Panapofuka moshi panaficha moto...

Panapofuka moshi panaficha moto...

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,506
Reaction score
123,776
Pasipo na moto hapana moshi.

Je, kuna moto unawaka chini kwa chini Tanzania? Maana moshi kila sehemu.

Cha kujiuliza ni kutafakari, huu moshi unaofuka kila sehemu ni wa mazingaombwe tu na hakuna moto au kuna moto kweli uliowaka au uliowashwa lakini zimamoto yetu haiuoni au tunaoamini kuwa ndiyo zimamoto wetu shupavu wao ndiyo wapepeaji wa huo moto?

Moto upi? Unawaka wapi? Utamuunguza nani na nini? Unaweza kuzimika? Au tunaweza kuuzima wenyewe? Au tunahitaji msaada wa kuuzima huu moto?

Wewe unauona huo moshi? Au tayari unauona moto?
 
Sioni kama unazimika, mpaka uondoke na mtu huu.

Anayeuwasha ndiye mwenye uwezo wa kuuzima, ila anasubiri mpaka umwondoe adui ndo auzime. Ingawa moto hautabiliki, unaweza kumwunguza hata asiye mlengwa na uharibifu ukawa mkubwa.
 
Hakuna Moshi. Hakuna moto.

Kilichopo ni kelele za mitandaoni tu.

Uraiani watu wapo kawaida tu wakiendelea na mishe mishe zao.

D97FF512-BA26-438D-8898-AF8B5E6BBF6B.jpeg
 
CAG ana siri nzito

Special audit report kuhusu matumizi ya trilioni 1.5 ambayo Spika ameikalia kwa mujibu wa Zitto, inaweza ikawa ni tone tu katika bahari.

Subirini ripoti ya CAG ya 2017/2018 hii inaweza kuwa ni atomic bomb lenye madhara kama lille la Hiroshima nchini Japan.

Naomba CAG akomae na asitetereke katika hii vita.
 
Hakuna Moshi. Hakuna moto.

Kilichopo ni kelele za mitandaoni tu.

Uraiani watu wapo kawaida tu wakiendelea na mishe mishe zao.

View attachment 995933
Kujifanya huumwi hakuzuii ugonjwa kukuondoa duniani. Mtu mmoja mpumbavu aliwahi kusema Dar es Salaam hakuna shida ya maji. Alipoulizwa anaishi wapi, bila kushughulisha akili yake akajibu MIKOCHENI
 
CAG ana siri nzito

Special audit report kuhusu matumizi ya trilioni 1.5 ambayo Spika ameikalia kwa mujibu wa Zitto, inaweza ikawa ni tone tu katika bahari.

Subirini ripoti ya CAG ya 2017/2018 hii inaweza kuwa ni atomic bomb lenye madhara kama lille la Hiroshima nchini Japan.

Naomba CAG akomae na asitetereke katika hii vita.
Bila shaka! Report yake ya ukaguzi wa mahesabu ya mwaka 2017/2018 iko due mwezi April halaf wanamchachafya ili ajiuzulu sasa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CAG ana siri nzito

Special audit report kuhusu matumizi ya trilioni 1.5 ambayo Spika ameikalia kwa mujibu wa Zitto, inaweza ikawa ni tone tu katika bahari.

Subirini ripoti ya CAG ya 2017/2018 hii inaweza kuwa ni atomic bomb lenye madhara kama lille la Hiroshima nchini Japan.

Naomba CAG akomae na asitetereke katika hii vita.
tutahakikisha ripoti hiyo inawafikia wananchi hata kwa kudukuliwa , Ndugai hafai kuwa spika na anatakiwa kukamatwa .
 
Back
Top Bottom