zidi ya Zanzibar na Wananchi wake, hii hii inatokanaa kupandikiza chuki baina ya Wananchii wa Zanzibar na watu wenye asili ya Tanganyika wanao ishi visiwani humo.
Agenda hii haitosaidia chochote bali itaibua hasira na chuki zidi ya Wazanzibar na watu wenye asili ya Tanganyika, agenda hii haitoletafaidaa yoyote zaidi ya hasara na kupandikizaa mbegu ya uhasama na chuki miongoni mwa jamii na kuwaondoshea utulivu watu wenye asili ya Tanganyika waishio Zanzibar .
Kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kushadidia shari ,nisawa na kuongeza petrol kwenye moto jee utafaidika nini ?.
Kuhusu matokeo ya machafuko Zanzibar nimapema mno kujuwa ni watu gani waliofanya vitendo hivyo vya uharibifu wa mali za uma likiwemo kanisa maduka vituo vya pombe na magari binafsi.
Tuwashie washunguzi wafanye kazi yao na badae watupe takuwimu zao sio magazeti na vyombo vya habari kupurushuka tu na kutowa habari zisizo na ukweli na kuongeza chumi hii itakuwa hatari katika pande mbili za Muungano na watu wake kwa kujengeana uhasama ,jee yupi atakaye faidikaaa kwa kujengeana uhasama?.
Tusisahau kuwa hii tulionayo ni Tanzania ile ile , kuna agenda nyingi ndani ya mfumo wetu wa maisha , nikigusia kidogo tu , nyuma tulikotoka katika harakati za kisiasa.
Kwa upande wa Zanzibar kumeshazoweleka vitendo vingi vya uvunjaji wa sheria vikiongozwa na makundi wanayo yadengeneza chama tawala ccm ili kupaka matope vyama vengine au watu waliokuwa hawawaungi mkono.
Kumbuka kupigwa risasi 2001 26/27 Wazanzibar, Kundi lilolosemekana lilikuwa likipiga minyororo na kuvamia matuka ya wafuasi wa vyama vengine na kuiba mali zao, kuchomeana moto makaa zi yao kwa utashi wa kisiasa, hizi zote nihistoria hapa kwetu Zanzibar zimetokea na vitimbi vingi tu huko nyuma tutorage?.
Sasa hivi sasa kumeingia mivutanoo Baina ya wananchi wa Zanzibar na Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar Smz/Suk.
Wameona Serekali yao imeshindwa kuwatekekezea ile dimand yao ya kutaka kura ya maoni kwanza halafu kujadiliwa uhalali wa Muungano kuwepo na kuto kuwepo hayo ni matokeo ya baada ya Wananchi kuamua ama kuwauliza wananchi wa pande zote mbili husika za Muungano au kutumia ibara ya 10 ya Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuitisha kura ya maoni.
Sasa haya yote ya Serekali ya Zanzibar na ile ya Muungano kujifanya kutia pamba za mashikio na kuwapuza wananchi dimand yao matokeo yake ndio hii kuuibuka makundi yakidini , makudi ya kisiasa na makundi ya Serekali kila mtu anavutaana upande wake bila kujulikana chanzo ni nini?.
Tukisema tulaumu Jumuia ya Muamsho tu na kuwabebesha lawama la matokeo haya basi itakuwa hatukwenda mbali katika kufikiri na inaweza kuibua hasira na visasi vya udini , Waiislamu na Wakristo ,Magowa na Wahindu, Mabuda na wengineo .
Hii italipeleka taifa pabaya na itakuwa vita hivi nitabu kuvizima vile vya Uganda tulivyopigana Tanzania na vikatushukuwa miaka mingi na kupoteza wengi na Tanzania kuto kujirudi hali Kiiuchumi mpaka leo vitakuwa ni afazali kulikonii vita vya Udini na civil war.
Tulipigana na Uganda na tuliwajuwa waganda ni watu gani na nitaifa gani ? Lakini jee kupigana wenyewe kwa wenyewe kwa njia ya udini, Utanganyika na Uzanzibar rizalty zake zitakuwa vipi na yupi atakuwa winer na kujisifia ushindi wake? Mzanzibar au Mtanganyika? Hii itakuwa ni hatari na asari yake itakuja katika jamiina na kufanya ndugu wawiki wa Tanganyika na Wazanzibar kujengeana visasi vya maisha .
Kwa hio nilazima media zetu ziwe natahazari sana na wanacho kiandika na kukisoma wananchi wa Tanzania , kinaweza kuligawa taifa katika misingi miwili Utanganyika na Uzanzibar Udini na Ukabila.
Mungu ibariki Zanzibar na umbilici Tanzania yote .
 
Hivi sasa ni media wao ndio wenye kupotosha habari kukuza kwa kuandika na kuongeza chumvi na hali kuwa mbaya kwa kuonyesha baadhi ya picha za Matokeo ya uchaguzi na fujo zilizokuwa zikifanyika katika chaguzi za nyuma za Zanzibar.

Hii hii nikuvuja na sio kujenga amani na mshikamano ,nikuleta chuki baina ya watu wa pande mbili za Muungano.
 
Hizi ni faida na hasara za kutegemea mitandao badala ya kuwa au kutafuta watu waliopo katika tukio, ni rahisi sana na wanaokoa gharama kubwa wanapochukua picha toka mtandaoni kuliko kutuma mtu ama kutafuta mtu aliye eneo la tukio, hii ni download and paste on paper itajatugharimu sana siku moja.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Back
Top Bottom