Pages From My JF Diary 📝

Pages From My JF Diary 📝

Kulikuwa na binti mmoja, maisha yalikuwa yamembana sana
bad situation.

Alikuwa amechoka kupita kiasi kimwili, kiakili na hata moyoni

Siku moja jioni, baada ya mawazo kumzidi, akajisemea

Ngoja nitoke kidogo, nipate fresh air, maybe nitatulia

Akatembea polepole bila mwelekeo maalum, akijaribu kupunguza mzigo wa mawazo

Ghafla, macho yake yakatua kwenye chupa ya ajabu iliyokuwa imekaa peke yake kama inamsubiri

Alipoisogelea mambo yakabadilika
Ile chupa ikaanza kumsemesha

Ndiyo, ikaanza kumsemesha kwa sauti laini, yenye utulivu, yenye maneno matamu ya kuvutia maneno yaliyomfanya ahisi kueleweka kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu

Ilikuwa ajabu sana lakini ilikuwa halisi 🫰 not movie

Binti alisimama kimya, akisikiliza

Ghafla, ile chupa ikafunguka taratibu kisha ikasema kwa upole😊

Kunywa kilichopo ndani yangu
Binti, akiwa amechoka na maisha, bila kusita akainyanyua na kunywa

Lahaula…!

Ndani ya sekunde chache, kila kitu kikabadilika

Akahisi kama mzigo wote aliokuwa amebeba umetoweka
Moyo ukatulia

Mawazo yakapoa
Ni kama amezaliwa upya ajabu ya kweli 🙌

Baada ya kuridhika na ile hali ya utulivu na furaha, ile chupa ikajifunga yenyewe tena, kimya kimya😢

kama haijawahi kufanya chochote🙌

Binti alitabasamu kidogo, akaiangalia ile chupa kwa mshangao na shukrani

Na hapo ndipo alipoamua kuipa jina
CHUPA YA MAAJABU

This is my magic bottle✨
kuna kipindi ilikua avatar now ipo kabatini
Baada ya Shetani kumuona akiwa na njaa akamwambia Geuza chupa hii kuwa mkate.
Binti akasema mtu hatoishi kwa mkate bali kwa Smartphone.
 
Safari Yangu Kutoka Lilongwe Hadi Dar es Salaam: Je, Umewahi Kuwa na Imani Kali Kiasi Hiki? 😂 Noma sana

Mwaka fulani nilikuwa Malawi, mjini Lilongwe Wakati huo nilikuwa na miaka 14, naelekea kutimiza 15

Nilikuwa nimeenda likizo, ikafika muda wa kurudi Tanzania

Mama akanipa nauli na kuniambia:

Shika hii pesa vizuri, nenda ukate tiketi.
Kwa nini hakunisindikiza sitasema leo. 😅

Basi nikachukua begi langu lenye nguo chache na mkoba mdogo uliokuwa na pesa za nauli, pesa ya kula, pamoja na kibari changu cha kusafiria Malawi

Nikafika stand ya Lilongwe ambapo magari ya Dar es Salaam yalikuwa yanapatikana

Kipindi hicho kulikuwa na kampuni moja maarufu sana, Taqwa
Sasa sijui ilikuwa bahati mbaya, uzembe sielewi mpka leo nilipochunguza mkoba wangu nikakuta umepotea 😭

Pesa zote zimeenda
Kibari kimeenda
Nauli imeenda
Kila kitu kimepotea

Aisee nilichanganyikiwa vibaya sana. Nikalia mpaka macho yakachoka
Lakini jambo moja nililokuwa na uhakika nalo ni hili

Sirudi nyumbani
Na hii ni hata leo nikisema hapana ni hapana

Kwa sababu mama yangu alikuwa mkali sana
Nilijiona nikirudi kumwambia nimepoteza nauli basi hakuna rangi ningeacha kuona

Nikajiwaza🤔

Kati ya kukutana na mama au kuvuka mipaka bila pesa, bora nijaribu bahati yangu

Nikajikaza nikamfuata dereva
Nikamsalimia kwa heshima zote za dunia
Shikamoo

Akanijibu
Marahaba binti, unasemaje?

Hapo ndipo nilipoanzisha filamu yangu ya kwanza ya maisha Uongooo pro 🤣
Nikaanza
Mimi nilikuja Malawi kufanya kazi za ndani : Astghafirullah 🙌

Dereva aliposikia hivyo akasema
Hebu njoo huku kidogo
Tukakaa pembeni

Sasa hapo nikaanza kusuka hadithi ya uongo kwa kasi ambayo hata nikikumbuka nachoka maana uongo sio tabia yangu mtu muongo na mnafiki hawajaachana mbali

Nikamuambia bosi wangu ananitesa sana, nimeamua kukimbia na kurudi Tanzania lakini sina hata senti

Dereva akaniangalia, akaangalia sura yangu ya mtoto mtulivu, akasikitika

Akamwita konda

Wakakubaliana kunibeba bure.
Mimi ndani ya moyo nikasema:
Asante Mungu, operation usirudi kwa mama imeanza rasmi🤣
Safari ikaanza

Usiku ulivyoingia, konda naye akaingia kwenye shughuli zake akanisahau kabisa kuhusu chakula
😭
Lakini Mungu alikuwa mbele
Nilikaa karibu na kaka mmoja ambaye kila alichonunua alikuwa ananipa sehemu bila kuniuliza hata MashaAllah 😍

Nilikuwa nakula kama nimepewa huduma ya full board😂

Tulipofika Karonga polisi wa Malawi walikuwa wanakagua
Konda akaniambia
Shuka ujifiche kwanza he kasheshe
Nikashuka

Ukaguzi ukaisha
Yaani simple tu ikawa imeisha hiyoo
Nikapanda tena

Mpaka leo nikiikumbuka najiona kama nilikuwa kwenye mission ya siri 🤣
Lakini ni kasheshe la kweli lilikuwa
Linaendela nahisi ningefaa kwa ujasusi🤪
Konda akasema shuka
Sisi tutapita hapa rasmi, wewe shuka upande ule vuka kwa mtumbwi 🙄
Nikabaki namtazama

Mtumbwi? Mimi ambaye hata kuangalia maji kwa muda mrefu naogopa? 😭

Akanipa hela kidogo ya kuvukia
Nikakuta mzee wa mtumbwi yupo tayari kazini Inaonekana ni michongo yake
Nikapanda

Tukiwa katikati ya mto nikaanza kuona mbele polisi kama anatusubiri kabisa 😂😂😂 heh

Moyo ukaanza kwenda mbio kuliko mtumbwi

Nilipofika upande wa pili, kweli polisi akaniita
Umetoka wapi?
Malawi
Ulikuwa unafanya nini?
Hapo nikarudia script ile ile akili mtu wangu 🤭

Nilikuwa nafanya kazi za ndani, bosi ananitesa, nimekimbia 🤣
Akauliza kitambulisho
Hakuna
Kibari
Hakuna
Simu
Hakuna
Kila kitu kilikuwa hakuna😂
Yule polisi akaniangalia halafu akasema
Wewe mtoto una ujanja sana
Akaandika namba yake kwenye karatasi na kuniambia

Ukifika Dar nitafute🤣😒
Mimi nikasema sawa, lakini kichwani nilikuwa nawaza basi lisiniondokee tu
🤣
Nikakimbia mpaka sehemu niliyoelekezwa

Baada ya muda gari likafika
Nikapanda
Safari ikaendelea mpaka Dar es Salaam

Leo nikikumbuka hii safari, najiuliza nilikuwa na ujasiri au nilikuwa na hofu ya mama yangu? 😂😂😂

Mom S 🥹🙌

Kwa sababu uongo wote huo, mipango yote hiyo, kuvuka mipaka, mtumbwi, polisi na hatari zote hizo tena mtoto wakike mdogo baso sijakomaa sura katika ya majangili (wanaume jokes)

chanzo chake kilikuwa kimoja tu

Mama yangu alikuwa mkali mno! 😭😭
Lakini pamoja na yote

Mama, nakupenda sana ❤️ ila ukweli ni kwamba ulikuwa mkali mnoooo!
 
❤️🎵
 

Attachments

  • 6299110-fd0995bb6c929071d3abc95c281f4c3.mp4
    28.6 MB
Safari Yangu Kutoka Lilongwe Hadi Dar es Salaam: Je, Umewahi Kuwa na Imani Kali Kiasi Hiki? 😂 Noma sana

Mwaka fulani nilikuwa Malawi, mjini Lilongwe Wakati huo nilikuwa na miaka 14, naelekea kutimiza 15

Nilikuwa nimeenda likizo, ikafika muda wa kurudi Tanzania

Mama akanipa nauli na kuniambia:

Shika hii pesa vizuri, nenda ukate tiketi.
Kwa nini hakunisindikiza sitasema leo. 😅

Basi nikachukua begi langu lenye nguo chache na mkoba mdogo uliokuwa na pesa za nauli, pesa ya kula, pamoja na kibari changu cha kusafiria Malawi

Nikafika stand ya Lilongwe ambapo magari ya Dar es Salaam yalikuwa yanapatikana

Kipindi hicho kulikuwa na kampuni moja maarufu sana, Taqwa
Sasa sijui ilikuwa bahati mbaya, uzembe sielewi mpka leo nilipochunguza mkoba wangu nikakuta umepotea 😭

Pesa zote zimeenda
Kibari kimeenda
Nauli imeenda
Kila kitu kimepotea

Aisee nilichanganyikiwa vibaya sana. Nikalia mpaka macho yakachoka
Lakini jambo moja nililokuwa na uhakika nalo ni hili

Sirudi nyumbani
Na hii ni hata leo nikisema hapana ni hapana

Kwa sababu mama yangu alikuwa mkali sana
Nilijiona nikirudi kumwambia nimepoteza nauli basi hakuna rangi ningeacha kuona

Nikajiwaza🤔

Kati ya kukutana na mama au kuvuka mipaka bila pesa, bora nijaribu bahati yangu

Nikajikaza nikamfuata dereva
Nikamsalimia kwa heshima zote za dunia
Shikamoo

Akanijibu
Marahaba binti, unasemaje?

Hapo ndipo nilipoanzisha filamu yangu ya kwanza ya maisha Uongooo pro 🤣
Nikaanza
Mimi nilikuja Malawi kufanya kazi za ndani : Astghafirullah 🙌

Dereva aliposikia hivyo akasema
Hebu njoo huku kidogo
Tukakaa pembeni

Sasa hapo nikaanza kusuka hadithi ya uongo kwa kasi ambayo hata nikikumbuka nachoka maana uongo sio tabia yangu mtu muongo na mnafiki hawajaachana mbali

Nikamuambia bosi wangu ananitesa sana, nimeamua kukimbia na kurudi Tanzania lakini sina hata senti

Dereva akaniangalia, akaangalia sura yangu ya mtoto mtulivu, akasikitika

Akamwita konda

Wakakubaliana kunibeba bure.
Mimi ndani ya moyo nikasema:
Asante Mungu, operation usirudi kwa mama imeanza rasmi🤣
Safari ikaanza

Usiku ulivyoingia, konda naye akaingia kwenye shughuli zake akanisahau kabisa kuhusu chakula
😭
Lakini Mungu alikuwa mbele
Nilikaa karibu na kaka mmoja ambaye kila alichonunua alikuwa ananipa sehemu bila kuniuliza hata MashaAllah 😍

Nilikuwa nakula kama nimepewa huduma ya full board😂

Tulipofika Karonga polisi wa Malawi walikuwa wanakagua
Konda akaniambia
Shuka ujifiche kwanza he kasheshe
Nikashuka

Ukaguzi ukaisha
Yaani simple tu ikawa imeisha hiyoo
Nikapanda tena

Mpaka leo nikiikumbuka najiona kama nilikuwa kwenye mission ya siri 🤣
Lakini ni kasheshe la kweli lilikuwa
Linaendela nahisi ningefaa kwa ujasusi🤪
Konda akasema shuka
Sisi tutapita hapa rasmi, wewe shuka upande ule vuka kwa mtumbwi 🙄
Nikabaki namtazama

Mtumbwi? Mimi ambaye hata kuangalia maji kwa muda mrefu naogopa? 😭

Akanipa hela kidogo ya kuvukia
Nikakuta mzee wa mtumbwi yupo tayari kazini Inaonekana ni michongo yake
Nikapanda

Tukiwa katikati ya mto nikaanza kuona mbele polisi kama anatusubiri kabisa 😂😂😂 heh

Moyo ukaanza kwenda mbio kuliko mtumbwi

Nilipofika upande wa pili, kweli polisi akaniita
Umetoka wapi?
Malawi
Ulikuwa unafanya nini?
Hapo nikarudia script ile ile akili mtu wangu 🤭

Nilikuwa nafanya kazi za ndani, bosi ananitesa, nimekimbia 🤣
Akauliza kitambulisho
Hakuna
Kibari
Hakuna
Simu
Hakuna
Kila kitu kilikuwa hakuna😂
Yule polisi akaniangalia halafu akasema
Wewe mtoto una ujanja sana
Akaandika namba yake kwenye karatasi na kuniambia

Ukifika Dar nitafute🤣😒
Mimi nikasema sawa, lakini kichwani nilikuwa nawaza basi lisiniondokee tu
🤣
Nikakimbia mpaka sehemu niliyoelekezwa

Baada ya muda gari likafika
Nikapanda
Safari ikaendelea mpaka Dar es Salaam

Leo nikikumbuka hii safari, najiuliza nilikuwa na ujasiri au nilikuwa na hofu ya mama yangu? 😂😂😂

Mom S 🥹🙌

Kwa sababu uongo wote huo, mipango yote hiyo, kuvuka mipaka, mtumbwi, polisi na hatari zote hizo tena mtoto wakike mdogo baso sijakomaa sura katika ya majangili (wanaume jokes)

chanzo chake kilikuwa kimoja tu

Mama yangu alikuwa mkali mno! 😭😭
Lakini pamoja na yote

Mama, nakupenda sana ❤️ ila ukweli ni kwamba ulikuwa mkali mnoooo!
Tabia za wapambanaji hizo.
Hongera kwa ujasiri
 
Nahisi hicho kitu kitakuwa kimekufanya uwe jasiri hata kwenye mishe zingine.
Kuna hali ambazo ukizipitia zinakuwa kama kamuongozo fulani hivi.
Yes nilipata ujasiri sana sana
Na nikaamini kila kitu kinawezekana
Nilijifunza kusimamia kitu ninachokiamini japo hofu hazikosekani
 
 
Back
Top Bottom