Pendekezo la hii kodi linawafaa TRA?

Pendekezo la hii kodi linawafaa TRA?

Habari TRA !

Naomba kuuliza hii kodi eti inafaa hapa nchini?

"MOTOR VEHICLE CROSS REGION TAX"

Karibu.
Yaani unakaa Kibaha kazi Dar es Salaam ulazimike kulipa kodi kila uingiapo na kutoka Dar! Na daladala za Kibaha kwenda Magufuli kila tripu zilipe kodi ya kuingia na kutoka! Bora nitembee kwa miguu.
 
Haaaaahaaaaa Rasilimali moja wapo ndani ya Taifa letu ni uwepo pia wa Vyombo vya moto rafiki.
Ni kweli ,, ila nasisitiza Bado tumejaliwa rasilimali lukuki hakuna haja ya kuwa na Kodi zisizo na mantiki sana ,, visimamiwe vyema . Tuwe na serekali tatu. Na Habari ya kuziuza ikome mara Moja .
 
Habari TRA !

Naomba kuuliza hii kodi eti inafaa hapa nchini?

"MOTOR VEHICLE CROSS REGION TAX"

Karibu.
Freedom of movement ambayo kikatiba imetolewa wewe unataka kuitoza pesa, aisee uchawa ni janga la taifa.
 
Haina shida utalipia tu hiyo mikoa minne rafiki.
Kwamaana nitoke Kilimanjaro nikifika Arusha nilipe manyara nilipe... Then singida.... Taboraa.... Shinyanga.... Geita...... Kama naenda muleba means nilipe Kagera pia.

Mikoa 7 nalipa TU...
 
Kwamaana nitoke Kilimanjaro nikifika Arusha nilipe manyara nilipe... Then singida.... Taboraa.... Shinyanga.... Geita...... Kama naenda muleba means nilipe Kagera pia.

Mikoa 7 nalipa TU...
Lipa Baba.
Kama utahisi ni kero, wewe panda Magari yenye kulipa hiyo Kodi. Mbona ni rahisi sana.
 
Freedom of movement ambayo kikatiba imetolewa wewe unataka kuitoza pesa, aisee uchawa ni janga la taifa.
There is no freedom of movement for Motor Vehicle in this world. Wewe umesomea wapi?
 
Ni kweli ,, ila nasisitiza Bado tumejaliwa rasilimali lukuki hakuna haja ya kuwa na Kodi zisizo na mantiki sana ,, visimamiwe vyema . Tuwe na serekali tatu. Na Habari ya kuziuza ikome mara Moja .
Hakuna rasilimali ambayo haitumiki kwa usahihi. Hizo lukuki zako zipo kichwani na sio halisia. Tambua hakuna kodi isiyo na mantiki.

Hizo Serikali zako unazozitaka zitatumia mawe au mchanga kujiendesha?

Simama kiume rafiki.
 
Yaani unakaa Kibaha kazi Dar es Salaam ulazimike kulipa kodi kila uingiapo na kutoka Dar! Na daladala za Kibaha kwenda Magufuli kila tripu zilipe kodi ya kuingia na kutoka! Bora nitembee kwa miguu.
Shida haipo. Wewe kama utakuwa na Gari, Pikipiki, Bajaji au Chombo chochote cha moto na ukahisi hutaweza kumudu gharama si utapanda Usafiri mwingine wa Umma ambao wao hatasita kulipa hizo kodi kabisa.

Mbona wapo watu wengi wanashindwa kuagiza Magari yaliyotengenezwa miaka ya hivi karibuni zaidi sababu ni Kodi iko juu, mbona hawalalamiki wanatumia usafiri mwingine na maisha yanaenda vizuri tu mbona.
 
mfano magari ya abiria hujui kila yanapoingia stendi yanaacha mapato
Najua. Huo ushuru wa 200 mpaka 500 najua kwa stand.

Mimi nilichoshauri hapa watozwe ndio kwa kuvuka Mkoa asilia. Ipo maana ndani yake. Mfano; Usalama, Afya, kudumu kwa miundombinu, kuboresha huduma za maendeleo nk
 
Lipa Baba.
Kama utahisi ni kero, wewe panda Magari yenye kulipa hiyo Kodi. Mbona ni rahisi sana.
SASA MWIGULU nashauri ondoa Kodi moja wapo inayotuumiza kwenye ununuzi WA magari ili kikokotoo kipoe kidogo then njoo na hii.
 
SASA MWIGULU nashauri ondoa Kodi moja wapo inayotuumiza kwenye ununuzi WA magari ili kikokotoo kipoe kidogo then njoo na hii.
Huyo Mwigulu akiona hii atacheka sana.
Mimi na yeye hata hatujuani ila nashukuru kwa kuweka nia yenu ya kunifananisha na Kiongozi wa kitaifa.
 
Utatambuaje kwamba hicho chombo ni kipya kwenye huo mkoa wakti anayefanya usjili ni TRA kwa kutumia TIN ya mtu ambye ameijilia mwanza lakini anaishi Dar?
Ili uweze kutoza hiyo kodi ni lazima uhuishe Plate namba ziwe na maana.
Mfano UK plate number inayoanza na M ni kwa gari ambazo zimesajiliwa Mancheter kwa inakuwani rahii kuitambua ikienda mkoa mwingine.
Easy brother; mbona wanaupdate to taarifa za mfumo na makazi ya mkoa wako ulipo/ asilia unakoishi. Huhitaji mambo mengi. Kuhusu kukujua tutaweka Barrier Check Point kila Mkoa wanascan Plate Number inasoma Full Details kukuhusu. Maisha yanaendelea
 
Kuna magari mabovu barabarani yasiyostahili kupewa leseni hata ya kupita barabarani kuelekea sehemu ya vyuma chakavu.

Magari kama yake yanayobeba wanafunzi, magari ya mkaa na majitaka mabasi madogo yanayotoa huduma pembezoni mwa miji na vijijini, haya yote kwa wingi wake na madhara yanayotokana nayo, yanapaswa kutozwa kodi zaidi ya asilimia 50.

Hiki ni chanzo kizuri cha mapato ya Serikali hasa kule kwenye halmashauri za wilaya na miji midogo.
 
Back
Top Bottom