Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Kinguluira iko Morogoro barabara ya Dsm, ukishapita Moro junior Seminary kama unakuja DSM toka Moro,kuna kimji kinafuata, unapomaliza kimji kushoto na kulia yanaanza mashamba ya mkonge. Sasa linapoanza shamba la kushoto kwako kuna njia inaingia kushoto na kuna kibao kimeandikwa kituo cha samaki au uliza wale madogo wa pikipiki,kwamba nataka kwenda FAO, ni buku moja kwa pikipiki.

Niliahidi huko nyuma kuwa nitatoa feedback ya jaribio la ufugaji. Nilianza jaribio may 2010, na sasa ni miezi sita imefika. Niliwaweka sato ktk fishpond isiyo na outlet wala inlet. Wamekuwa na kufikia kiwango cha kuliwa na wamezaliana vizuri sana.

Pamoja na kwamba nilipata darasa la kutosha toka Kinguluira,sikubadilisha mazingira ya bwawa lile. Desemba nitakwenda Kinguluira ili nichukue mbegu bora na nifugie ktk mazingira yanayokubalika kitalaam, lakini bwawa lingine nitaendelea kutumia mbegu niliyozalisha pale kwangu ili nione matokeo baada ya miezi sita mingine, hawa ni sato sio Kambale.

Nawatia shime,mwenye nafasi afuge samaki, mbegu zipo nyingi.
Niliwahi kumsikia Mtaalam mmoja akisema kuwa, "samaki wanaofugwa katika maji yasiyotembea hawawezi kuzaliana kwa kuwa samaki hutaga mayai anapoogelea dhidi ya mkondo".

Naomba ufafanuzi wa Kitaalamu kuhusu uzalishaji wa samaki ktk mapipa. Je, wanazaliana ama la?
 
Niliwahi kumsikia Mtaalam mmoja akisema kuwa, "samaki wanaofugwa katika maji yasiyotembea hawawezi kuzaliana kwa kuwa samaki hutaga mayai anapoogelea dhidi ya mkondo".

Naomba ufafanuzi wa Kitaalamu kuhusu uzalishaji wa samaki ktk mapipa. Je, wanazaliana ama la?
Ndiyo maana ukiwa na hela unaweka fountain inatengeneza mkondo
 
Niliwahi kumsikia Mtaalam mmoja akisema kuwa, "samaki wanaofugwa katika maji yasiyotembea hawawezi kuzaliana kwa kuwa samaki hutaga mayai anapoogelea dhidi ya mkondo".

Naomba ufafanuzi wa Kitaalamu kuhusu uzalishaji wa samaki ktk mapipa. Je, wanazaliana ama la?
Samaki anayetaga kulingana na kupanda na kushuka kwa kina cha maji ni catfish(kambale), lakini Sato(Tilapia), hao kwa kuzaliana ni popote kambi.
 
Niliwahi kumsikia Mtaalam mmoja akisema kuwa, "samaki wanaofugwa katika maji yasiyotembea hawawezi kuzaliana kwa kuwa samaki hutaga mayai anapoogelea dhidi ya mkondo".

Naomba ufafanuzi wa Kitaalamu kuhusu uzalishaji wa samaki ktk mapipa. Je, wanazaliana ama la?
Kitaalamu, samaki wa kufugwa haitaji kuzaliana. Kumbuka unafuga samaki katika eneo ambalo ukubwa wake uko defined, na tayari unakuwa na budget ya ulishaji ambayo iko pre determined na idadi ya samaki waliopo in terms ya chakula, oxygen etc.


Kitendo cha kuacha samaki wazaliane, kitakufanya mfugaji kutojua idadi halisi ya samaki katika bwawa. Wanaweza wakawa wengi kuliko chakula unachowapa, na kusababisha wadumae, au kufa kwa kukosa oxygen ya kutosha.

Kwa iyo kinachofanyika ni kutumia homones maalumu kubadili jinsia ya samaji na kuwafanya wote wawe jinsia moja (Mono sex). Hii inazuia kuzaliana na kufanya management ya bwawa kuwa rahisi na matokeo kuwa poa.

So, hii ya samaki kutozaliana hakutokani na maji yaliotuama, ni vifaranga vyao kuwa mono sex
 
Kitaalamu, samaki wa kufugwa haitaji kuzaliana. Kumbuka unafuga samaki katika eneo ambalo ukubwa wake uko defined, na tayari unakuwa na budget ya ulishaji ambayo iko pre determined na idadi ya samaki waliopo in terms ya chakula, oxygen etc.


Kitendo cha kuacha samaki wazaliane, kitakufanya mfugaji kutojua idadi halisi ya samaki katika bwawa. Wanaweza wakawa wengi kuliko chakula unachowapa, na kusababisha wadumae, au kufa kwa kukosa oxygen ya kutosha.

Kwa iyo kinachofanyika ni kutumia homones maalumu kubadili jinsia ya samaji na kuwafanya wote wawe jinsia moja (Mono sex). Hii inazuia kuzaliana na kufanya management ya bwawa kuwa rahisi na matokeo kuwa poa.

So, hii ya samaki kutozaliana hakutokani na maji yaliotuama, ni vifaranga vyao kuwa mono sex
Samahani mkuu, hivi kwa haraka haraka tu nikitaka kuanza na samaki elf naweza kuhitaji budget ya kiasi gani kwa makadirio mpaka nitakapoweza kuwavuna kiongozi...?
 
Nina eneo kubwa mkoani Tabora natafuta mtu wakuwekeza tufunge samaki
Biashara za kushirikiana ni ngumu sana sana sanaa
Unakuta wewe unamawazo na malengo ya kwenda mbali zaidi mwenzio akiona mmepaata faida ya milioni 20 tuu tayari anataka mgawane anunue IST 😁😁
Sitokaa nikashirikiana na mtu tena kwenye biashara
 
Back
Top Bottom