Pengo amtolea uvivu Kikwete

Pengo amtolea uvivu Kikwete

Haya umeona sasa! wewe imekuwaje utoke kwenye mada hii unakuja na video iliyoletwa na Mkristu mwingine ili ijewe!...Je, nikikuletea video za wachungaji wa Kikristu kina Jimmy Swagat wanaotukana Uislaam na kuita dini ya mashetani - utasema nini?..Sisi Waislaam hatuna muda huo na hakika nyie ndio mnazo video nyingi zinazoukashifu Uislaam lakini huwezi kuta video inayokashifu Ukristu isipokuwa tunakashifu matendo maovu kama kuuza unga, pombe, kula nguruwe n.k... Sasa maadam wewe pengine unawajua wakristu anaouza unga, unafikiri Waislaam wanawazungumzia Wakristu kumbe sivyo - unga ni haramu pande zote mbili..

Anyway nilikuwepo sasa hivi nawaageni endeleeni na mjadala na nawaombea kila la kheri lakini kumbukeni usia wangu.. Mnaiweka mahala pabaya sana Chadema..
Mzee wangu Mkandara,nisome vyema kwenye bandiko langu liliopita.Na bado naona umerudia kosa lile lile,pengine labda ni kwasababu postings ni nyingi na kusoma post smtime kwa umakini it takes time.

Hapo kwenye bold naona umeshindwa kutofautisha kati ya sheria zinazotawala nchi vs zile zinazotawala dini.Wakati kula nguruwe ni uovu ama kosa kwa mujibu wa dini,issue ya madawa ya kulevya certainly ni tofauti.Hayo ni illegal kwa sheria zetu za nchi na mtu anayekula nguruwe hawezi kuchukuliwa hatua sawa na yule anayeuza ama kubwia unga kwa mujibu wa sheria za nchi.Na kudeal na issues hizo ni kwa namna ya tofauti.Sijui kama umeona tofauti hapo mkuu?

Na ndiyo maana nikasema hapo nyuma kuwa,wale wanaochochea udini ni wale wanaounganisha na kufananisha makosa yanayofanywa under mamlaka ya dini ama dhehebu flani vs yale yaliyoko chini ya mamlaka ya serikali pale yanapofanyiwa kazi/uchunguzi.

Katiba ni sheria mama.Sote tunaishi kwa kufuata katiba bila kujali dini zetu.Hilo ndilo la msingi.Issue hii inagusa katiba kwasababu inamgusa rais,serikali yake na vyombo vyake vya dola.Wakati sheria hizo za dini zina govern hayo madhehebu husika pekee.Hii ni iisue yenye maslahi ya kitaifa.Wote bila kujali dini tunapingana nayo.Kula nguruwe hakuathiri maslahi yoyote ya taifa.

Kwa hiyo tusijikute kama crabs in a bucket kwa kuingizwa mkenge na wanasiasa wenye personal agendas.Nchi yetu inahitaji more than this b.s especially these times.

Mkuu Mkandara naamini kabisa kuwa Mh Rais kalianzisha hili makusudi kwasababu anajuwa kuna wanaoendeshwa na emotions.Hiyo ni political tactic.Lakini ukweli ni kwamba badala ya kulishughulikia tatizo hilo,ameamua kulipiga dan dana na kulitumia kimaslahi ya kisiasa.Malumbano ya nini rais mzima?Unawajuwa wauza madawa,wakamate na si ngonjera!Huo ndo ukweli.Route aliyoichagua inaonyesha mawili.

1)Either anawaogopa wauza madawa(listi ni kubwa zaidi ya hao viongozi wachache wa dini)Ina wezekana anawatumia hao viongozi wa dini kama karata ya kuizima issue hii(inawezekana kuna ambao wako protected)

2)Inawezekana pia anawaogopa hao wauza madawa maybe walichangia harakati zake za kuwania urais.(Ili kuwalinda,wamekamata hao vibaka wachache na kuipakazia dini nzima ya ukristo/ukristu kuwa ni ya viongozi wauza madawa.Hili nalo pia litawafanya wafunge mdomo ama ku neutrealize isue nzima.
Under both scenarios.Mh Rais ataumbuka eventually kufuata siasa za kipuuzi.
 
JMushi1,
Majibu hayo ulliyo ya wrap hapo juu sikuyatoa kwako mkuu wangu isipokuwa kwa Kiloni ambaye kaiona video inayokashifu ilihali hii imetolewa na mtu anayeshabikia UDINI. Hizi video zipo nyingi sana na ndio maana nikasema huwezi kukuta waislaam wanatengeneza video kuudhalilisha Ukristu isipokuwa video za kupinga matendo yaliyoharamishwa..haijalishi nani anayafanya kwani Muislaam ni yule aliyejisalimisha kwa bwana.

Na Kafir kwa maana halisi ya neno hili, ni yule asiyemkubali mwenyezi Mungu kwani jina hili la ukafir halikuanza jana. Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W) wakristu walikuwepo tena Wakatoliki tu na waliitwa Wanasarah, Jews wakaitwa Wayahudi na Makafir walikuwepo pia.. kwa hiyo hizi habari za kkusema Wakristu ndio makafir ni hofu ya wenye matendo maovu na sio Ukristu..Tunapozungumzia Infidel sio lazima wawe Wayahudi na wakristu mkuu wangu ni yeyote yule anayepinga ibada za Mweneyezi Mungu kwa kutukuza maovu kwani hata ktk Uislaam ipo surat inayosema Tofauti baina ya Muislaam na Kafir ni SALA.. hivyo Muislaam asiyesali hana tofauti na Kafir yaani pale ni Muislaam jina tu... Je, huoni uzito wa kauli hizi za Mwenyezi Mungu..
 
JMushi1,
Majibu hayo ulliyo ya wrap hapo juu sikuyatoa kwako mkuu wangu isipokuwa kwa Kiloni ambaye kaiona video inayokashifu ilihali hii imetolewa na mtu anayeshabikia UDINI. Hizi video zipo nyingi sana na ndio maana nikasema huwezi kukuta waislaam wanatengeneza video kuudhalilisha Ukristu isipokuwa video za kupinga matendo yaliyoharamishwa..haijalishi nani anayafanya kwani Muislaam ni yule aliyejisalimisha kwa bwana.

Na Kafir kwa maana halisi ya neno hili, ni yule asiyemkubali mwenyezi Mungu kwani jina hili la ukafir halikuanza jana. Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W) wakristu walikuwepo tena Wakatoliki tu na waliitwa Wanasarah, Jews wakaitwa Wayahudi na Makafir walikuwepo pia.. kwa hiyo hizi habari za kkusema Wakristu ndio makafir ni hofu ya wenye matendo maovu na sio Ukristu..Tunapozungumzia Infidel sio lazima wawe Wayahudi na wakristu mkuu wangu ni yeyote yule anayepinga ibada za Mweneyezi Mungu kwa kutukuza maovu kwani hata ktk Uislaam ipo surat inayosema Tofauti baina ya Muislaam na Kafir ni SALA.. hivyo Muislaam asiyesali hana tofauti na Kafir yaani pale ni Muislaam jina tu... Je, huoni uzito wa kauli hizi za Mwenyezi Mungu..
Nimekupata na nilikupata sawia mkuu,najuwa uliilekeza posti ile kwa Kiloni.However niliona ni mfano tosha wa jinsi tunavyo mix up issues kwenye mjadala huu.Issue ya madawa ya kulevya si issue ya kiimani.Si issue ya kikristo ama kiislam.Na rais hakutakiwa kuitolea majibu huko ili kuanzisha mijadala yenye ukinzani wa kidini.Ama vita dhidi ya madawa ya kulevya imegeuka kuwa vita dhidi ya dini mbili?Nilitaka kuweka wazi kuwa kuna utofauti kati ya wauza madawa na nature ya makosa yao vs issues ambazo ziko governed na dini ie ulaji nguruwe nk.

Tusikubali two individual personalities(dini)kutugawanya coz hii si issue kama ya kishabiki ie wa kidini.
Mkuu wa nchi anapenda sana malumbano.Sasa mimi naona ni kama foul play kwasababu amebanwa na wananchi wamechoshwa nahali mbaya ya maisha,ni sawa na kushindwa kwenye ngumi ukaanza kung'ata.Lol!
 
Nimekupata na nilikupa sawia mkuu,najuwa uliilekeza posti ile kwa Kiloni.However niliona ni mfano tosha wa jinsi tunavyo mix up issues kwenye mjadala huu.Issue ya madawa ya kulevya si issue ya kiimani.Si issue ya kikristo ama kiislam.Na rais hakutakiwa kuitolea majibu huko ili kuanzisha mijadala yene ukinzani wa kidini.Nilitaka kuweka wazi kuwa kuna utofauti kati ya wauza madawa na nature ya makosa yao vs issues ambazo ziko governed na dini ie ulaji nguruwe nk.

Tusikubali two individual personalities kutugawanya coz hii si issue kama ya kishabiki ie wa kidini.
Mkuu wa nchi anapenda sana malumbano.Sasa mimi naona ni kama foul play kwasababu amebanwa na wananchi wamechoshwa nahali mbaya ya maisha,ni sawa na kushindwa kwenye ngumi ukaanza kung'ata.Lol!
Ebu nambie rais Muislaam anapokaribishwa ktk jukwaa la wakristu unafikiri anatakiwa kuzungumza vitu gani? He is the President jamani azungumzie mambo ya dini asiyoijua?.. nakuomba tena soma Upinzani wa Askofu against ule wa Kardinali labda utaweza kunielewa kwa nini nakubaliana na askofu sana tu, lakini sikubaliani na Kardinali..

Mkuu nimechoka nimejaribu sana kuwafahamisha lakini naona ile royalty yenu kwa kiongozi wa dini imewashinda hata kuona makosa ya Pengo ila ya JK ambaye kusema kweli sijui as a President angesema kitu gani kuwafurahisha hata baada ya kukamatwa kwa wachungaji wakijihusisha na madawa. It's not easy thing kujua madhehebu yenu na taratibu za kuwakilisha kwa sababu when it comes to Christian issues, U all come as one!
 
Ebu nambie rais Muislaam anapokaribishwa ktk jukwaa la wakristu unafikiri anatakiwa kuzungumza vitu gani? He is the President jamani azungumzie mambo ya dini asiyoijua?.. nakuomba tena soma Upinzani wa Askofu against ule wa Kardinali labda utaweza kunielewa kwa nini nakubaliana na askofu sana tu, lakini sikubaliani na Kardinali..

Mkuu nimechoka nimejaribu sana kuwafahamisha lakini naona ile royalty yenu kwa kiongozi wa dini imewashinda hata kuona makosa ya Pengo ila ya JK ambaye kusema kweli sijui as a President angesema kitu gani kuwafurahisha hata baada ya kukamatwa kwa wachungaji wakijihusisha na madawa. It's not easy thing kujua madhehebu yenu na taratibu za kuwakilisha kwa sababu when it comes to Christian issues, U all come as one!
Una uhakika kuwa hao wauza madawa walikuwa ni viongozi wa katoliki?Tena kama hakuna ndiyo mbaya zaidi.
Mimi sina loyalty yoyote kwa Pengo.Isipokuwa naelewa tofauti kubwa kati ya JK na Pengo.Naelewa sana kwamba kama mh rais yuko serious on the issue ya wauza madawa,basi wala hasingekuwa na haja ya kwenda kupigana vijembe makanisani kama vile wauza madawa wote kwenye hiyo listi yake ni wakatoliki,kwenye hii issue ambayo ilitakiwa iwe ya kuchukuliwa hatua kwasababu alisema lists anazo.Nilisema hapo mwanzo kuwa sasa inaelekea anaitumia hii listi kisiasa zaidi.Kwasababu si kweli kuwa kwenye listi hiyo kuna viongozi wa dini ya kanisa la katoliki.

Je kuna matajiri,wanasiasa nk ambao inasemekana wako kwenye listi amewasema kama alivyofanya kwa hao aliowaita "viongozi wa dini"?
Hakuna niliposema kuna taratibu za kimadhehebu kuwasilisha.Hii ni just a common sense issue.Hii si chrstian issue vs. islam issue,hii ni issue ya kitaifa,ama unataka kusema listi aliyonayo JK ni ya "viongozi wa dini wa kikristo wauza unga" ama ni listi ya wauza unga persee?

Muislam anapokaribishwa kuzungumza kwenye jukwaa la wakristo,inategemea na shughuli inayoendelea.Issue zinazohusisha uchunguzi wa wauzaji wa madawa ya kuleva unahusiana vipi na kuwekwa wakfu na kusimikwa kwa askofu wa kanisa la katoliki?Amefanya generalization kwa nia zake binafsi or maybe za kisiasa or maybe both.
 
Una uhakika kuwa hao wauza madawa walikuwa ni viongozi wa katoliki?Tena kama hakuna ndiyo mbaya zaidi.
Mimi sina loyalty yoyote kwa Pengo.Isipokuwa naelewa tofauti kubwa kati ya JK na Pengo.Naelewa sana kwamba kama mh rais yuko serious on the issue ya wauza madawa,basi wala hasingekuwa na haja ya kwenda kupigana vijembe makanisani kama vile wauza madawa wote kwenye hiyo listi yake ni wakatoliki,kwenye hii issue ambayo ilitakiwa iwe ya kuchukuliwa hatua kwasababu alisema lists anazo.Nilisema hapo mwanzo kuwa sasa inaelekea anaitumia hii listi kisiasa zaidi.Kwasababu si kweli kuwa kwenye listi hiyo kuna viongozi wa dini ya kanisa la katoliki.

Je kuna matajiri,wanasiasa nk ambao inasemekana wako kwenye listi amewasema kama alivyofanya kwa hao aliowaita "viongozi wa dini"?
Hakuna niliposema kuna taratibu za kimadhehebu kuwasilisha.Hii ni just a common sense issue.Hii si chrstian issue vs. islam issue,hii ni issue ya kitaifa,ama unataka kusema listi aliyonayo JK ni ya "viongozi wa dini wa kikristo wauza unga" ama ni listi ya wauza unga persee?

Muislam anapokaribishwa kuzungumza kwenye jukwaa la wakristo,inategemea na shughuli inayoendelea.Issue zinazohusisha uchunguzi wa wauzaji wa madawa ya kuleva unahusiana vipi na kuwekwa wakfu na kusimikwa kwa askofu wa kanisa la katoliki?Amefanya generalization kwa nia zake binafsi or maybe za kisiasa or maybe both.
hakuna sababu ya kubishana zaidi...Soma habari nzima ya Askofu Judae ..Bofya.

 
hakuna sababu ya kubishana zaidi...Soma habari nzima ya Askofu Judae ..Bofya.

Nimekupata mkuu,ni afadhali nimeisoma sasa.Je kuna tofauti yoyote kati ya habari hii na yale niliyokuwa nikiyasema kwenye postings zilizopita?Nashukuru tupo ukurasa mmoja.Alichosema ndicho nilichosema mkuu.
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Rwai'chi apinga kauli ya Kikwete
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"]Send to a friend
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Sunday, 07 August 2011 11:54
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]0diggsdigg

Na Frederick Katulanda, Mwanza
RAIS wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC), Mhashamu Askofu Judae Thaddeus Ruwai'chi, amesema kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwashutumu viongozi wa dini kuwa wanahusika katika biashara ya dawa za kulevya hakuitoa wakati na mahali maufaka.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi Jumapili, mjini hapa juzi, Askofu Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, alisema hakuona busara ya shutuma zile kutolewa na kiongozi wa nchi mahali pale.

Alisema sehemu alipozitolea hapakuwa sahihi kwa vile zinaweza kutafsiriwa kama zilikuwa na lengo la kuwapaka matope maaskofu waliokuwa katika sherehe ya Jubiliee ya Kumsimika Askofu John Ndimbo.

"Sidhani kama kuna Askofu ama Padre aliyekamatwa kwa shutuma hizo zilizotajwa.
Kiongozi wa nchi anapotoa shutuma kama zile ni lazima aamue mahali pa kuzitoa, namna ya kuzitoa na jinsi ya kuzifanyia kazi," alieleza Askofu Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Mwanza.

Juni 5, mwaka huu akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki la Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kuwekwa wakfu na kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kuwa Askofu wa Jimbo la Mbinga, Mhashamu John Ndimbo, Rais Kikwete alisema: "Inasikitisha kuona biashara hii haramu (ya dawa za kulevya) sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, Taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili, baadhi yenu tumewakamata...

Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuielimisha jamii, hususani vijana waweze kuepuka na matumizi ya madawa ya kulevya."

Askofu Mkuu Rwai'chi alisema kama wapo viongozi wanaojihusisha na biashara ya dawa ya kulevya, hilo linajulikana kuwa ni kosa la jinai ambalo halikubaliki kwa sababu linaharibu raia wa nchi na akaitaka Serikali kuwachukulia hatua.

"Sasa kama Rais anajua viongozi wa dini wanaojihusisha na dawa za kulevya, tunapenda kumtia moyo kwamba aviwezeshe vyombo vya sheria kuwashughulikia. Ni lazima ihakikishwe kwamba vyombo vya dola havisaidii uhuni huo, maana haiwezekani nchi yetu ifikiriwe kuwa ni daraja la kuvushia dawa za kulevya," alisisitiza.

Askofu Ruwai'chi alisema kwa sasa Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazotumika kama kituo cha kusafirishia dawa za kulevya Afrika, jambo ambalo lilimshangaza na kuhoji mpaka nchi inafikia hatua hiyo vyombo vya dola vinafanya nini.

"Leo hii Tanzania inafikiliwa kuwa ni kituo muhimu cha kuvushia dawa za kulevya, hivi vyombo vyetu vya sheria vinavyopaswa kusimamia jambo hilo viko wapi, je, serikali yetu imekatwa mikono?" alihoji Askofu.

Hii ni mara ya pili kwa Rais Kikwete kushutumiwa na viongozi wa dini baada ya kutoa kauli hiyo. Kauli ya kwanza kumpiga kauli hiyo ilitolewa na viongozi wa Jumuia ya Makanisa ya Kikristo Tanzania CCT ambao walimpa Rais Kikwete saa 48 za kuwataja kwa majina viongozi wote wa dini anaowatuhumu kuhusika na biashara haramu ya dawa za kulevya. Maaskofu hao walisema endapo Rais atashindwa kufanya hivyo, basi itakuwa aibu kwa nchi.

Akizungumzia hali ya kisiasa na jinsi Bunge la sasa linavyoendeshwa, Askofu Ruwai'chi alisema wabunge wasiposhikamana na kuwa kitu kimoja kwa ajili ya kutetea maslahi ya taifa, nchi haitasonga mbele kimaendeleo.

Rwai'chi alisisitiza kuwa wabunge wanatakiwa kuwakilisha maslahi ya taifa na siyo ya kikundi cha matajiri, kikundi cha dini, kikundi cha kabila au kikundi cha chama.

Askofu huyo alisema lazima Watanzania wakubali kwa dhati kuwa nchi yao kwa sasa ni ya vyama vingi na kwamba, kuwa katika mfumo huo sio kosa.

"Naomba kuweka bayana, tukitaka kupiga hatua ni lazima tukubali haya yafuatayo, kwamba Tanzania ni nchi ya vyama vingi na hili siyo lakujadili leo ni ukweli, lakini pia Tanzania kuwa nchi ya vyama vingi siyo kosa ni mojawapo ya mfumo wa kisiasa ambao unawapa wananchi fursa ya kuchagua na pili unaipa serikali changamoto ya kuwajibika," alieleza Askofu huyo.

Alisema Tanzania ambayo imekuwa chini ya utawala chama kimoja kwa muda mrefu, watu walizoea kufanya mambo bila ya kujua kuwa kuna mbadala, lakini kwa sasa katika mfumo wa vyama vingi kila anayekuwa katika Serikali lazima atambue kuna chama mbadala.

"Katika utawala chama kimoja watu wanaweza wakajifanyia mambo yao jinsi wanavyotaka bila ya kujua kwamba kuna mbadala, lakini katika vyama vingi lazima kila mtu ajue kuna vingine mbadala vya siasa," alisema
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Nimekupata mkuu,ni afadhali nimeisoma sasa.Je kuna tofauti yoyote kati ya habari hii na yale niliyokuwa nikiyasema kwenye postings zilizopita?Nashukuru tupo ukurasa mmoja.Alichosema ndicho nilichosema mkuu.
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Rwai'chi apinga kauli ya Kikwete
[/TD]
[TD="class: buttonheading, align: right"]Send to a friend
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Sunday, 07 August 2011 11:54
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]0diggsdigg

Na Frederick Katulanda, Mwanza
RAIS wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC), Mhashamu Askofu Judae Thaddeus Ruwai'chi, amesema kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwashutumu viongozi wa dini kuwa wanahusika katika biashara ya dawa za kulevya hakuitoa wakati na mahali maufaka.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi Jumapili, mjini hapa juzi, Askofu Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, alisema hakuona busara ya shutuma zile kutolewa na kiongozi wa nchi mahali pale.

Alisema sehemu alipozitolea hapakuwa sahihi kwa vile zinaweza kutafsiriwa kama zilikuwa na lengo la kuwapaka matope maaskofu waliokuwa katika sherehe ya Jubiliee ya Kumsimika Askofu John Ndimbo.

"Sidhani kama kuna Askofu ama Padre aliyekamatwa kwa shutuma hizo zilizotajwa. Kiongozi wa nchi anapotoa shutuma kama zile ni lazima aamue mahali pa kuzitoa, namna ya kuzitoa na jinsi ya kuzifanyia kazi," alieleza Askofu Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Mwanza.

Juni 5, mwaka huu akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki la Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kuwekwa wakfu na kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kuwa Askofu wa Jimbo la Mbinga, Mhashamu John Ndimbo, Rais Kikwete alisema: "Inasikitisha kuona biashara hii haramu (ya dawa za kulevya) sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, Taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili, baadhi yenu tumewakamata...

Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuielimisha jamii, hususani vijana waweze kuepuka na matumizi ya madawa ya kulevya."

Askofu Mkuu Rwai'chi alisema kama wapo viongozi wanaojihusisha na biashara ya dawa ya kulevya, hilo linajulikana kuwa ni kosa la jinai ambalo halikubaliki kwa sababu linaharibu raia wa nchi na akaitaka Serikali kuwachukulia hatua.

"Sasa kama Rais anajua viongozi wa dini wanaojihusisha na dawa za kulevya, tunapenda kumtia moyo kwamba aviwezeshe vyombo vya sheria kuwashughulikia. Ni lazima ihakikishwe kwamba vyombo vya dola havisaidii uhuni huo, maana haiwezekani nchi yetu ifikiriwe kuwa ni daraja la kuvushia dawa za kulevya," alisisitiza.

Askofu Ruwai'chi alisema kwa sasa Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazotumika kama kituo cha kusafirishia dawa za kulevya Afrika, jambo ambalo lilimshangaza na kuhoji mpaka nchi inafikia hatua hiyo vyombo vya dola vinafanya nini.

"Leo hii Tanzania inafikiliwa kuwa ni kituo muhimu cha kuvushia dawa za kulevya, hivi vyombo vyetu vya sheria vinavyopaswa kusimamia jambo hilo viko wapi, je, serikali yetu imekatwa mikono?" alihoji Askofu.

Hii ni mara ya pili kwa Rais Kikwete kushutumiwa na viongozi wa dini baada ya kutoa kauli hiyo. Kauli ya kwanza kumpiga kauli hiyo ilitolewa na viongozi wa Jumuia ya Makanisa ya Kikristo Tanzania CCT ambao walimpa Rais Kikwete saa 48 za kuwataja kwa majina viongozi wote wa dini anaowatuhumu kuhusika na biashara haramu ya dawa za kulevya. Maaskofu hao walisema endapo Rais atashindwa kufanya hivyo, basi itakuwa aibu kwa nchi.

Akizungumzia hali ya kisiasa na jinsi Bunge la sasa linavyoendeshwa, Askofu Ruwai'chi alisema wabunge wasiposhikamana na kuwa kitu kimoja kwa ajili ya kutetea maslahi ya taifa, nchi haitasonga mbele kimaendeleo.

Rwai'chi alisisitiza kuwa wabunge wanatakiwa kuwakilisha maslahi ya taifa na siyo ya kikundi cha matajiri, kikundi cha dini, kikundi cha kabila au kikundi cha chama.

Askofu huyo alisema lazima Watanzania wakubali kwa dhati kuwa nchi yao kwa sasa ni ya vyama vingi na kwamba, kuwa katika mfumo huo sio kosa.

"Naomba kuweka bayana, tukitaka kupiga hatua ni lazima tukubali haya yafuatayo, kwamba Tanzania ni nchi ya vyama vingi na hili siyo lakujadili leo ni ukweli, lakini pia Tanzania kuwa nchi ya vyama vingi siyo kosa ni mojawapo ya mfumo wa kisiasa ambao unawapa wananchi fursa ya kuchagua na pili unaipa serikali changamoto ya kuwajibika," alieleza Askofu huyo.

Alisema Tanzania ambayo imekuwa chini ya utawala chama kimoja kwa muda mrefu, watu walizoea kufanya mambo bila ya kujua kuwa kuna mbadala, lakini kwa sasa katika mfumo wa vyama vingi kila anayekuwa katika Serikali lazima atambue kuna chama mbadala.

"Katika utawala chama kimoja watu wanaweza wakajifanyia mambo yao jinsi wanavyotaka bila ya kujua kwamba kuna mbadala, lakini katika vyama vingi lazima kila mtu ajue kuna vingine mbadala vya siasa," alisema
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Yes mkuu wangu ipo tofauti kubwa kati ya maelezo ya Kardinali Pengo, Mokiwa siku zile akimpa JK masaa 48 na huyu Askofu Judae....Huwezi kuhalailisha makosa kwa makosa mengine.. halafu hii list sio ile ya Amina Chifupa bali ni hotuba yake ktk sherehe ya Kikristu ambayo hakusema anayo list ya wauza unga ila hawakupenda JK kulizungumzia swala hilo pale..

Askofu Judae kaonyesha hekima na busara kubwa sana tofauti na viongozi wengine kwa sababu hata mimi Muislaam au nisiyekuwa na dini naweza kumwelewa na kukubaliana naye lakini sio hawa jamaa wengine walioonyesha dharau as if nchi hii inatawaliwa kidini.. Yes, JK made a mistake lakini haiwapi nafasi viongozi wa dini nao kufanya makosa.. two wrong can't make it right..
 
Ebu nambie rais Muislaam anapokaribishwa ktk jukwaa la wakristu unafikiri anatakiwa kuzungumza vitu gani? He is the President jamani azungumzie mambo ya dini asiyoijua?.. nakuomba tena soma Upinzani wa Askofu against ule wa Kardinali labda utaweza kunielewa kwa nini nakubaliana na askofu sana tu, lakini sikubaliani na Kardinali..

Mkuu nimechoka nimejaribu sana kuwafahamisha lakini naona ile royalty yenu kwa kiongozi wa dini imewashinda hata kuona makosa ya Pengo ila ya JK ambaye kusema kweli sijui as a President angesema kitu gani kuwafurahisha hata baada ya kukamatwa kwa wachungaji wakijihusisha na madawa. It's not easy thing kujua madhehebu yenu na taratibu za kuwakilisha kwa sababu when it comes to Christian issues, U all come as one!
mkuu nilikuwekea bandiko la JK alivyosema akiwa mwanza na maaskofu kuhusu madawa ya kulevya na alichosema wiki moja baadaye alivyokutana mbinga na maaskofu wa kikatoliki..! Rudi nyuma soma alichosema alipokuwa mwanza halafu tafakari..! Kule mwanza hakusema baadhi yenu tumewakamata ila alizungumzia vizuri tu kuhusu madawa ya kulevya! kuna mtu alipiga kelele? No ...! Kile alichokifanya mbinga hakikuwa bahati mbaya bali killikuwa intentional kabisa....!
 
Mkuuu wangu hakika nimekusoma wewe pamoja na majibu ya wengine woote ya kutambua ya kwamba hapa ni swala la IMANI.. chuki yenu kwa Kikwete sio kwa sababu nyingine isipokuwa Muislaam.. Na wala usijali mimi sina jazba kama mlokuwa nayo nyie, Hata huyo Pengo anaweza kuja siku ya Idd Fitr akazungumzia wauzaunga wanaokwenda Hijja namadawa ya kulevya - hakuna shida yeyote maadam anasema Ukweli! na wala hatakuwa na haja ya kuwataja wauza Unga.
Acheni Udini wenu kusema JK hakutakiwa kusema hayo kwenye sherehe ya Wakristu lakini Pengo anaruhusiwa kumsema JK na mambo ya Unga kwenye sherehe ya Wakristu...
- Kardnali Pengo alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, alipokuwa akiongoza ibada ya maadhimisho ya miaka 50 ya Tanzania, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Kristu Mfalme Parokia ya Tabata.


Sasa, wewe ulitegemea Kardinali Pengo atumie venue gani kujibu tuhuma za Kikwete? Aende TBC au kuitisha mkutano na Waandishi wa Habari? Hawezi kufanya hivyo, sababu yeye ni Kiongozi wa dhehebu la Wakatoliki, na kama angeamua kujibu (kama alivyofanya), basi ni sahihi kuwa amefanya hivyo mbele ya walengwa wa tuhuma hizi, ambao ni Waumini wake.

Kwa kukukumbusha tu, tofauti na Kiwete, Mhashamu Kardinali Pengo hakuteuliwa au kuchaguliwa na Waislamu, Wahindu, Wapagani au sijui nani. Anawakalisha Dhehebu la Wakatoliki, kwa hiyo hana ulazimu wala wajibu wa kuwaridhisha Watanzania wenye imani tofauti zaidi ya ile anayowakilisha.
 
Fredy Azzah na Ibrahim Yamola

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amesema Watanzania wanasherehekea miaka 50 ya uhuru huku kukiwa na makundi ya viongozi na vigogo nchini wanaojineemesha kupitia migongo ya wananchi bila kujali wanawasaliti, wanawaongezea umaskini na kuwaua.

Kardinali Pendo alilaani akisema: “hayo yamekuwa yakitendeka kinyume na misingi iliyoainishwa na waasisi wa taifa wakati wakidai uhuru kutoka kwa wakoloni ambapo walitamani kujenga Tanzania yenye utukufu.

Kardnali Pengo alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, alipokuwa akiongoza ibada ya maadhimisho ya miaka 50 ya Tanzania, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Kristu Mfalme Parokia ya Tabata.

“Waasisi wetu walipokuwa wanapigania uhuru wa taifa hili, lengo na maono yao yalikuwa kutengeneza taifa lenye utukufu, lenye kutawala mataifa mengine …,” alisema Kardinali Pengo na kuongeza:

“Katika miaka 50 tunayoikamilisha, kumekuwa na mafanikio na changamoto nyingi tu, inabidi tujipange ili watakao kuja kuadhimisha miaka 100, au hata miaka 25 ijayo wasije wakasema afadhali wakati wa mkoloni.”

Katika ibada hiyo ambayo pia ilitumika kuliombea taifa, Pengo alisema wakati wa kupigania uhuru lengo ilikuwa ni kulifanya sehemu salama na bora ya kuishi watu wake.

Kardnali Pengo alitahadharisha akisema: “Lakini sasa Taifa lina makundi ya watu wasaliti, wenye ubinafsi na ambao wako tayari kujitafutia utukufu hata ikibidi kuwakandamiza na kuwaua wenzao”.

Kwa sababu hiyo akawataka Watanzania kutafakari katika kipindi hiki cha kuadhimisha miaka 50 ya uhuru, wajiulize wamekuwa wakijitafutia utukufu binafsi au ule ulioasisiwa na taifa wa wananchi wote kufaidi matunda yake.

Kwamba, tumepata utukufu wa aina gani?” Alisema Kardinali Pengo na kuonya; "Baadhi ya watu wanapata utukufu bila hata kujali kama watu wengine wanakufa, jambo ambalo ni hatari kwa taifa."

Kardinali Pengo aliwaonya waliopewa dhamana ya uongozi na kutumia nafasi hiyo kujitajirisha, kuwa ni usaliti kwa Taifa na Watanzania kwa ujumla.

Tuhuma za dawa za kulevya
Katika hatua nyingine, Kadinali Pengo, alilaumu mtindo wa viongozi wa Serikali na dola kutotaja hadharani majina ya watu wanaowatuhumu kuhusika na biashara ya dawa za kulevya huku wakiendelea kulalamika kuwa wapo na wamewakamata.
Alisema hali hiyo haionyeshi nia yao ya dhati katika kupambana na biashara hiyo haramu.

Akikumbushia kauli aliyoitoa Rais Jakaya Kikwete wakati wa Sikukuu ya kumwekwa wakfu na kumsimika Mhashamu Askofu John Ndimbo kuwa Askofu wa Jimbo la Mbinga kuwa baadhi ya viongozi wa dini huuza dawa za kulevya, alisema alitakiwa kuwataja.

Kardinali Pengo alisema kitendo cha Rais Kikwete pamoja na baadhi ya viongozi waliojitokeza kuzungumzia suala hilo huku wakisema hawawezi kuwataja kwa majina, huo ni usaliti mkubwa kwa taifa.

“Haiwezekani mtu mkubwa tu, wala siyo mdogo kuja katika eneo la Kanisa la Katoliki, kukiwa kumejaa Maaskofu kutoka karibu nchi nzima, unasema maneno haya halafu unasema, siyo nyie ni viongozi wa makanisa madogomadogo," alilalamika Kardinali Pengo.

Aliongeza kwamba: "Kama ndivyo hivyo kwa nini sasa uje kuyasema maneno hayo katika eneo la Kanisa Katoliki."

Akasisitiza: "Mapadri, watawa; naomba tujiangalie kama sisi tunaguswa na hii kauli, kama haitugusi tumshukuru Mungu, lakini ni vyema hawa watu wakatajwa.

Hata kama ni mimi njoo uniambie, ukisema hunitaji kwa sababu ni kiongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam, huo ni usaliti mkubwa kwa taifa.”

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Uratibu na Bunge, William Lukuvi, aliwahi kuliambia Bunge hivi karibuni kuwa Serikali ina safari ndefu katika kufanikisha mkakati wa kukomesha biashara hiyo haramu.

Alisema Serikali inaamini kuwa vita ya kuwakamata wanaojihusisha na dawa za kulevya ni ngumu lakini akasisitiza kuwa anaamini mwishowe watashinda uhalifu huo.

Lukuvi alisema mbali na kuwataja hadharani baadhi ya viongozi wa dini, imebainika kuwa wana mtandao mkubwa.

“Hapa sio kuwataja tu maana kama ni kuwataja tayari Serikali ilikwisha wataja na watu wanajua kuwa kiongozi wao ni yule Askofu wa Nigeria, lakini hapa suala ni namna ya kupambana na kuwajua wengine,’’ alisema Lukuvi.

Hata hivyo, mara baada ya Rais Kikwete kutoa kauli hiyo, Jumuia ya Kikristo Tanzania (CCT), ilikuja juu na kumpa saa 48 za kuwataja hadharani viongozi wa madhehebu ya dini wanaohusika na biashara hiyo haramu.

"Rais ataje majina ni kina nani wanahusika na ndani ya saa 48 awe ameyataja la sivyo itakuwa ni aibu zaidi kwake na Serikali," alisema Makamu Mwenyekiti wa CCT, Askofu Dk Valentino Mokiwa.

Rais Kikwete alijibu wito huo kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu kwamba, viongozi wa dini siyo malaika kwa hivyo wasijivune kuwa hakuna miongoni mwao ambao ni wahalifu.

Source: Gazeti la Mwananchi

My take:
Kweli Pengp amesummarise vizuri behaviour za Kikwete kuwa ni msaliti maana kuna matukio mengi yametokea na hajatoa kauli wala kuchukua hatua zozote sasa kama huu si usaliti kwa wananchi ni nini?

Mimi nampongeza sana Pengo, ****** analeta unafiki wake kanisani!
 
Mtoto akizoea kudekezwa. Kufa afi ila Sasa chamoto atakiona

Nimekumbuka JKT RUVU combania A kwa Sir meja URASA.

Hiyo mama iyo lele, hiyo mama iyo lele.
mtoto analilia nini?
Mtoto analilia jeshi?
Sisi waalimu tutatangulia mbele.
tembea shoto kulia mwisho tutafika
...
..
 
mkuu nilikuwekea bandiko la JK alivyosema akiwa mwanza na maaskofu kuhusu madawa ya kulevya na alichosema wiki moja baadaye alivyokutana mbinga na maaskofu wa kikatoliki..! Rudi nyuma soma alichosema alipokuwa mwanza halafu tafakari..! Kule mwanza hakusema baadhi yenu tumewakamata ila alizungumzia vizuri tu kuhusu madawa ya kulevya! kuna mtu alipiga kelele? No ...! Kile alichokifanya mbinga hakikuwa bahati mbaya bali killikuwa intentional kabisa....!

Ni lazima kuwaweka wazi hawa, ni wauza Madawa wakubwa na 40 ZAO ZIMEFIKA. sAFARI HII MAPAMBANO YATAANZIA Kanisani. Huwezi kurtumia Biblia kuuza madawa ya kulevya.
 
mkuu mkandara bado upo humu...! Mkuu ile kauli ya kikwete ilitukwaza sisi wakatoliki wote ...kwa hiyo ondoa kabisa katika mawazo yako eti kwa sababu tu Pengo kasema ndiyo maana tunamtetea kwa sababu tunaamini yeye hawezi kufanya makosa! Pengo ni binadamu na ana mapungufu yake mengi tu kama binadamu. Sema kauli yake kama kiongozi wa kanisa katoliki ina uzito fulani kama vile ya Kikwete ambaye ni rais wetu.

Tunafahamu wazi, unapoambiwa mtoto wako ni MWIZI ITAWAKERA UKOO MZIMA. Lakini huu ndio ukweli, na kama tunataka kukomesha madawa ya kulevya ni lazima tuanzie huko. Pole sana kwa kukereka, Rais kama kiongozi wa nchi lazima aseme ukweli.
 
Nimesoma maoni mengi kwenye makala hii.ni wazi Pengo alifanya makosa kumtumpia rais bango,kwani angeweza kumwambia faragha.lakini jeuri ya kanisa ya mtandao,taasisi na mazoe yamfanya Pengo akose subira na kutoa ya moyoni kwake.Dunia ya sasa,jitihada za JK zafanya mazoea hayo ya kanisa yasipate mashiko
 
Tunafahamu wazi, unapoambiwa mtoto wako ni MWIZI ITAWAKERA UKOO MZIMA. Lakini huu ndio ukweli, na kama tunataka kukomesha madawa ya kulevya ni lazima tuanzie huko. Pole sana kwa kukereka, Rais kama kiongozi wa nchi lazima aseme ukweli.
Ni lazima kuwaweka wazi hawa, ni wauza Madawa wakubwa na 40 ZAO ZIMEFIKA. sAFARI HII MAPAMBANO YATAANZIA Kanisani. Huwezi kurtumia Biblia kuuza madawa ya kulevya.
-----------------------

Exactly tunachokitaka sisi wakatoliki! Awaweke wazi...umesema mwenyewe kwa maneno yako..! Na sisi tunataka afanye hivyo ..siyo anakuja kwenye ibada yetu halafu anasema baadhi yenu tumewakamata mnajihusisha na madawa ya kulevya lakini mwisho wa siku inakuja kujulikana aliyekamatwa ni mchungaji wa kanisa la kijiweni waki Nigeria! Naona sasa tumefikia pazuri maana naona na baadhi ya waislam mnmtaka kikwete awaweke wazi hao watu! Tunamkaribisha sana aanzie kanisani kuwaweka wazi na kuwashughulikia hao watu akimaliza aendeleze zoezi lake sehemu nyingine....! Kikwete awe na ujasiri wa mwanamke mjamzito..period!
 
Nimesoma maoni mengi kwenye makala hii.ni wazi Pengo alifanya makosa kumtumpia rais bango,kwani angeweza kumwambia faragha.lakini jeuri ya kanisa ya mtandao,taasisi na mazoe yamfanya Pengo akose subira na kutoa ya moyoni kwake.Dunia ya sasa,jitihada za JK zafanya mazoea hayo ya kanisa yasipate mashiko
In short ...JK kauli zake mwenyewe nidyo hazina mashiko......hawezi kuzitetea kauli zake wala kuzisimamia!
 
Back
Top Bottom