PreGE2025 Patrick Assenga avuliwa Uanachama CHADEMA

PreGE2025 Patrick Assenga avuliwa Uanachama CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Timu Lissu inafanya udiktekta. Mtu kupinga mtazamo wa chama haimaanishi afukuzwe uanachama.
 
Lissu alikiuka taratibu za chama kwa kufanya mikutano bila idhini ya chama, kuongea na wanachama bila idhini ya chama na nafasi yake hairuhusu kufanya hivyo, mbona hakufukuzwa?

Waliogawana pesa ambazo Lissu anasema ni za mama Abdul wamefukuzwa lini?

Wenje alipeleka rushwa kwa Lissu kwanini hafukuzwi?

Lissu anasema mbowe alitafuna pesa za chama, kwanini Mbowe hafukuzwi?
Wewe shida yako nini?
 
Chama kinachopigania uhuru wa kutoa maoni chafanya udikteta kwa kufukuza wanachama wanaotoa maoni mbadala.
 
Misingi ya demokrasia kuifuata yote ni kazi ngumu mno.maana demokrasia inataka hata wachache,wenye mawazo tofauti na ya wengi,nao waheshimiwe!
inatakiwa mawazo yao wachache wasikilizwe, ila nao wasilazimishe mawazo yao kufuatwa
wakitoa mawazo yao na yakakataliwa wawe wapole
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Tawi la Msimbazi, Kata ya Tabata, Jimbo la Segerea mkoa wa kichama wa chama hicho wa Ilala mkoani Dar es Salaam kimemvua rasmi uanachama mwanachama wake Patrick John Assenga, kwa kile kilichoelezwa kupinga hadharani maazimio rasmi ya chama, yakiwemo ya ajenda ya No Reforms No Election.

Katika barua iliyoandikwa Mei 6, 2025 na Katibu wa Tawi, Jacob Roman kwenda kwa Assenga, chama kimesema Assenga ambaye ni mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa, amevuliwa uanachama kwa kukiuka Katiba ya chama toleo la mwaka 2019, hasa Kanuni ya Maadili kifungu kidogo (iii) kinachokataza kupinga misimamo ya chama nje ya vikao.

“Chama kilikupa siku 14 kuwasilisha maelezo yako kwa njia ya maandishi hukufanya hivyo, Hivyo basi chama hakitasita kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yako kwa kosa ulilotenda makusudi ukijua unavunja katiba ya chama ya mwaka 2006 toleo la 2019 kipenele cha 03 kanuni ya maadili kifungu kidogo cha (iii)”, imeeleza sehemu ya barua hiyo.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Tawi limeeleza kuwa kwa msingi wa Ibara ya 5.4.3 ya Katiba ya CHADEMA, Assenga anakosa sifa ya kuendelea kuwa mwanachama, na hivyo amevuliwa rasmi uanachama wake kutokana na mwenendo unaodaiwa kuwa kinyume cha itikadi, falsafa, madhumuni, maadili na sera za chama.

Pia soma: Pre GE2025 - John Mrema avuliwa uanachama wa CHADEMA

“Pamoja na kushindwa kuwasilisha maelezo yako katika siku za nyongeza kamati tendaji ya Tawi imeketi na kupitia kwa umakini tuhuma zako ambazo ukiwa kiongozi hukupaswa kuzitenda, hivyo basi kwa kosa hili adhabu yake inaangukia Ibara ya 5.4 inayosema "kukoma kwa uanachama" ukiwa mwanachama wa CHADEMA mwenye usajili wa kadi No. cdme 11126 ya tarehe 22/06/2021 ambayo ni ya kidijiti”, imeeleza barua hiyo.

Chama kimetoa taarifa kuwa Assenga ana haki ya kukata rufaa katika ngazi ya juu ya chama kama ilivyoainishwa katika Katiba.

View attachment 3326318
Fukuzeni mamluki wote hadi wabakie wanachama na viongozi waaminifu wa Cdm.

Mkicheka na nyani mtaambulia mabua.
 
Chama kinachopigania uhuru wa kutoa maoni chafanya udikteta kwa kufukuza wanachama wanaotoa maoni mbadala.
Maoni mbadala nje ya kikao ni usaliti, bahati nzuri kanuni hiyo viongozi hao wanaijua ni wimbo wao wa kila siku wa kimaadili.

Tena kati kati ya mkwamo unaopitia Cdm, huko ni kuonesha nia ya wazi ya kugawana fito.

Wacha wapumzishwe tu, maana hakuna namna.
 
Hakuna democracy chadema kwasasa, kinachoendelea ni udikteta, Nina imani mishale aliyopigwa Mbowe akipigwa Lissu na Heche watafukuza kilamtu 🤣
Wa Kishumundu wewe bila shaka. Mbowe ameondoka kiroho safi yale yalikuwa mambo ya kampeni mbona na Lissu naye alitukanwa saba. Shida mliokuwa mnabunya ruzuku pale HQ ndiyo mnaendelea kubweka na wewe kama siyo John Mrema bahati. Kubalini matokeo.
 
Lissu alikiuka taratibu za chama kwa kufanya mikutano bila idhini ya chama, kuongea na wanachama bila idhini ya chama na nafasi yake hairuhusu kufanya hivyo, mbona hakufukuzwa?

Waliogawana pesa ambazo Lissu anasema ni za mama Abdul wamefukuzwa lini?

Wenje alipeleka rushwa kwa Lissu kwanini hafukuzwi?

Lissu anasema mbowe alitafuna pesa za chama, kwanini Mbowe hafukuzwi?
mbona kama unafoka sasa
 
Maoni mbadala nje ya kikao ni usaliti, bahati nzuri kanuni hiyo viongozi hao wanaijua ni wimbo wao wa kila siku wa kimaadili.

Tena kati kati ya mkwamo unaopitia Cdm, huko ni kuonesha nia ya wazi ya kugawana fito.

Wacha wapumzishwe tu, maana hakuna namna.
Kama nje ni madikteta hivi kwenye hicho kikao ndo angepewa uhuru wa kutoa maoni?
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Tawi la Msimbazi, Kata ya Tabata, Jimbo la Segerea mkoa wa kichama wa chama hicho wa Ilala mkoani Dar es Salaam kimemvua rasmi uanachama mwanachama wake Patrick John Assenga, kwa kile kilichoelezwa kupinga hadharani maazimio rasmi ya chama, yakiwemo ya ajenda ya No Reforms No Election.

Katika barua iliyoandikwa Mei 6, 2025 na Katibu wa Tawi, Jacob Roman kwenda kwa Assenga, chama kimesema Assenga ambaye ni mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa, amevuliwa uanachama kwa kukiuka Katiba ya chama toleo la mwaka 2019, hasa Kanuni ya Maadili kifungu kidogo (iii) kinachokataza kupinga misimamo ya chama nje ya vikao.

“Chama kilikupa siku 14 kuwasilisha maelezo yako kwa njia ya maandishi hukufanya hivyo, Hivyo basi chama hakitasita kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yako kwa kosa ulilotenda makusudi ukijua unavunja katiba ya chama ya mwaka 2006 toleo la 2019 kipenele cha 03 kanuni ya maadili kifungu kidogo cha (iii)”, imeeleza sehemu ya barua hiyo.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Tawi limeeleza kuwa kwa msingi wa Ibara ya 5.4.3 ya Katiba ya CHADEMA, Assenga anakosa sifa ya kuendelea kuwa mwanachama, na hivyo amevuliwa rasmi uanachama wake kutokana na mwenendo unaodaiwa kuwa kinyume cha itikadi, falsafa, madhumuni, maadili na sera za chama.

Pia soma: Pre GE2025 - John Mrema avuliwa uanachama wa CHADEMA

“Pamoja na kushindwa kuwasilisha maelezo yako katika siku za nyongeza kamati tendaji ya Tawi imeketi na kupitia kwa umakini tuhuma zako ambazo ukiwa kiongozi hukupaswa kuzitenda, hivyo basi kwa kosa hili adhabu yake inaangukia Ibara ya 5.4 inayosema "kukoma kwa uanachama" ukiwa mwanachama wa CHADEMA mwenye usajili wa kadi No. cdme 11126 ya tarehe 22/06/2021 ambayo ni ya kidijiti”, imeeleza barua hiyo.

Chama kimetoa taarifa kuwa Assenga ana haki ya kukata rufaa katika ngazi ya juu ya chama kama ilivyoainishwa katika Katiba.

View attachment 3326318
View attachment 3326414
Barua makini iliyoandikwa kitaalamu (professionalized letter) tena toka kwa kiongozi wa ngazi ya chini ya tawi tu...

Lakini barua za kina afande kamanda Jumanne Muliro (RPC - kanda maalumu DSM), ni hovyo, unprofessional utadhani viongozi hawa wenye dhamana kubwa kuongoza taasisi nyeti na muhimu, polisi kama hakwenda shule kabisa...

Kamanda mzima anaaindika "Father Charles Kitima alikuwa akipata kinywaji...🤔🤔🤔🤔"
 
Misingi ya demokrasia kuifuata yote ni kazi ngumu mno.maana demokrasia inataka hata wachache,wenye mawazo tofauti na ya wengi,nao waheshimiwe!
Mawazo tofauti yanaheshimiwa kwenye vikao halali lakini kupinga maamuzi halali ya vikao ni uhaini!
 
Back
Top Bottom