Pamoja na bei ya mafuta kupanda, watu wanaendelea kutumia magari na vyombo vingine vinavyotumia mafuta. Je ni kweli wako vizuri kipesa?

Kuna wakati ukiona maisha magumu usifikiri na wenzio wanalia kilio hichohicho unaweza kujikuta uko peke yako na unapolalamika wenzio wanajifanya mnalalamika wote kumbe wanakuchora.

Kuna wakati tujikite kutafuta mbinu za kutukwamua na kuendana na kasi ya ulimwengu, vinginevyo hii dunia itakutesa peke yako.

Wakati unalalamika maisha magumu kuna wenzio kule Mbweni, Goba, Madale nk wanashusha maghorofa na kuweka mpaka swimming pools.
Hapa tunaongelea hali kiujumla, wewe unaongelea isolated cases za watu wachache wanaoporomosha mijengo na kuweka swimming pool ambao huenda ni walewale walamba asali ambao wana kamba za kujipimia. Tunapoongelea hali ya kiuchumi au hali ya maisha tunakuwa tunalenga nchi kwa ujumla wake, Je ni asilimia ngapi ya wananchi wanamudu angalau zile gharama muhimu za kujikimu kimaisha?
 
Mafuta ACHA yapande na watu wataendelea kuendesha gari zao,kwani kila mmoja anapambana ili kuhakikisha maisha yanasonga mbele kwa namna iwavyo
 
Kwa maelezo ya waziri mkuu mstaafu mhe. Msuya akiwa kwenye kipindi cha dk 45 cha ITV, ni kama amemaanisha kwamba uwepo wa magari mengi mjini au barabarani ni kutokana na hali za maisha kutofanana.

Ni kama vile wanaotumia vyombo hivyo hawaoni tofauti ya kupanda kwa bei. Na kwamba wana hali nzuri kifedha.
Je, ni kweli? Au wanapambana tu na hali kwa kuwa hakuna namna nyingine?
Tufanyaje Sasa...Maisha Lazima yasonge Mkuu.
 
Back
Top Bottom