Part 2: TISS bado safari ngumu

Part 2: TISS bado safari ngumu

Sioni shida kwenye Sheria ya TISS wala ma DG wa TISS walipita na waliopo. Naliona tatizo kwa Boss wa DG TISS wa sasa hivi yaani Jiwe kuwa yeye ndiye anataka TISS ifanye kazi anavyotaka yeye na siyo Sheria ya TISS ya mwaka 1996.

Jiulize ni TISS hiyo hiyo ilikuwapo miaka 8 ya BWM na miaka 10 ya JK. Kumetokea nini sasa isi perform mpaka tukafanye marekebisho?

Je ukiifumua sasa na kuitengenezea mfumo mzuri lakini Rais ni huyu huyu unadhani kutakuwa na mabadiliko?

Enzi za BWM hata CCM ilikuwa na Intelligence unit yake kwa ajili ya masilahi ya chama. Lakini wakati huu wa Jiwe TISS imegeuzwa ndiyo Intelligence Unit ya CCM.
Amini nawaambia hata Diwani Athmani hatamaliza na Jiwe akiwa Rais. Muda ndiyo jibu.
 
Kijana wangu kunywa maji ya chemchem ya Nyakageni upunguze kiu yako! Ungeongea hivi kwa huku, 'ungeshakalia chupa' ukiwa mtupu na unarekodiwa

Ukitoka hapo kimyaaaaaa........
 
Naendelea.

Baada ya kupitia upya sheria ya usalama wa taifa.

Sheria itafanyiwa marekebisho na ufahamike wazi kwamba TISS ipo kwa ajili ya kulinda demokrasia ya bunge ikiwemo haki ya wabunge kupinga uteuzi wa mkurugenzi mkuu endapo itaonekana hana sifa.

Pia TISS inalinda maslahi ya taifa kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa pamoja na kukabiliana na vitendo cha kigaisi, ujasusi wa kimataifa na uhujumu uchumi.

Mapendekezo ya Muundo mpya wa TISS na idara zake muhimu chini yake.

Kama nilivyosema hapo awali TISS ni Usalama wa taifa yaani National Security Organization/ Agency ambayo inaongozwa na mkurugenzi mkuu.

Naibu mkurgenzi yeye atashughulikia idara zingine khasa ya nje kwenye mabalozi, upelelezi wa ndani yaani domestic Surveillance na kuhudhuria vikao vya kamati za usalama zote za wiyala na mikoa.

TISS iwe inasimamiwa shughuli zake kwa ukaribu na kamati ya bunge la JMT ya U;inzi na Usalama na iwe inaangaliwa kwa jicho kali kwenye bajeti yake, shughuli zake na hata utaratibu wake wa kuajiri watumishi wake.

Kwa kuwa kamati ya Bunge inajumuisha wabunge kutoka vyama vyote hapo tayari ushiriki wao kuikosoa TISS unakuwa umekamilika yaani "accomplished".

Ntaendelea.
 
Mkuu pamoja na bandiko lako zuri, hebu jifunze pia siasa za kijamaa na kibepari then unganisha na stori za Tiss
Idara ya usalama wa taifa, ndo idara nyeti, nzito na muhimu kuliko idara zote za serikali.
Kwa hiyo panatakiwa pawe na wafanyakazi ma genius hasa ktk idara hiyo, na wasiwe na mapenzi ya chama chochote cha siasa, bali wawe na mapenzi na nchi yao tu.
Wawe wabunifu kwa ajili ya usalama wa taifa lao, usaili wa ajira ufanyike bila kuangalia kiwango cha Elimu ya mtu (kwa baadhi ya vitengo) bali uwezo, weledi, uzalendo wa nchi na akili za mtu.
Neno usalama wa taifa ni neno pana sana, naipenda sana nchi yangu Tanzania ndo maana naamini ushauri wangu kuna siku utafanyiwa kazi vilivyo.
Usalama wa taifa ni lazima wahakikishe nchi ina uchumi mzuri, kwa sababu watu wakilala njaa na kukosa mahitaji muhimu matokeo yake nchi inaweza kuingia kwenye vurugu kubwa mno na hivyo kufanya usalama kutoweka.
Ndo maana nasema hii ni idara nyeti mno, taifa lolote lenye uchumi mbovu na maisha magumu kwa watu wake ina maana pia usalama wa taifa ni dhaifu hauwezi kulinda usalama wa nchi kwa uhakika.
Kutisha watu,na kuua wapinzani ni kuzidi kupanda mbegu za chuki na bomu ambalo mwisho wa siku ni lazima lilipuke .
Kama idara ya usalama wa taifa haina kitengo cha kufanya hujuma za kiuchumi kwa mataifa ya nje kwa faida ya nchi ina maana bado kitengo ni dhaifu na kina watu ambao hawajapikwa na kuiva hasa.
Kila napokuja nyumbani Tanzania na kuangalia mazingira ya nchi yapo duni mno, vijana wengi wakishinda vijiweni hawana kazi za kufanya, huwa najiuliza nini hatima ya nchi Kama hii?
Lowassa aliwahi kusema, ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiria kulipuka siku moja.
Basi idara ya usalama wa taifa inatakiwa ihakikishe hilo bomu halilipuki kwa gharama yoyote, ikibidi kufanya ujambazi (ujasusi) wa kiuchumi kwa mataifa ya nje na kuleta nyumbani ili watoto wale.
Urusi ilikuwa taifa la kwanza Duniani kupeleka chombo na wanaanga kwenye mwezi .
Marekani ilipoona hivyo, ikajaa wivu na ilipojaribu kwenda, chombo chao kililipuka kwa sababu ya hitilafu kwenye engine, wakajiuliza kwa nini warusi waliweza na sisi kushindwa?
Walichofanya ni kuiba teknolojia ya Urusi ya engine hadi wakafanikiwa kwenda.
Sisi tuna wivu wa kichawi, tunapigana vita ndugu kwa ndugu, hatutaki wapinzani waingie ikulu, badala ya kupigana Vita ya kumaliza umaskini, tunamalizana sisi kwa sisi.
Halafu anasimama mtu na kusema eti tutafanikiwa, tutafanikiwa kwa lipi wakati mikono yetu ina Damu za watu zinazolia kwa Mungu zikidai kisasi?
Yaani idara ya usalama wa taifa ilishuhudia kabisa viwanda zaidi ya 400 alivyoacha Mwl Nyerere vikiuliwa, lakini idara hiyo haiko tayari kushuhudia mkosoaji wa serikali akisimama hadharani na kuikosoa serikali ,labda awe nyuma ya keyboard Kama mimi hapa

INAENDELEA
 
haina kitengo cha kufanya hujuma za kiuchumi kwa mataifa ya nje kwa faida ya nchi ina maana bado kitengo ni dhaifu na kina watu ambao hawajapikwa na kuiva hasa.
Naona uko kwenye theory za economic Hitman.Hizo hazitumiei na vinchi vidogo Kama vyetu zonatumiwa na mataifa makubwa yenye nguvu kubwa Sana ya kiuchumi dhidi ya nchi ndogo zisizo na.nguvu kwa kutumia vitu Kama vikwazo vya kiuchumi,masharti ya mikopo na misaada,Kutumia nguvu ya soko na Bei SI unajua beo za vya kwetu hatupangi Bei Ila vya kwao Bei wanaipanga wao.Unapngea vitu vya kusoma kwenye Novel.Tanzania Ina ubavu gani wa kuhujumu mfano uchumi wa marekani? Marekani inaweza ndio.maana Iran wanalia,Korea kaskazini wanalia nk unaongea kwa kujiamini Lakini Sio Siri kichwani uko mweupe una confidence za ujasiri wa kuonyesha ujinga
 
Sioni shida kwenye Sheria ya TISS wala ma DG wa TISS walipita na waliopo. Naliona tatizo kwa Boss wa DG TISS wa sasa hivi yaani Jiwe kuwa yeye ndiye anataka TISS ifanye kazi anavyotaka yeye na siyo Sheria ya TISS ya mwaka 1996.

Jiulize ni TISS hiyo hiyo ilikuwapo miaka 8 ya BWM na miaka 10 ya JK. Kumetokea nini sasa isi perform mpaka tukafanye marekebisho?

Je ukiifumua sasa na kuitengenezea mfumo mzuri lakini Rais ni huyu huyu unadhani kutakuwa na mabadiliko?

Enzi za BWM hata CCM ilikuwa na Intelligence unit yake kwa ajili ya masilahi ya chama. Lakini wakati huu wa Jiwe TISS imegeuzwa ndiyo Intelligence Unit ya CCM.
Amini nawaambia hata Diwani Athmani hatamaliza na Jiwe akiwa Rais. Muda ndiyo jibu.

Pole sana ndugu yangu,

TISS haiendeshwi KWA kutumia Sheria moja tu ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1996,zipo Sheria zingine pia, Kanuni za Sheria hizi, Katika ya nchi, NA Miongozo mbalimbali ambayo hutolewa NA Kurekebishwa Mara KWA mara.

Ingawaje Kanuni za Sheria hizi (baadhi) NA miongozo yake, haziruhusiwi kuwekwa publicly, lakini ukweli unabaki kuwa Sheria hizi hazifai, mbaya, zimepitwa NA wakati.

Kinachotakiwa sasa ni kuifumua TISS yote kabisa KWA kutunga Sera mpya ya Usalama wa Taifa, Sheria NA Kanuni mpya, pamoja na Kuunda Muundo mpya kabisa wa Utendaji ktk taasisi hii. Baadhi ya mambo machache mazuri yaliyomo kwenye Sheria zilizopo hivi sasa yachukuliwe, mambo mabaya yaachwe, pia yaongezwe mambo mengine mazuri zaidi KWA mustakabali bora wa nchi yetu, ikitiliwa mkazo suala LA UJASUSI wa Kiuchumi, KWA sababu Uchumi Mbaya ktk nchi hii ndilo tatizo kubwa zaidi tulilonalo wananchi wa Tz KWA sasa. Ufukara ndio adui yetu mkubwa.KWA sasa Watanzania wanahitaji "Ukombozi wa Kiuchumi KWA sababu Ukombozi wa Kisiasa tayari tunao, tulishaupata tangu 1961.

Hivyo basi, consultations za kutosha zinahitajika ktk mchakato mzima wa kutunga hizo Sheria mpya zitakazosimamia taasisi hii nyeti kabisa ktk nchi.

Watanzania kwa sasa Tunahitaji TISS ya " UKOMBOZI WA KIUCHUMI "
 
Pole sana ndugu yangu,

TISS haiendeshwi KWA kutumia Sheria moja tu ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1996,zipo Sheria zingine pia, Kanuni za Sheria hizi, Katika ya nchi, NA Miongozo mbalimbali ambayo hutolewa NA Kurekebishwa Mara KWA mara.

Ingawaje Kanuni za Sheria hizi (baadhi) NA miongozo yake, haziruhusiwi kuwekwa publicly, lakini ukweli unabaki kuwa Sheria hizi hazifai, mbaya, zimepitwa NA wakati.

Kinachotakiwa sasa ni kuifumua TISS yote kabisa KWA kutunga Sera mpya ya Usalama wa Taifa, Sheria NA Kanuni mpya, pamoja na Kuunda Muundo mpya kabisa wa Utendaji ktk taasisi hii. Baadhi ya mambo machache mazuri yaliyomo kwenye Sheria zilizopo hivi sasa yachukuliwe, mambo mabaya yaachwe, pia yaongezwe mambo mengine mazuri zaidi KWA mustakabali bora wa nchi yetu, ikitiliwa mkazo suala LA UJASUSI wa Kiuchumi, KWA sababu Uchumi Mbaya ktk nchi hii ndilo tatizo kubwa zaidi tulilonalo wananchi wa Tz KWA sasa. Ufukara ndiomadui yetu mkubwa.KWA sasa Watanzania wanahitaji "Ukombozi wa Kiuchumi KWA sababu Ukombozi wa Kisiasa tayari tunao, tulishaupata yangu 1961.

Hivyo basi, consultations za kutosha zinahitajika ktk mchakato mzima wa kutunga hizo Sheria mpya zitakazosimamia taasisi hii nyeti kabisa ktk nchi.

Watanzania kwa sasa Tunahitaji TISS ya " UKOMBOZI WA KIUCHUMI "
Nipo nawaza watunzi wa hizo Sheria watakua kina nani?!
Je watakua tayari kutunga kwa maslahi mapana ya taifa?! Maana wanaweza fumua mfumo halafu watunzi wakiwa sio wenye weledi inakua kazi bure.

Mungu atusaidie
 
Watumishi wengi ukiachana na walimu wamekuwa wakitumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii wakichati na wengine wakirusha picha kwenye status za WhatsApp.
Wengine utawakuta Instagram, mara Facebook huo ni muda wa kazi .
Sasa unabaki kujiuliza hivi huyu mtumishi anafanya kazi muda gani?
Na hawa ndio ikifika may mosi wananyanyua mabango wakidai kuongezewa mishahara na kupandishwa madaraja na kudai allowance mbali mbali zikiwemo house allowance, communication allowance, electricity allowance n.k.

Namshauri yafuatayo Mzee wetu mzalendo nambari moja Dr Magufuli.

1. Tathimini ya kina ifanyike kwa watumishi wote wa umma kama kweli wanalipwa mshahara kulingana na majukumu yao.

2. OPRAS ya makaratasi iliyopo sasa ifanyiwe maboresho na iwe ya ki electronics ambayo mtumishi ataweza kujaza majukumu yake tarajiwa kwa mwaka wa fedha husika, utekelezaji wa majukumu kwa siku, kwa mwezi,kwa robo mwaka na hadi mwaka. ( hii itasaidia kujua uhaliasia wa mipango inayopangwa).

3.OPRAS iunganishwe na mifumo ya ya bajeti ya Serikali kuu na Serikali za mitaa ( mifumo iwasiliane).

4. Faida ya kuwa na electronic OPRAS itasaidia kutrack add hoc overtime vile vile kutrack extra duties zisizokuwa na uhalisia ambazo mara nyingi utakuta mtumishi anazidai kwa justification za uongo.

5. Kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi kupewa communication allowance kila mwezi lakini hawazitumii ipasavyo badala yake maafisa na watumishi wa kada za chini wasiopewa hizo fedha hutumia fedha zao kuwasiliana ( kuratibu) na watumishi wenzao pindi wanapohitaji kujua mambo kadhaa. Kuna haja ya Serikali kuweka system ya kutrack matumizi halisi ya hizi fedha za mawasiliano Kwa wakuu wa idara.

6. Na mwisho kabisa nimpongeze mh Rais wetu Dr Magufuli kwa maamuzi yake ya kishujaa aliyofanya kwa kutujengea sisi watanzania wa hali ya chini hospitali za wilaya zaidi ya 60 na vituo vya afya na zahanati nyingi ndani ya miaka 4. Tena kwa fedha za ndani. Fedha ambazo zilikuwa zikipotea kwa udanganyifu mbali mbali.

Karibu kwa machango wenu wa kujenga tu na sio matusi .
Kwa hiyo unataka mitandao ya kijamii ifungwe kwa watumishi wa umma? Hivi vyuo mlivyosoma vya ajabu sana, una maana sekta binafsi hawa chat????

Fikirieni kwanza! Halafu ni kwa utafiti gani huo kuwa walimu hawa chat? Hawana bundle au wako busy? Kama ni u busy hakuna kazi yenye uhuru kama ualimu

Bora ungesemea kada kama za afya, ambazo wako busy na foleni inawasubiri.
 
Tatizo ni wanasiasa kuingilia taasisi badala ya kuziache zifanye kazi zake kitalaamu.

Sio TISS tu ambayo ni tatizo/inalalamikiwa, bali hata vyombo kama Bunge,Mahakama na vinginevyo vingi navyo vinalalamikiwa kufanya kazi kwa kufuata matakwa ya wanasiasa badala ya weledi.

Tatizo lote hili la hizi taasisi kushindwa kufanya kazi kwa kufuata katiba ni kutokana na madaraka makubwa aliyonayo rais. Unakuta rais ni mwenyekiti wa chama, kwa hiyo anatumia madaraka yake kulinda maslahi ya chama chake, na kwakuwa rais ndio anakuwa amiri jeshi mkuu, basi taasisi zote hizo zinajikuta zinatii itikadi za chama cha rais. Sasa hivi imefikia mahali viongozi wa taasisi zote za nchi hawaoni aibu kujihusisha na chama cha rais, kwakuwa sheria ziko chini ya madaraka ya rais.
 
Watumishi wengi ukiachana na walimu wamekuwa wakitumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii wakichati na wengine wakirusha picha kwenye status za WhatsApp.
Wengine utawakuta Instagram, mara Facebook huo ni muda wa kazi .
Sasa unabaki kujiuliza hivi huyu mtumishi anafanya kazi muda gani?
Na hawa ndio ikifika may mosi wananyanyua mabango wakidai kuongezewa mishahara na kupandishwa madaraja na kudai allowance mbali mbali zikiwemo house allowance, communication allowance, electricity allowance n.k.

Namshauri yafuatayo Mzee wetu mzalendo nambari moja Dr Magufuli.

1. Tathimini ya kina ifanyike kwa watumishi wote wa umma kama kweli wanalipwa mshahara kulingana na majukumu yao.

2. OPRAS ya makaratasi iliyopo sasa ifanyiwe maboresho na iwe ya ki electronics ambayo mtumishi ataweza kujaza majukumu yake tarajiwa kwa mwaka wa fedha husika, utekelezaji wa majukumu kwa siku, kwa mwezi,kwa robo mwaka na hadi mwaka. ( hii itasaidia kujua uhaliasia wa mipango inayopangwa).

3.OPRAS iunganishwe na mifumo ya ya bajeti ya Serikali kuu na Serikali za mitaa ( mifumo iwasiliane).

4. Faida ya kuwa na electronic OPRAS itasaidia kutrack add hoc overtime vile vile kutrack extra duties zisizokuwa na uhalisia ambazo mara nyingi utakuta mtumishi anazidai kwa justification za uongo.

5. Kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi kupewa communication allowance kila mwezi lakini hawazitumii ipasavyo badala yake maafisa na watumishi wa kada za chini wasiopewa hizo fedha hutumia fedha zao kuwasiliana ( kuratibu) na watumishi wenzao pindi wanapohitaji kujua mambo kadhaa. Kuna haja ya Serikali kuweka system ya kutrack matumizi halisi ya hizi fedha za mawasiliano Kwa wakuu wa idara.

6. Na mwisho kabisa nimpongeze mh Rais wetu Dr Magufuli kwa maamuzi yake ya kishujaa aliyofanya kwa kutujengea sisi watanzania wa hali ya chini hospitali za wilaya zaidi ya 60 na vituo vya afya na zahanati nyingi ndani ya miaka 4. Tena kwa fedha za ndani. Fedha ambazo zilikuwa zikipotea kwa udanganyifu mbali mbali.

Karibu kwa machango wenu wa kujenga tu na sio matusi .
Umeielewa mada llm Mkuu? Au unajaribu kupotosha ukweli?
 
Idara ya usalama wa taifa, ndo idara nyeti, nzito na muhimu kuliko idara zote za serikali.
Kwa hiyo panatakiwa pawe na wafanyakazi ma genius hasa ktk idara hiyo, na wasiwe na mapenzi ya chama chochote cha siasa, bali wawe na mapenzi na nchi yao tu.
Wawe wabunifu kwa ajili ya usalama wa taifa lao, usaili wa ajira ufanyike bila kuangalia kiwango cha Elimu ya mtu (kwa baadhi ya vitengo) bali uwezo, weledi, uzalendo wa nchi na akili za mtu.
Neno usalama wa taifa ni neno pana sana, naipenda sana nchi yangu Tanzania ndo maana naamini ushauri wangu kuna siku utafanyiwa kazi vilivyo.
Usalama wa taifa ni lazima wahakikishe nchi ina uchumi mzuri, kwa sababu watu wakilala njaa na kukosa mahitaji muhimu matokeo yake nchi inaweza kuingia kwenye vurugu kubwa mno na hivyo kufanya usalama kutoweka.
Ndo maana nasema hii ni idara nyeti mno, taifa lolote lenye uchumi mbovu na maisha magumu kwa watu wake ina maana pia usalama wa taifa ni dhaifu hauwezi kulinda usalama wa nchi kwa uhakika.
Kutisha watu,na kuua wapinzani ni kuzidi kupanda mbegu za chuki na bomu ambalo mwisho wa siku ni lazima lilipuke .
Kama idara ya usalama wa taifa haina kitengo cha kufanya hujuma za kiuchumi kwa mataifa ya nje kwa faida ya nchi ina maana bado kitengo ni dhaifu na kina watu ambao hawajapikwa na kuiva hasa.
Kila napokuja nyumbani Tanzania na kuangalia mazingira ya nchi yapo duni mno, vijana wengi wakishinda vijiweni hawana kazi za kufanya, huwa najiuliza nini hatima ya nchi Kama hii?
Lowassa aliwahi kusema, ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiria kulipuka siku moja.
Basi idara ya usalama wa taifa inatakiwa ihakikishe hilo bomu halilipuki kwa gharama yoyote, ikibidi kufanya ujambazi (ujasusi) wa kiuchumi kwa mataifa ya nje na kuleta nyumbani ili watoto wale.
Urusi ilikuwa taifa la kwanza Duniani kupeleka chombo na wanaanga kwenye mwezi .
Marekani ilipoona hivyo, ikajaa wivu na ilipojaribu kwenda, chombo chao kililipuka kwa sababu ya hitilafu kwenye engine, wakajiuliza kwa nini warusi waliweza na sisi kushindwa?
Walichofanya ni kuiba teknolojia ya Urusi ya engine hadi wakafanikiwa kwenda.
Sisi tuna wivu wa kichawi, tunapigana vita ndugu kwa ndugu, hatutaki wapinzani waingie ikulu, badala ya kupigana Vita ya kumaliza umaskini, tunamalizana sisi kwa sisi.
Halafu anasimama mtu na kusema eti tutafanikiwa, tutafanikiwa kwa lipi wakati mikono yetu ina Damu za watu zinazolia kwa Mungu zikidai kisasi?
Yaani idara ya usalama wa taifa ilishuhudia kabisa viwanda zaidi ya 400 alivyoacha Mwl Nyerere vikiuliwa, lakini idara hiyo haiko tayari kushuhudia mkosoaji wa serikali akisimama hadharani na kuikosoa serikali ,labda awe nyuma ya keyboard Kama mimi hapa

INAENDELEA

Bila shaka wewe upo ndani ya TISS....
Kuna kitu nimekigundua juu yako!
 
Hiyo yatakiwa iwe ni ajenda ya taifa na kwa maslahi ya taifa.

Hiyo ni pamoja na mawaziri wa ulinzi na mambo ya ndani kukutana na kujadili namna ya kuipitia upya sera ya usalama wa taifa.

Usalama wa taifa usiwe unajihusisha na masuala ya kisiasa.

Hapo ndipo penye tatizo kubwa la TISS, inatuhumiwa kujihusisha na matukio au matokeo ya kisiasa.

Hapa Richard nakuunga mkono kwa kuuona ukweli na kuthubutu kuusema. Ila tatizo kubwa la ufanyaji kazi wa hizi idara nyeti hasa za dola, ni kutokana na madaraka makubwa ya rais aliyopewa kikatiba. Madaraka ya rais ndio yanayochangia taasisi za kimamlaka kufanya kazi kwa kumtii yeye, hata yale yasiyo ndani ya maelekezo ya kazi zao. Ukichunguza vizuri utakuta taasisi nyingi za kimamlaka ni dhaifu kiutendaji, kwakuwa zinaingiliwa na nguvu za rais, kwenye hayo madaraka ya rais yasiyodhibitiwa na sheria ndio hutokea ile amri yenye nguvu kuliko sheria iitwayo amri toka juu.
 
Dawa ni kutunga sheria kuiwezesha Usalama wa Taifa kuwa huru kutoka kwa wanasiasa na hata raisi.
 
Wapo hapa, wanasoma masaa 24

Wananchi wamekuwa wanailalakimia idara na serikali inabidi ikae chini kuangalia wapi pa kurekebisha.

🙂

Serikali haiwezi kurekebisha hili tatizo kwakuwa wao ni wahusika wa huo udhaifu,na yote hayo yanaletwa na madaraka makubwa ya rais yasiyokuwa na sababu za msingi, yanayopelekea kuwa na matumizi mabaya ya madaraka ya urais.
 
TISS Haipaswi kuwa ndo rais au waziri au chama. Kwa hiyo haipaswi kupata maagizo au maelekezo ya mamlaka tu bali kuzingatia malengo yake makuu. Naunga mkono hoja
Tatizo ni wanasiasa kuingilia taasisi badala ya kuziache zifanye kazi zake kitalaamu.

Sio TISS tu ambayo ni tatizo/inalalamikiwa, bali hata vyombo kama Bunge,Mahakama na vinginevyo vingi navyo vinalalamikiwa kufanya kazi kwa kufuata matakwa ya wanasiasa badala ya weledi.
 
Nipo nawaza watunzi wa hizo Sheria watakua kina nani?!
Je watakua tayari kutunga kwa maslahi mapana ya taifa?! Maana wanaweza fumua mfumo halafu watunzi wakiwa sio wenye weledi inakua kazi bure.

Mungu atusaidie

Tena usishangae huo mfumo ukifumuliwa ukaja mbovu kuliko ulivyo hivi sasa. Rejea kilichotokea kwenye mchakato wa katiba mpya, rais na chama chake walijimilikisha mchakato wa katiba mpya, hadi kujipa mamlala ya kubadili maoni ya wananchi tena kwa maslahi ya chama chao. Hapo ndio usalama wa Taifa walipaswa kusimama na kusema maoni ya wananchi ndio yatumike kuunda katiba mpya.
 
Back
Top Bottom