PreGE2025 Patrick Assenga avuliwa Uanachama CHADEMA

PreGE2025 Patrick Assenga avuliwa Uanachama CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Lissu alikiuka taratibu za chama kwa kufanya mikutano bila idhini ya chama, kuongea na wanachama bila idhini ya chama na nafasi yake hairuhusu kufanya hivyo, mbona hakufukuzwa?

Waliogawana pesa ambazo Lissu anasema ni za mama Abdul wamefukuzwa lini?

Wenje alipeleka rushwa kwa Lissu kwanini hafukuzwi?

Lissu anasema mbowe alitafuna pesa za chama, kwanini Mbowe hafukuzwi?
Hao umeona wanapinga msimamo wa chama wa REFORMS? Wako kimya kwahiyo watulie hivo hivo
 
Barua makini iliyoandikwa kitaalamu (professionalized letter) tena toka kwa kiongozi wa ngazi ya chini ya tawi tu...

Lakini barua za kina afande kamanda Jumanne Muliro (RPC - kanda maalumu DSM), ni hovyo, unprofessional utadhani viongozi hawa wenye dhamana kubwa kuongoza taasisi nyeti na muhimu, polisi kama hakwenda shule kabisa...

Kamanda mzima anaaindika "Father Charles Kitima alikuwa akipata kinywaji...🤔🤔🤔🤔"
Sure mkuu huyu katibu anapaswa apate promosheni..
Kwa ngazi ya tawi na barua ya level hiyo pongezi kwake.
 
Kama nje ni madikteta hivi kwenye hicho kikao ndo angepewa uhuru wa kutoa maoni?
Sielewi principles za vikao vyao kama kunakuminya maoni ya wajumbe.

Lakini je, nje waneonesha udikteta gani kwa wanachana ama viongozi wake?

Tuje upande 'B' je Ccm unaweza kuchongoroa mdomo wa kutoa maoni kipinzani nje ya utaratibu wa vikao wakakuacha?
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Tawi la Msimbazi, Kata ya Tabata, Jimbo la Segerea mkoa wa kichama wa chama hicho wa Ilala mkoani Dar es Salaam kimemvua rasmi uanachama mwanachama wake Patrick John Assenga, kwa kile kilichoelezwa kupinga hadharani maazimio rasmi ya chama, yakiwemo ya ajenda ya No Reforms No Election.

Katika barua iliyoandikwa Mei 6, 2025 na Katibu wa Tawi, Jacob Roman kwenda kwa Assenga, chama kimesema Assenga ambaye ni mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa, amevuliwa uanachama kwa kukiuka Katiba ya chama toleo la mwaka 2019, hasa Kanuni ya Maadili kifungu kidogo (iii) kinachokataza kupinga misimamo ya chama nje ya vikao.

“Chama kilikupa siku 14 kuwasilisha maelezo yako kwa njia ya maandishi hukufanya hivyo, Hivyo basi chama hakitasita kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yako kwa kosa ulilotenda makusudi ukijua unavunja katiba ya chama ya mwaka 2006 toleo la 2019 kipenele cha 03 kanuni ya maadili kifungu kidogo cha (iii)”, imeeleza sehemu ya barua hiyo.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Tawi limeeleza kuwa kwa msingi wa Ibara ya 5.4.3 ya Katiba ya CHADEMA, Assenga anakosa sifa ya kuendelea kuwa mwanachama, na hivyo amevuliwa rasmi uanachama wake kutokana na mwenendo unaodaiwa kuwa kinyume cha itikadi, falsafa, madhumuni, maadili na sera za chama.

Pia soma: Pre GE2025 - John Mrema avuliwa uanachama wa CHADEMA

“Pamoja na kushindwa kuwasilisha maelezo yako katika siku za nyongeza kamati tendaji ya Tawi imeketi na kupitia kwa umakini tuhuma zako ambazo ukiwa kiongozi hukupaswa kuzitenda, hivyo basi kwa kosa hili adhabu yake inaangukia Ibara ya 5.4 inayosema "kukoma kwa uanachama" ukiwa mwanachama wa CHADEMA mwenye usajili wa kadi No. cdme 11126 ya tarehe 22/06/2021 ambayo ni ya kidijiti”, imeeleza barua hiyo.

Chama kimetoa taarifa kuwa Assenga ana haki ya kukata rufaa katika ngazi ya juu ya chama kama ilivyoainishwa katika Katiba.

View attachment 3326318
View attachment 3326414
Kwani hayahamia CHAUMA huyu?
 
Misingi ya demokrasia kuifuata yote ni kazi ngumu mno.maana demokrasia inataka hata wachache,wenye mawazo tofauti na ya wengi,nao waheshimiwe!
Mawazo yao wapeleke kwenye vikao na sio kuanzisha nje ya chama kwa kivuli cha CDM

Kabla ya vyama vingi kila mtu alikuwa CCM lkn leo kuna vyama kibao

Kama wana itkadi zao waanzishe vyama vyao

Kuitwa chama cha demokrasia haimaanishi demokrasia ni haki ya chadema peke yake.
 
Sidhani kama kuwafukuza chama ni busara.
Mkuu hivi ukimfumania live mkeo anatafunwa na jirani yako ukimpa talaka ni kukosa busara? Hao watu wanatumika na CCM kuihujuma Chadema wazi wazi, wamediriki hata kufungua kesi mahakamani Chadema isimamishwe kufanya shughuli za kisiasa na mratibu wa hujuma hiyo ni Ofisi ya Msajili wa vyama kwa maelekezo ya CCM.
 
Misingi ya demokrasia kuifuata yote ni kazi ngumu mno.maana demokrasia inataka hata wachache,wenye mawazo tofauti na ya wengi,nao waheshimiwe!
Ni sawa ila maazimio yakishafikiwa na vikao vya juu, kinachofuata ni utekelezaji wala si kuwa kinyume....
 
Mkuu hivi ukimfumania live mkeo anatafunwa na jirani yako ukimpa talaka ni kukosa busara? Hao watu wanatumika na CCM kuihujuma Chadema wazi wazi, wamediriki hata kufungua kesi mahakamani Chadema isimamishwe kufanya shughuli za kisiasa na mratibu wa hujuma hiyo ni Ofisi ya Msajili wa vyama kwa maelekezo ya CCM.
Then hii ni hatari....niliadhani wana mashiko. Wanapotaka chadema ifungiwe shughuli za kisiasa watafaitikaje sasa?
 
Hivi Tawi la Chama linaweza kumfuta mwanachama wa chamq cha siasa uanachama?
 
Sielewi principles za vikao vyao kama kunakuminya maoni ya wajumbe.

Lakini je, nje waneonesha udikteta gani kwa wanachana ama viongozi wake?

Tuje upande 'B' je Ccm unaweza kuchongoroa mdomo wa kutoa maoni kipinzani nje ya utaratibu wa vikao wakakuacha?
Acha uvivu soma baru hapo juu alafu sema kama kuna kanuni/sheria haijafuatwa
 
Back
Top Bottom