Picha: Ibada ya kumuaga Regia Mtema iliyofanyika Tabata

poleni sana wafiwa
ungekuwa mwana JF umepewa mamlaka ya Mungu Nani ungemchukua kati ya hawa kwa wakati huu


makinda-cheyo.jpg
 
Jamani Inauma sana!

Bwana alitoa na Bwana

ametwaa!!!!

Jina lake na lihimidiwe!

Amen!
 
Baadhi yetu wana JF tuliokutana msibani leo katika Ibada pale Kanisa katoliki Segerea, tumeamua kwamba tutapanga siku maalumu hivi karibuni na tutakutana British Council na kujadili yale yote aliyosimamia Regia na nini cha kufanya ikiwa ni namna ya JF kumuenzi marehemu. Yote tutayajulisha maana tutashirikiana na uongozi wa JF.

Mimi si mwandikaji sana, lakini leo wacha niandike machache.Machache haya ninayoweza kusema ni kuwa, Mwaka 2010 tulipoendesha shindano la "JF Woman of the Year 2010" Regia alichaguliwa na Wana JF na akashinda. Hii ni uthibitisho tosha kuwa Regia alikuwa anapendwa, anathaminiwa na anakubalika katika hoja zake. Ni Regia huyu huyu aliyethubutu kuweka pembeni ID yake ya JF ya "Gender Sensitive" na kutumia jina lake halisi Regia Mtema! Ni wachache sana wanaweza na wanaojiamini kwa hilo.

Lakini kikubwa na ambacho wengi hamjui ni kuwa, katika Mwaka wa uchaguzi 2010 JF ilijizolea umaarufu sana toka ndani na nje ya Nchi katika kutoa habari za uchaguzi mkuu. Binafsi niliendesha threads kuu kama za Uzinduzi wa Kampeni wa Chadema jangwani, Uzinduzi wa Kampeni wa CCM ambayo yote ilifanyikia jangwani. Reporting ile ilikuwa ni LIVE nikiaangalia TV, kusikiliza na hatimaye kuandika kadiri nilvyoona katika Luninga na huku napost JF. Hii ilifanya baadhi wakaniita "Mzee wa Matukio"

Wakati wa Uzinduzi wa Kampeni wa CHADEMA wote mnajua kuwa Matangazo yalikatishwa na TBC. Ni katika kipindi hiki nilianza kuhaha ni vipi sasa nitawaletea wadau matangazo live. Unajua kipindi kile kulikuwa na watu wengi sana online. Na wengi walisononeka. Niliwasiliana na Maxence (Founder wa JF) na kumuuliza kama kuna mtu yeyote anaweza akanisaidia kupost live ambaye yuko jangwani.

Maxence alinipata namba ya simu ya Regia, akaniambia yuko Jangwani na atakupa updates zote. Huo ndiyo ukawa Mwanzo wa Mimi na Regia kufahamiana. Mwanzoni nilimjua tu kama Gender Sensitive na Baadaye Regia Mtema.

Naam . . . Nilipompigia Regia akaniambia kuwa haina tabu, yeye atanipa updates kwa simu, naam, hatukukata simu, Yeye akieleza matukio na hotuba nami pia nikisikiliza kwa mbali na wakati huo huo nikipost JF. Huyo ndiye Regia ninayemfahamu ambaye alikuwa tayari wakati wowote kufanya kile anachokiamini na kukusimamia. Ulemavu wake wa mguu kweke yeye haukuwa na nafasi ya kumnyima fursa yoyote au kufanya jambo lolote alilitaka. Wakati mwingi aliwazidi hata wasio na ulemavu wowote.

Niliposikia msiba huu, niliumia. Na leo sikuwa na jinsi, ilibidi nisitishe kila kitu na kwenda kumwaga Mwanamapinduzi huyu, naamu, Kumwanga Regia.

Kwa heri Kamanda Regia, kalale pema peponi Kamanda, umefanya sehemu yako. Inatupasa na sisi tufanye sehemu yetu na kuiga na kuendeleza mazuri yote aliyoyafanya.

Regia, wewe ni kama Mshumaa uliokuwa unaleta Mwanga wa matumaini katika kiza kinene sana na sasa Mshumaa huo umepulizwa na upepo na kuzima.

Regia, yo are a Tanzanian Rose & Gold, you are like Candle in the wind.

We will miss you Regia. You were the JF icon.

Kalale pema peponi Kamanda

Amen.
 
Natamani dada Regia azikwe...siwezi vumilia kuendelea kusikia habari za kifo chake.
 
Katika kipindi hiki ambacho watanzania wamechoshwa na uoza wa viongozi waliopo madarakani, tunapoondokewa na kijana mahiri Kama Regia, ni pigo kubwa kwa taifa. Taifa linahitaji kuwa na mamilioni ya vijana kama Regia ili kuleta mapinduzi ya kifikra na ya kiutendaji. Regia ametoa mchango mkubwa kwa taifa, nasi tumuenzi kwa kuendeleza angalau asilimia 10 ya yale aliyoyaamini na kuanza kuyatekeleza. Bwana ameba na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihidimiwe. Amen
 
Thanks The Finest. Kwa picha hizi hata sisi tumeshiriki ktk safari ya mwisho ya mpendwa wetu Regia. Apumzike kwa amani. Amina.
 
RIP dada Regia Mtema! Tutakukumbuka kwa ujasiri na umakini wako ndani na nje ya bunge. Again, RIP bwana alitoa na bwana ametwa jina la bwana lihimidiwe, amen!
 
Asante sana mkuu TF kwa kutuwakilisha sisi tulio mbali
Rest in eternal peace our beloved sister Regia
 
Kusoma tu maandisha iliniuma sana . Kuangalia hizi picha sasa naamii ni kweli imetokea.
Dunia ni nyumba ya kupanga tu, ipo siku tutaungana nawe mahali tunapopaita "Nyumbani kwa baba"
umetupa majonzi mengi kwa kutangulia kwako. Kama ingelikuwa ni uamuzi wetu tungeomba ubaki nasi milele.
Pumziko la milele Regia. Tuliumbwa kwa udongo na tutarudi udongoni. Amen..

The Finest asante kwa picha..
 
Tunashukuru sana makamanda kwa kutushirikisha matukio yaliyojiri kw njia ya picha, kusema kweli ni kama vile wote tulikuwa hapo, endeleeni kutujuza kila hatua inayoendelea, kama mlivyofanya. Asanteni sana
 
Katika kipindi hiki ambacho watanzania wamechoshwa na uoza wa viongozi waliopo madarakani, tunapoondokewa na kijana mahiri Kama Regia, ni pigo kubwa kwa taifa. Taifa linahitaji kuwa na mamilioni ya vijana kama Regia ili kuleta mapinduzi ya kifikra na ya kiutendaji. Regia ametoa mchango mkubwa kwa taifa, nasi tumuenzi kwa kuendeleza angalau asilimia 10 ya yale aliyoyaamini na kuanza kuyatekeleza. Bwana ameba na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihidimiwe. Amen
Ndugu kwa kasi ya mapinduzi tunayoitaka asilimia 100 za utendaji wa Regia zinahitajika na Bwana Mungu atuongezee watu wengine kama yeye lukuki ili tusichelewe kupata ukombozi maana kama tutafanya asililmia kumi tu ya aliyokuwa anayafanya itatuchukua miaka mingi sana kukombolewa mimi naona tuongeze zaidi. Bwana atufariji kwa kutupa kina Regia wengine wengi.

Bwana ametoa na bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe.
 
poleni sana wafiwa
ungekuwa mwana JF umepewa mamlaka ya Mungu Nani ungemchukua kati ya hawa kwa wakati huu


makinda-cheyo.jpg

Pdidy, nipo kwenye majonzi lakini swali lako dah! limeniacha hoi, pengine matoto ya ndege.
 
Back
Top Bottom