Part 2: TISS bado safari ngumu

Part 2: TISS bado safari ngumu

Haya mambo ni pasua kichwa! Ningetamani hiyo idara iwe chungu cha maarifa na suluhu za kitaifa.

Hebu rejea kuhusu katiba, Rais A ana ruhusu mchakato wa maboresho ya katiba, mara umeishia njiani, mara Rais B anaamuru sio suala la kipaumbele, mchakato usiendelee.

Jiulize, lilipokuwa suala la kipaumbele vigezo gani vilitumika?

Mchakato wa katiba na yaliyotokea ni mfano tu. Huwa najiuliza, nafasi ya raia kuonesha kutoridhishwa kwao iwe ni kwa njia ya kura tu?

Nini nafasi ya TISS kwa maamuzi ya vyombo vikuu yanayo fanana na kulamba sumu?

Tuendelea kukua na kujifunza, tutafikia ukomavu hatua kwa hatua.
 
OK kwa hiyo unashauri tukisome vizuri kitabu cha Yerico Nyerere

Yeriko Nyerere ameyaandika hayo yote kwenye kitabu chake

Mkuu umewahi kukisoma kitabu cha ujasusi cha Yeriko

Angeruhusu ningekipandisha hapa Jukwaani ni kitabu kizuri sana

Try to read, Soma page zinazokuhusu kila kitu kipo kwenye kitabu

Sana sana umejidai mjuaji ukiona umefanya cha maana, hata kama Yote amesema ameandika mjomba wako, kuna nengine sie hatujasikia!
 
Hahaha!

Sawa mkuu vipi kifanyike waingizwe na cdm, act, cuf ndani Tiss?

Ni kubadili sheria hiyo taasisi isiwe chini ya rais, bali rais awe anapata muongozo toka TISS jinsi ya kuendesha nchi. Watumishi wa TISS wawe ni watanzania wazalendo, na sio wateuliwe kwa msukumo wa chama chochote cha siasa.
 
Hebu tuangalie sheria za intelligence and security agencies za baadhi ya mataifa kwa nchi zinazoendelea halafu tujilinganisha , then ndio tujue cha kushauri. Tuache kuongea maneno matupu au kulaumu bila kutoa ushaurii. Ujue wahusika wapo humu na wanapitaga kusoma hasa kwa mada nyeti kama hii.
Tuanze na jirani yetu wa kaskazini, Kenya.
NIS act 2012
 

Attachments

Hakuna sudden change of technology Duniani, it happens gradually,mbona wewe ni mweupe kichwani kiasi hicho?
You can't introduce a new phase of technology at work without having made proof on its efficiency otherwise,what if the version fails? it must be tested in the variety of uses before beforehand.
Ndo maana hata makombora na ndege za kivita hufanyiwa majaribio kwanza kabla ya kuanza kutumika rasmi.
Hiyo teknolojia yako ya Siri ni ya CCM kuteka watu.
Huwa tunaiita lagging time

Au lag phase

Achana nae huyo
 
Mleta mada, kwa nini baada ya uongozi wa juu wa TISS kubadlishiwa ndiyo unakuja na mada kama hizi...

Kuna nini? Tuambie, hatutakusemea...


Cc: mahondaw
 
Tusome na hii ya Research and Analysis Wing(RAW) ya INDIA. Someni mpate cha kushauri. Itawaongezea elimu. Ukitaka kuwa mwanafasihi mzuri, basi soma kazi za fasihi za wanafasihi wengine au waliokutangulia.
 

Attachments

Hii inawezekuwa ni mada muhimu sana kama tutakuwa tunatoa maono yetu kwa hizi taasisi zetu bila ya kuwananga,nina imani hizo idara zote zinaongozwa na binadam kama mimi na wewe,kukosea ama kupitiwa nako ni kwa mwanadamu,Kubwa tuzidi kutoa maono yetu yaliyo mema kwani kuimarikaka kwa taasisi hizo ndio maendeleo ya taifa letu wote.
 
Ushauri ni kwamba sheria inayounda TISS ipitiwe upya na ikiwezekana kuwe na sheria mpya kabisa ya kuundwa kwa idara hii na vitengo vingine ndani yake vitakavyokuwa na majukumu tofauti ya TISS.

Yaani: TISS ni Usalama wa taiifa chini ya mkurugenzi wake mkuu na mitandao yake yote nchi nzima.

Mkurugenzi wake mkuu ateuliwe na raisi lakini aidhinishwe na Bunge kwa sababu katika nchi zingine huyu bosi ana level moja na waziri yoyote yule yaani anakaa kwenye kikao cha BLM.

Akiidhinishwa Bunge anakuwa amepitia chujio.

Huyu DG anakuwa kama inavyojulikana anatoa PDB (taarifa za kila siku) kwa raisi kila usubuhi na hii PDB huwa inatoka kwenye idara zote nchi nzima na hata nje.

Hivyo DG wa TISS anaiongoza na kuielekeza TISS kwenye masuala na mpango mzima wa Usalama wa Taifa na pia ni mshauri wa raisi kama nilivyosema hapo juu kuhusu PDB.

Itaendelea, ntaongelea mapendekezo ya TISS mpya na vitengo vyake kikiwemo kitengo cha ujasusi wa nje ya Tanzania , maana suala la kuzuiwa ndege yetu ya ATCL kule Afrika Kusini limetutia aibu sana.

Pia ntaongelea tofauti yake na polisi lakini uwiano wake wa kazi na JWTZ.

Pia ntaongelea nini maana ya jumuiya ya wanausalama na umuhimu kwake kwa taifa la Tanzania linaloelekea kwenye hatua ya kila mwananchi kupata maziwa na asali.
Hivi Richard unadhani bado kuna umuhimu wa kuwaachia TISS wawe wanafanya kazi za ujasusi wa ndani na ujasusi wa nje kwa wakati mmoja ???

CC: Chige
 
Hivi Richard unadhani bado kuna umuhimu wa kuwaachia TISS wawe wanafanya kazi za ujasusi wa ndani na ujasusi wa nje kwa wakati mmoja ???

CC: Chige

Ndio, kwa sababu hiyo ndo kazi yao walojifunza.

Pili kukiwa na hizo idara (ya ndani na nje) kunarahisisha kuongeza upana na wigo wa usalama wa ndani na wa nje.

Kwani unadani ni nani kama si TISS mwenye jukumu hilo?
 
Ndio, kwa sababu hiyo ndo kazi yao walojifunza.

Pili kukiwa na hizo idara (ya ndani na nje) kunarahisisha kuongeza upana na wigo wa usalama wa ndani na wa nje.

Kwani unadani ni nani kama si TISS mwenye jukumu hilo?

Mkuu Richard nadhani swali langu hukulielewa vizuri, labda niulize kwa lugha nyingine. Hivi kwanini The Foreign Directorate isitolewa ndani ya TISS na ikawa inajitegemea yenyewe kama idara mpya chini ya ofisi ya Raisi ???

Au tuendelee hivihivi kuyaweka mayai yote ndani ya kapu moja tu, hakuna tatizo lolote ???
 
Mkuu Richard nadhani swali langu hukulielewa vizuri, labda niulize kwa lugha nyingine. Hivi kwanini The Foreign Directorate isitolewa ndani ya TISS na ikawa inajitegemea yenyewe kama idara mpya chini ya ofisi ya Raisi ???

Au tuendelee hivihivi kuyaweka mayai yote ndani ya kapu moja tu, hakuna tatizo lolote ???

Mkuu pitia kwenye uzi wangu wa mapendekezo sehemu ya tatu na ya nne, nimeelezea jinsi ya kuifanya idara hiyo ijitegemee na iwe chini ya naibu mkurugenzi mkuu.

Upitie uzi wangu huo hapa: https://www.jamiiforums.com/threads...-ya-ccm-tu-basi-kwa-maslahi-ya-taifa.1628845/
 
Back
Top Bottom