Pendekezo: Rais akishamaliza muhula wake ndio uwe ukomo wake kwenye utumishi wa umma

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,754
Rais ni madaraka ya juu kabisa kwenye Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yeye ndiye mkuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama.

Sheria ya Wastaafu inampa Rais unafuu mkubwa kuendelea kuhudumiwa na Hazina kwani pamoja na kujengewa makazi na serikali, anaokea mshahara 100% ya rais aliyepo madarakani na marupurupu kadhaa.

Anapewa ofisi na wahudumu wa ofisi hiyo wanalipwa kutoka Hazina.

Lakini cha ajabu ni kwamba wanarudi kinyemela kwenye ofisi za umma kwa teuzi kadhaa. Hawa wakuu wa vyuo ambao ni wastaafu ni aibu kwa nchi yetu. Chuo Kikuu kipo chini ya Waziri mhusika na kinapokuwa na mkuu wake ambaye ni rais Mstaafu ni jambo linaloaibisha sana.

Rais Mstaafu halali yake iwe ni kuongoza Tume za Kikanda ama zinazojumuisha diplomasia ya nchi na nchi. Anaweza kuongoza convoy maalum inayotupeleka dunianina siyo kuziba ajira za watu hapa nchini

Katiba Mpya iweke wazi kuwa mtu akishamaliza muhula wake wa urais basi ha-qualify kushika ofisi yeyote ya umma. Wajifunze kuridhika maana kwanza hawalipi kodi na wanaendelea kufaidi Hazina maisha yao yote. Ni kama tunageuzwa mchwa-manamba kumlisha malkia wa mchwa

Uzi tayari
 
Rais mstaafu ni rasilimali adimu kwa nchi. Duniani kote hakuna sehemu wanafanya hicho unachokipendekeza. Labda kama rais huyo alikuwa ma matatizo makubwa wakati wa uongozi wake kama ilivyokuwa kwa Gorbachev wa Urusi na sasa Trump wa USA.
 
Mkuu wa Chuo ni ceremonial, sio msimamizi wa kazi za kila siku za chuo
 
Rais mstaafu ni rasilimali adimu kwa nchi. Duniani kote hakuna sehemu wanafanya hicho unachokipendekeza. Labda kama rais huyo alikuwa ma matatizo makubwa wakati wa uongozi wake kama ilivyokuwa kwa Gorbachev wa Urusi na sasa Trump wa USA.
Mifano michache itasaidia kuelewa angle unayosimamia.

Pia athari zake utudadavulie
 
Mkuu wa Chuo ni ceremonial, sio msimamizi wa kazi za kila siku za chuo
Mkuu
Kwa nini Waziri asiwe mkuu wa Chuo.
Kwa nini waliopo utumishi wa umma wasipewe hizo nafasi....
 
Mifano michache itasaidia kuelewa angle unayosimamia.

Pia athari zake utudadavulie
Kikwete amestaafu lakini kaajiriwa tena na serikali. Analipwa mshahara wa nafasi aliyokuwa nayo, anapewa gari na jipya kila baada ya miaka mitano, Nafasi aliyo staafu anapewa magari 3 mapya kila baada ya miaka mitano na walinzi.

Kapewa Nyumba mpya kama rais mstaafu, kana kwamba alikuwa anaishi NHC.

Cheo alichonacho leo analipwa mshahara mnono na gari jipya na mafuta ya serikali. Huu ni ubinafsi uliopilitiza.

Kwa nafasi aliyokuwanayo angekuwa mshauri tu, kwa sababu tayari analipwa na magari matatu anapewa, na kwa mswaada mpya, mkewe ambaye ni mbunge naye atalipwa mshahara na magari juu tena na madereva wa serikali.

Huku Kina Rizwani wabunge wanalipiwa ada na Marehemu Rais Mkapa hahaha.

Hivi pesa za watanzania ni mali yao peke yako?
 
Back
Top Bottom