Nasikia kila mwaka hutumia zaidi ya milioni 50 kuandaa shughuri hizo, ingekuwa jambo la maana zaidi kama hiyo pesa kila mwaka angekuwa anaitumia kuwalipia gharama za shule hao walemavu, Kwani wengi wao wanasoma shule za msingi na waliobahatika kuendelea ni ktk shule za kata, ambapo kwa kiwango hicho angewasaidia walemavu wengi sana kuliko kuwaita na kuwafariji kwa chakula na mziki wa masaa machache tu, huku wakikabiliwa na changamoto nyingi za kimaisha??? Mi nadhani washauri wake walione hili japo anajitahidi ila aangalie njia bora ya kuwasaidia zaidi ambayo itakuwa ya kudumu kwa wahusika nayo ni kupitia elimu.