Pengo amtolea uvivu Kikwete

Pengo amtolea uvivu Kikwete

Ni lazima kuwaweka wazi hawa, ni wauza Madawa wakubwa na 40 ZAO ZIMEFIKA. sAFARI HII MAPAMBANO YATAANZIA Kanisani. Huwezi kurtumia Biblia kuuza madawa ya kulevya.
-----------------------

Exactly tunachokitaka sisi wakatoliki! Awaweke wazi...umesema mwenyewe kwa maneno yako..! Na sisi tunataka afanye hivyo ..siyo anakuja kwenye ibada yetu halafu anasema baadhi yenu tumewakamata mnajihusisha na madawa ya kulevya lakini mwisho wa siku inakuja kujulikana aliyekamatwa ni mchungaji wa kanisa la kijiweni waki Nigeria! Naona sasa tumefikia pazuri maana naona na baadhi ya waislam mnmtaka kikwete awaweke wazi hao watu! Tunamkaribisha sana aanzie kanisani kuwaweka wazi na kuwashughulikia hao watu akimaliza aendeleze zoezi lake sehemu nyingine....! Kikwete awe na ujasiri wa mwanamke mjamzito..period!

Mbona ameshaweka mambo wazi ndio maana Pengo anajikanyaga.

Sasa ni wajibu wa Pengo na wenzake kujisafisha kwa hilo kabla kuumbuliwa.
Kwani Rai ametumia njia ya kiungwana kufikisha ujumbe. Ni kama vile polisi wanapotoa hadhali kuwa wenye silaha wote zisizo halali wazisalimishe polisi na kutakuwa hakuna kesi lakini wakija na kukukamata nayo basi watakuchukulia kama mwalifu.

Hongera Kikwete
 
Mbona ameshaweka mambo wazi ndio maana Pengo anajikanyaga.

Sasa ni wajibu wa Pengo na wenzake kujisafisha kwa hilo kabla kuumbuliwa.
Kwani Rai ametumia njia ya kiungwana kufikisha ujumbe. Ni kama vile polisi wanapotoa hadhali kuwa wenye silaha wote zisizo halali wazisalimishe polisi na kutakuwa hakuna kesi lakini wakija na kukukamata nayo basi watakuchukulia kama mwalifu.

Hongera Kikwete
kaka una swaumu kali? hebu niambie pengo atajisafishaje kwa hilo kabla ya kuumbuliwa?? Hii si issue ya kuumbuana...ni issue ya kuwataja,kuwakamata na kuwachukulia hatua wote wanaohusika na mdawa ya kulevya! Sasa hayo mambo ya kutoa tahadhari ndo pengo hayataki....ndiyo maana anasema JK awe na ujasiri wa mwanamke mjamzito!
 
kaka una swaumu kali? hebu niambie pengo atajisafishaje kwa hilo kabla ya kuumbuliwa?? Hii si issue ya kuumbuana...ni issue ya kuwataja,kuwakamata na kuwachukulia hatua wote wanaohusika na mdawa ya kulevya! Sasa hayo mambo ya kutoa tahadhari ndo pengo hayataki....ndiyo maana anasema JK awe na ujasiri wa mwanamke mjamzito!

Nafikiri unahitaji usome lama za nyakati. Rais ni mkuu wa nchi na anaweza kutumia njia yoyote ile kufikisha ujumbe kwa jamii au wananchi wake. Sasa hapo JK ameamua kutumia njia ya kistaharabu ya kutoa hadhari. sasa nashangaa Pengo ana wasi wasi gani kama yeye na wenzake kanisani ni safi sasa anapapatika nini?

ndio tunasema bila shaka amejihisi sasa anataka kujikosha kwa jamii. kama haimuhusu inamshughulisha nini?
Au pilipili yaliwa shamba yeye inamuwashia nini?
 
Wizi mkubwa mkubwa a.k.a ufisadi ndio uliomwingiza Jk madarakani na akilifahamu hilo aliamua kuvunja sheria za nchi kwa kuwapa fursa wezi kurudisha na kuungama kwake kisiri kukwepa kuchukuliwa hatua za kisheria. Hili kila mwenye akili timamu anafahamu ujanja huu ulitumiwa kwa sababu ni ukweli usiopingika kwamba pesa ya kagoda ni sehemu ya pesa chafu zilizoiingiza ccm madarakani hasa mgombea urais. Kwa hili nalo la madawa ya kulevya tuseme labda nalo ni la mazingira kama ya ufisadi wa epa? Hata walengwa kupewa fursa ya kuungama kisiri kinyume na sheria za nchi? Kama mkulu alikuwa anafahamu hivyo kulikuwa hakuna sababu ya kulitumia hilo kama fimbo ya kisiasa dhidi ya mahasimu wake katoliki. Ona sasa linavyomgharimu, kutakiwa awataje ama kuwakamata huku dhamira yake ikimsuta kwamba kufanya hivyo ni kuhatarisha zaidi ama yeye binafsi au washiriki wake wa karibu wa harakati za kuingia ikulu.
Jambo hili linanikumbusha kauli aliyowahi kutoa mwalimu siku za nyuma kwamba 'kuna watu wanaotaka kuingia ikulu kwa pesa za bangi'
.
 
Wizi mkubwa mkubwa a.k.a ufisadi ndio uliomwingiza Jk madarakani na akilifahamu hilo aliamua kuvunja sheria za nchi kwa kuwapa fursa wezi kurudisha na kuungama kwake kisiri kukwepa kuchukuliwa hatua za kisheria. Hili kila mwenye akili timamu anafahamu ujanja huu ulitumiwa kwa sababu ni ukweli usiopingika kwamba pesa ya kagoda ni sehemu ya pesa chafu zilizoiingiza ccm madarakani hasa mgombea urais. Kwa hili nalo la madawa ya kulevya tuseme labda nalo ni la mazingira kama ya ufisadi wa epa? Hata walengwa kupewa fursa ya kuungama kisiri kinyume na sheria za nchi? Kama mkulu alikuwa anafahamu hivyo kulikuwa hakuna sababu ya kulitumia hilo kama fimbo ya kisiasa dhidi ya mahasimu wake katoliki. Ona sasa linavyomgharimu, kutakiwa awataje ama kuwakamata huku dhamira yake ikimsuta kwamba kufanya hivyo ni kuhatarisha zaidi ama yeye binafsi au washiriki wake wa karibu wa harakati za kuingia ikulu.
Jambo hili linanikumbusha kauli aliyowahi kutoa mwalimu siku za nyuma kwamba 'kuna watu wanaotaka kuingia ikulu kwa pesa za bangi'
.

pamoja na yote uliyoandika. sasa ni ipindi muafaka pengo na wenzake kama wapo wajisafishe kabla mkono wa sheria kuwafikia. habari ndio hiyo.
 
pamoja na yote uliyoandika. sasa ni ipindi muafaka pengo na wenzake kama wapo wajisafishe kabla mkono wa sheria kuwafikia. habari ndio hiyo.
Wako juu ya sheria wao? mbona vibaka wadogo hawapewi muda? Ni jela tu!!
Huu ni uropokaji wa watu wenye akili ndogo tu.
 
pamoja na yote uliyoandika. sasa ni ipindi muafaka pengo na wenzake kama wapo wajisafishe kabla mkono wa sheria kuwafikia. habari ndio hiyo.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Okay sasa mkuu nimekupata. Kumbe Pengo ni comfirmed kuwa ni dealer, ila wenzake haijawa comfirmed bali wanadhaniwa, maana umesema 'kama wapo'. Kujisafisha wanakotakiwa ni kwa namna gani na ni kipindi cha mda gani walipewa kabla mkono wa sheria kuwafikia? Mie naomba huo mkono wa sheria uwafikie angalau tufarijike kwa kuona sheria ikianza kuheshimiwa tena.<br />
.
 
Nafikiri unahitaji usome lama za nyakati. Rais ni mkuu wa nchi na anaweza kutumia njia yoyote ile kufikisha ujumbe kwa jamii au wananchi wake. Sasa hapo JK ameamua kutumia njia ya kistaharabu ya kutoa hadhari. sasa nashangaa Pengo ana wasi wasi gani kama yeye na wenzake kanisani ni safi sasa anapapatika nini?

ndio tunasema bila shaka amejihisi sasa anataka kujikosha kwa jamii. kama haimuhusu inamshughulisha nini?
Au pilipili yaliwa shamba yeye inamuwashia nini?
BuruBuru siku zote nakuona una akili etc etc, lakini kusemwa mtu wa dini yako au anayejifanya ni dini yako basi ustaarabu na werevu wako wote umekuruka? au umepitiwa?
suala la msingi ni kwamba Raisi wa nchi mwenye nafasi nyingi za kutoa ujumbe kama hotuba za mwisho wa mwezi, shughuli nyingine za kitaifa nk nk ameshindwa kutoa ujumbe huo katika nafasi hizo? na kama tatizo ni hao wakatoliki kama yeye ana ujasiri.wa mamlaka ya uraisi ...... mbona ameshindwa kuwataja? muhula wa kwanza hadithi ilikuwa hiyo hiyo, muhala wa pili unaongelea makanisa sijui madogo madogo kwa mgongo wa kanisa au dhehebu kubwa nia yako nini hasa? kuongoza watu au kuleta mfarakano? leo hii mtu asiye dini yako aongele mapungufu ya dini nyingine itakuwaje? kama sio hukumu ya kifo inayotolewa kwa hasira kwa baadhi yetu? bila kufuata ukweli wa mambo? je jk orijinale aliwahi kushutumu dini isiyo yake ? licha ya kuwa kiongozi wa nchi kwa miongo miwili? mimi mwenyewe kwa ustaarabu tuliofundishwa wakati wa orijino tulikuwa na tuna chinja kuku, ili kiwe tunu kwa marafiki zangu, majirani zangi nk nk, iweje ili jirani akija siku ya noeli au pasaka ajione nyumbani na anakaribishwa, sasa leo hii baada ya kuishi vizuri miaka yote hiyo tunaona fahari ya kuutukuza udini? leo hii uta watenga wakatoliki, kesho walutheri, kesho kutwa wasabato, na siku za mbeleni kakobe. lwakatare, mwingira nk nk, baada ya hapo watabaki sunni, shite , kojani, bohora, agha khan nk nk itakuwaje?
nafikiri wewe burabura ni mtu muelewa ukipingana na mwenz\io pingana kwa kitu cha haki nk nk
 
BuruBuru siku zote nakuona una akili etc etc, lakini kusemwa mtu wa dini yako au anayejifanya ni dini yako basi ustaarabu na werevu wako wote umekuruka? au umepitiwa?
suala la msingi ni kwamba Raisi wa nchi mwenye nafasi nyingi za kutoa ujumbe kama hotuba za mwisho wa mwezi, shughuli nyingine za kitaifa nk nk ameshindwa kutoa ujumbe huo katika nafasi hizo? na kama tatizo ni hao wakatoliki kama yeye ana ujasiri.wa mamlaka ya uraisi ...... mbona ameshindwa kuwataja? muhula wa kwanza hadithi ilikuwa hiyo hiyo, muhala wa pili unaongelea makanisa sijui madogo madogo kwa mgongo wa kanisa au dhehebu kubwa nia yako nini hasa? kuongoza watu au kuleta mfarakano? leo hii mtu asiye dini yako aongele mapungufu ya dini nyingine itakuwaje? kama sio hukumu ya kifo inayotolewa kwa hasira kwa baadhi yetu? bila kufuata ukweli wa mambo? je jk orijinale aliwahi kushutumu dini isiyo yake ? licha ya kuwa kiongozi wa nchi kwa miongo miwili? mimi mwenyewe kwa ustaarabu tuliofundishwa wakati wa orijino tulikuwa na tuna chinja kuku, ili kiwe tunu kwa marafiki zangu, majirani zangi nk nk, iweje ili jirani akija siku ya noeli au pasaka ajione nyumbani na anakaribishwa, sasa leo hii baada ya kuishi vizuri miaka yote hiyo tunaona fahari ya kuutukuza udini? leo hii uta watenga wakatoliki, kesho walutheri, kesho kutwa wasabato, na siku za mbeleni kakobe. lwakatare, mwingira nk nk, baada ya hapo watabaki sunni, shite , kojani, bohora, agha khan nk nk itakuwaje?
nafikiri wewe burabura ni mtu muelewa ukipingana na mwenz\io pingana kwa kitu cha haki nk nk

Kama ulivyosema. Rais ana nafasi nyingi sana za kutoa matamko yake kwa jamii yake. na hivyo ndivyo alivyofanya rais wenu.

Mbona mnakuwa mnashangilia pale RAIS huyo huyo akiongea na wanajumuiya ya chuo kikuu au watanzania waishia nje a nchi au kikundi chochote akazungumzia ufusadi au hata madawa. Kwanini iwaume akitoa kauli zake akizungumza na mapadre.

Au ndio njia ya kutaka kumziba mdomo. Mimi namini hapa kuna kitu hapa naomba tu tuwe na subra tutakiona.
 
KANISA Katoliki nchini limesema haliridhishwi na utaratibu wa unaotumiwa na serikali kulituhumu kanisa hilo kuwa linajihusisha na biashara ya dawa za kulevywa.

Kanisa limetoa kauli hiyo siku siku chache baada ya semina ya wabunge kuhusu athari za dawa za kulevya nchini iliyofanyika hivi karibuni mjini Dodoma. Semina hiyo ili kuwa ni ahadi ya serikali kutekeleza ahadi iliyoahidi kuhusu kuonesha mkanda wa video wa wafanyabiashara wa dawa za kulevya kuonesha hadharani. Kanisa Katoliki nchini na Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) yalikuwa miongoni mwa taasisi za dini ambazo zilitajwa kutumiwa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu kufanya biashara ya dawa za kulevya.

Taarifa iliyosainiwa na Katibu wa Baraza la Maaskofu (TEC), Padri Anthony Makunde na kusambazwa kwa vyombo vya habari jana ilieleza kanisa hilo linaamini kwamba biashara hiyo itakomeshwa iwapo wahusika wote, pasipo kujali wadhifa wao katika jamii, watakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria na si kwa malumbano na kauli zenye utata ambazo malengo yake yanatia shaka.

"Tumepokea habari hizo kwa mshtuko mkubwa kwa kuzingatia hadhi na ushawishi ambao kanisa inao mbele ya jamii pamoja na maadili yanayofudishwa na kusimamiwa na taasisi hiyo. "Habari hizi zimelisikitisha na kulifadhaisha sana Kanisa Katoliki kwa vile, kwa mujibu wa vyombo hivyo vya habari kauli hiyo imetolewa katika semina ambayo sisi kama Taasisi hatukualikwa au kuwepo hivyo kushidwa kutoa maelezo juu ya shauri hili. Alisema kuwa kanisa hilo limeshangazwa na taarifa hizo kwa sababu halijawahi kudokezwa ama kushirikishwa juu ya suala hilo ili kutoa ufafanuzi na pengine ushirikiano iwapo ungehitajika.

Ni kwa mantiki hiyo, Kanisa Katoliki linasubiri maelezo na taarifa rasmi kutoka mamlaka husika ili liweze kutoa ufafanuzi na pengine ushirikiano iwapo utahitajika.

"Tukio lililotajwa katika magazeti ni Kongamano la Vijana lililofanyika huko Australia 2008. Katika tukio hilo ni kweli kwamba Baraza la Maaskofu liliratibu safari ya vijana na walezi wao waliohudhuria Kongamano hilo. Kwa mujibu wa taarifa zetu, vijana na walezi waliopitia TEC walienda na kurudi wote. "Hatuna taarifa za vijana waliobaki Australia kutoka katika kundi la vijana ambao safari yao iliratibiwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.

"Hata hivyo inashangaza kuona kwamba safari iliyofanyika miaka mitatu iliyopita inanukuliwa katika siku hizi katika hali ambayo Kanisa Katoliki halijawahi kuulizwa, au kuamriwa na mamlaka husika kutoa taarifa zozote kuhusu kundi ambalo safari yao ya kwenda Australia iliratibiwa na Kanisa hili ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.Ilieleza kuwa hata hivyo mwaka huu kuanzia tarehe 16/8/2011 vijana wa Kitanzania wakiwa na walezi wao walikuwa Madrid- Hispania kwa Kongamano la aina hiyo. Kilele chake kimefanyika Agosti 21 mwaka huu kwa Ibada ya Misa iliyoongozwa na Baba Mtakatifu Benedicto VI.

"Ikumbukwe kuwa si mara ya kwanza Kanisa Katoliki kuratibu safari za Kiroho na Kichungaji kwa makundi mbali mbali ya waamini wake. Ziko safari za kwenda nchi Takatifu, Roma, Fatima, Lurdi na sehemu nyinginezo za Hija. "Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limekuwa ikiratibu safari hizo baada ya kujiridhisha kwamba wale wote wanaokwenda kushiriki katika Hija hizo wamefuata taratibu zilizowekwa kikanisa na kuridhika kwamba wanakwenda huko kwa lengo la kuhiji na si vinginevyo. "Kwa vile si sera ya Kanisa Katoliki kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya, Kanisa Katoliki linaamini kwamba hata ikitokea kwamba mmoja wa mahujaji amebainika kujihusisha na biashara hiyo, atakuwa amefanya hivyo kama mtu binafsi na si kwa jina ama kwa niaba ya Kanisa.

"Kanisa linaunga mkono harakati zote za serikali na watu wote wenye mapenzi mema za kupiga vita biashara hiyo haramu. Hata hivyo taarifa ilisema kanisa halitaunga mkono kauli za jumla jumla zinazotolewa na baadhi ya watu kuhusu dawa za kulevya ambazo pengine zinatia shaka iwapo lengo lake ni kweli kupiga vita dawa za kulevya ama kulichafua, kulidhalilisha na kulipotezea hadhi na mvuto lililonao mbele ya jamii.

Chanzo: Majira
 
Kwa nini serikali haiwataji wahusika na hiyo biashara ya madawa ya kulevya badala yake inaendelea na danadala kati ya wahusika na kutoa tu tuhuma za jumla bila kutaja jina la wahusika na hatua stahiki? Je ni propaganda za kuwapakazia kashfa viongozi wa dini? Rais anaposema watu wa Mungu wanafanya biashara ya madawa ya kulevya inawalenga watu binafsi au hao viongozi wa dini? Woga gani ulioishika serikali kwikwi ya kutaja hadharani majina ya wauza unga?
 
Are we really sincere in fighting against drug trafficking war? Otherwise we should shut up and remain silence forever. Sheria ziko wazi, kwanini hazitumiki kama mkatoliki au bakwata wamejihusisha na biashara ya madawa ya kulevya? Vinginevyo ni yale yale tuliozoea ya hadithi zisizo kwisha, hata kwenye mambo ya hatari kabisa na uwepo wetu
 
serikali legekege hachukuimaamzi imekalia usanii na majungu..kama unajua fulani anajihusisha na madawa na ushahidi unaona kumkamata mpaka ufanye semina na wabunge kweli magamba mmeishiwa mbinu...
 
Awali taarifa ya rais ilisema maaskofu wanajihusisha na madawa ya kulevya, kauli yake ilipokosolewa na kutakiwa kusahihisha na kwenda mbali zaidi kwa kuwataja majina, viongozi waandamizi wa serikali wakiongozwa na waziri mkuu wakaanza kuifanyia ukarabati kauli ile ya rais kwa kusema rais alimaanisha maaskofu wa makanisa madogomadogo na wakaahidi kuonyesha Video ya wahusika hao.

Sasa hapa linakuja suala lingine la kushangaza, eti waliitwa waandishi wa habari wakaonyeshwa mkanda ukiwaonyesha wahusika wakiwemo kutoka kanisa Katoliki na BAKWATA sasa hawa wanaingia vipi hapa? Au tuseme BAKWATA wanaingia vipi katika suala hili wakati hawakuwahi guswa kuhusu suala hili tangu mwanzo.

Hapa nadhani serikali inataka kutulazimisha tuanze kuhoji ukweli na uhalisi wa mkanda huo wa washutumiwa, na kama inatulazimisha kuamini picha hizi basi itabidi wananchi twende mbali zaidi na kwa makusudi kuanza kuamini picha alizowahi tuhumiwa nazo rais wetu ukianzia zile ambazo hazikuwahi toka hadharani , mpaka zile ambazo zilipelekea mtandao fulani wa kidharirirshaji kufungiwa.

Yeah sidhani kama tutakuwa tumekosea kwa kufanya hivyo, kwasababu serikali inajaribu kutuona na kutufanya wajinga na sasa tutawahahakikishia kuwa wamefanikiwa kutufanya wajinga
 
Hii inatuaminisha wengine kwamba wafanyabiashara wa madawa ya kulevya ni viongozi wa serikali na washirika wao. Kutapatapa huku kwa serikali ni moja ya uthibitisho.
 
Wakatoliki walishamuambia Kikwete 'njoo utukamate kama tunahusika'.

Wakaongeza kuwa ukimya wa Kikwete kutowakamata wauza madawa ni usaliti.
 
Serikali legelege inafanya kazi kwa Majungu majungu tu..kama wanajulikana kwa si muwakamate?!! ama mnaogopa moto wa Roma?!! nyie fanyeni usanii wenu kwenye maisha ya watu
 
Ninamuonea huruma Kikwete sura yake ataificha wapi? Ninamshauri bila kumumunya afukuze washauri wake ni afadhali achukue ushauri wa humu Jf utamsaidi kumaliza nng'we yake iliyobaki. Akiendelea hivi hafiki mbali. Baba wa watu atashikwa presha, presha itapanda wakati wanaomshauri wanachapa usingizi.
 
JK ameshindwa kuwadhibiti na kuwachukulia hatua wafanya biashara ya madawa ya kulevya, sasa anatafuta 'scapegoats'. Kama anao ushahidi mbona hakuuweka hadharani alipotakiwa kufanya hivyo? Shame on him! Wanaohusika na biashara hiyo anawajua sana na anaendelea kuwakumbatia. Hizi ni njama zake tu za kulichafua na kulisambaratisha kanisa. Kama kazi imemshinda aachie ngazi, sio kutoa tuhuma zisizokuwa na ukweli!
 
Hivi ni sababu gani zinampelekea Kikwete kutomwita nyerere baba wa taifa?
Huwa anamuita hayati mwalimu nyerere
 
Back
Top Bottom