Hakuna Shaka kuwa magazeti haya yana agenda ya siri zidi ya Zanzibar na Wananchi wake, hii hii inatokanaa kupandikiza chuki baina ya Wananchii wa Zanzibar na watu wenye asili ya Tanganyika wanao ishi visiwani humo.
Agenda hii haitosaidia chochote bali itaibua hasira na chuki zidi ya Wazanzibar na watu wenye asili ya Tanganyika, agenda hii haitoletafaidaa yoyote zaidi ya hasara na kupandikizaa mbegu ya uhasama na chuki miongoni mwa jamii na kuwaondoshea utulivu watu wenye asili ya Tanganyika waishio Zanzibar .
Kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kushadidia shari ,nisawa na kuongeza petrol kwenye moto jee utafaidika nini ?.
Kuhusu matokeo ya machafuko Zanzibar nimapema mno kujuwa ni watu gani waliofanya vitendo hivyo vya uharibifu wa mali za uma likiwemo kanisa maduka vituo vya pombe na magari binafsi.
Tuwashie washunguzi wafanye kazi yao na badae watupe takuwimu zao sio magazeti na vyombo vya habari kupurushuka tu na kutowa habari zisizo na ukweli na kuongeza chumi hii itakuwa hatari katika pande mbili za Muungano na watu wake kwa kujengeana uhasama ,jee yupi atakaye faidikaaa kwa kujengeana uhasama?.
Tusisahau kuwa hii tulionayo ni Tanzania ile ile , kuna agenda nyingi ndani ya mfumo wetu wa maisha , nikigusia kidogo tu , nyuma tulikotoka katika harakati za kisiasa.
Kwa upande wa Zanzibar kumeshazoweleka vitendo vingi vya uvunjaji wa sheria vikiongozwa na makundi wanayo yadengeneza chama tawala ccm ili kupaka matope vyama vengine au watu waliokuwa hawawaungi mkono.
Kumbuka kupigwa risasi 2001 26/27 Wazanzibar, Kundi lilolosemekana lilikuwa likipiga minyororo na kuvamia matuka ya wafuasi wa vyama vengine na kuiba mali zao, kuchomeana moto makaa zi yao kwa utashi wa kisiasa, hizi zote nihistoria hapa kwetu Zanzibar zimetokea na vitimbi vingi tu huko nyuma tutorage?.
Sasa hivi sasa kumeingia mivutanoo Baina ya wananchi wa Zanzibar na Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar Smz/Suk.
Wameona Serekali yao imeshindwa kuwatekekezea ile dimand yao ya kutaka kura ya maoni kwanza halafu kujadiliwa uhalali wa Muungano kuwepo na kuto kuwepo hayo ni matokeo ya baada ya Wananchi kuamua ama kuwauliza wananchi wa pande zote mbili husika za Muungano au kutumia ibara ya 10 ya Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuitisha kura ya maoni.
Sasa haya yote ya Serekali ya Zanzibar na ile ya Muungano kujifanya kutia pamba za mashikio na kuwapuza wananchi dimand yao matokeo yake ndio hii kuuibuka makundi yakidini , makudi ya kisiasa na makundi ya Serekali kila mtu anavutaana upande wake bila kujulikana chanzo ni nini?.
Tukisema tulaumu Jumuia ya Muamsho tu na kuwabebesha lawama la matokeo haya basi itakuwa hatukwenda mbali katika kufikiri na inaweza kuibua hasira na visasi vya udini , Waiislamu na Wakristo ,Magowa na Wahindu, Mabuda na wengineo .
Hii italipeleka taifa pabaya na itakuwa vita hivi nitabu kuvizima vile vya Uganda tulivyopigana Tanzania na vikatushukuwa miaka mingi na kupoteza wengi na Tanzania kuto kujirudi hali Kiiuchumi mpaka leo vitakuwa ni afazali kulikonii vita vya Udini na civil war.
Tulipigana na Uganda na tuliwajuwa waganda ni watu gani na nitaifa gani ? Lakini jee kupigana wenyewe kwa wenyewe kwa njia ya udini, Utanganyika na Uzanzibar rizalty zake zitakuwa vipi na yupi atakuwa winer na kujisifia ushindi wake? Mzanzibar au Mtanganyika? Hii itakuwa ni hatari na asari yake itakuja katika jamiina na kufanya ndugu wawiki wa Tanganyika na Wazanzibar kujengeana visasi vya maisha .
Kwa hio nilazima media zetu ziwe natahazari sana na wanacho kiandika na kukisoma wananchi wa Tanzania , kinaweza kuligawa taifa katika misingi miwili Utanganyika na Uzanzibar Udini na Ukabila.
Mungu ibariki Zanzibar na umbilici Tanzania yote .