Pengo amtolea uvivu Kikwete

Pengo amtolea uvivu Kikwete

Inampasa Pengo kusoma alama za nyakati. na kuelewa kuwa Si kila wakati jogoo anawika na kuwa kuwika kwa jogoo kunahitaji Busara.



Atumie hekma kabla kutoa matamko.

Hivi yule msaidizi wake mahir sana Askofu Kilaini yupo wapi? kwani huyu alikuwa na busara sana na kuweza kumfanya kila wakti bosi wake isimpuruchuke
 
Hivi eneo la kanisa sio Tanzania??


UKIISIKIZA HII VIDEO UTAJUA KANISA TZ NI KITU GANI

KAMA HUNA WAKATI (PELEKA MBELE) SIKILIZA JAPO DAKIKA 10 ZA MWISHO

[video]http://blip.tv/mzalendonet/wakristo-wa-tanganyika-walishirikiana-na-wajerumani-kuwaua-waislam-2-5442111[/video]
 
Kwanini asiliseme hilo kwenye kanisa la lutheran, pentekoste, anglikana, victor gospol church aende akaseme kanisa katoliki? Na ni kwanini akiambiwa awataje viongozi wa dini wanaouza madawa hawataji? HUYU ****** NI MNAFKI SN NIA YAKE ILIKUA KULICHAFUA KANISA KATOLIKI, KUMBUKA DR SLAA NI MKATOLIKI ANAANDAA MAZINGIRA YA KUMTENGENEZEA KESI.

Kama huna hoja nyamaza! unaambiwa aliyasema hayo alipokuwa katika misa ya kuadhimisha miaka 50 ya uhuru, wewe unasema kwanini asiliseme hilo kwenye kanisa la lutheran, pentekoste etc! kwani yeye ni Kardinali wa kanisa gani? Nyie ndio mliolishwa sumu eti Dr. Slaa amepandikizwa na kanisa Katoliki, hivyo kila kinachohusu kanisa hilo mnakiunganisha na Dr. Slaa - mmeishiwa!

Awaye yeyote yule bado hoja iliyosemwa ni muhimu na ndio ijadiliwe hiyo. kama kwako miaka 50 ya uhuru una maisha bora yenye full umeme, maji safi 24 hrs, huduma za kijamii kama hospitali na shule mnapata bila wasiwasi tuache sie tunaopigika tujadili.
 
Inampasa Pengo kusoma alama za nyakati. na kuelewa kuwa Si kila wakati jogoo anawika na kuwa kuwika kwa jogoo kunahitaji Busara.



Atumie hekma kabla kutoa matamko.

Hivi yule msaidizi wake mahir sana Askofu Kilaini yupo wapi? kwani huyu alikuwa na busara sana na kuweza kumfanya kila wakti bosi wake isimpuruchuke
Ni busara ya kutosha aliyoitumia kumjibu mwalikwa mmoja mpuuzi aliyemkaribisha kwenye hafla yake na kumtusi mbele ya wageni wake. Ni busara kubwa aliyoitumia kutokumjibu huyo mpuuzi pale pale. Ni tafakari kubwa sana aliyofanya kukaa na hilo tusi hadi wakati huu. Na huu usipotoshwe aliwaeleza viongozi wenzake kuwa kitendo cha kiongozi mkuu wa aliyekosa busara kutumia maeneo ya kanisa kutoa kauli chochezi kiasi hiki inaashiria kuwa kuna tatizo ndani ya kanisa. Kama kweli kiongozi huyu wa nchi asipowataja hao mapadri na viongozi wa dini wauzaji wa mihadarati ili kumsaidia Pengo kufanya maamuzi magumu ambayo yeye JK wakati wote ameshindwa NI USALITI. turudie wote NI USALITI. MKUBWA.
 
Kwanza kabisa, usijaribu hata kidogo kumlinganisha kiboda kama Kikwete na Obama. There's simply no comparison. Kubali, usikubali, Marekani siyo Tanzania, sawa? Pili, ni wazi hii ishu huielewi, vinginevyo usije kuja na kauli za namna ya "kama Mkapa angekuja na usema kuna baadhi ya Masheikh wanajihusisha na biashara za Unga iwe siku ya Maulidi au sijui Idd Fitr , mimi sioni makosa unless Mkapa ktk hotuba yake ahalalishe matumizi ya Unga."

Pengo siyo tu kwamba amehudhunishwa sana bali pia ni wazi amekosewa heshima na kudhalilishwa na Rais ambaye amechaguliwa na wapiga kura waliyo Waislamu na Wakristo na ambaye alialikwa kwenye shughuli hiyo kwa nia njema, na baadaye kuwageuka walioyomulika kwa kuanza kubwata kuhusu "ufahamu wake wa wauza unga" mbele ya kadamnasi ya Wakristo Wakatoliki tu. Jee, hii inaashiria nini kwa mtu mwenye akili zake timamu?

Nakuunga mkono mia kwa mia! kauli ya JK kuhusu viongozi wa dini wauza unga haikupaswa kutolewa katika mwaliko ule aliopewa na wakatoliki kule Songea. Hoja yake hata kama ilikuwepo rais hakuwa amesoma mazingira, kwani kabla hajatoa kauli kama hizo alipaswa kujiuliza kama audience inafaa, muda ni muafaka,etc na si tu kwa kuwa ni rais basi anaweza kusema chochote kwa yeyote na saa yoyote - ataonekana juha! rais anapaswa kuongozwa na uhalisia zaidi kuliko kuongozwa kwa hisia! Hoja nzuri inaweza kuharibiwa na approach inayotumiwa!
 
Huyo Kikwete alifanya makusudi kabisa kutumia wadhifa wake na occasion au hafla husika, ambayo ilikuwa mbele ya "waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kupewa daraja la uaskofu" kuja na kauli zake ambazo mpaka leo ameshindwa kuthibitisha licha ya kutakiwa kufanya hivyo na walengwa.

Kwa hiyo, kutokana na mazingira kama haya, ni nini cha kushangaza kwa hatua hii ya Kadinali Pengo kama Mkuu wa Kanisa Katoliki ku-react kwa kutoa kauli ya wazi kwa Watanzania wote kama alivyofanya Kikwete mbele ya umma ya Watanzania wote? Tunasubiri Kikwete atoe kauli kama hiyo mbele ya Iddi Baraza ijayo dhidi ya wauza unga wa Kislamu ambao kwa miaka mingi wamekithiri na wamekuwa wakitumia kivuli cha kwenda hijja Mekka kuingiza madawa kutoka nchi za Kiislamu kama Afghanistan, Iran na Pakistan.
Mkuuu wangu hakika nimekusoma wewe pamoja na majibu ya wengine woote ya kutambua ya kwamba hapa ni swala la IMANI.. chuki yenu kwa Kikwete sio kwa sababu nyingine isipokuwa Muislaam.. Na wala usijali mimi sina jazba kama mlokuwa nayo nyie, Hata huyo Pengo anaweza kuja siku ya Idd Fitr akazungumzia wauzaunga wanaokwenda Hijja namadawa ya kulevya - hakuna shida yeyote maadam anasema Ukweli! na wala hatakuwa na haja ya kuwataja wauza Unga.
Acheni Udini wenu kusema JK hakutakiwa kusema hayo kwenye sherehe ya Wakristu lakini Pengo anaruhusiwa kumsema JK na mambo ya Unga kwenye sherehe ya Wakristu...
- Kardnali Pengo alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, alipokuwa akiongoza ibada ya maadhimisho ya miaka 50 ya Tanzania, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Kristu Mfalme Parokia ya Tabata.

 
wEwE uNafiKiRi jInA lA kWaNzA lItAkUwA lA nAnI kAMa SiO lA.........! nafikiri mamlaka ya kuzuia madawa ya kulevya inafaa kulaumiwa pia japo wanalinda maslahi ya matumbo yao manake mbona vikaragosi wanawataja bila kuwafikisha kwa Prezidaa!!
 
Mkuu Mkandara,kuna tofauti kati ya "wakristu" na "wakristro"
Tuhuma za madawa ya kulevya si za dini moja ama nyingine.Janga lake ie madhara,ni kwa wote bila kujali dini.Waathirika si wa dini moja peke yake.Hili ni janga la kitaifa,ambalo lilitakiwa liwe treated accordingly.

Mkuu wa nchi anapowafahamu watuhumiwa,hiyo ni furaha kwa wananchi kwasababu wanajuwa sasa hatua itachukuliwa.However isue hii imegeuzwa na mkuu wa nchi kuwa ya kisiasa na zaidi kama mipasho na vijembe ili kuweza tu ku score political points bila kujali madhara yake ie udini.JF ni kipimo tosha kabisa cha yale yanayotokea huko mitaani in reality kwasababu sisi ndo wanajamii.Hivyo naona kwa kiasi fulani JK and compan have succeeded on spreading these politics of divisions.

Kama mkuu wa nchi,tulitarajia angesema viongozi wa madhehebu flani na flani wamefikishwa mahakamani na serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwa kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.Hakufanya hivyo.

Nimegunduwa pia kuna dalili za kutoelewana kati ya dini zetu, pamoja na tafsiri zinazofanywa na upande mmoja wa dini kutofahamu yale ya wenzao wa dini ya tofauti na hivyo tafsiri nyingi kama nilivyoona humu zimeonekana kuwapotosha baadhi yetu zaidi,badala ya kuwapa ufahamu kuhusu dini za tofauti za wenzao na namna ya kuchukuliana.Hapa sasa naona kuna wanaounganisha yanayotokea ndani ya kanisa la katoliki "wakristu" vs yale yanayotokea nchini kwa ujumla ie bishara ya madawa ya kulevya.Na pia yale yanayotokea kwenye madhehebu ya "wakristo"

Kufananisha issues za dini/madhehebu vs zile za kitaifa na zenye kutakiwa kuchukuliwa hatua na serikali ya jamuhuri,ni issue mbili tofauti kabisa ambazo wenye nia mbaya na taifa hili ambao wanamshabikia JK wanajaribu kuziunganisha ili kuscore political points.Wakati issue hizo wanazozizungumzia ie ubakaji wa baadhi ya mapadri,humalizwa ndani ya kanisa kwa mujibu wa taratibu zao kama hakuna kesi.Where as issue ya madawa ya kulevya humalizwa na serikali.

Ni iisue ya kuchukuliwa hatua na si kufanywa kuwa ya kisiasa.Serikali ya jamuhuri ndiyo inawashitaki wauza unga where as mapadri wanashitakiwa chini ya sheria zao za dini ama vatcan.Issue ya unga ni majukumu ya serikali,inachotakiwa ni wao kutuambia wamefikia wapi na uchunguzi na si kusema eti tunawajua.Sana sana ni kama anawapa muda wa kuficha ushahidi wale ambao inaonekana hathubutu kuwagusa.Na hapo ndo mashaka yakuja kama ni kweli serikali hii ina nia ya kuwashughulikia wauzaji hao wa madawa ya kulevya.Serikali haitaki kufanya hivyo,na ina kila sababu ya ku divert attention kwasababu imeprove failure in almost everything that has to do with accountability.

Rais angekuwa ni smart enough na mwenye kujuwa majukumu na nguvu alizonazo kikatiba,pamoja nakuwa yeye ni amiri jeshi muu,pia ana mahakama,polisi na bunge.Vyote ni rubberstamps zake,kwa nguvu hizo hakutakiwa kuja na porojo na mipasho.Kiungawana, asingeisemea kauli ile mahali pale.Unless nia yake ni kuwapaka matope wakristu kuwa viongozi wao wa dini ni wauza unga.Hata hivyo wale wanaigeria walikoamatwa si kwakristu bali ni "wakristo."Mh Rais ameshindwa kugundua utofauti wa mgawanyiko wa kimadhehebu kwenye dini za watanzania anaowatawala.Ambao wengi wao walimpigia kura na sasa wanaamibiwa kuwa hawampendi eti kwasababu yeye ni muislam?Hizi ni siasa za sewage.Ninashangazwa sana ni kwanini inaonekana kama vile mh rais ana instigate udini.

Kwa kumalizia,nimesikitishwa sana na wale walioingia mkenge wa JK na wafuasi wake wenye mwelekeo wa kidini na ambao wamejipanga kujilinda kwa namna hiyo endapo wakiondolewa madarakani.Kama ni listi ya madawa,JK alikuwa nayo toka 2006.Na akaikalia hadi hapo alipokwenda huko kwenye kanisa la katoliki na kudai kuwa viongozi wa dini ni wauza unga.Hiyo si nia mbaya na usaliti kwa watanzania?Hata wale wenye kuremba na kusema hajawasaliti.Kiukweli amewasaliti watanzania big times!Kuna watu waliokuwa wakiuliza na kufuatilia haya mambo huko bungeni ie the late Amina Chifupa.Maisha yao yamekatika ghafla like a candle in the wind.Wako wapi?Anajuwa kuwa hii issue inahitaji nguvu na mamlaka yake.Unless atueleza nini kinamfunga kuchukua hatua.

Mh rais acha kuliingiza Taifa kwenye matatizo makubwa zaidi ya yale ambayo umeshalisababishia taifa hili either kwa kujuwa,kutokujuwa ama kushauriwa na wale wanaokuzunguka ambao wanafikri kama wewe.Nina amini kwenye ile listi yako ya 2006 kuna wafanyabishara,na hata viongozi wa kisiasa.Sasa utagenerilise na kusema wafanyabishara ni wauza unga kwenye uzinduzi wa biashara?Ama utasema wanasiasa wanachama wa ccm ni wauza unga kwenye kwenye hafla ya kumwampisha katibu mkuu wa ccm ama kiongozi wa chama?Acheni siasa za hatari.Mnashindwa kuwa na empathy,na ninadhani mnafanya haya makusudi.Na nyie washauri wa JK pia ninawaonya muachane na hizi siasa kwasababu Taifa tayari liko pabaya.Ni maoni tu.
Tuendelee na mjadala.
 
JMushi1,

Mkuu hapana utanisamehe sana, sitokubaliana na wewe ktk hili kwa sababu hata mimi nataka sana JK aondolewe madarakani lakini sio kwa njia hii ya Udini na ufitini.. Hapa inaonyesha wazi UDINI wanaojaribu kuupandikiza hawa jamaa zangu na kama unaweza rudia kusoma hoja za watu humu.. It's all about JK being a Muslim na Pengo Mtukufu wa kikristu kamtolea uvivu JK ktk jambo ambalo halipo.. That is the deal.

Ukweli upo wapi? rudia kasome kichwa cha mada hii..Soma malalamiko ya Pengo with an open mind, halafu tazama maelezo ya Lukuvi akiwa bungeni utaona hapakuwa na sababu kabisa ya malumbano.. Hii mada mkuu wangu hadi sasa hivi imetazamwa na watu zaidi ya 7,000 kwa sababu gani kama sii Majibu ya Kardinali Pengo!.. na tunaendelea kulumbana sababu gani? kama sii hamtaki kuamini Pengo kafanya PIA makosa.. wamefikia hata kuhalalisha Unga ktk vikao vya kidini ati visizungumziwe.. Hapana mkuu wangu, hata sisi tutumie logic ya kwamba haitakuwa vizuri kama JK angetaka kuhalalisha biashara ya Unga ktk jukwaa la dini yoyote lakini sii kuwakanya vionmgozi wanaofanya vitu hivyo waache! where else angeweza kuupeleka ujumbe kama huu kwa viuongozi wa dini kama sii ktk majukwaa ya dini..

Haya utasikia kwa nini liwe jukwaa la Kikatoliki, I mean jamani toka lini tunakuwa na utengano kwa sababu ya madhehebu? Hivi kweli rais akizungumza swala la Ukabila akiwa Mwanza basi kawatukana wasukuma.. kwa nini asizungumzie akiwa Chalinze?.. Noo mkuu wangu ubaguzi tunauanza sisi wenyewe..
Kwa kila tunachomlaumu JK ndicho Pengo kakifanya lakini yeye sii mnafiki kwa sababu gani?.. kama sii utukufu wake kwa wakristu. JK asizungumze maswala ya unga ktk sherehe za kikristu, Kardinali anakuja ktk jukwaa la dini kama lile analopinga yeye kuzungumzia maswala ya wauza unga na JK wakati angeweza kabisa kwenda Ikulu na kuonana na rais na tusingekuwa namalumbano hapa JF..

Kwa nini JK haruhusiwi kuzungumzia hayo jukwaa la wakristu, sipati jibu zaidi ya mila na desturi ambazo JK hazijui. Kwa nini Pengo anataka majina ya wauza unga - sipati jibu isipokuwa JK kashindwa kuwataja! yaani vurugu tupu hakuna tunachosimamia na chenye kuingia akilini. Mkuu wangu, kama wapo wauza unga rais anaruhusiwa kuwasema popote pale na kama sii mila za Kikristu basi hata Pengo hakuruhusiwa (kumtolea uvivu JK) zungumzia maswala ya Unga ktk sherehe za Kikristu..

Acha khili la kanisani, ni JK huyu huyu alipopewa list ya wauza Unga na Marehemu Amina Chifupa ktk moja ya sherehe za Kitaifa alisema anayo list ya wauza unga na kuonya wanaofanya vitendo hivyo.... Alisema nakumbuka vizuri na tukaanza kusubiri lini ataifanyia kazi..Sasa tunachoweza kumlaumu ni kwa nini hajaifanyia kazi hadi leo hii na uzembe wake utokane na kutoifanyia kazi siii kwa sababu alisema ktk mkutano wa Kitaifa kwamba anayo list na majina ya wauza Unga!..Na hili halihitaji mkuu wa dini yoyote kutufahamisha kwamba JK sii rais mzuri tunalijua sana kuliko hawa viongozi wa dini ambao wote kwa ujumla wao walimpa support JK ktk chaguzi zote mbili zilizopita... Siii viongozi wa kiiislaam wala wakristu.

Hivyo mkuu wangu namalizia kwa kusema hivi, hoja nzima ya kumkashifu JK haina mshiko isipokuwa ni UDINI unaoendeshwa na vuyombo vya kidini.. Na samahani sana nitarudia kusema JK anachukiwa ktk hili sii kwa sababu nyingine isipokuwa yeye ni Muislaam kawakashifu wakristu na maswala ya kuuza unga ingawa kweli wapo waliokamatwa.. Ilitakiwa Usiri fulani, sio kuyasema maswala ya unga hadharani kwani sii utamaduni wa kanisa -Sawa na mtu kumwambia mzazi aliyejamba - Umejamba, hili ni kosa la kitamaduni...
 
JMushi1,

Mkuu hapana utanisamehe sana, sitokubaliana na wewe ktk hili kwa sababu hata mimi nataka sana JK aondolewe madarakani lakini sio kwa njia hii ya Udini na ufitini.. Hapa inaonyesha wazi UDINI wanaojaribu kuupandikiza hawa jamaa zangu na kama unaweza rudia kusoma hoja za watu humu.. It's all about JK being a Muslim na Pengo Mtukufu wa kikristu kamtolea uvivu JK ktk jambo ambalo halipo.. That is the deal.

Ukweli upo wapi? rudia kasome kichwa cha mada hii..Soma malalamiko ya Pengo with an open mind, halafu tazama maelezo ya Lukuvi akiwa bungeni utaona hapakuwa na sababu kabisa ya malumbano.. Hii mada mkuu wangu hadi sasa hivi imetazamwa na watu zaidi ya 7,000 kwa sababu gani kama sii Majibu ya Kardinali Pengo!.. na tunaendelea kulumbana sababu gani? kama sii hamtaki kuamini Pengo kafanya PIA makosa.. wamefikia hata kuhalalisha Unga ktk vikao vya kidini ati visizungumziwe.. Hapana mkuu wangu, hata sisi tutumie logic ya kwamba haitakuwa vizuri kama JK angetaka kuhalalisha biashara ya Unga ktk jukwaa la dini yoyote lakini sii kuwakanya vionmgozi wanaofanya vitu hivyo waache! where else angeweza kuupeleka ujumbe kama huu kwa viuongozi wa dini kama sii ktk majukwaa ya dini..

Haya utasikia kwa nini liwe jukwaa la Kikatoliki, I mean jamani toka lini tunakuwa na utengano kwa sababu ya madhehebu? Hivi kweli rais akizungumza swala la Ukabila akiwa Mwanza basi kawatukana wasukuma.. kwa nini asizungumzie akiwa Chalinze?.. Noo mkuu wangu ubaguzi tunauanza sisi wenyewe..
Kwa kila tunachomlaumu JK ndicho Pengo kakifanya lakini yeye sii mnafiki kwa sababu gani?.. kama sii utukufu wake kwa wakristu. JK asizungumze maswala ya unga ktk sherehe za kikristu, Kardinali anakuja ktk jukwaa la dini kama lile analopinga yeye kuzungumzia maswala ya wauza unga na JK wakati angeweza kabisa kwenda Ikulu na kuonana na rais na tusingekuwa namalumbano hapa JF..

Kwa nini JK haruhusiwi kuzungumzia hayo jukwaa la wakristu, sipati jibu zaidi ya mila na desturi ambazo JK hazijui. Kwa nini Pengo anataka majina ya wauza unga - sipati jibu isipokuwa JK kashindwa kuwataja! yaani vurugu tupu hakuna tunachosimamia na chenye kuingia akilini. Mkuu wangu, kama wapo wauza unga rais anaruhusiwa kuwasema popote pale na kama sii mila za Kikristu basi hata Pengo hakuruhusiwa (kumtolea uvivu JK) zungumzia maswala ya Unga ktk sherehe za Kikristu..

Acha khili la kanisani, ni JK huyu huyu alipopewa list ya wauza Unga na Marehemu Amina Chifupa ktk moja ya sherehe za Kitaifa alisema anayo list ya wauza unga na kuonya wanaofanya vitendo hivyo.... Alisema nakumbuka vizuri na tukaanza kusubiri lini ataifanyia kazi..Sasa tunachoweza kumlaumu ni kwa nini hajaifanyia kazi hadi leo hii na uzembe wake utokane na kutoifanyia kazi siii kwa sababu alisema ktk mkutano wa Kitaifa kwamba anayo list na majina ya wauza Unga!..Na hili halihitaji mkuu wa dini yoyote kutufahamisha kwamba JK sii rais mzuri tunalijua sana kuliko hawa viongozi wa dini ambao wote kwa ujumla wao walimpa support JK ktk chaguzi zote mbili zilizopita... Siii viongozi wa kiiislaam wala wakristu.

Hivyo mkuu wangu namalizia kwa kusema hivi, hoja nzima ya kumkashifu JK haina mshiko isipokuwa ni UDINI unaoendeshwa na vuyombo vya kidini.. Na samahani sana nitarudia kusema JK anachukiwa ktk hili sii kwa sababu nyingine isipokuwa yeye ni Muislaam kawakashifu wakristu na maswala ya kuuza unga ingawa kweli wapo waliokamatwa.. Ilitakiwa Usiri fulani, sio kuyasema maswala ya unga hadharani kwani sii utamaduni wa kanisa -Sawa na mtu kumwambia mzazi aliyejamba - Umejamba, hili ni kosa la kitamaduni...
Jamani msigeuze sana: labda nikumbuke Pengo alikuwa akiwaonya viongozi wenzake kuwa mazingira aliyotumia Rais kuongea mambo hayo ni njia ya kutoa ujumbe kwa kanisa kuwa tatizo hilo lipo kanisani. Aliwaambia watafakari binafsi wajikague na wabadilike.
Kitendo cha JK au vyombo vyake kutokutaja majina ya hawa wauaji hakiwezi kulisaidia kanisa au jamii athirika ndiyo maana ya neno "usaliti" kwa maana ya kutokusaidia kutatua tatizo hili.
Jamani achaneni na UDINI hapa.
 
Jamani msigeuze sana: labda nikumbuke Pengo alikuwa akiwaonya viongozi wenzake kuwa mazingira aliyotumia Rais kuongea mambo hayo ni njia ya kutoa ujumbe kwa kanisa kuwa tatizo hilo lipo kanisani. Aliwaambia watafakari binafsi wajikague na wabadilike.
Kitendo cha JK au vyombo vyake kutokutaja majina ya hawa wauaji hakiwezi kulisaidia kanisa au jamii athirika ndiyo maana ya neno "usaliti" kwa maana ya kutokusaidia kutatua tatizo hili.
Jamani achaneni na UDINI hapa.
Sawa mkuu lakini kazi ya Dola sio kutaja majina ya wahusika iwe hadharani au Kanisani bali kuwakamata. Kosa la JK lingekuwa kutowakamata wahalifu lakini sio kuwataja! awataje ili iwe nini? itaweza vipi kulisaidia kanisa!... Hamnijibu..

Na hata kama akiwataja sii Kardinali Pengo wala kanisa hawawezi kufanya kitu kutokana na Usiri wa kikanisa wakati hapa tunajadili Utaifa na sheria zake. Labda nambie kwamba kutokana na desturi za Usiri wa kanisa ilitakiwa mambo haya yazungumzwe chini ya pazia... JK kaharibu , makosa kama haya husameheka kwa sababu hakujua...
Jamani hao Wanigeria mnawatetea wa nini tena kama mimi ningekuwa Kardinali Pengo ningemwambia JK fukuza kabisa wachungaji wauza unga wape 24 hrs na niko nyuma yako - hatuwahitaji nchini..
 
UKIISIKIZA HII VIDEO UTAJUA KANISA TZ NI KITU GANI

KAMA HUNA WAKATI (PELEKA MBELE) SIKILIZA JAPO DAKIKA 10 ZA MWISHO

[video]http://blip.tv/mzalendonet/wakristo-wa-tanganyika-walishirikiana-na-wajerumani-kuwaua-waislam-2-5442111[/video]
Nimeisikiliza na kuiangalia Video yote. Ukweli ni uchochezi uliokithiri.
Uadilifu unahitajika unaposikiliza ni kashfa za kutisha na mengine ya kutunga. Kwa mfano sikujua kama kwenye Koran kuna ujumbe kuwa makafir hawaaminiki/hawana fadhila! Nimeshtuka sana.
Jamani kila kitu kina Historia mbaya na nzuri tuache huu uchafu wa kuangalia Historia kwa mtindo hasi kila wakati.
Jamani hatutaki haya malumbano! ni uchafu! ni ujinga! ni upumbavu.
Wakristo tafadhali msijibu lolote.
yako mambo mengi sana kwenye Historia yanayoweza kutugombanisha.
mfano waendeshaji wa Biashara ya utumwa (historia). Ukianzisha mjadala huu utagombana na uislamu.
Ukienda kwenye umafia wa Italy utagombana na wakatoliki.
Tuachane nayo!!!
 
Sawa mkuu lakini kazi ya Dola sio kutaja majina ya wahusika iwe hadharani au Kanisani bali kuwakamata. Kosa la JK lingekuwa kutowakamata wahalifu lakini sio kuwataja! awataje ili iwe nini? itaweza vipi kulisaidia kanisa!... Hamnijibu..

Na hata kama akiwataja sii Kardinali Pengo wala kanisa hawawezi kufanya kitu kutokana na Usiri wa kikanisa wakati hapa tunajadili Utaifa na sheria zake. Labda nambie kwamba kutokana na desturi za Usiri wa kanisa ilitakiwa mambo haya yazungumzwe chini ya pazia... JK kaharibu , makosa kama haya husameheka kwa sababu hakujua...
Jamani hao Wanigeria mnawatetea wa nini tena kama mimi ningekuwa Kardinali Pengo ningemwambia JK fukuza kabisa wachungaji wauza unga wape 24 hrs na niko nyuma yako - hatuwahitaji nchini..
UBISHI wangu ni kuwa hakuna UDINI hapa.
Maneno ya JK yalimpa Pengo mahubiri ya kuwaonya wenzie. Ametekeleza hilo. Pengo ni kiongozi wa Nchi hawezi kuvumilia kupata tuhuma juu ya watu anaowaongoza. Mojawapo ya kazi zake ni kuwasimamisha utumishi viongozi kama hao. JK angemsaidia sana kama angewakamata/kuwatuhumu watu badala ya "blank" statement kanisani. Pale palikuwepo na wageni kutoka sehemu mbali mbali ndani na nje ya nchi tuhuma ambazo hazifanyiwi kazi ni madhara makubwa kwa taasisi ya kanisa.
 
JMushi1,

Mkuu hapana utanisamehe sana, sitokubaliana na wewe ktk hili kwa sababu hata mimi nataka sana JK aondolewe madarakani lakini sio kwa njia hii ya Udini na ufitini.. Hapa inaonyesha wazi UDINI wanaojaribu kuupandikiza hawa jamaa zangu na kama unaweza rudia kusoma hoja za watu humu.. It's all about JK being a Muslim na Pengo Mtukufu wa kikristu kamtolea uvivu JK ktk jambo ambalo halipo.. That is the deal.

Ukweli upo wapi? rudia kasome kichwa cha mada hii..Soma malalamiko ya Pengo with an open mind, halafu tazama maelezo ya Lukuvi akiwa bungeni utaona hapakuwa na sababu kabisa ya malumbano.. Hii mada mkuu wangu hadi sasa hivi imetazamwa na watu zaidi ya 7,000 kwa sababu gani kama sii Majibu ya Kardinali Pengo!.. na tunaendelea kulumbana sababu gani? kama sii hamtaki kuamini Pengo kafanya PIA makosa.. wamefikia hata kuhalalisha Unga ktk vikao vya kidini ati visizungumziwe.. Hapana mkuu wangu, hata sisi tutumie logic ya kwamba haitakuwa vizuri kama JK angetaka kuhalalisha biashara ya Unga ktk jukwaa la dini yoyote lakini sii kuwakanya vionmgozi wanaofanya vitu hivyo waache! where else angeweza kuupeleka ujumbe kama huu kwa viuongozi wa dini kama sii ktk majukwaa ya dini..

Haya utasikia kwa nini liwe jukwaa la Kikatoliki, I mean jamani toka lini tunakuwa na utengano kwa sababu ya madhehebu? Hivi kweli rais akizungumza swala la Ukabila akiwa Mwanza basi kawatukana wasukuma.. kwa nini asizungumzie akiwa Chalinze?.. Noo mkuu wangu ubaguzi tunauanza sisi wenyewe..
Kwa kila tunachomlaumu JK ndicho Pengo kakifanya lakini yeye sii mnafiki kwa sababu gani?.. kama sii utukufu wake kwa wakristu. JK asizungumze maswala ya unga ktk sherehe za kikristu, Kardinali anakuja ktk jukwaa la dini kama lile analopinga yeye kuzungumzia maswala ya wauza unga na JK wakati angeweza kabisa kwenda Ikulu na kuonana na rais na tusingekuwa namalumbano hapa JF..

Kwa nini JK haruhusiwi kuzungumzia hayo jukwaa la wakristu, sipati jibu zaidi ya mila na desturi ambazo JK hazijui. Kwa nini Pengo anataka majina ya wauza unga - sipati jibu isipokuwa JK kashindwa kuwataja! yaani vurugu tupu hakuna tunachosimamia na chenye kuingia akilini. Mkuu wangu, kama wapo wauza unga rais anaruhusiwa kuwasema popote pale na kama sii mila za Kikristu basi hata Pengo hakuruhusiwa (kumtolea uvivu JK) zungumzia maswala ya Unga ktk sherehe za Kikristu..

Acha khili la kanisani, ni JK huyu huyu alipopewa list ya wauza Unga na Marehemu Amina Chifupa ktk moja ya sherehe za Kitaifa alisema anayo list ya wauza unga na kuonya wanaofanya vitendo hivyo.... Alisema nakumbuka vizuri na tukaanza kusubiri lini ataifanyia kazi..Sasa tunachoweza kumlaumu ni kwa nini hajaifanyia kazi hadi leo hii na uzembe wake utokane na kutoifanyia kazi siii kwa sababu alisema ktk mkutano wa Kitaifa kwamba anayo list na majina ya wauza Unga!..Na hili halihitaji mkuu wa dini yoyote kutufahamisha kwamba JK sii rais mzuri tunalijua sana kuliko hawa viongozi wa dini ambao wote kwa ujumla wao walimpa support JK ktk chaguzi zote mbili zilizopita... Siii viongozi wa kiiislaam wala wakristu.

Hivyo mkuu wangu namalizia kwa kusema hivi, hoja nzima ya kumkashifu JK haina mshiko isipokuwa ni UDINI unaoendeshwa na vuyombo vya kidini.. Na samahani sana nitarudia kusema JK anachukiwa ktk hili sii kwa sababu nyingine isipokuwa yeye ni Muislaam kawakashifu wakristu na maswala ya kuuza unga ingawa kweli wapo waliokamatwa.. Ilitakiwa Usiri fulani, sio kuyasema maswala ya unga hadharani kwani sii utamaduni wa kanisa -Sawa na mtu kumwambia mzazi aliyejamba - Umejamba, hili ni kosa la kitamaduni...

It seems umechagua maneno na maeneo ya kuyaelewa na bahati mbaya umeyaelewa utakavyo yaani kinyume na yalivyokusudiwa thats a problem of being a 'genius' tena kinyume na yaliyokusudiwa.
Soma mchezo mapema....
 
Nimeisikiliza na kuiangalia Video yote. Ukweli ni uchochezi uliokithiri.
Uadilifu unahitajika unaposikiliza ni kashfa za kutisha na mengine ya kutunga. Kwa mfano sikujua kama kwenye Koran kuna ujumbe kuwa makafir hawaaminiki/hawana fadhila! Nimeshtuka sana.
Jamani kila kitu kina Historia mbaya na nzuri tuache huu uchafu wa kuangalia Historia kwa mtindo hasi kila wakati.
Jamani hatutaki haya malumbano! ni uchafu! ni ujinga! ni upumbavu.
Wakristo tafadhali msijibu lolote.
yako mambo mengi sana kwenye Historia yanayoweza kutugombanisha.
mfano waendeshaji wa Biashara ya utumwa (historia). Ukianzisha mjadala huu utagombana na uislamu.
Ukienda kwenye umafia wa Italy utagombana na wakatoliki.

Tuachane nayo!!!
Haya umeona sasa! wewe imekuwaje utoke kwenye mada hii unakuja na video iliyoletwa na Mkristu mwingine ili ijewe!...Je, nikikuletea video za wachungaji wa Kikristu kina Jimmy Swagat wanaotukana Uislaam na kuita dini ya mashetani - utasema nini?..Sisi Waislaam hatuna muda huo na hakika nyie ndio mnazo video nyingi zinazoukashifu Uislaam lakini huwezi kuta video inayokashifu Ukristu isipokuwa tunakashifu matendo maovu kama kuuza unga, pombe, kula nguruwe n.k... Sasa maadam wewe pengine unawajua wakristu anaouza unga, unafikiri Waislaam wanawazungumzia Wakristu kumbe sivyo - unga ni haramu pande zote mbili..

Anyway nilikuwepo sasa hivi nawaageni endeleeni na mjadala na nawaombea kila la kheri lakini kumbukeni usia wangu.. Mnaiweka mahala pabaya sana Chadema..
 
JMushi1,

Mkuu hapana utanisamehe sana, sitokubaliana na wewe ktk hili kwa sababu hata mimi nataka sana JK aondolewe madarakani lakini sio kwa njia hii ya Udini na ufitini.. Hapa inaonyesha wazi UDINI wanaojaribu kuupandikiza hawa jamaa zangu na kama unaweza rudia kusoma hoja za watu humu.. It's all about JK being a Muslim na Pengo Mtukufu wa kikristu kamtolea uvivu JK ktk jambo ambalo halipo.. That is the deal.

Ukweli upo wapi? rudia kasome kichwa cha mada hii..Soma malalamiko ya Pengo with an open mind, halafu tazama maelezo ya Lukuvi akiwa bungeni utaona hapakuwa na sababu kabisa ya malumbano.. Hii mada mkuu wangu hadi sasa hivi imetazamwa na watu zaidi ya 7,000 kwa sababu gani kama sii Majibu ya Kardinali Pengo!.. na tunaendelea kulumbana sababu gani? kama sii hamtaki kuamini Pengo kafanya PIA makosa.. wamefikia hata kuhalalisha Unga ktk vikao vya kidini ati visizungumziwe.. Hapana mkuu wangu, hata sisi tutumie logic ya kwamba haitakuwa vizuri kama JK angetaka kuhalalisha biashara ya Unga ktk jukwaa la dini yoyote lakini sii kuwakanya vionmgozi wanaofanya vitu hivyo waache! where else angeweza kuupeleka ujumbe kama huu kwa viuongozi wa dini kama sii ktk majukwaa ya dini..

Haya utasikia kwa nini liwe jukwaa la Kikatoliki, I mean jamani toka lini tunakuwa na utengano kwa sababu ya madhehebu? Hivi kweli rais akizungumza swala la Ukabila akiwa Mwanza basi kawatukana wasukuma.. kwa nini asizungumzie akiwa Chalinze?.. Noo mkuu wangu ubaguzi tunauanza sisi wenyewe..
Kwa kila tunachomlaumu JK ndicho Pengo kakifanya lakini yeye sii mnafiki kwa sababu gani?.. kama sii utukufu wake kwa wakristu. JK asizungumze maswala ya unga ktk sherehe za kikristu, Kardinali anakuja ktk jukwaa la dini kama lile analopinga yeye kuzungumzia maswala ya wauza unga na JK wakati angeweza kabisa kwenda Ikulu na kuonana na rais na tusingekuwa namalumbano hapa JF..

Kwa nini JK haruhusiwi kuzungumzia hayo jukwaa la wakristu, sipati jibu zaidi ya mila na desturi ambazo JK hazijui. Kwa nini Pengo anataka majina ya wauza unga - sipati jibu isipokuwa JK kashindwa kuwataja! yaani vurugu tupu hakuna tunachosimamia na chenye kuingia akilini. Mkuu wangu, kama wapo wauza unga rais anaruhusiwa kuwasema popote pale na kama sii mila za Kikristu basi hata Pengo hakuruhusiwa (kumtolea uvivu JK) zungumzia maswala ya Unga ktk sherehe za Kikristu..

Acha khili la kanisani, ni JK huyu huyu alipopewa list ya wauza Unga na Marehemu Amina Chifupa ktk moja ya sherehe za Kitaifa alisema anayo list ya wauza unga na kuonya wanaofanya vitendo hivyo.... Alisema nakumbuka vizuri na tukaanza kusubiri lini ataifanyia kazi..Sasa tunachoweza kumlaumu ni kwa nini hajaifanyia kazi hadi leo hii na uzembe wake utokane na kutoifanyia kazi siii kwa sababu alisema ktk mkutano wa Kitaifa kwamba anayo list na majina ya wauza Unga!..Na hili halihitaji mkuu wa dini yoyote kutufahamisha kwamba JK sii rais mzuri tunalijua sana kuliko hawa viongozi wa dini ambao wote kwa ujumla wao walimpa support JK ktk chaguzi zote mbili zilizopita... Siii viongozi wa kiiislaam wala wakristu.

Hivyo mkuu wangu namalizia kwa kusema hivi, hoja nzima ya kumkashifu JK haina mshiko isipokuwa ni UDINI unaoendeshwa na vuyombo vya kidini.. Na samahani sana nitarudia kusema JK anachukiwa ktk hili sii kwa sababu nyingine isipokuwa yeye ni Muislaam kawakashifu wakristu na maswala ya kuuza unga ingawa kweli wapo waliokamatwa.. Ilitakiwa Usiri fulani, sio kuyasema maswala ya unga hadharani kwani sii utamaduni wa kanisa -Sawa na mtu kumwambia mzazi aliyejamba - Umejamba, hili ni kosa la kitamaduni...

haha.. kweli wewe ni great thinker! RESPECT! nimeipenda hiyo ya kujamba.....lakini mkuu kujamba ni involuntary action...gesi ikijaa sana hamna technique ya kuizuia! na ni kweli hata mama mkwe akijamba , watu wanaendelea na mazunguzo kama hawajasikia kitu...! hii ya kikwete alikuwa amenuia kabisa kusema kile kitu...nasema hivyo kwa sababu wiki moja kabla ya kwenda mbinga..alikuwa mwanza kwa ziara ya siku tatu...na aligusia isssue ya madawa ya kulevya kwenye sherehe ya kumweka wakfu askofu fulani. Alipokwenda mbinga ndiyo akapiga msumari wenyewe...! Mbona alivyokuwa na maaskofu wa kanisa la Mennonite alitoa ujumbe mzuri tu kuhusu madawa ya kullevya..! Mkuu sisi wengine hatuna udini hata chembe ..hata raisi angekuwa shivji au bakhresa ili mradi tu nchi inakwenda mbele ..! Waislam ndiyo wanamatatizo kwa sababu wanafikiri kikwete anakosolewa kwa sababu ya dini yake...! hembu angalia hapo chini nimekuwekea link ya alichosema kikwete alipokuwa mwanza kabla ya kwenda mbinga wiki moja baadaye! Na ujiuleze ni kwanini alisema statement kama ile alipokuwa na maaskofu wakatoliki!

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...kwanza-jijini-mwanza-baada-ya-uchaguzi-5.html
JK – Nitaunda chombo kupambana na dawa za kulevya

Na Mwandishi wetu
30th May 2011


Rais Jakaya Kikwete, ametangaza kuwa ataunda chombo maalum cha kupambana na ongezeko kubwa la tatizo kubwa la biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

Aidha, Rais Kikwete amewaomba viongozi wa dini na taasisi za dini nchini kusaidiana na Serikali katika kupambana na tatizo hilo lenye madhara makubwa kwa jamii, na hasa miongoni mwa vijana ambao wanaunda asilimia 60 hadi 80 ya Watanzania wanaotumia dawa za kulevya ambazo zinaharibu mwili na akili ya mtumiaji.

Vile vile, Rais amesema kuwa wakati ni kweli kuwa mikoa yote ya Tanzania inakabiliwa na tatizo hilo, lakini ni mikoa saba inayoongoza kwa kuwa na tatizo kubwa zaidi ikiwa ni Dar es Salaam, Mwanza, Mjini Magharibi – Zanzibar, Arusha, Tanga, Mbeya na Dodoma.

Rais Kikwete alitangaza kusudio lake la kuunda chombo maalum cha kupambana na dawa za kulevya jana wakati wa sherehe za kusimikwa kwa Askofu Mteule Albert Jella Randa wa Kanisa la Mennonite, Tanzania, kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mwanza ambako alikuwa mgeni.

Sherehe hizo zilifanyika kwenye makao ya Dayosisi hiyo Nyakato, mjini Mwanza.

Akihutubia mamia ya waumini wa Kanisa hilo pamoja na wananchi wengine waliohudhuria sherehe hizo, Rais Kikwete amewaomba viongozi wa dini, madhehebu ya dini mbali mbali nchini kuongeza juhudi za kupambana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.

Akisema kuwa pamoja na kwamba matunda ya juhudi za Serikali katika kupambana na tatizo hilo yameanza kuonekana bado kazi iliyoko mbele ya jamii ya Tanzania ni "kubwa sana".

"Mwaka jana, 2010, watu 12,119 walikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya. Katika kipindi hicho, dawa za kulevya zilizokamatwa ni heroine kilo 190 na gramu 780, cocaine kilo 65, morphine kilo 11, bangi kilo 279,520 na mirungi kilo 10,317. Takwimu zinaonyesha kuwa mkoani Mwanza tatizo linakua kwa kasi sana," amesema Rais Kikwete na kuongeza:

"Dawa za kulevya zina madhara makubwa kwa watumiaji na kwa jamii. Kwa watumiaji hatima yake ni mtu kuharibikiwa kimwili na kiakili. Watu huwa mazezeta na hivyo kushindwa kutokuwa na manufaa kwa jamii. Hii ni hasara kwa familia, jamii na taifa. Bahati mbaya sana waathirika wengi ni vijana. Tafiti zilizopo zinaonyesha kwamba asilimia 60-80 ya watu wanaotumia dawa hizo ni vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 30, alisema."

Aliongeza: "Hii ni hasara kubwa kwani vijana ndio nguvukazi ya leo na kesho. Ndiyo roho ya taifa na warithi wa familia, jamii na taifa. Wakiharibikiwa taifa letu litaangamia. Tusikubali. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kulichukia tatizo hili na kulikemea kwa nguvu zake zote ili kuokoa taifa letu. Nawaomba viongozi wa dini kushirikiana na Serikali na watu wote wenye mapenzi wa nchi yetu kupambana mpaka tufanikiwe kudhibiti na hatimaye kulitokomeza tatizo hili."

Sherehe za leo za kusimikwa Askofu Randa (50) kuwa Askofu wa Kanisa Mennonite, Jimbo la Mwanza, pia zilihudhuriwa na mamia kwa mamia ya waumini wa Kanisa hilo na wananchi wengine.

Kwenye sherehe hizo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Mennonite Tanzania (KMT), Mhashamu Severin Watson Mang'ana amemkabidhi askofu huyo mpya nguvu kuu ishara za mamlaka na madaraka ya uaskofu ikiwamo Biblia, Katiba ya KMT, Cheti cha Uaskofu na vitabu vya taratibu ya kuendesha ibada za Kanisa hilo na nyimbo.

Kanisa la Mennonite lililoanzishwa duniani mwaka 525 na Mchungaji Menno Simon mjini Zurich, Uswisi, liliingia nchini miaka 77 iliyopita mwaka 1934 na liko katika maeneo yote ya Tanzania isipokuwa Zanzibar, Ruvuma na Pwani. Kanisa hilo lina makao yake mkoani Mara.

SOURCE: NIPASHE.

=======================================

 
Sawa mkuu lakini kazi ya Dola sio kutaja majina ya wahusika iwe hadharani au Kanisani bali kuwakamata. Kosa la JK lingekuwa kutowakamata wahalifu lakini sio kuwataja! awataje ili iwe nini? itaweza vipi kulisaidia kanisa!... Hamnijibu.. <br />
<br />
Na hata kama akiwataja sii Kardinali Pengo wala kanisa hawawezi kufanya kitu kutokana na Usiri wa kikanisa wakati hapa tunajadili Utaifa na sheria zake. Labda nambie kwamba kutokana na desturi za Usiri wa kanisa ilitakiwa mambo haya yazungumzwe chini ya pazia... JK kaharibu , makosa kama haya husameheka kwa sababu hakujua...<br />
Jamani hao Wanigeria mnawatetea wa nini tena kama mimi ningekuwa Kardinali Pengo ningemwambia JK fukuza kabisa wachungaji wauza unga wape 24 hrs na niko nyuma yako - hatuwahitaji nchini..
<br />
<br />

Kuwakamata kwenyewe hathubutu ndio umwambie awafukuze.
Kinachokanganya hapa ni ile dhamira ya jk kutolea tangazo lake kwenye jukwaa la wakatoliki ilhali alikuwa anafahamu huyo aliye naye ni mnaijeria na sii mkatoliki. Tena hakutaka kumtaja ila inaweza dhaniwa kuwa jk alikuwa akimuunganisha mnaigeria wake na Pengo ama mapadre, sasa sisemi kuwa kina pengo au mapadre hawawezi kufanya biashara hiyo, bali kuondoa kiwingu na ukizingatia rais ndie mwenye dola alipaswa hadi wakati Pengo anatoa kauli wawe washakamatwa ama kuchukuliwa hatua ya kutajwa hadharani. Ingefanyika hivyo mbona kauli ya Pengo na viongozi wengine makini wangelikuwa wametoa kauli ya kumpongeza rais kwa kazi nzuri na dhamira safi ya kupambana na wauza unga nchini? Badala yake rais ameamua kunyamaza na kuiacha kauli yake ikining'inia na kusababisha mtafaruku wote huu, na hawezi hata kidogo kukwepa lawama.
.
 
Haya umeona sasa! wewe imekuwaje utoke kwenye mada hii unakuja na video iliyoletwa na Mkristu mwingine ili ijewe!...Je, nikikuletea video za wachungaji wa Kikristu kina Jimmy Swagat wanaotukana Uislaam na kuita dini ya mashetani - utasema nini?..Sisi Waislaam hatuna muda huo na hakika nyie ndio mnazo video nyingi zinazoukashifu Uislaam lakini huwezi kuta video inayokashifu Ukristu isipokuwa tunakashifu matendo maovu kama kuuza unga, pombe, kula nguruwe n.k... Sasa maadam wewe pengine unawajua wakristu anaouza unga, unafikiri Waislaam wanawazungumzia Wakristu kumbe sivyo - unga ni haramu pande zote mbili..

Anyway nilikuwepo sasa hivi nawaageni endeleeni na mjadala na nawaombea kila la kheri lakini kumbukeni usia wangu.. Mnaiweka mahala pabaya sana Chadema..
Afadhali uende kabisa! maanake umerukia hii tu. Siyo wewe uliyeleta hii nafikiri. Mimi napinga kwa nguvu zote kuleta video za kichochezi humu JF
 
Guyz, Nimerudi kwa sababu ya ustaarabu wenu kwani nilianza kuziona dalili za Udini kugeukia kwangu.. Nini alichesema JK?
Rais Kikwete alisema: "Inasikitisha kuona biashara hii haramu (ya dawa za kulevya) sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, Taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili, baadhi yenu tumewakamata...Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuielimisha jamii, hususani vijana waweze kuepuka na matumizi ya madawa ya kulevya."
What's wrong with that!... eeeeeh..
Hata hivyo, sina sababu ya kuendelea na Ubishi lakini angalia tofauti ya kimatamshi baina ya Askofu Judae Thaddeus Ruwai'chi na Kardinali Pengo.. hawa wote ni viongozi wa dini ya Kikristu kanisa moja hivyo sina sababu ya kutopenda maelezo ya Pengo nikayapenda ya Judae ..
Rais JK was wrong (then) so is Kardinal Pengo - toka pande mbili za mtazamo..
Kifupi namuelewa Askofu Judae vizuri lakini nashindwa kumweleza Kardinali Pengo.. na Naweza kumsamehe JK kwa sababu hajui taratibu za kikanisa kama vile Obama alivyokipaka Uingereza kwa Queen, hapakuwa na sababu ya Pengo kuja na Jazba hizo unless anataka kurudisha vurugu za Udini ambazo zlikwisha poa...

Soma habari nzima ya Askofu Judae utaona tofauti ya kimatamshi hakuna dharau kama Pengo..Bofya.

 
Back
Top Bottom