Yaani kama ni alama Mkuu umepata 99.99%..tatizo siyo TISS au CCM hayo ni matokeo tu ya tatizo kubwa tulilo nalo wote kama watanzania, mfumo wetu wa elimu ulifail kitambo sana, mfumo ambao uliwekwa ili kila anayepata elimu anaelimika na elimu inambadilisha zile tabia na mazoea yasiyo na tija yanakufa, anakuwa mtu mpya..tabia za ubinafsi, chuki kwa wengine, wivu, ushirikina, kujiona bora kuliko wengine, kiburi na dharau nk Tanzania ina watu wachache sana walioelimika, wengi wamekusanya vyeti tu..maarifa ZERO! bahati mbaya sana watu wa aina hii ndiyo wapo TISS, kugeuza hali hii inahitaji nguvu ya wananchi kupitia sanduku la kura ili wpatikane wawakilishi walioelimika waanze kuweka misingi upya hasa kwenye maeneo strategic kama wizara ya Elimu, wizara ya fedha, TISS nk elimu yetu ndio chimbuko la yote haya, nilitarajia waziri wa elimu alete mabadiliko ya msingi kwenye elimu yetu badala ya kukimbizana na ishu ambazo mtu yeyote hata mwenye elimu ya darasa la saba anaweza kuzifanya..kwa mfano bado ni sahihi kuchagua maeneo ya fani kama sheria, elimu, uhandisi, mambo ya jamii nk kwa ngazi ya chuo kikuu kwa kutizama ufaulu wa kidato cha sita..nadhani ufaulu wa kwenye makaratasi ni kitu kidogo sana kupima uwezo wa mtu husika kwenye jambo fulani, wengine walishaacha mfumo huu, kwa nini kuchagua mtu kwa matokeo ambayo si yako..mfano mwingine, hao TISS kila anapokuja Rais mpya nilitarajia wao wasaidie kuweka mazingira mazuri kimuundo hasa kwenye kubuni wizara kulingana na mabadiliko yanayoathiri utendaji wa wizara zetu, sikutarajia wakati Rais huyu anaanza kuwe na wizara ya VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI kama wizara moja, ukipima mambo hayo 3 kila moja linaweza kuwa wizara peke yake..lakini kwa vile wahusika wanafanya kwa mazoea na pengine hawataki kufikiri zaidi ya wanachokijua na kukiona tunaishia kuja kulaumu Mwijage, mara Kakunda, hata huyu kijana aliyepo hamna analofanya, tatizo si yeye, tatizo ni waliounda hiyo wizara, msimamizi anataka wizara ifanye anayotarajia, waliomsaidia kuiunda wizara walipishana na vision yake kwa wizara hii..unadhani tutatoka hapo, thubutu! Tutatue tatizo la msingi kwanza ELIMU, tufanye elimu yet itubadilishe, itufanye tuwe na kiu ya kujifunza mambo mapya, kusoma vitabu, kufahamu matatizo yetu na kuleta majibu nk not business as usual au nikipata kazi basi ndio nimefika, dont need more! nabaki kuwa KEEPER hadi nistaafu, hilo siyo lengo la ELIMU!
[/QUOTE
Lete suluhisho badala ya kutetea udhaifu kwa kuleta udhaifu wa maeneo na sekta nyingine.
Suluhisho lipo na hata nikilileta hapa jukwaani litafanya nini smartass?