mzee wa njaa
JF-Expert Member
- Jun 16, 2011
- 1,363
- 224
Huwa mi si muumini wa kauli za JK, manake asilimia 99 zina unafiki na utata mwingi.............................
Mkuu wangu Bakwata waseme nini?.. kama kuna watu wamekamatwa na mkanda upo umeonyesha wauza unga, wao wanatakiwa kujitetea kitu gani... Jamani tuwe wakweli hivyo vyombo vya dini siku hizi ni biashara tupu hakuna cha Saint kamba tupu..kote huko unga na biashara haramu kwa kwenda mbele sii kanisani wala misikitini..Uliona wapi mtu mwenye msikiti au Kanisa ndio hutajirika! - Yaani kanisa au msikiti imekuwa biashara - kwa kuuza kitu gani?
Bakwata imechomekwa hapo ili jk aukwepe mtego wa kuitwa yeye mdini lakini ukweli ndo huo raisi aliapa kuitete kuilinda na kuisimamia katiba ya jamhuri ya muungano leo badala ya kuwashitaki au kuwatafuta wauza madawa anaanzisha mipasho. Siku nikipata visa ya Rwanda hamnioni Tz
Mkuu wangu Bakwata waseme nini?.. kama kuna watu wamekamatwa na mkanda upo umeonyesha wauza unga, wao wanatakiwa kujitetea kitu gani... Jamani tuwe wakweli hivyo vyombo vya dini siku hizi ni biashara tupu hakuna cha Saint kamba tupu..kote huko unga na biashara haramu kwa kwenda mbele sii kanisani wala misikitini..Uliona wapi mtu mwenye msikiti au Kanisa ndio hutajirika! - Yaani kanisa au msikiti imekuwa biashara - kwa kuuza kitu gani?
<br />Nitoe shukrani zangu za dhati kwa msimamo wa JK. Asikate tamaa kuibana kanisa na misikiti wazidi kuona aibu na hatimaye kuacha (kama kweli wanafanya hiyo biashara chafu).<br />
<br />
Kazi ni ngumu ... kila mtu anajua institutions hizi za makanisa ni za nchi kubwa kubwa za kimagharibi na kupambana nazo lazima utembee kwenye mstari mwembamba sana! Kumbukumbu ya watu wa mungu kubaka watoto bado mbichi (kanisa lilikana sana hili!) na lisemwalo hapa lipo.
Kwa nini serikali haiwataji wahusika na hiyo biashara ya madawa ya kulevya badala yake inaendelea na danadala kati ya wahusika na kutoa tu tuhuma za jumla bila kutaja jina la wahusika na hatua stahiki? Je ni propaganda za kuwapakazia kashfa viongozi wa dini? Rais anaposema watu wa Mungu wanafanya biashara ya madawa ya kulevya inawalenga watu binafsi au hao viongozi wa dini? Woga gani ulioishika serikali kwikwi ya kutaja hadharani majina ya wauza unga?
<br />Binafsi naona wengi wetu waliochangia hii habari wanaingiza "bias" zao bila kugusa issue husika!Madawa ya kulevya ni haramu na sheria zetu za nchi ziko wazi kabisa kuhusu hilo!Kama kuna watu wanajulikana kuwa ni wauza/wasambazaji madawa hayo na mpaka mikanda ya video ikaandaliwa,je kwa nini wasikamatwe na kufunguliwa mashtaka?kwa nini mikanda ikaonyeshwe wabunge na sio kupelekwa mahakamani? Tukumbuke wakati wa kampeni na hata baada ya uchaguzi Jk aling'ang'ania sana hoja ya udini! Isijekuwa ni mwendelezo wa sumu hiyo na ndo maana alitolea pia kauli hiyo ktk hadhara ya wakatoliki kwa kuamini kuwa mpinzani wake mkuu i.e Dr Slaa alitumwa na alipewa nguvu na kanisa katoliki!!!&nbsp;<br>Yote tisa,kumi ni kwamba JK alipoapishwa kuwa raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania aliweka kiapo cha kulinda nchi na watu wake!Kulinda nchi kumeshamshinda kwani hata ndege za kijeshi za nchi nyingine zimeweza kuingia nchini na kubeba wanyama wetu hai bila kubughudhiwa na yeyote! Sasa la kulinda watu wake nalo limeshamshinda pia kwani kama anawajua wauza unga kwa nini asitumie mamlaka tuliyompa kuwalinda watu wake wasiendelee kuangamizwa na madawa hayo,kwa kuwakamata wahusika badala ya kupiga porojo?<br>Nafikiri wabunge walioona huo mkanda na kulia ni wanafiki tu,kwani wangalikuwa na uchungu wa kweli walipomaliza kuuona wangalitoka na tamko zito la kumtaka rais achukue hatua za haraka ama vinginevyo apigiwe kura ya kutokuwa na imani naye!!!<br>Tukumbuke athari za madawa hayo hazichagui kama mtumiaji ni mkristo au mwislamu,ni cuf au ccm,ni mmatumbi au mpare,ni msomi au bongolala,kijana au mzee nk nk. Kumshambulia JK kuhusu hili la kutokuwajibika hakuhusiani na uislamu wake wala u ccm wake bali unahusika ni kiapo
alichokula cha kukubali kuwa raisi wa Jamhuri hii. Tuunganishe nguvu zetu
wote.<br><br><br>